Makundi saba ya chawa kindaki ndaki yanayotatiza mabadiliko

Makundi saba ya chawa kindaki ndaki yanayotatiza mabadiliko

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
1. Chawa bila kujali sekta ni janga lisilokuwa na tija.

2. Chawa huwa hawaoni wala kusikia dosari kuwahusu.

3. Kaulii hizi: "barabara ndefu haikosi kona" au "mwanamke mrembo hakosi kasoro," hazina maana yoyote kwao.

Makundi haya yanahusika:

a) Chawa wa mama: Hawa huwaambii kitu kumhusu bi mkubwa. Wao ni kusifu, kumshukuru na mapambio ya sifa kwa lolote.

b) Chawa wa Mwamba: Hawa nao huwaambii kitu kumhusu mwamba. Wao ni kusifu, kumshukuru na mapambio ya sifa kwa lolote. Mwamba hakosolewi. Kumkosoa mwamba, ni uhaini.

c) Chawa wa CCM: Hawa huwaambii kitu kuhusu CCM. Hakuna cha kukosoa. Yote ya CCM ni mema.

d) Chawa wa CHADEMA. Hawa huwaambii kitu kuhusu CHADEMA. Hiki chama hakikosolewi. Ukiwa na mawazo tofauti, ondoka.

e) Wafia Uislam: Hawa kwao dini ni uislam tu, tena ule wa kwao. Huwashangaa wengine wote na dini zao. Haiwaingii akilini iweje usiwe mwislam wa aina yao. Hawana uvumilivu na wengine. Mbingu na pepo wanayoijua ni ile yao tu, si ya wengine. Adui yao mkuu ni yeyote asiyekuwa mwislam na hasa mwisraeli.

f) Wafia Ukristo: Hawa wanaamini dini ni ukristo tu, tena ule wa kwao. Wanaamini Israeli ni taifa teule na kuwa tena si binadamu wa kawaida. Lolote afanyalo mwisraeli ni sawa tena dunia yote ilipaswa kuwasabiria. Hakuna ovu lolote dhidi ya Israel, na waarabu kwao, hawana haki yoyote.

g) Wajuaji: Hawa huamini kwenye lile tu wanaolijua wao. Wajuzi wa Kila kitu ni wao. Kwamba 'JF ina watu wa kada zote," haina maana yoyote kwao. Nafasi ya mafikara mapya hawana ila yale ya kwao tu. Kwamba "elimu ni bahari, elimu haina mwisho, tembea uone nk;" havina maana yoyote kwao.

4. Uchawa ni janga na chawa wenyewe ni wadudu wachafu.

IMG_20240402_054957.jpg


5. Chawa ni chawa tu, bila kuupiga vita uchawa hakuna mabadiliko.

Tuungane kuupiga vita uchawa.
 
Duh!, sasa hapo umeliacha kundi gani ambalo lipo JF?!

Kwa huo mtazamo wako, naona umetumaliza wote kwa kutuita machawa!.

Halafu hilo kundi la wajuaji naona linaingia kwenye hiyo quote ya Nyerere uliyoiweka hapo chini, hao ndio vijana Nyerere alitaka wawepo kwa mtazamo wangu, sio ndio mzee kila mahali..

Now, iweje wajuaji nao uwaite machawa?!
 
Duh!, sasa hapo umeliacha kundi gani ambalo lipo JF?!

Kwa huo mtazamo wako, naona umetumaliza wote kwa kutuita machawa!.

Halafu hilo kundi la wajuaji naona linaingia kwenye hiyo quote ya Nyerere uliyoiweka hapo chini, hao ndio vijana Nyerere alitaka wawepo kwa mtazamo wangu, sio ndio mzee kila mahali..

Now, iweje wajuaji nao uwaite machawa?!

1. Mbona nimeacha wengi tu wenye kuamini katika hoja?

2. Ila Kwa hakika wengi mko humu.

3. Tujitafakari, vinginevyo hatuwezi kutoboa.

4. Tofautisha wajuaji na wenye hoja. Wajuaji hudhani wanaojua ni wao tu. Huwa na mashaka hata na alichoandika mtu kama amekisoma au kukijua. Hudhani kiingereza wanajua wao tu. Si nadra kudhani wangeombwa kutafsiri.

5. Kimsingi ujuaji ni ugonjwa wenye kuhitaji tiba.
 
1. Mbona nimeacha wengi tu wenye kuamini katika hoja?

2. Ila Kwa hakika wengi mko humu.

3. Tujitafakari, vinginevyo hatuwezi kutoboa.
Nitajie makundi matatu ya JF ambao sio machawa uliyoyaacha kwa mtazamo wako..
 
Nitajie makundi matatu ya JF ambao sio machawa uliyoyaacha..

1. Kabla ya kukutajia nikuombe kurejea post yangu ya awali kwani sikuwa nimekujibu eneo la wajuaji. Hilo nimeliongeza.

2. Humu JF ni muhimu kujua wapo wengi waliomo kivyao vyao. Hata hivyo hii haiondoi uwezekano wa uwepo wa makundi yakiwamo ya kulipwa.

3. Hawano humo wasiofungamana na upande wowote. Wasioshikiwa akili. Wenye mawazo huru. Hilo ni kundi kamili lenye wajumbe wanaoweza kuhesabika.

4. Nimelazimika kuandika uzi huu kutokana na uzoefu na observation yangu ya kina ya muda mrefu.

5. Hata watoto mapacha hutofautiana. Iweje mtu hana maoni yake au tofauti kuhusu mtu, kitu, jambo nk na kwa siku zote?

6. Hapo #5 hiyo ndiyo tafsiri ya unafiki, kama siyo u chawa.

7. Ni wajibu wetu wote kuhimiza mawazo tofauti ya watu. Kusifia chochote hakupaswi kumfanya kufungamanishwa nacho. Kukosoa chochote hakuna maana ya kutofungamanishwa nacho.
 
1. Kabla ya kukutajia nikuombe kurejea post yangu ya awali kwani sikuwa nimekujibu eneo la wajuaji. Hilo nimeliongeza.

2. Humu JF ni muhimu kujua wapo wengi waliomo kivyao vyao. Hata hivyo hii haiondoi uwezekano wa uwepo wa makundi yakiwamo ya kulipwa.

3. Hawano humo wasiofungamana na upande wowote. Wasioshikiwa akili. Wenye mawazo huru. Hilo ni kundi kamili lenye wajumbe wanaweza kuhesabika.

4. Nimelazimika kuandika uzi huu kutokana na uzoefu na observation yangu ya kina ya muda mrefu.

5. Hata watoto mapacha hutofautiana. Iweje mtu hana maoni yake au tofauti kuhusu mtu, kitu, jambo nk na kwa siku zote?

6. Hapo #5 hiyo ndiyo tafsiri ya unafiki, kama siyo u chawa.

7. Ni wajibu wetu wote kuhimiza mawazo tofauti ya watu. Kusifia chochote hakupaswi kumfanya kufungamanishwa nacho. Kukosoa chochote hakuna maana ya kutofungamanishwa nacho.
Naona hapo juu umeona vile last time nilivyokujibu kisha nikaja ku edit baadae, ajabu ukaanza kunilaumu mpaka kufikia hatua ya kunishtaki kwa mods!.

Nikakwambia wacha usanii, hukunielewa, nikaamua kukaa kimya tu sababu nilijua hujui unachokitetea, hope leo umekiona nilichokuwa nikimaanisha siku ile.

Sasa simply tu kwa huo mfano hapo juu, hujioni hata nawe huwa unakosea humu ndani, so iweje ujipe uhalali wa kuwafanyia wengine observation? huo uhalali umeutoa wapi!

Naona nikwambie tu, hii observation yako ni fake, umejipa mamlaka ya kuingilia uhuru wa wengine kutoa mawazo yao kinyume cha sheria, ambao huo kwangu ni sawa na udikteta.

Hapo nimekupa jibu la jumla tu, ambapo hata ningeamua kukupa majibu specific kwa vitu ulivyoandika hapo juu, naona bado nina mengi ya kukuelewesha, tatizo muda.

Mfano, hapo kwenye #5 umezungumzia mtu kuwa na msimamo usioyumba kwa mtu mwingine au kitu, kwamba huu kwako ni mfano wa uchawa.

Sasa tukichukulia mfano wa Mbowe, ambae wengi ukiwemo wewe huwa mnataka aondoke madarakani/apishe wengine, akitokea mtu akamtetea Mbowe kwa mtazamo wako unamuita chawa!.

Kwanini nisiwe na msimamo usioyumba kumtetea Mbowe ikiwa yupo madarakani kihalali kwa kushinda uchaguzi kidemokrasia? ajabu kwa mtazamo wako na msimamo wangu huu unaniita chawa!.

Ndio maana nakwambia tena, hii observation yako ina mapungufu.
 
Naona hapo juu umeona vile last time nilivyokujibu kisha nikaja ku edit baadae, ajabu ukaanza kunilaumu mpaka kufikia hatua ya kunishtaki kwa mods!.

Nikakwambia wacha usanii, hukunielewa, nikaamua kukaa kimya tu sababu nilijua hujui unachokitetea, hope leo umekiona nilichokuwa nikimaanisha siku ile.

Sasa simply tu kwa huo mfano hapo juu, hujioni hata nawe huwa unakosea humu ndani, so iweje ujipe uhalali wa kuwafanyia wengine observation? huo uhalali umeutoa wapi!

Naona nikwambie tu, hii observation yako ni fake, umejipa mamlaka ya kuingilia uhuru wa wengine kutoa mawazo yao kinyume cha sheria, ambao huo kwangu ni sawa na udikteta.

Hapo nimekupa jibu la jumla tu, ambapo hata ningeamua kukupa majibu specific kwa vitu ulivyoandika hapo juu, naona bado nina mengi ya kukuelewesha, tatizo muda.

1. Jitofautishe nami kwa kukuitisha nilichoongeza kuhakikisha tunakwenda sawa.

2. Kwamba nimejipa uhalali? Mimi kama binadamu ninayo haki ya kufanya assessment yangu mwenyewe na hata kuyaweka wazi maoni yàngu yatokanayo na observation hiyo.

3. Zingatia hapo #2 ni haki yangu na hoja hupingwa kwa hoja.

4. Ninao ushahidi wa kila statement niliyotoa. Nilichoongelea ni uhalisia wenye lengo la kuwaasa ukiwamo wewe kuwa wewe (be yourself).

5. Uchawa hauna tija. Uchawa ndiyo uliotufikisha huku kwa Kuna @lucas_mwashambwa.

6. Hapo #5, chawa ni chawa tu!

7. Tuupige vita uchawa huu.
 
Back
Top Bottom