Bahati furaha
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 3,054
- 1,415
Huwa nikisikia tu "nyimbo yangu" hata kama angekuwa anajieleza nani, maelezo yote hata yawe mazuri vipi nalazimika kuyasahau.Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kusema ' mwimbo' badala ya wimbo.Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Hapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo niNahisi ilikua ni kutafuta urahisi katika utamkaji wa baadhi ya maneno ambapo matokeo yake ata ule utamkaji pia tukauleta kwenye uandishi.
mfano neno "zumuni" linatamkika kirahisi mdomoni zaidi ya neno "dhumuni"
neno "angu" ni jepesi kutamka kuliko neno "wangu"
Kadhalika, mimi pia hukerwa na hili. Sijui hawakufundishwa kuwa 'nyimbo' inawakilisha wingi. Ni kero kwa kweli.Huwa nikisikia tu "nyimbo yangu" hata kama angekuwa anajieleza nani, maelezo yote hata yawe mazuri vipi nalazimika kuyasahau.
Sijui walimu wao walikuwa wanawafundishi huu ujinga?
Hiyo sentensi kaichambua kama sentensi za kiingereza ndiyo maana amejikuta anaona kuna makosa.Hahahaha! Mkuu wangu, binafsi sio mtalaamu kiasi hicho hususani linapokuja suala la uchambuzi wa sarufi, kwa sababu mimi ni mwandishi tu wa kawaida ambae msisitizo wangu ni kuhakikisha naandika tungo sahihi kisarufi. Kimsingi, sina uwezo wa kuichambua sarufi kiufundi namna hiyo.
Lakini nikirudi katika matumizi ya kawaida tu, hiyo sentensi sioni kama ina tatizo lolote. Na wala siioni kama ni miongoni mwa zile sentensi ambazo huwa tunafanya sana makosa! Kwa mfano:
Mimi binafsi napenda kutumia Kiswahili kuliko lugha nyingine yoyote ile.
Ukiangalia kwenye hiyo sentensi, utaona maneno mawili ya mwanzo, lolote moja wapo halikutakiwa kuwepo.
Na hicho nilitaka kuongea kabla lakini nikachelea kusema wazi wazi wakati sina utaalamu huo!Hiyo sentensi kaichambua kama sentensi za kiingereza ndiyo maana amejikuta anaona kuna makosa.
Ila ukiangalia viambishi vyote katika sentensi hiyo vinajitosheleza na kuipa sentensi maana.
Kwenye kuongea, watu kama hawa wanavumilika manake unajua kabisa ni athari za makabila yao! Lakini wanaposhindwa hata kuadika!!!Hapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo ni
R
L
Kuna yale ambayo irabu huzitamka kama consonant H mfano wakerewe lakini kuna mengine hayana hizi dh na th hivyo yanatumia z
Hivyo makosa mengine ya matumizi ya herufi yanachangiwa na lugha mama na siyo mwandishi kutokujua.
Nikweli mkuu upo sahihi lakini niliyoeleza pia ni moja kati ya sababu nyingi zinazochangia hili tatizoHapana kuna makabila hayana matumizi kwa baadi ya herufi mfano wa herufi hizo ni
R
L
Kuna yale ambayo irabu huzitamka kama consonant H mfano wakerewe lakini kuna mengine hayana hizi dh na th hivyo yanatumia z
Hivyo makosa mengine ya matumizi ya herufi yanachangiwa na lugha mama na siyo mwandishi kutokujua.
Mengine ni kama: nimefulai badala ya nimefurahi, vifua mbere badala ya vifua mbele, Daslam badala ya Dar es Salaam nkHabari za asubuhi wana JF?
Kumekuwa na tatizo la kiuandishi kwa watu wengi kuanzia humu JF mpaka kwingineko kote kwenye mitandao ya kijamii mwanzo nilidhani ni kujisahau lakini sasa naona kama imezoeleka na kuonekana kama ni maneno ya kawaida kwenye kiswahili na watu wala hawastuki kuona kama ni makosa,yaani makosa yakirudiwa rudiwa mara nyingi huzoeleka na kuonekana ni usahihi
Naomba nitoe mifano michache ya hayo maneno hapa chini;
Nisamee badala ya Nisamehe
Eshima badala ya Heshima
Asubui badala ya Asubuhi
Mdogo angu badala ya Mdogo wangu
Kiac badala ya kiasi
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei
Utamsikia Mtangazaji anasema Nyimbo hii badala ya kusema wimbo huu
Yako maneno mengi sana yanayopotoshwa na wadau wengi humu ndani,ombi langu tu ndugu zangu tubadilike tuandike maneno kwa usahihi wake kwa sababu humu ndani panapitiwa na wanafunzi kuanzia Shule za Msingi,Sekondari na hata Vyuo wanajifunza nini juu ya tunayoyaandika humu?
Eti hapo ndio tunawadharau Wakenya hawajui Kiswahili hawajui kiswahili wakati sisi wenyewe ndio tunavuruga tu.
Ni hayo tu wadau muwe na Jumapili njema
Asante!
Hata wewe sasa hapo kwenye maredio , hatuna neno hilo. Haya mambo ya umoja na uwingi lazima uwe makini kwenye maneno kama sufuria......, mbwa......, jiko....... na hapo uwingi wa jiko ni nini? (sidhani kama litakuacha salama neno hilo)Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
Wengine wanakwenda mbali zaidi kwa kusema ' mwimbo' badala ya wimbo.
Jiko= mekoHata wewe sasa hapo kwenye maredio , hatuna neno hilo. Haya mambo ya umoja na uwingi lazima uwe makini kwenye maneno kama sufuria......, mbwa......, jiko....... na hapo uwingi wa jiko ni nini? (sidhani kama litakuacha salama neno hilo)
Duuuu big up mzee baba πππππJiko= meko
Utakua unamaanisha neno 'my'Mkuu lengo kuu la kuwa na lugha ni kisaidia mawasiliano.
Kwahio basi as long as tukiongea tunaelewana basi hio lugha ni sahihi.
Sisi ni binadamu kwahio kamusi zinatakiwa kutufwata sisi na sio sisi kuzifwata kamusi..
Halufu badala ya harufuAfadhali ya hao kuliko wale wa R anaweka L inatia kinyaa!
Onyo-maonyeshoUmenikumbusha kitu nimekuwa nikijiuliza siku nyingi kichwani.
Kama neno MAONYESHO siku hizi limegeuka na kuwa MAONESHO; Je KUJA nayo inatakiwa iwe KUKUJA na KULA iwe KUKULA, pamoja na maneno mengie yanayofanana na haya?
Je, kwenye KIswahili hatuna IRREGULAR VERBS kama ilivyo kwenye Kiingereza? Kama hatuna, hayo maneo mawili nimetolea mfano hapa, yanaitwaje kwenye Kiswahili, sababu hayafuati utaratibu wa vitenzi vingine kama ilivyo kawaida kwenye Kiswahili?
Mfano mwingine
kitenzi kuta: mfano maneno siku-kukuta, nime-kukuta. Kinaanza na ku- kama ilivyo kwa mifano miwili hapo juu, lakini unaweza kuona mkanganyiko ulioko katika maneo haya mawili. Hili pamoja na kwamba limeanza na ku- lakini bado linaongezwa ku nyingine tena, tofauti na yale maneno mawili ya mwanzo niliyoyatolea mfano hapo juu
watafiti wa Kiswahili mpo hapa?