Makosa katika maandishi ya lugha ya Kiswahili, kwanini yanashamiri?

Makosa katika maandishi ya lugha ya Kiswahili, kwanini yanashamiri?

Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Huwa nikisikia tu "nyimbo yangu" hata kama angekuwa anajieleza nani, maelezo yote hata yawe mazuri vipi nalazimika kuyasahau.

Sijui walimu wao walikuwa wanawafundishi huu ujinga?
 
Nayaona sana haya makosa kwenye maandiko ya wasanii wetu nyota kupitia akaunti zao za mitandao ya kijamii

Mwanzo nilidhani kiwango cha elimu ya sasa ndiyo chanzo cha makosa ya kiuandishi kuzidi ila nayaona hadi kwa wasanii wakongwe waliopata elimu ya zamani
 
Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kusema ' mwimbo' badala ya wimbo.
 
Nahisi ilikua ni kutafuta urahisi katika utamkaji wa baadhi ya maneno ambapo matokeo yake ata ule utamkaji pia tukauleta kwenye uandishi.

mfano neno "zumuni" linatamkika kirahisi mdomoni zaidi ya neno "dhumuni"
neno "angu" ni jepesi kutamka kuliko neno "wangu"
Hapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo ni
R
L
Kuna yale ambayo irabu huzitamka kama consonant H mfano wakerewe lakini kuna mengine hayana hizi dh na th hivyo yanatumia z
Hivyo makosa mengine ya matumizi ya herufi yanachangiwa na lugha mama na siyo mwandishi kutokujua.
 
Hahahaha! Mkuu wangu, binafsi sio mtalaamu kiasi hicho hususani linapokuja suala la uchambuzi wa sarufi, kwa sababu mimi ni mwandishi tu wa kawaida ambae msisitizo wangu ni kuhakikisha naandika tungo sahihi kisarufi. Kimsingi, sina uwezo wa kuichambua sarufi kiufundi namna hiyo.

Lakini nikirudi katika matumizi ya kawaida tu, hiyo sentensi sioni kama ina tatizo lolote. Na wala siioni kama ni miongoni mwa zile sentensi ambazo huwa tunafanya sana makosa! Kwa mfano:

Mimi binafsi napenda kutumia Kiswahili kuliko lugha nyingine yoyote ile.

Ukiangalia kwenye hiyo sentensi, utaona maneno mawili ya mwanzo, lolote moja wapo halikutakiwa kuwepo.
Hiyo sentensi kaichambua kama sentensi za kiingereza ndiyo maana amejikuta anaona kuna makosa.
Ila ukiangalia viambishi vyote katika sentensi hiyo vinajitosheleza na kuipa sentensi maana.
 
Hiyo sentensi kaichambua kama sentensi za kiingereza ndiyo maana amejikuta anaona kuna makosa.
Ila ukiangalia viambishi vyote katika sentensi hiyo vinajitosheleza na kuipa sentensi maana.
Na hicho nilitaka kuongea kabla lakini nikachelea kusema wazi wazi wakati sina utaalamu huo!
 
Hapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo ni
R
L
Kuna yale ambayo irabu huzitamka kama consonant H mfano wakerewe lakini kuna mengine hayana hizi dh na th hivyo yanatumia z
Hivyo makosa mengine ya matumizi ya herufi yanachangiwa na lugha mama na siyo mwandishi kutokujua.
Kwenye kuongea, watu kama hawa wanavumilika manake unajua kabisa ni athari za makabila yao! Lakini wanaposhindwa hata kuadika!!!

(Mahali) ninakoenda ni mbali sana, halafu unaandika mahari ninakoenda ni mbari sana kwa sababu tu, labda ni Mkurya! Hapana kwa kweli.. mambo mengine nahisi ni kama tunajiendekeza tu!
 
Hapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo ni
R
L
Kuna yale ambayo irabu huzitamka kama consonant H mfano wakerewe lakini kuna mengine hayana hizi dh na th hivyo yanatumia z
Hivyo makosa mengine ya matumizi ya herufi yanachangiwa na lugha mama na siyo mwandishi kutokujua.
Nikweli mkuu upo sahihi lakini niliyoeleza pia ni moja kati ya sababu nyingi zinazochangia hili tatizo
 
Habari za asubuhi wana JF?

Kumekuwa na tatizo la kiuandishi kwa watu wengi kuanzia humu JF mpaka kwingineko kote kwenye mitandao ya kijamii mwanzo nilidhani ni kujisahau lakini sasa naona kama imezoeleka na kuonekana kama ni maneno ya kawaida kwenye kiswahili na watu wala hawastuki kuona kama ni makosa,yaani makosa yakirudiwa rudiwa mara nyingi huzoeleka na kuonekana ni usahihi

Naomba nitoe mifano michache ya hayo maneno hapa chini;
Nisamee badala ya Nisamehe
Eshima badala ya Heshima
Asubui badala ya Asubuhi
Mdogo angu badala ya Mdogo wangu
Kiac badala ya kiasi
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei
Utamsikia Mtangazaji anasema Nyimbo hii badala ya kusema wimbo huu

Yako maneno mengi sana yanayopotoshwa na wadau wengi humu ndani,ombi langu tu ndugu zangu tubadilike tuandike maneno kwa usahihi wake kwa sababu humu ndani panapitiwa na wanafunzi kuanzia Shule za Msingi,Sekondari na hata Vyuo wanajifunza nini juu ya tunayoyaandika humu?

Eti hapo ndio tunawadharau Wakenya hawajui Kiswahili hawajui kiswahili wakati sisi wenyewe ndio tunavuruga tu.

Ni hayo tu wadau muwe na Jumapili njema

Asante!
Mengine ni kama: nimefulai badala ya nimefurahi, vifua mbere badala ya vifua mbele, Daslam badala ya Dar es Salaam nk
 
Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Hata wewe sasa hapo kwenye maredio , hatuna neno hilo. Haya mambo ya umoja na uwingi lazima uwe makini kwenye maneno kama sufuria......, mbwa......, jiko....... na hapo uwingi wa jiko ni nini? (sidhani kama litakuacha salama neno hilo)
 
Hata wewe sasa hapo kwenye maredio , hatuna neno hilo. Haya mambo ya umoja na uwingi lazima uwe makini kwenye maneno kama sufuria......, mbwa......, jiko....... na hapo uwingi wa jiko ni nini? (sidhani kama litakuacha salama neno hilo)
Jiko= meko
 
Mkuu lengo kuu la kuwa na lugha ni kisaidia mawasiliano.
Kwahio basi as long as tukiongea tunaelewana basi hio lugha ni sahihi.

Sisi ni binadamu kwahio kamusi zinatakiwa kutufwata sisi na sio sisi kuzifwata kamusi..
Utakua unamaanisha neno 'my'
mai
 
Umenikumbusha kitu nimekuwa nikijiuliza siku nyingi kichwani.
Kama neno MAONYESHO siku hizi limegeuka na kuwa MAONESHO; Je KUJA nayo inatakiwa iwe KUKUJA na KULA iwe KUKULA, pamoja na maneno mengie yanayofanana na haya?
Je, kwenye KIswahili hatuna IRREGULAR VERBS kama ilivyo kwenye Kiingereza? Kama hatuna, hayo maneo mawili nimetolea mfano hapa, yanaitwaje kwenye Kiswahili, sababu hayafuati utaratibu wa vitenzi vingine kama ilivyo kawaida kwenye Kiswahili?

Mfano mwingine

kitenzi kuta: mfano maneno siku-kukuta, nime-kukuta. Kinaanza na ku- kama ilivyo kwa mifano miwili hapo juu, lakini unaweza kuona mkanganyiko ulioko katika maneo haya mawili. Hili pamoja na kwamba limeanza na ku- lakini bado linaongezwa ku nyingine tena, tofauti na yale maneno mawili ya mwanzo niliyoyatolea mfano hapo juu
watafiti wa Kiswahili mpo hapa?
Onyo-maonyesho
Ona-maonesho.
Kwa upande wa kibiashara ni maonesho
 
Back
Top Bottom