Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Mzee...
Vijana wako wanashangaa eti kwanini nyerer hakitaja ukweli wa historia yake.

Hivi mwenye dhamira unajiuliza kwnini anadhamiri tena?

Mzee una kipaji na elimu ya kuwavumilia Waefeso hawa, ila sisi tunawaona wasumbufu kama Walawi wa Musa
Badee unauliza swali nyeti sana.

Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza matatizo yaliyotokea 1962 pale TANU kwa ushauri wa Mwalimu Kihere ilipoamua kuandika historia yake.

Katika mazungumzo haya alikuwapo Dossa Aziz na Nyerere.

Ikaamuliwa Abdul aandike historia hiyo na msaidizi wake akawa Dr. Wilbard Kleruu.

Abdul akatumia nyaraka alizokuwanazo toka 1929 baba yake alipokuwa mmoja wa waasisi wa African Association kama Secretary na nyingine yeye alipochukua uongozi wa TAA 1950 kama Secretary na Dr. Vedasto Kyaruzi akiwa President.

Ikawa historia hii anaiandika kutoka yale ambayo yeye kapokea kutoka kwa baba yake ambayo yalikuwa katika mswada wa kitabu na yake mwenyewe akiwa Burma Vita Kuu ya Pili (1939 - 1945) walipoamua kuunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Inaelekea historia hii haikuweza kukubalika kama ndiyo historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Pakawa na sintofahamu Abdul akajitoa akabakia Dr. Kleruu katika uandishi ule wa historia ya chama cha TANU.

Mswada huu haukuchapwa ukabakia ofisi ya TANU hadi ulipoibiwa na kuchapwa kitabu mwaka wa 1971 jina la mwandishi likiwa Abubakar Ulotu.

Hili neno ''kuibiwa,'' alilikataa mhariri wa kitabu cha Abdul Sykes alinitahadharisha kuwa tunaweza kuingia matatani.

TANU ikaja juu kuhusu kitabu hiki kakini walilalamika kimya kimya.

Mwaka wa 1977 ndipo Chuo Cha CCM Kivukoni kikaandika historia nyingine ya TANU.

Ukivisoma vitabu hivi utasema vyote vimeandikwa na mtu mmoja.
Vitabu vyote hivi viwili Abdul Sykes hayumo na wazalendo wengine wengi pia.

Matokeo ya haya ni kuwa pakawa hakuna historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika hadi kilipotoka kitabu cha Abdul Sykes 1998.

Kitabu hiki kiliwashtua watu wengi mmojawapo Prof. Haroub Othman.

Vyuo Vikuu Marekani na Ulaya wakakipenda kwani kilikuwa kitabu kilichokuja na elimu mpya.

Prof. Haroub akaenda kwa Mwalimu kutaka kusadikisha historia ya Nyerere na Abdul Sykes kama vile nilivyoandika ndivyo kweli ilivyokuwa.

Lakini Prof. Haroub kabla hajakwenda kwa Mwalimu alizungumza na rafiki yake Abdul Sykes Ahmed Rashaad Ali kutafuta ithibati ya kile nilichoandika ambayo aliipata.

Prof. alikuwa na hoja kuwa Mwalimu na yeye aandike ili upande wake wa historia hii ufahamike vinginevyo historia yake itaingia doa.

Kulikuwa na mambo makubwa mawili ambayo Prof. Haroub alitaka Mwalimu ayaweke wazi.

Kwanza mchango wa Ukoo wa Sykes katika kupigania uhuru wa Tanganyika na pili uhusiano wa Nyerere na Waislam kabla na baada ya uhuru.

Bahati mbaya Mwalimu alikuwa mgonjwa hana nguvu tena za kunyanyua kalamu kuandika.

Yapo mengi lakini nakuomba utosheke na haya.

1672669703372.jpeg

Nakala ya toleo la kwanza la kitabu kilichochapwa na Minerva Press, London 1998

1672670601607.jpeg

1672671227824.jpeg


1672670249286.jpeg

Mwalimu Kihere

1672669802124.jpeg

Kushoto Prof. Haroub Othman, Ahmed Rashaad Ali na Sheikh Ahmed Islam picha hii niliwapiga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tulikuwa tunakwenda Jeddah na Air Tanzania Corporation (ATC) kwa ajili ya Umra 1997​
 
Ndugu yangu Mohamed,

Picha ninayoipata ni kuwa kuna watu waliamua kupindisha historia wakiamini kuwa wangemfurahisha Nyerere kwa kumpa baadhi ya sifa ambazo hazikuwa zake.

Sababu zinazonisukuma kuamini hivyo ni hizi mbili:

- Hadi wakati anastaafu, bado watu wengi walioshuhudia maisha yake baada ya kuacha ualimu Pugu walikuwepo hai. Asingekuwa mpumbavu kuukana ukarimu wa familia ya Sykes huku akijua mashuhuda wa ukarimu huo wapo hai wengi.

Lakini pia katika hutuba yake ya kuagana na wazee wa Dar 1985, alieleza kwa ufasaha jinsi wenyeji wa Dar (moslems in particular) walivyochangia katika harakati za uhuru. Alikwenda mbali akaeleza mpaka baadhi ya matambiko waliyofanya wazee wa kiislamu akiwa peke yake wa imani tofauti.

- Na hili la kuweka historia sawa, nakumbuka wakati wa kukabidhiwa nyumba aliyojengewa na jeshi aliongelea kufurahishwa kwake kuwa kwa ukubwa wa nyumba ile, jopo la watu ambao wangemsaidia kuandika kitabu wakiongozwa na Haroub wangepata nafasi ya kukaa bila bugudha, bahati mbaya baada ya hapo ndipo ugonjwa na baadaye umauti vikamkuta.
 
Ndugu yangu Mohamed,

Picha ninayoipata ni kuwa kuna watu waliamua kupindisha historia wakiamini kuwa wangemfurahisha Nyerere kwa kumpa baadhi ya sifa ambazo hazikuwa zake.

Sababu zinazonisukuma kuamini hivyo ni hizi mbili:

- Hadi wakati anastaafu, bado watu wengi walioshuhudia maisha yake baada ya kuacha ualimu Pugu walikuwepo hai. Asingekuwa mpumbavu kuukana ukarimu wa familia ya Sykes huku akijua mashuhuda wa ukarimu huo wapo hai wengi.

Lakini pia katika hutuba yake ya kuagana na wazee wa Dar 1985, alieleza kwa ufasaha jinsi wenyeji wa Dar (moslems in particular) walivyochangia katika harakati za uhuru. Alikwenda mbali akaeleza mpaka baadhi ya matambiko waliyofanya wazee wa kiislamu akiwa peke yake wa imani tofauti.

- Na hili la kuweka historia sawa, nakumbuka wakati wa kukabidhiwa nyumba aliyojengewa na jeshi aliongelea kufurahishwa kwake kuwa kwa ukubwa wa nyumba ile, jopo la watu ambao wangemsaidia kuandika kitabu wakiongozwa na Haroub wangepata nafasi ya kukaa bila bugudha, bahati mbaya baada ya hapo ndipo ugonjwa na baadaye umauti vikamkuta.
Gagnija,
Naomba nikueleze vitu ambavyo nimekutananavyo katika historia ya Mwalimu Nyerere na kuandikwa kwa maisha yake.

Shika hapo ulipoachia na sasa tusonge mbele lakini turudi nyuma mwaka wa 1963.

Mwaka wa 1963 Lady Judith Listowel alikuja Tanganyika kwa nia ya kutafiti na kuandika kitabu,, ''The Making of Tanganyika.''

Listowel mwenyeji wake Nairobi alikuwa Peter Colmore na Peter Colmore akamuunganisha Listowel na Ally Sykes Dar es Salaam.

Haya kanieleza Peter Colmore mwenyewe wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Ally Sykes, ''Under the Shadow of British Colonialism in Tanganyika,'' (hakijachapwa).

Ally Sykes akamkutanisha Listowel na wazalendo takriban wote waliokuwa Dar es Salaam walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika pamoja na Nyerere.

Listowel ndiye mtafiki pekee aliyesema kuwa Nyerere aligombea urais wa TAA na Abdul Sykes na Nyerere alipata ushindi mdogo sana.

Inaelekea Nyerere hakutoa ushirikano kwa Listowel na kuna malalamiko kuwa alimkatalia Listowel kuandika maisha yake kiasi palitokea ugomvi kidogo baina yao Nyerere alipogundua kuwa maisha yake yamo ndani ya kitabu yameelezwa.

Katika vitabu vyote vilivyoandikwa kabla ya kitabu cha Abdul Sykes kitabu hiki ndicho kilichokuwa karibu sana na ukweli wa historia ya TANU.

Abdul Sykes alizungumza na Listowel lakini hakumweleza chochote cha maana na sababu yake alichelea akieleza historia ya TANU huenda Nyerere akajihisi vibya.

Haya Listowel kaeleza katika kitabu chake.

Abdul hakutaka kueleza chochote kuhusu mchango wake katika kuunda TANU kwa kuchelea isije Nyerere rafiki yake akajihisi vibaya.

Hii ilitokana na yeye kujitoa katika uandishi wa historia ya TANU mwaka wa 1962 baada ya kuona kuna mambo aliyokuwa ameandika hayakupokelewa vyema.

Mimi nimefanyakazi na Oxford University Press, (OUP) Nairobi na wamechapa vitabu vyangu viwili na tukawa na uhusiano mzuri kiasi nilizungumza nao mengi kuhusu kitabu cha Abdul Sykes ambacho walikikataa kwa sababu maalum ingawa waliniambia kina historia nzuri sana ya Julius Nyerere.

OUP walinifahamisha kuwa juhudi zao zote za kutaka kuandika maisha ya Mwalimu zimeshindikana kwa kuwa hakutaka maisha yake yaandikwe.

Kwa nini hakutaka ni swali ambalo angeweza kujibu yeye mwenyewe peke yake.

Wengine wanachoweza kusema ni kuwa labda alihofu kuwa ikiwa maisha yake yataandikwa basi maisha ya wengine wa wakati wake lazima nayo yatokee pamoja na yeye.

Sehemu muhimu ya maisha yake ni jinsi alivyoingizwa katika siasa za Dar es Salaam ya 1950 na kujenga msingi wake kutokana na watu kama akina Sykes, Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Baraza la Wazee wa TANU likiongozwa na Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) ambao viongozi wake wawili Secretary Ali Mwinyi Tambwe na Iddi Faiz Mafungo walikuwa katika uongozi wa juu wa TANU.

Mwalimu alikuwa na hofu kubwa sana na historia ya Waislam na ni kitu ambacho hakupenda kusikia kikitajwa katika maisha yake wala katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uislam ukafanywa kitu nyeti sana ambacho ni mwiko mkubwa kuongelewa.
Inawezekana kabisa hii ikawa sababu ya Mwalimu kukataa kuaandika maisha yake.

142224138_884215868992459_6238156843396961714_n.jpg
1672686974493.jpeg


 
1672685995816.jpeg


Ukiitazama picha vizuri utabaini duka lilikuwa likiuza bidhaa nyingine zaidi ya mafuta ya taa.

Naliona bango la Coca Cola na mabango mengine ya bidhaa mbali mbali.

Kwakuwa picha hii umeileta mwenyewe Mohamed Said na dhahiri imeonyesha bidhaa mbali mbali zaidi ya mafuta ya taa,litakuwa jambo la uungwana kukiri hadithi yako ya historia ya TAA na TANU ina mapungufu pia.
 
View attachment 2467042

Ukiitazama picha vizuri utabaini duka lilikuwa likiuza bidhaa nyingine zaidi ya mafuta ya taa.

Naliona bango la Coca Cola na mabango mengine ya bidhaa mbali mbali.

Kwakuwa picha hii umeileta mwenyewe Mohamed Said na dhahiri imeonyesha bidhaa mbali mbali zaidi ya mafuta ya taa,litakuwa jambo la uungwana kukiri hadithi yako ya historia ya TAA na TANU ina mapungufu pia.
Ngongo,
Hakika kukosa kueleza kuwa alikuwa anauza na Coca-Cola ni kupunguza taarifa katika biashara ya Mama Maria.

Lakini nimeandikiwa kuwa Mama Maria Nyerere alikuwa anauza soda hiyo na alikuwa akipelekewa dukani kwake pale Majumba Sita na mtu mmoja anaitwa Amal Bafadhil.

Huyu mtu sasa ni marehemu.
 
Gagnija,
Naomba nikueleze vitu ambavyo nimekutananavyo katika historia ya Mwalimu Nyerere na kuandikwa kwa maisha yake.

Shika hapo ulipoachia na sasa tusonge mbele lakini turudi nyuma mwaka wa 1963.

Mwaka wa 1963 Lady Judith Listowel alikuja Tanganyika kwa nia ya kutafiti na kuandika kitabu,, ''The Making of Tanganyika.''

Listowel mwenyeji wake Nairobi alikuwa Peter Colmore na Peter Colmore akamuunganisha Listowel na Ally Sykes Dar es Salaam.

Haya kanieleza Peter Colmore mwenyewe wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Ally Sykes, ''Under the Shadow of British Colonialism in Tanganyika,'' (hakijachapwa).

Ally Sykes akamkutanisha Listowel na wazalendo takriban wote waliokuwa Dar es Salaam walioshiriki katika kupigania uhuru wa Tanganyika pamoja na Nyerere.

Listowel ndiye mtafiki pekee aliyesema kuwa Nyerere aligombea urais wa TAA na Abdul Sykes na Nyerere alipata ushindi mdogo sana.

Inaelekea Nyerere hakutoa ushirikano kwa Listowel na kuna malalamiko kuwa alimkatalia Listowel kuandika maisha yake kiasi palitokea ugomvi kidogo baina yao Nyerere alipogundua kuwa maisha yake yamo ndani ya kitabu yameelezwa.

Katika vitabu vyote vilivyoandikwa kabla ya kitabu cha Abdul Sykes kitabu hiki ndicho kilichokuwa karibu sana na ukweli wa historia ya TANU.

Abdul Sykes alizungumza na Listowel lakini hakumweleza chochote cha maana na sababu yake alichelea akieleza historia ya TANU huenda Nyerere akajihisi vibya.

Haya Listowel kaeleza katika kitabu chake.

Abdul hakutaka kueleza chochote kuhusu mchango wake katika kuunda TANU kwa kuchelea isije Nyerere rafiki yake akajihisi vibaya.

Hii ilitokana na yeye kujitoa katika uandishi wa historia ya TANU mwaka wa 1962 baada ya kuona kuna mambo aliyokuwa ameandika hayakupokelewa vyema.

Mimi nimefanyakazi na Oxford University Press, (OUP) Nairobi na wamechapa vitabu vyangu viwili na tukawa na uhusiano mzuri kiasi nilizungumza nao mengi kuhusu kitabu cha Abdul Sykes ambacho walikikataa kwa sababu maalum ingawa waliniambia kina historia nzuri sana ya Julius Nyerere.

OUP walinifahamisha kuwa juhudi zao zote za kutaka kuandika maisha ya Mwalimu zimeshindikana kwa kuwa hakutaka maisha yake yaandikwe.

Kwa nini hakutaka ni swali ambalo angeweza kujibu yeye mwenyewe peke yake.

Wengine wanachoweza kusema ni kuwa labda alihofu kuwa ikiwa maisha yake yataandikwa basi maisha ya wengine wa wakati wake lazima nayo yatokee pamoja na yeye.

Sehemu muhimu ya maisha yake ni jinsi alivyoingizwa katika siasa za Dar es Salaam ya 1950 na kujenga msingi wake kutokana na watu kama akina Sykes, Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Baraza la Wazee wa TANU likiongozwa na Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) ambao viongozi wake wawili Secretary Ali Mwinyi Tambwe na Iddi Faiz Mafungo walikuwa katika uongozi wa juu wa TANU.

Mwalimu alikuwa na hofu kubwa sana na historia ya Waislam na ni kitu ambacho hakupenda kusikia kikitajwa katika maisha yake wala katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Uislam ukafanywa kitu nyeti sana ambacho ni mwiko mkubwa kuongelewa.
Inawezekana kabisa hii ikawa sababu ya Mwalimu kukataa kuaandika maisha yake.

Mwalimu hajawahi kuuogopa uislam. Hiyo ya Wistowel kukosa ushirikiano wa Nyerere pengine ilitokana na makosa ya Colmore na baadhi ya wazee wako waliopigania uhuru.

Waeleze wasiojua hapa jinsi Colmore alivyotaka kumtumia mmoja wa wazee wenu kwa ukaribu wake na Nyerere kupata uwakala wa BAT.

Mwalimu alikuwa smart toka mwanzo. Alikuwa akipigania uhuru wa watanganyika, si hao waliotaka kuwa mawakala wa kina Colmore.

Kwa wadogo wasiojua, hayo ndio yalimkosanisha Nyerere na Kambona pia.
 
Badee unauliza swali nyeti sana.

Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza matatizo yaliyotokea 1962 pale TANU kwa ushauri wa Mwalimu Kihere ilipoamua kuandika historia yake.

Katika mazungumzo haya alikuwapo Dossa Aziz na Nyerere.

Ikaamuliwa Abdul aandike historia hiyo na msaidizi wake akawa Dr. Wilbard Kleruu.

Abdul akatumia nyaraka alizokuwanazo toka 1929 baba yake alipokuwa mmoja wa waasisi wa African Association kama Secretary na nyingine yeye alipochukua uongozi wa TAA 1950 kama Secretary na Dr. Vedasto Kyaruzi akiwa President.

Ikawa historia hii anaiandika kutoka yale ambayo yeye kapokea kutoka kwa baba yake ambayo yalikuwa katika mswada wa kitabu na yake mwenyewe akiwa Burma Vita Kuu ya Pili (1939 - 1945) walipoamua kuunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika.

Inaelekea historia hii haikuweza kukubalika kama ndiyo historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Pakawa na sintofahamu Abdul akajitoa akabakia Dr. Kleruu katika uandishi ule wa historia ya chama cha TANU.

Mswada huu haukuchapwa ukabakia ofisi ya TANU hadi ulipoibiwa na kuchapwa kitabu mwaka wa 1971 jina la mwandishi likiwa Abubakar Ulotu.

Hili neno ''kuibiwa,'' alilikataa mhariri wa kitabu cha Abdul Sykes alinitahadharisha kuwa tunaweza kuingia matatani.

TANU ikaja juu kuhusu kitabu hiki kakini walilalamika kimya kimya.

Mwaka wa 1977 ndipo Chuo Cha CCM Kivukoni kikaandika historia nyingine ya TANU.

Ukivisoma vitabu hivi utasema vyote vimeandikwa na mtu mmoja.
Vitabu vyote hivi viwili Abdul Sykes hayumo na wazalendo wengine wengi pia.

Matokeo ya haya ni kuwa pakawa hakuna historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika hadi kilipotoka kitabu cha Abdul Sykes 1998.

Kitabu hiki kiliwashtua watu wengi mmojawapo Prof. Haroub Othman.

Vyuo Vikuu Marekani na Ulaya wakakipenda kwani kilikuwa kitabu kilichokuja na elimu mpya.

Prof. Haroub akaenda kwa Mwalimu kutaka kusadikisha historia ya Nyerere na Abdul Sykes kama vile nilivyoandika ndivyo kweli ilivyokuwa.

Lakini Prof. Haroub kabla hajakwenda kwa Mwalimu alizungumza na rafiki yake Abdul Sykes Ahmed Rashaad Ali kutafuta ithibati ya kile nilichoandika ambayo aliipata.

Prof. alikuwa na hoja kuwa Mwalimu na yeye aandike ili upande wake wa historia hii ufahamike vinginevyo historia yake itaingia doa.

Kulikuwa na mambo makubwa mawili ambayo Prof. Haroub alitaka Mwalimu ayaweke wazi.

Kwanza mchango wa Ukoo wa Sykes katika kupigania uhuru wa Tanganyika na pili uhusiano wa Nyerere na Waislam kabla na baada ya uhuru.

Bahati mbaya Mwalimu alikuwa mgonjwa hana nguvu tena za kunyanyua kalamu kuandika.

Yapo mengi lakini nakuomba utosheke na haya.

View attachment 2466827
Nakala ya toleo la kwanza la kitabu kilichochapwa na Minerva Press, London 1998

View attachment 2466834
View attachment 2466843

View attachment 2466830
Mwalimu Kihere

View attachment 2466828
Kushoto Prof. Haroub Othman, Ahmed Rashaad Ali na Sheikh Ahmed Islam picha hii niliwapiga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tulikuwa tunakwenda Jeddah na Air Tanzania Corporation (ATC) kwa ajili ya Umra 1997​
Mzee Mohammed...

Aisee Historia ina maajabu, Allah akujaxe aya njema
 
Mwalimu hajawahi kuuogopa uislam. Hiyo ya Wistowel kukosa ushirikiano wa Nyerere pengine ilitokana na makosa ya Colmore na baadhi ya wazee wako waliopigania uhuru.

Waeleze wasiojua hapa jinsi Colmore alivyotaka kumtumia mmoja wa wazee wenu kwa ukaribu wake na Nyerere kupata uwakala wa BAT.

Mwalimu alikuwa smart toka mwanzo. Alikuwa akipigania uhuru wa watanganyika, si hao waliotaka kuwa mawakala wa kina Colmore.

Kwa wadogo wasiojua, hayo ndio yalimkosanisha Nyerere na Kambona.
Gagnija,
Hili la hofu ya Waislam na tuliache.

Hapana haja ya lugha kali kuwa niwaeleze ''wasiojua.''

Ni kweli kuwa Peter Colmore alitaka sana kupanua biashara yake Tanganyika na tayari alishafungua ofisi hapa Dar es Salaam.

Umenikumbusha mbali sana.

Nilikuwa nikenda na baba yangu kwenye ofisi hii iliyokuwa Mtaa wa Lindi karibu na International Hotel.

Hapa ndipo kwa mara yangu ya kwanza mimi niliona kiyoyozi (air condition) na reel to reel tape deck.

Ilikuwa ofisi ya kupendeza sana.

Nilipata kumwambia siku moja kuwa nilikuwa nikenda pale ofisini kwake na baba yangu.

Hakukumbuka.

Kuhusu uwakala wa BAT Peter Colmore alikuwanao kabla.

Ally Sykes na Peter Colmore walikuwa wanataka mambo makubwa sana kupita hayo.

Peter Colmore aliamini kuwa Ally Sykes atafungua milango yote kwa kuwa alikuwa ni mtu hodari mchapa kazi na ana wasta, yaani ana uwezo wa kufanya lile aliytakalo na hakuna wa kumzuia.

Bahati mbaya mambo hayakwenda hivyo.

Naona unaandika umeghadhibika lugha ina kuwa kali.

Niwie radhi kama nimekuudhi kwa maneno yangu.

(Mwalimu wangu Sheikh Haruna alikuwa akinambia nakuombea kwa Allah akupe ''kubul'' na Insha Allah utaipata.

Kubul ni tabu kuieleza lakini kwa ufupi ni kuwa juu ya kila kitu.
Mathalan akitaka mtu kukudhalilisha anashindwa.

Akaniasa akasema ili upate kubul lazima ujishushe na waweke juu wengine wewe kaa miguuni kwao na tosheka na kuwa mtumishi wao).

Ally Sykes hakuwa wakala wa Peter Colmore.

Colmore akimuheshimu Ally Sykes na wakatajirika pamoja.

Haya nayajua kuwa watu hawa wawili walitaka kuifanyia Tanganyika makubwa katika biashara za kimataifa.

Nimejifunza mengi kutokana na barua nilizosoma wakati naandika kitabu cha Ally Sykes ''Under the Shadow of British Colonialism: The Life of Ally Kleist Sykes.''

Makampuni haya tayari alikuwa anayo na Ally Sykes akiwa mshirika wake:

''With Colmore as my partner we set up an office in Dar es Salaam.

Our company advertised from cigarettes to petroleum products.

We represented, promoted, and were consultants to Coca Cola (East Africa) Ltd; The Cooper Motors Corporation Ltd; Allsopp (EA) Ltd; The Shell Company of East Africa Ltd, Aspro Nicholas Ltd; Gailey and Roberts Ltd; Bata Shoes Company Ltd; Kenya Broadcasting Service, Cotton Lint and Seed Marketing Board, Raleigh Industries of East Africa Ltd; Commercial Representative in Kenya for Tanganyika Broadcasting Corporation.

The head office of this massive sales promotion venture was in Nairobi Delamere Avenue, now Kenyatta Avenue.

Peter Colmore then founded his own recording company - High Fidelity Productions Limited.

Peter Colmore built some products into household names in East Africa.

The best musicians East Africa had ever known promoted some products.

Apart from this Colmore also ventured into film making with Dr. Johnson who owned the recording company Jambo of which the talented singer and bandmaster Salum Abdallah recorded.

Colmore signed Edouard Masengo the gifted guitarist from Elizabethville, Belgian Congo to promote Coca-Cola.''

1672696654792.jpeg


1672696949544.jpeg

Na Peter Colmore nyumbani kwake Muthaiga, Nairobi 1995​
 
Hakuna muasisi wa TANU, apart from Ally Sykes, aliyekwenda na Colmore kwa Nyerere kuomba favor asaidiwe kuanzisha biashara ya uwakala?!

Unalijua vyema, umeamua kulikwepa tu.
 
Ngongo,
Hakika kukosa kueleza kuwa alikuwa anauza na Coca-Cola ni kupunguza taarifa katika biashara ya Mama Maria.

Lakini nimeandikiwa kuwa Mama Maria Nyerere alikuwa anauza soda hiyo na alikuwa akipelekewa dukani kwake pale Majumba Sita na mtu mmoja anaitwa Amal Bafadhil.

Huyu mtu sasa ni marehemu.
Ningependa kufahamu MAGOMENI MAJUMBA SITA kwa inaitwa Magomeni ipi au mtaa gani
Yaan hilo Duka lilikuwa ENEO gani kwa MAGOMENI ya sasa
 
Hakuna muasisi wa TANU, apart from Ally Sykes, aliyekwenda na Colmore kwa Nyerere kuomba favor asaidiwe kuanzisha biashara ya uwakala?!

Unalijua vyema, umeamua kulikwepa tu.
Gagnija,
Simfahamu huyo muasisi si kama nitakuwa najua kila kitu.

Nami nikiwa kitu sikijui nasema sijui.

Mimi siko hapa kufanya ushindani nishinde.

Mimi niko hapa kueleza historia ya wazee wangu.

Ndiyo wakati mwingine husema umenikumbusha mbali.

Jambo nakuwa nimelisahau na kitu kinatokea nakumbuka.
 
Juu ya hayo yote makala hii imeruka sehemu muhimu sana katika maisha yake na kwa kweli si yake tu bali na ya mumewe Mwalimu Nyerere na historia ya TANU na pia kuandika mengine ambayo si ya kweli.
Ungetusaidia uweke link yake
 
Hilo la kuwa Mwalimu aliwaogopa waislamu halina ukweli. Mwalimu aliwashughulikia wote ambao aliamini kuwa wana nia mbaya na taifa lake bila kujali dini zao. Mmoja wa watu wa kwanza kukumbwa na sheria ya kutia watu kizuizini alikuwa mkristu mwenzake Kasanga Tumbo. Wote tunajua yaliyowapata wakina Kambona ambao wote walikuwa wakristu ukimuondoa Bibi Titi Mohammed. Tunajua alitaifisha shule zote ili kutoa nafasi sawa kwa raia wote kupata elimu ingawa katika hizo shule nyingi zilikuwa ni za wakristu. Ukweli ni kuwa asingetaifisha zile shule ingewachukuwa waislamu miaka mingi kuwafikia wakristu kielimu. Wakati Nyerere anakazia siasa zake za ujamaa na kujitegemea aliwaachia wakina Sykes waendelee na biashara zao za Commission Agent na Travel Agency. Mtu ilikuwa ukitaka kusafiri kwenda nje ilikuwa lazima ukanunue cheti cha chanjo katika ofisi ya Sykes Travel Agency iliyokuwa mtaa wa Mkwepu. Wakina Sykes walikuwa ni wafanyabiashara na baada yakupata uhuru waliachana na mambo ya siasa.

Mara nyingi mfano wa chuki za Mwalimu dhidi ya waislamu unaotolewa ni wa kuvunjika kwa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) kilichoanzishwa rasmi 1954 mjini Mombasa chini ya Agakhan. Ni ajabu kuwa chuki hizi hazikumzuia kuwapa kiwanja Chang'ombe na kuweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu cha Kiislamu. Chuo Kikuu hicho hakikujengwa na mara ya mwisho nasikia kiwanja kilikabidhiwa kwa tajiri wa kiislamu (Chuo Kikuu cha Kiislamu kilichopo Morogoro kilitolewa kwa waislamu na Rais Mkapa ambae alikuwa ni Mkatoliki). Nia kubwa ya EAMWS ilikuwa ni kupambana na kuenea kwa kasi kwa ukristu kwa kuwekeza kwenye elimu. Lakini pamoja na nia hiyo njema, EAMWS ilitiliwa shaka na waislamu weusi ( pamoja na Chief Fundikira kushika hatamu 1960) ambao walikiona kama taasisi inayolinda maslahi ya wahindi na waarabu. Mbaya zaidi ilikuwa ni wahindi hao walikuwa mashia na Ahmaddiya ambao waislamu wasunni wana shida nao. Ndio maana kuvunjika kwa EAMWS kulichangiwa sana na kitendo cha Karume kukilaani na kukitimua Zanzibar.

Kwa sababu hizi tutaona kuwa Nyerere wala ukristu wakati wake haukuwahofia waislamu bali waislamu wengi walihofia kuwa wasipokuwa makini wakristu wataishika nchi ambayo waliona kama ni yao. Ndio maana wanalalamika kutotambuliwa mchango wa waislamu katika kulikomboa taifa hili wakati wanasahau kuwa bila viongozi wa kikristu na wenye dini za asili huko mikoani kuunga juhudi za Nyerere huo ukombozi usingepatikana. Kinachonisikisha ni kuwa wakina Sykes, Mwapachu, Nyerere, Kambona, Bibi Titi na wengine wengi walipambana kama watanganyika na sio kama waumini wa dini zao au makabila yao. Inabidi tuwaenzi kwa hilo.

Amandla...
 
Fundi...
Nimepokea taarifa kuwa Mama Maria pamoja na mafuta ya taa alikuwa akiuza Coca-Cola:

Hapana sababu ya sisi kuvutana na historia ya Abdul Sykes kama unaikubali au la.

KWA HIYO UNAKIRI kwamba ulikosea, ulimpinga mwandishi wa awali na Mchundo, ambae ametumia picha zako mwenyewe na basic logic kuonyesha unachemka, na umesahihishwa huko pembeni na vyanzo vingine. Sasa usituambie hakuna haja ya kuvutana. Wewe ndio ulileta mvutano, ubishi na taarifa potofu.

Waombe msamaha wote wawili, fanya ustaarabu.

Hatuna sababu ya kuvutana maana yake nini, angekuacha utupotoshe????
 
Hilo la kuwa Mwalimu aliwaogopa waislamu halina ukweli. Mwalimu aliwashughulikia wote ambao aliamini kuwa wana nia mbaya na taifa lake bila kujali dini zao. Mmoja wa watu wa kwanza kukumbwa na sheria ya kutia watu kizuizini alikuwa mkristu mwenzake Kasanga Tumbo. Wote tunajua yaliyowapata wakina Kambona ambao wote walikuwa wakristu ukimuondoa Bibi Titi Mohammed. Tunajua alitaifisha shule zote ili kutoa nafasi sawa kwa raia wote kupata elimu ingawa katika hizo shule nyingi zilikuwa ni za wakristu. Ukweli ni kuwa asingetaifisha zile shule ingewachukuwa waislamu miaka mingi kuwafikia wakristu kielimu. Wakati Nyerere anakazia siasa zake za ujamaa na kujitegemea aliwaachia wakina Sykes waendelee na biashara zao za Commission Agent na Travel Agency. Mtu ilikuwa ukitaka kusafiri kwenda nje ilikuwa lazima ukanunue cheti cha chanjo katika ofisi ya Sykes Travel Agency iliyokuwa mtaa wa Mkwepu. Wakina Sykes walikuwa ni wafanyabiashara na baada yakupata uhuru waliachana na mambo ya siasa.

Mara nyingi mfano wa chuki za Mwalimu dhidi ya waislamu unaotolewa ni wa kuvunjika kwa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) kilichoanzishwa rasmi 1954 mjini Mombasa chini ya Agakhan. Ni ajabu kuwa chuki hizi hazikumzuia kuwapa kiwanja Chang'ombe na kuweka jiwe la msingi la Chuo Kikuu cha Kiislamu. Chuo Kikuu hicho hakikujengwa na mara ya mwisho nasikia kiwanja kilikabidhiwa kwa tajiri wa kiislamu (Chuo Kikuu cha Kiislamu kilichopo Morogoro kilitolewa kwa waislamu na Rais mkapa ambae alikuwa ni Mkatoliki). Nia kubwa ya EAMWS ilikuwa ni kupambana na kuenea kwa dhati kwa ukristu kwa kuwekeza kwenye elimu. Lakini pamoja na nia hiyo njema, EAMWS ilitiliwa shaka na waislamu weusi ( pamoja na Chief Fundikira kushika hatamu 1960) ambao walikiona kama taasisi inayolinda maslahi ya wahindi na waarabu. Mbaya zaidi ilikuwa ni wahindi hao walikuwa mashia na Ahmaddiya ambao waislamu wasunni wana shida nao. Ndio maana kuvunjika kwa EAMWS kulichangiwa sana na kitendo cha Karume kukilaani na kukitumua Zanzibar.

Kwa sababu hizi tutaona kuwa Nyerere wala ukristu wakati wake haukuwahofia waislamu bali waislamu wengi walihofia kuwa wasipokuwa makini wakristu wataisha nchi ambayo waliona kama ni yao. Ndio maana wanalalamika kutotambuliwa mchango wa waislamu katika kulikomboa taifa hili wakati wanasahau kuwa bila viongozi wa kikristu na wenye dini za asili huko mikoani kuunga juhudi za Nyerere huo ukombozi usingepatikana. Kinachonisikisha ni kuwa wakina Sykes, Mwapachu, Nyerere, Kambona, Bibi Titi na wengine wengi walipambana kama watanganyika na sio kama waumini wa dini zao au makabila yao. Inabidi tuwaenzi kwa hilo.

Amandla...
Fundi...
Ahsante nimekusoma.

Ukweli ni kuwa huna ujuzi wa kujadili jambo hili.

Katika hayo uliyoandika kuna makosa mengi.

Kwa kuwa sitaki kujadili suala hili nitabakia kimya na sababu ni kuwa historia ya EAMWS nimeiandika na sasa ni mashuhuri kwa Waislam wa leo.

Wanaijua.

Waislam tumevuka mtihani huo na hapa tulipo si busara kuijadili BAKWATA kwani hapana tija itakayopatikana.

Katika suala la EAMWS ni watu wawili tu ndiyo waliofanya utafiti wake na kuandika.

Wa kwanza ni Dr. Kataroge Mayanja Kiwanuka "Islam Politics in Bukoba," (1973) na wa pili ni Mohamed Said "Islam and Politics in Tanzania," (1989).

Paper zote hizi mbili zinapatikana Maktaba ya MSAUD Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Paper ya Mohamed Said ndiyo jibu la paper ya Dr. Kiwanuka.

Waislamu washatoa hukumu nani ameandika kweli.
 
Hivi unadhani kila kitu lazima kiandikwe? Unajua Nyerere aliolea kwa nani akiwa anafundisha Tabora? Huyo Sykes wako unamtukuza hadi unaboa
Sijasoma, lakini kwa jibu lako, naona hujamwelewa. Mzee wetu anachodai hakuna Uhuru bila ya watu wake....Jaza mwenyewe. Na Ukisoma vizuri anachodai ya kuwa kulikuwa hakuna duka mara lilikwepo mara lilisogezwa mtaa mara likarudi, utaona ni majina gani alitaka kuweka humo. Majina na Dini. Subiri na hapa nyimbo ya mduara ukiisha atakavyo rukia na Picha za vitabu.

Yaani kimduara duara. na Ukimsema unasema dini yake.

Usiboreke mjibu na hoja tu atakuelewa.
 
KWA HIYO UNAKIRI kwamba ulikosea, ulimpinga mwandishi wa awali na Mchundo, ambae ametumia picha zako mwenyewe na basic logic kuonyesha unachemka, na umesahihishwa huko pembeni na vyanzo vingine. Sasa usituambie hakuna haja ya kuvutana. Wewe ndio ulileta mvutano, ubishi na taarifa potofu.

Waombe msamaha wote wawili, fanya ustaarabu.

Hatuna sababu ya kuvutana maana yake nini, angekuacha utupotoshe????
Kwameh,
Kwangu si tabu kusema nilikosea.
Kukosea ni ubinadamu.

Lakini tambua kuwa biashara kuu ya Mama Maria ilikuwa mafuta ya taa toka wakati wa duka lake Mchikichi hadi nyumbani kwa Ali Msham, Mtaa wa Jaribu.

Hili la kuwa aliuza pia Coca-Cola limejulikana hizi siku mbili zilizopita.

Wachangiaji waliuliza mbona pana bango la Coca-Cola?

Mimi sikuwa na jibu ila kusema nililolijua.

Hata kitabu cha Nyerere (2020) kinaeleza duka la mafuta ya taa.

Uthibitisho kuwa Mama Maria aliuza na soda hamkuleta nyie umetoka kwangu kwa mimi kuandikiwa na akina Bahdoury nami nikauweka hapa ili sote tunufaike.
 
Back
Top Bottom