Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Na wewe vile vile unaniwekea maneno kinywani. Hakuna mahali nilipopinga historia ya Abdul Sykes au Sykes mwingine yeyote kupewa uzito. Ninachopinga ni wewe kufanya hao ndio nzima ya mapambano yetu ya uhuru. Hawakuwa peke yao kama vile Nyerere hakuwa peke yake.

Historia ipi hiyo ya Mama Maria inayosema marafiki zake walikuwa ni hao wakina mama wa kiislamu peke yake. Kwa akili za kawaida tu zingesema kuwa huyu mama ni lazima alikuwa na marafiki zake ambao walikuwa ni wakristo wenzake na sio waislamu peke yao.

Sikupingi kuwa Nyerere alikaa katika nyumba ya wakina Sykes. Lakini kwa vile haujasema alikaa kwa muda gani, kuna uwezekano kuwa baada ya hapo alihamia kwenye mojawapo ya nyumba za John Rupia.

Hilo la wakina Issa Shivji, Dr. Salim Ahmed na Hashim Mbita ni la kwako. Lakini kwa vile najua Mwalimu mwenyewe alikuwa na vitabu mpaka nyumba yake ilikuwa haitoshi nasita kuamini kuwa ulikuwa na kumbukumbu za historia yake kuliko yeye mwenyewe.

Kwa vile wewe binafsi haujawahi kusikia kuwa mama Maria alikuwa anauza soda pamoja na mafuta ya taa hakumfanyi aliyesema hivyo kuwa muongo. Picha uliyoweka inaonyesha kuwa kuna uwezekano kuwa ni kweli. Kwa vile haujaweka chanzo ya hayo madai, ni vigumu kujua kama mwandishi aliambiwa hivyo na mama Maria mwenyewe.

Amandla...
Ukweli kuwa Mama Maria Nyerere aliuza mafuta ya taa tu au na vitu vingine unaweza kupatikana kwa kumuuliza muhusika mwenyewe.

Huyu mama bado yupo hai, na anafikika kwa njia yoyote ambayo mtaona ni sawia kwenu na yeye.
 
Ukweli kuwa Mama Maria Nyerere aliuza mafuta ya taa tu au na vitu vingine unaweza kupatikana kwa kumuuliza muhusika mwenyewe.

Huyu mama bado yupo hai, na anafikika kwa njia yoyote ambayo mtaona ni sawia kwenu na yeye.
Algore,
Mama Maria ni mtu mzima sana.

Pana haja gani ya kumuhangaisha na jambo dogo kama hili la mafuta ya taa na Coca-Cola?
 
Mzee kanena haya kuhusu makala...
Nimeisoma na imenifurahisha na kunielimisha katika mengi ambayo sikuwa nayajua vyema.
ninavyo chukulia hapo ni kuwa kaelimika na kudai kuwa mengi alikuwa hayajui.

....halafu Mzee Wetu akaendelea na kuongeza, nitamnukuu hapa chini....
Makala hii inazungumza duka alilofungua Mama Maria Magomeni.
Akaongeza...
Mwandishi anaeleza duka hili kuwa duka lililokuwa linauza bidha kadhaa.

Hii si kweli Mama Maria alikuwa na duka dogo la kuuza mafuta ya taa
Mzee hapa anadai sio kweli Mama Maria alikuwa na duka dogo, hususani la kuuza mafuta ya Taa.
Amebaini hayo.... na kuendelea kudai anarakabisha..... kwa haya

Katika akina mama wa mwanzo kufahamiana na Mama Maria Nyerere alikuwa Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu kwa jina la Mama Daisy.

Duka la mafuta ya taa la Mama Maria alilifungua Mtaa wa Mchikichi na Livingstone wakati wanaishi nyumbani kwa Abdul Sykes.
Hapoooo sasa... sawa, lakini....
Duka la mafuta ya taa la Magomeni Mapipa Mama Maria alilifungua nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu.
Kikubwa alichotaka kusema, kurekebisha katika makala hio, kwa maoni yangu na nilivyomsoma ni haya...nitamnukuu kiunagaubaga.....
Juu ya hayo yote makala hii imeruka sehemu muhimu sana katika maisha yake na kwa kweli si yake tu bali na ya mumewe Mwalimu Nyerere na historia ya TANU na pia kuandika mengine ambayo si ya kweli.
na haya....
Katika akina mama wa mwanzo kufahamiana na Mama Maria Nyerere alikuwa Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu kwa jina la Mama Daisy.

Walifahamiana kwa kuwa Mama Daisy alikuwa mke wa Abdul Sykes na kama tujuavyo Mwalimu Nyerere baada ya kuacha kazi ya ualimu alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.
na mengine aliyotaka kusema au kwa lugha yake "anarekebisha"
Juu ya hayo yote makala hii imeruka sehemu muhimu sana katika maisha yake na kwa kweli si yake tu bali na ya mumewe Mwalimu Nyerere na historia ya TANU na pia kuandika mengine ambayo si ya kweli.

Akina mama ambao walikuwa jirani na duka hili walikuwa Bi. Chiku bint Said Kisusa ambae alikuwa anaishi mtaa huo wa Mchikichi kona na New Street (sasa Lumumba Avenue).

Ali Msham alikuwa amefungua tawi la TANU nyumbani kwake na Mwalimu alipohamia Maduka Sita Magomeni ikabidi Mama Maria awe anakwenda Kariakoo kila siku.
Kwa namna moja au nyingine "Historia kubwa ya Tanganyika/ Tanzania" imekosa majina mengi tu ya Waliowaleta mjini J.K. Nyerere R.I.P na Mke wake Mama yetu mpendwa Maria.
Kwamba bila hao kutajwa historia haiko sawa, hata aiandike nani; na nimesema hivyo kwa kudadavua anavyodai humu jamvini. Niko tayari kusahahishwa....lakini ndio maono yangu, ndio maoni yangu.
Mengine yote ni kurusha rusha vitambaa kwenye mduara(spinning) unapokolea. Anazunguka wee mpaka....

Nimuache....Heri ya Mwaka mpya.
Amani
 
Sijasoma, lakini kwa jibu lako, naona hujamwelewa. Mzee wetu anachodai hakuna Uhuru bila ya watu wake....Jaza mwenyewe. Na Ukisoma vizuri anachodai ya kuwa kulikuwa hakuna duka mara lilikwepo mara lilisogezwa mtaa mara likarudi, utaona ni majina gani alitaka kuweka humo. Majina na Dini. Subiri na hapa nyimbo ya mduara ukiisha atakavyo rukia na Picha za vitabu.

Yaani kimduara duara. na Ukimsema unasema dini yake.

Usiboreke mjibu na hoja tu atakuelewa.
Naanza kumuona mpuuzi na Sykes wake
 
Naanza kumuona mpuuzi na Sykes wake
Kolola,
Wala hapakuwa na haja ya kunitukana ndugu yangu.
Hapa tunaelimishana si uwanja wa kutukanana.

Lakini nitakuaga na kitu:
In June, TAA headquarters announced its executive committee with J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer and Ally K. Sykes as Assistant Treasurer.

Committee members were Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo and Patrick Aoko.[1]

The composition of the TAA leadership showed East African solidarity that existed during the struggle for independence.

Kenyan patriots were elected as office bearers side by side with Tanganyikans.

It is said that it was about that time, in the last months of 1953, that Abdulwahid talked to Nyerere seriously about forming an open political party to replace TAA.


[1] Tanganyika Standard, 19 th June 1953.

The Life and Times of Abdulwahid Sykes
(1924-1968)
The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika
Mohamed Said

1672720363994.jpeg

Na Dome Okochi Budohi TANU Card No, 6 Ruiru, Nairobi, 1972

1672720492760.jpeg

Na Ally Sykes TANU Card No. 2 Muthaiga Club, Nairobi 1989

Nimekuwekea picha hizi mbili za walimu wangu na wote wametangulia mbele ya haki hawa ndiyo walionifundisha historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Unamjua yeyote ambae amepata bahati kama hii yangu ya kufahaiana na watu walokuwa na Nyerere kuanzia mwanzo wa kutafuta uhuru wa Tanganyika?
 
Umezidi na udini na Huyo Sykes wako
Kalola,
Si mimi hata wewe ungebahatika kuwa katika nafasi yangu na ukaishi na watu hawa na ukajua historia ya uhuru kisha ukakuta historia ya uhuru imefutwa imepachikwa nyingine ungekaa kitako na kuandika historia ya kweli.

Vipi na hawa waliowatia Sykes katika kitabu hicho hapo chini ''Modern Tanzanians,'' (John Iliffe) wa (Cambridge) na katika Dictionary of African Biography (DAB) Prof. Emmanuel Akyeampong (Harvard) na wao unawatukana vilevile?

1672721333874.jpeg
1672721390790.png


Sasa tuwapongeze ndugu zetu waliofuta historia ya mashujaa hawa na kuandika historia isiyokuwa historia ya kweli katika vitabu hivyo hapo chini?

Kupachika historia ya kutunga ndiyo siyo udini?:

1672721572706.jpeg
1672721619383.jpeg
 
Fundi...
Ahsante nimekusoma.

Ukweli ni kuwa huna ujuzi wa kujadili jambo hili.

Katika hayo uliyoandika kuna makosa mengi.

Kwa kuwa sitaki kujadili suala hili nitabakia kimya na sababu ni kuwa historia ya EAMWS nimeiandika na sasa ni mashuhuri kwa Waislam wa leo.

Wanaijua.

Waislam tumevuka mtihani huo na hapa tulipo si busara kuijadili BAKWATA kwani hapana tija itakayopatikana.

Katika suala la EAMWS ni watu wawili tu ndiyo waliofanya utafiti wake na kuandika.

Wa kwanza ni Dr. Kataroge Mayanja Kiwanuka "Islam Politics in Bukoba," (1973) na wa pili ni Mohamed Said "Islam and Politics in Tanzania," (1989).

Paper zote hizi mbili zinapatikana Maktaba ya MSAUD Chuo Kikuu Cha Dar-es-Salaam.

Paper ya Mohamed Said ndiyo jibu la paper ya Dr. Kiwanuka.

Waislamu washatoa hukumu nani ameandika kweli.
Unarudia tena kosa lako lile lile la kujiona kuwa wewe ni Alpha Omega katika masuala ya kihistoria yanayohusu waislamu Tanganyika. Mtafiti mzuri hawezi kusema kuwa ni kitabu/article chake yeye na mwengine mmoja ndio pekee ndio viaminiwe pekee yake katika tukio la kihistoria ambalo limeandikwa na wengi. Kuna watu kama August Nimtz walioandika kwa undani kuhusu uislamu Tanganyika na kitabu chake kimekuwa cited zaidi ya mara 400 wakati article haijawa cited mahali popote. Citations ndio kipimo kuwa wasomi wenzako wanakuchukua serious.

Unarudia kosa lile lile ambalo unawatuhumu wakristu kufanya kwa kufanya historia ya TANU kuwa basically ya Nyerere. Sijui unamfahamu mwandishi aliyeitwa Brother Mohammed Saeed ambae aliandika article inaitwa " Islam and Politics in Tanzania "? Saeed alimtuhumu muislamu kutoka Bukoba aitwae Adam Nasibu kuwa chanzo cha mmonyoko katika EAMWS. Katika article hiyo Saeed anaizungumzia EAMWS kana kwamba ilianza shughuli zake chini ya uongozi wa Tewa Said Tewa na kukaa kimya kuhusu uanzishwaji wake rasmi ( kilianzishwa informally 1937 Kampala)chini ya Aga Khan 1954 na kuwa Said Fundikira alikuwa Rais wake wa kwanza Muafrika mweusi.

Badala ya kunituhumu tu kuwa nilichoandika Kilimanjaro makosa ingekuwa vyema kama ungeainisha makosa yenyewe.

Amandla...
 
Unarudia tena kosa lako lile lile la kujiona kuwa wewe ni Alpha Omega katika masuala ya kihistoria yanayohusu waislamu Tanganyika. Mtafiti mzuri hawezi kusema kuwa ni kitabu/article chake yeye na mwengine mmoja ndio pekee ndio viaminiwe pekee yake katika tukio la kihistoria ambalo limeandikwa na wengi. Kuna watu kama August Nimtz walioandika kwa undani kuhusu uislamu Tanganyika na kitabu chake kimekuwa cited zaidi ya mara 400 wakati article haijawa cited mahali popote. Citations ndio kipimo kuwa wasomi wenzako wanakuchukua serious.

Unarudia kosa lile lile ambalo unawatuhumu wakristu kufanya kwa kufanya historia ya TANU kuwa basically ya Nyerere. Sijui unamfahamu mwandishi aliyeitwa Brother Mohammed Saeed ambae aliandika article inaitwa " Islam and Politics in Tanzania "? Saeed alimtuhumu muislamu kutoka Bukoba aitwae Adam Nasibu kuwa chanzo cha mmonyoko katika EAMWS. Katika article hiyo Saeed anaizungumzia EAMWS kana kwamba ilianza shughuli zake chini ya uongozi wa Tewa Said Tewa na kukaa kimya kuhusu uanzishwaji wake rasmi ( kilianzishwa informally 1937 Kampala)chini ya Aga Khan 1954 na kuwa Said Fundikira alikuwa Rais wake wa kwanza Muafrika mweusi.

Badala ya kunituhumu tu kuwa nilichoandika Kilimanjaro makosa ingekuwa vyema kama ungeainisha makosa yenyewe.

Amandla...
Fundi...
Kuhusu hili la historia ya Waislam Tanganyika ukweli ni kuwa hakuna wa kunipita katika utafiti wake.

Mimi kuikataa elimu hii aliyonijaalia Allah ni kukanusha nema zake kwangu.
Mgogoro wa EAMWS umetafitiwa na mimi na Dr. Mayanja Kiwanuka.

Na Dr. Kiwanuka ananiheshimu unaweza kumtafuta na kumuuliza.

Kuhusu August Nimtz kitabu chake "Islam and Politics in East Africa," aliniletea ndugu yake anaitwa Jean Fairfax ambae alikuja Tanzania miaka ya mwishoni 1980s kufanya utafiti na nilimpeleka hadi Bagamoyo kwenye Zawiyya ya Sheikh Mohamed Ramiyya.

Jean alinitafuta kwa kuwa alikuwa keshanisoma na aliniomba nimkutanishe na Ally Sykes.

Hili nililifanya.
Jean aliniletea nakala ya kitabu hiki cha Nimtz (hard copy) lakini kimepotea.

Hivi sasa katika Maktaba nina nakala nyingine aliyoniletea Brendan Mc Sherry msomi mwingine wa Kimarekani aliyenifata Tanga kunihoji kuhusu historia ya Tanzania.

Brendon sasa ni Muislam na jina lake ni Ahmed na alisilimishwa na Sheikh Ali Basaleh.

Huyu Brother Mohamed Saeed ni mimi.
Nimekuwekea link ya paper hapo chini.

Narudia tena kukufahamisha kuwa huna maarifa ya kutosha kujadili na mimi chochote kuhusu historia ya EAMWS.

Mimi nina nyaraka za Tewa Said Tewa na Nyaraka za Bilal Rehani Waikela hawa walikuwa viongozi wa EAMWS serikali ilipovunja jumuia hii na kuunda BAKWATA.

Nyaraka hizi ndizo zilizonisaidia mimi kuandika historia nzima ya mgogoro wa EAMWS.

Wala usitegemee hapa kama nitaeleza historia ya mgogoro huu huko Waislam tumeshapita miaka mingi na tunaujua ukweli.

b6bb8378-1a32-4963-8ff8-637f150765a8-jean_fairfax.jpg

Jean Fairfax (1920 - 2019)

1672742527961.png

1672742550880.png

1672742656610.jpeg

 
Donne....
Kuna makala ya Mama Maria kufikisha miaka 93 leo imewekwa hapa leo asubuhi.

Nasahihisha makosa ndani ya makala hiyo.

Kwani vipi?
Nimefurahia hiyo nyongeza na masahihisho.
Uwe na mwaka wa baraka mzee Mohamedi
 
Fundi...
Kuhusu hili la historia ya Waislam Tanganyika ukweli ni kuwa hakuna wa kunipita katika utafiti wake.

Mimi kuikataa elimu hii aliyonijaalia Allah ni kukanusha nema zake kwangu.
Mgogoro wa EAMWS umetafitiwa na mimi na Dr. Mayanja Kiwanuka.

Na Dr. Kiwanuka ananiheshimu unaweza kumtafuta na kumuuliza.

Kuhusu August Nimtz kitabu chake "Islam and Politics in East Africa," aliniletea ndugu yake anaitwa Jean Fairfax ambae alikuja Tanzania miaka ya mwishoni 1980s kufanya utafiti na nilimpekeka hadi Bagamoyo kwenye Zawiyya ya Sheikh Mohamed Ramiyya.

Jean alinotafuta kwa kuwa alikuwa keshanisoma na aliniomba nimkutanishe na Ally Sykes.

Hili nililifanya.
Jean aliniletea nakala ya kitabu hiki cha Nimtz (hard copy) lakini kimepotea.

Hivi sasa katika Maktaba nina nakala nyingine aliyoniletea Brendan Mc Sherry msomi mwingine wa Kimarekani aliyenifata hadi Tanga kunihoji kuhusu historia ya Tanzania.

Brendon sasa ni Muislam na jina lake ni Ahmed na alisilimishwa na Sheikh Ali Basaleh.

Huyu Brother Mohamed Saeed ni mimi.

Narudia tena kukufahamisha kuwa huna maarifa ya kutosha kujadili na mimi chochote kuhusu historia ya EAMWS.

Mimi nina nyaraka za Tewa Said Tewa na Nyaraka za Bilal Rehani Waikela hawa walikuwa viongozi wa EAMWS serikali ilipovunja jumuia hii na kuunda BAKWATA.

Nyaraka hizi ndizo zilizonisaidia mimi kuandika historia nzima ya mgogoro wa EAMWS.

Wala usitegemee hapa kama nitaeleza historia ya mgogoro huu huko Waislam tumeshapita miaka mingi na tunaujua ukweli.

b6bb8378-1a32-4963-8ff8-637f150765a8-jean_fairfax.jpg

Jean Fairfax (1920 - 2019)

View attachment 2467761

View attachment 2467765
View attachment 2467766
Kujisifu na kusifiwa ni vitu viwili tofauti. Kuulizwa maswali na mtafiti ni jambo la kawaida. Wewe ukitembelewa na msomi basi unaamini mara moja kuwa ni kwa sababu wewe ni authority pekee katika field yako. Watafiti makini huwa wanakuwa na sources nyingi na sio kila source wanaitumia au kuikubali.
Mimi ungesema umetafiti sana kuhusu mgogoro wa tawi la EAMWS lililokuwa Tanzania ningekuelewa ingawa nisingekubaliana nawe.
Ytafiti wowote unaegemea upande mmoja ndio maana unakuwa kama si utafiti bali ni simulizi. Ndio maana una kawaida ya kucherry pick na ku insinuate mambo bila kutoa ushahidi kamili ili tu kujenga hoja yako ya kupigania dini yako. Mfano ni duka la Mama Nyerere. Mtafiti makini yeyote angehoji uwezekano mama Maria kutegemea uuzaji wa mafuta ya taa peke yake. Wewe badala ya kuangalia ile picha kama mtafiti uliiangalia Kama ushahidi wa simulizi za wazee wako. Huo sio utafiti.
Ukibanwa unasema ulisoma nyaraka zilizoandikwa na hao unaowaita ndugu zako. Hauwezi kuzungumzia historia ya EAMWS bila kuwazungumzia mabohora, makhoja na maahmaddiya hata kama haukubaliani na imani yao.

Amandla....
 
Alton Glenn Miller?
Mwanzilishi wa big band?
Kama ni huyo...ndio mzee Mohamed
Glenn...
Ahsante kaka.
Sina la kusema nimetosheka.

Umeona movie yake?
Kama bado naamini itakuwapo YouTube.
 
Glenn...
Ahsante kaka.
Sina la kusema nimetosheka.

Umeona movie yake?
Kama bado naamini itakuwapo YouTube.
Nafikiri umenipa hiyo changamoto mzee wangu, nitaifanyia kazi.
Asante sana na uwe na muda wa baraka za Mungu tele
 
Back
Top Bottom