Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Mkuu hata mimi nimejiuliza kuhusu hilo bango la Cocacola na mengine ambayo hayasomeki vizuri kwanini yawepo hapo wakati ni duka la mafuta taa tu? Nadhani huyu Mzee wetu akaongezee maelezo zaidi kuthibitisha hiki anachosema.
 
Kama umepata taarifa mpya kwamba alikuwa akiuza na Cocacola huoni kwamba uzi wako huu ni batili na unapaswa kufutwa?
 
Mkuu hata mimi nimejiuliza kuhusu hilo bango la Cocacola na mengine ambayo hayasomeki vizuri kwanini yawepo hapo wakati ni duka la mafuta taa tu? Nadhani huyu Mzee wetu akaongezee maelezo zaidi kuthibitisha hiki anachosema.
Mama...
Imethibitika kuwa pamoja na mafuta ya taa Mama Maria alikuwa akiuza CocaCola:

''SALESMAN ALIEKUA ANAMELETEA SODA ZA COCA-COLA NI MAREHEMU AMAL BI FADHIL''
 
Kama umepata taarifa mpya kwamba alikuwa akiuza na Cocacola huoni kwamba uzi wako huu ni batili na unapaswa kufutwa?
Mama...
Batili ni neno zito sana.

Ukisoma historia ya Mwalimu Nyerere na kusikiliza simulizi za wale aliokuwa nao wote watakueleza kuhusu duka la mafuta ya taa la Mtaa wa Mchikichi wakati Mwalimu anaishi na Abdul Sykes na mkewe Mama Daisy.

Halikadhalika katika kitabu cha maisha ya Mwalimu ''Nyerere Biography,'' kinaeleza duka la mafuta ya taa la Maduka Sita halitajwi la Mtaa wa Mchikichi wala lile nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu.

Nashangaa sana kuwa huu wa ubishi wa Mama Maria kuuza mafuta ya taa na Coke-Cola umepewa umuhimu mkubwa usiostahili.

Nashangaa vipi hatujadili kuhusu duka la Mama Maria alilofungua Mtaa wa Mchikichi na LIvingstone wala la Mtaa wa Jaribu.

Wala hatuulizi huyu Ali Msham aliyempa Mama Maria nafasi nyumbani kwake Magomeni kuweka duka lake la mafuta ya taa ni nani?

Haya kwao hayana umuhimu.

Wala hawataki kujua kwa nini duka la Mchikichi la Mama Maria ambalo ndilo duka lake la kwanza la mafuta ya taa halikutajwa wala hili la pili?

Kinachowahangaisha ni kuwa Mohamed kasema anauza mafuta ya taa lakini tunaona bango la Coca-Cola.

Katika vijana wa Ali Msham yuko mmoja yeye alipewa kazi ya kumsindikiza Mama Maria Maduka Sita kwa kuwa alikuwa anafunga duka lake maghrib na kiza kishaingia.

Siku zile kutoka hapo Mtaa wa Jaribu kwenda Maduka sita kulikuwa na nyumba chache na sehemu kubwa ni miembe na mikorosho kiza kitupu.

Huyu kijana aliyekuwa anamsindikiza Mama Maria nyumbani kila siku bado yu hai na sasa ni mtu mzima.

Mngependa kujua jina lake?


Abdul Sykes na mkewe Mama Daisy


Kulia wa kwanza ni Ali Msham na Julius Nyerere ni huyo aliyekaa kwenye meza hapo Mtaa wa Jaribu.
Hiyo meza na viti Ali Msham alitengeneza na kumbidhi Nyerere kwa matumizi ya ofisi yake New Street.
Sherehe ya kukabidhi ilifanyika kwenye tawi la TANU alilofungua nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu kulikokuwa pia na duka la Mama Maria

 
Mzee hayo mambo mengine uliyoyataja kwenye comment yako umeyaongezea wewe ila kwenye uzi ulioandika umewakosoa waandishi wengine kwamba kulikuwa hakuuzwi kitu kingine zaidi ya mafuta taa. Fundi mchundo alivyouliza kulingana na alichoona kwenye picha ndo baadae ukaja na taarifa kwamba umeambiwa pia kulikuwa na Cocacola. Hadi hapo huoni hata wewe mwenyewe umewakosoa waandishi wengine huku ukiwa na uhakika?
 
Mama . ..
Ni kweli usemayo na sababu ni kuwa umaarufu wa Mama Maria ulikuwa duka la mafuta ya taa.

Hayo ya Coke-Cola ndiyo tumeyajua sasa.
 
Ndugu Mohamed,
Katika andiko lako "ISLAM AND POLITICS IN TANZANIA" nimesoma kuwa baada ya sakata la EAMWS jaji Musa Kwikima alihamishwa toka Dar kupelekwa Mwanza kuwa hakimu mkazi.

Huku ni kushushwa cheo ambako hakujawahi kushuhudiwa. Ni kweli hili lilitokea?
 
Gagnija,
Sijui kwa nini kila unapokuja kwangu unakuja umeghadhibika.

Ghadhabu inapunguza uwezo wako kufikiri na kutafakari.

Hili swali zuri lakini umeliharibu kiasi naona aibu kukujibu kwani nitashusha heshima yako.

Ulitakiwa uniulize hivi: "Kwa nini unasema Mussa Kwikima kashushushwa cheo kwa kuwa Hakimu Mkazi?"

Badala yake unakuja na kibri na kejeli.
Mimi si mtu wa kughadhibika haraka lakini nafikiria kuacha mjadala na wewe.

Bora hivyo uko hapa umejificha sura yako na jina lako hujulikani.

Jibu lako.

Mussa Kwikima alichaguliwa kuwa Jaji na Rais Nyerere na baada ya kuvunjwa kwa EAMWS mwaka wa 1968 Kikwima akavuliwa cheo cha Ujaji.

Sababu ya kuondolewa katika nafasi hiyo ni kuwa alikuwa Katibu wa Kamati ya Waislam iliyokuwa inajaribu kutafuta sulhu katika mgogoro wa EAMWS.
 
Gagnija,
Sijui kwa nini kila unapokuja kwangu unakuja umeghadhibika.

unakuja na kibri na kejeli.
Mimi si mtu wa kughadhibika haraka lakini nafikiria kuacha mjadala na wewe.
Nimeuliza kwa nia njema kabisa ili nipate ufafanuzi, ambao nashukuru umeutoa, kwani awali sikuwa nimeisikia habari hii.

Kama nimekukwaza kwa namna yoyote naomba unisamehe. Sikusukumwa na kibri wala chuki kuuliza nilichouliza.

Nakuomba ukiondoe kitisho cha kusitisha kujadiliana nami; sioni kama zipo tofauti baina yetu za kuweza kutufikisha huko.
 
Nimejaribu kuwa na subira kama sijatoa hoja inayofanana na hii,,swali zuri mkuu.
Maelezo ya hilo bango yaakisi kuwa mama Nyerere alifanya biashara zaidi ya moja hapo.
 
Kuna mambo yanayotakiwa kupata ufafanuzi. Kwanza, ni je Jaji anaruhusiwa kuwa katika nafasi ya uongozi katika taasisi ya kidini? Je Jaji anaweza kuwa mchungaji? Najua Marehemu Augustino Ramadhani aliingia kwenye uongozi wa dini baada ya kustaafu. Sababu kubwa ni kuwa Jaji anatakiwa kuonekana "neutral" katika utoaji wa hukumu. Pili, je Rais alikuwa ana mamlaka ya kumuondoa mtu katika ujaji? Ninavyojua ni kuwa Jaji anaondolewa baada ya jopa la majaji wenzake kutoka Jumuia ya Madola kuridhia kuwa anastahili kufukuzwa. Rais mamlaka yake yanaishia kwenye kumsimamisha na sio kumfukuza. Lakini inawezekana kabisa kuwa yanayomkuta akaona kuwa amefanyiwa hivi kwa sababu ya dini yake.

Ni kama yule waziri wa Fedha aliyeondolewa na Mwinyi baada ya wafadhili wetu kulalamika kuhusu ubadhirifu uliokuwa ukiendelea Hazina lakini ikaonekana kuwa aliondolewa kwa sababu ya msimamo wake kuhusu dini yake. Hiyo ni pamoja na kuwa aliyemtoa alikuwa muislamu mwenzake, waziri aliyetoa taarifa ya uchunguzi alikuwa muislamu mwenzake lakini wako walioona kuwa Kighoma Malima aliondolewa kwa sababu ni muislamu.

Amandla...
 
Kuna mambo yanayotakiwa kupata ufafanuzi. Kwanza, ni je Jaji anaruhusiwa kuwa katika nafasi ya uongozi katika taasisi ya kidini? Je Jaji anaweza kuwa mchungaji?
Inaonekana kipindi hicho kulikuwa ni mikorogano mingi.

Tewa Said alikuwa waziri serikalini akiwa pia rais wa EAMWS. Akafanya ziara nchi za kiarabu kutafuta fedha kujenga chuo kikuu cha kiislamu.

Kilikuwa kipindi kigumu sana kwa serikali.
 
Mama . ..
Ni kweli usemayo na sababu ni kuwa umaarufu wa Mama Maria ulikuwa duka la mafuta ya taa.

Hayo ya Coke-Cola ndiyo tumeyajua sasa.
Kimsingi uliamua tu kukosoa uonekane wewe ndo unajua kuliko hao waandishi wengine kwa bahati nzuri ukafeli vibaya kusudio lako. Siku nyingine kosoa ukiwa na uhakika.
 
Inaonekana kipindi hicho kulikuwa ni mikorogano mingi.

Tewa Said alikuwa waziri serikalini akiwa pia rais wa EAMWS. Akafanya ziara nchi za kiarabu kutafuta fedha kujenga chuo kikuu cha kiislamu.

Kilikuwa kipindi kigumu sana kwa serikali.
Wakati Kighoma Malima alikuwa Waziri wa Elimu chini ya Rais Mwinyi baadhi ya viongozi wakristu waliondolewa katika nafasi zao. Inawezekana waliondolewa kutokana na mapungufu yao lakini wengi waliamini kuwa waliondolewa kwa sababu walikuwa wakristu. Hauwezi kuandika kuwa Kighoma Malima alikuwa mdini kwa kutegemea kitu ulichoambiwa na mmoja aliyeathirika bila kufanya utafiti kuthibitisha kuwa alikuwa na agenda hiyo. Ukifanya hivyo utakuwa unamuonea Kighoma Malima. Hivyo hivyo kuhusu Mwalimu na huyu Jaji.

Amandla...
 
Gagnija,
Yamepita tuendelee na mazungumzo yetu.
 
Fundi...
Kwangu mimi faraja yangu ni kuwa angalau kitabu cha Abdul Sykes kimefungua mjadala leo tunayazungumza haya hadharani.

Makala yangu ya kwanza iliyochapwa na Africa Events kueleza historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika gazeti lote toleo zima lilikusanywa na kutolewa kwenye mzunguko.

Makala ile iliwataja Abdul na Ally Sykes na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika historia ya kupambana na ukoloni.

Mwandishi akatukanwa na kutishwa asithubutu kutia mambo ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika TANU.

Aliyenitisha mwaka ule wa 1988 ni yule kiongozi wa jopo la Chuo Cha CCM Kivukoni waliokuwa mwaka wa 1981 wanaandika historia ya TANU aliyehakikisha kuwa historia ya Sykes haiandikwi kwenye kitabu cha TANU.

Iko siku In Shaa Allah nitamweleza Prof. Malima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…