Makundi ya vijana wa Kitanzania ambao hujihisi wameyapatia maisha

Makundi ya vijana wa Kitanzania ambao hujihisi wameyapatia maisha

Huo muda wa kukaa na kuchambua mitindo ya maisha ya watu utumie kuongeza kipato mkuu.
 
- Vijana wa kitanzania ambao kwa wakati fulani waliwahi kuishi Marekani au Uingereza halafu kwa sasa wamerudi bongo kupambana na msoto wa maisha.
- Wanajeshi vijana miezi yao kwanza kwenye ajira jeshini halafu uwakute uraiani wamevaa zile gwanda zao.
Hao watu wanaona maisha wameyapatia sana na mwanajeshi anamuona mtu hasiye mwanajeshi ni boya na hakuna tusi kubwa kwa mwanajeshi umwambie yeye ni RAIA na pia JW wanawaita polisi ni RAIA WAKAKAVU.
 
Kuhusu Marekani siwezi kujizuia kujiona nimeyapatia maisha. Asikudanganye maelfu kwa maelfu ya watu duaniani wanatamani waje USA
sizungumzii wale ambao bado wanaendelea kuishi huko.

nazungumzia wale ambao walishawahi kuishi huko ila sasa wamerudi bongo mazima wakipambana na ugumu wa maisha ya huku. ile mentality ya maisha ya kimarekani huwa haiwatoki haraka.
 
.................Mkuu bora umeanzisha huu uzi hapa.

Juzi jumamosi nikiwa natoka home na mvua hizi maji yametuama hovyo naelekea stand za huku mitaani maeneo ya Mbezi Kimara bwana mdogo mmoja yupo na gari yake Mazda model siikumbuki ila ni hizi saloons za 9.7/10.5mill mimi napita pembeni mwa barabara huku nazungumza na simu sina hili wala lile mara pwaa!

Mimaji michafu suruali yote mpaka raba nilizokuwa nimevaa zimebadilika rangi zimekuwa tope na nilivaa cadet ya khaki simple nyeusi na nyeupe,wala hakujali na sababu barabara ina mashimo alikuwa anaenda speed ndogo sana but alishindwa hata kushusha kioo kuniambia samahani nachokumbuka aligeuka kidharau akanitazama kisha huyoo akenda zake huku seat ya kushoto amekaa mwanamke wake ameweka miguu kwenye dushboard wala hawakujali.

Sehemu yenyewe ni karibu na CCM wanakolaza magari sasa jamaa waliokuwa wamekaa pale picha waliiona wakaniambia bwana huyu jamaa gari yake huwa inalalaga hapa yeye kapanga kwenye nyumba ile palee!nikajisemea kimoyo moyo hakika Tanzania ukiwa na gari wewe ndo tajiri yaani amepanga chumba na sebule ananimwagia mimi maji machafu hata haonyeshi ubinaadam?any way niliacha likapita ila siyo vizuri tusidharauliane sana tunapohisi tuna mafanikio fulani wakati mwengine unaemdharau anaweza kuwa amekuacha mbali sana wanojua wakakucheka.
Daah pole sana mkuu umeandika kwa hisia hadi nimekuonea huruma. Binadamu tuko tofauti sana, vitu kama gari ni mambo madogo tu.

Kuna dereva mmoja wa bus moro dar alikuwa ana-force kulipita gari sehemu isiyo sahihi. Alilazimisha akalipita na kama haitoshi alivyolipita akafungua kioo na kuonyesha "middle finger" asijue aliekua ndani ya hiyo gari ndogo ni mtu mzito.

Check point iliyofuata akasimamishwa na askari. Aisee palichimbika, ni hivi hatupaswi kudharauliana kwa na namna yeyote, tuheshimiane na tupendane.

Pole mkuu.
 
Unaizungumzia JF ipi mkuu?

JF hii ambayo topic ya kula mademu kimasihara inapata page 50 kwa siku mbili tu?

Unazingumzia JF ipi ambayo hakuna mashoga na makahaba

Jf ipi ambayo ni tofauti na fb,instagram na twitter?

Sikiliza mzee labda tofauti huku hatutupii picha zetu

Ila ujinga wa social media ni ule ule
Hujamuelewa, kasema huku tumegawanywa kwa majukwaa. So ukitaka mambo ya ovyo unaingia jukwaa lake na ukitaka kitu kingine unaingia jukwaa lake
 
Back
Top Bottom