Malalamiko hayatoshi tusinunue vocha

Malalamiko hayatoshi tusinunue vocha

Huoni Kama humu mitandaoni Kuna wajinga wengi sana?
ujinga unaouaona huo ndio unaokupa nafasi ya wewe kujiona muerevu..

Maisha siku zote yapo hivyo.. Usiliangalie kwa upande mmoja tu wa wajinga angalia katika wigo mpana sio wote wanatumia mitandao kwa masuala ya kijinga.. Wajinga hao hao ndio wanaonveza pato kupitia kulipia vifurushi.. Mpango wa mh samia ni kuweka kodi rafiki ili kila mtu awe na uwezo wa kuchangia kodi unapoongeza gharama ya vifurushi katika nchi masikini kama hii inayotegemea TEHAMA wananchi wao waliowengi kujiajiri na kiendesha na kupata taarifa kuhusu maisha ya kila siku unadhani ni akili?

Naweza nikatama suala hili katika pande kadhaa

1.sekta ya mawasiliano imekua ni sekta ya uhakika katika kupata kodi.. Hivyo serikali imeonveza nguvu huko.. Lakini kwa namna ambayo sio rafiki utapunguza watumiaji na wanunuaji wa vifurushi kodi pia itapungua.. Ukiweka bei rafiki wengi watachangia

2. kama ni mambo ya kisiasa kuna ubaya upi kufanya yale yanayopaswa kufanyika ili yale yanayosemwa yasiwepo..



Unapokuwa unaandika usiandike kwa sababu umejiunga kifurushi hicho cha 2000/= sisi pia tuliopo ndani tunaumia
 
Ni rahisi kwa ambao mko extra busy ila kwa ambao tuna muda wa kuflex ni ngumu😁 im so fuxin addicted with the internet and it eat most of my idle time throughout the day
Najua mpo "mateja". Ndiyo maana nikasema "kwa wote ambao wataweza".
 
Tukubali kuendelea kuumizwa?
The best way ni kuikataa ccm, yani hao sijui madiwani na wabunge hatuwapi ushirikiano wowote ule, na ninyi ambao ni wanachama wa ccm rudisheni kandi zao.

Tubaki na Mama Samia ambae ndio Rais wetu ndio pekee tumpe ushirikiano.

Tukifanya hiyo kila kitu kitakwenda sawasawa na matakwa yetu sisi wananchi
 
The best way ni kuikataa ccm, yani hao sijui madiwani na wabunge hatuwapi ushirikiano wowote ule, na ninyi ambao ni wanachama wa ccm rudisheni kandi zao.

Tubaki na Mama Samia ambae ndio Rais wetu ndio pekee tumpe ushirikiano.

Tukifanya hiyo kila kitu kitakwenda sawasawa na matakwa yetu sisi wananchi
Hahah.

Mama Samia wa chama gani mkuu?

Kupenda boga penda na ua lake mkuu.

#awamu ya sita
 
Internet ya mwanafunzi wala sio gharama, kudownload PDF hakuna gharama.
Mama Samia shikilia hapo hapo
PDF haitoshi bali utahitaji YOUTUBE ambapo utaweza kupata ufafanuzi wa kutosha kutoka kwa experts waliobobea kwenye sehumu fulani kutoka sehemu mbalimbali duniani.
hivyo lazima utahitaji YOUTUBE ambayo inakunywa MBs za kutosha ili ifanye kazi na ili uelewe kitu kwa upana zaidi.

kitakachotokea ni watalimit uwezo wa mwanafunzi kupata knowledge vilivyo na kupunguza rate ya ufaulu tanzania hasa vyuoni.

hivyo hayo maamuzi yao hayatoathiri wajinga peke yao ambao hawana madhara yoyote kwenye jamii bali wataathiri vitu, watu na mambo yenye mchango mkubwa zaidi kwenye jamii.
 
HAKUNA njia mbadala, waongeze Bei tena na Tena. Ni lazima mwaka huu wajinga mpungue mitandaoni
Hukufunzwa vyema wewe kitu gani kinachofanya uite wengine wajinga kisa bando mkuu je hujui kwa ujinga wako mara ngapi internet imekutoa ujinga au imekufunza jambo au kuongea tu na mtu imekufunza na kuelimishwa hata msg tu imekuelimisha heshima nikitu cha bure
 
Tunaibiwa Sana mambo yako hivi 1 (GB) data ina cost USD 0.26 India,. Ukilinganisha na USD 6.66 UK.
 
Hawa MBURUKENGE ni mpaka tuingie barabarani ndio akili zitawarudi..

Wao wamekaa kwenye viti, anakula mshahara wa bab kubwa, bado miposho huko,vikao,safari, kula kulala, usafiri wa serikali, matibabu kitonga..
Jitu kama hili halioni tabu kuja kusema utumbo

Itabidi sasa tuchukue hatua tupate kuheshimiana tu[emoji35][emoji34]
 
PDF haitoshi bali utahitaji YOUTUBE ambapo utaweza kupata ufafanuzi wa kutosha kutoka kwa experts waliobobea kwenye sehumu fulani kutoka sehemu mbalimbali duniani.
hivyo lazima utahitaji YOUTUBE ambayo inakunywa MBs za kutosha ili ifanye kazi na ili uelewe kitu kwa upana zaidi.

kitakachotokea ni watalimit uwezo wa mwanafunzi kupata knowledge vilivyo na kupunguza rate ya ufaulu tanzania hasa vyuoni.

hivyo hayo maamuzi yao hayatoathiri wajinga peke yao ambao hawana madhara yoyote kwenye jamii bali wataathiri vitu, watu na mambo yenye mchango mkubwa zaidi kwenye jamii.
mkuu wala usitumie nguvu kubwa sana kufikiria maneno ya kuandika ili kumfanya kile unachotamani akijue akijue..
hawa ni wale ambao wameijua internet kama chanjo ya mabaya tu.. Akili yao ni ndogo sababu ubongo wake umeshindwa kujishughulisha kufikiri kimapana zaidi yeye anachojua Ni hizo softcopy.. PDF ebu fikiri mtu kama huyo utamuelimisha nini kwa kuanzia mbali huko?

Hajui hata hii nafasi anayopata kuandika hapa ni ukuaji wa tekinolojia watu kila siku hawalali kuifanya dunia kuwa kama kijiji yeye anataka turudi katika ulimwengo wa 1880 huko..

Kuna wakati kuna vingi vya kuandika lakini hakika nakuambia
Ni ngumu sana kueleweka kwa mtu ambaye anaamini
kama huyu jamaa
 
Ongezeko jipya la bei za vifurushi bila shaka ni matokeo ya mazungumzo baina ya waziri mwenye dhamana na wamiliki wa mitandao ya simu.
Tuonyeshe kupinga kwa vitendo tusinunue vocha tuziache simu zetu hewani bila vocha mpaka pale watakaposhusha gharama za vifurushi tunaumizwa kwa kweli. Wenye mitandao watakosa fedha na hiyo itapelekea hata serikali kukosa fedha ambazo wanapata kama kodi lazima watakaa chini kuangalia upya vifurushi vya simu lakini kama tutakua tunalalamika halafu tunaendelea kununua vifurushi vyao hawatahangaika na sisi.

Juzi juzi hapa Rais S. S Hassan amelekeza Wizara ya fedha/TRA kuachana na tabia ovu ya kubambukizia kodi kubwa wafanya biashara, kutaifisha fedha zao na wakati mwingine kufunga maduka ya wafanya biashara - TRA ilikwisha fikia hatua ya kujifanya ni Miungu watu - TRA ubunifu wa kukusanya kodi hawana kabisa, wamekimbiza wawekezaji - tukumbuke kwamba Tanzania sio Taifa pekee barani Afrika linalo vutia wawrkezaji/wafanya biashara tukiwazengua wataondoka na kwenda kuwekeza pengine.

Tukija kwenye suala la Wizara ya mawasiliano kushirikiana na makampuni ya simu kuwakomoa wateja kwenye sekta ya matumizi ya bundles, ni wazi this is a delibarate move ya kutaka kudumaza Watanzania wasitumie internet kwenye masuala ya kujiendeleza/elimisha kupitia online tutorials and the like, na kikubwa zaidi Wizara na makampuni ya simu yanataka ku-muzzle access za kutumia mawasiliano ya simu kupitia internet (Voice over IP) ambayo ni free mradi uwe na bundle unawasiliana na mtu yeyote Duniani kwa gharama ndogo kupitia kwenye bundle, hii kitu makampuni ya simu hawakitaki kabisa ndio maana wanaipiga vita whatsapp, skype etc - bahati mbaya Wizara ya mawasiliano inaelekea kuwaunga mkono makampuni ya simu na sio wananchi/walala hoi ndio maana wamekubaliana kuongeza gharama za ununuzi wa bundle karibu mara tatu ya bei za awali, vile Wizara haipendi sana raia kupata habari kutoka kwenye channels za utube - kumbuka waliwahi kuzifungia wakati wa uchaguzi kitu ambacho hakikuwahi kujitokeza wakati wa chaguzi za mwaka 2015, mama anapashwa kurekebisha mambo haya fasta kabla hayajaleta malalamiko zaidi kutoka kwa watumiaji wa mitandao else tunako elekea siyo hata kidogo.

Access za Internet ziwe affordable kwa kila mtu na sio Govt officials na ma CEO wanao lipiwa airtime na bundles na Serikali na mashirika ya UMMA.
 
Hatuwezi kuacha kununua vocha mkuu
Inawezekana kupunguza,mimi sio mpigaji sana wa simu,huma najiunga pale ninapokuta missed call au ujumbe muhimu tu,kwa hali ilivyo sasa nitapunguza zaidi matumizi,kuingia online mara tatu kwa wiki itanitosha kabisa..
 
Hii tuifanye kampeni ili tupate unafuu wanatuita wanyonge ili tunyongwe hawayajui maumivu yetu
Nakuunga mkono chochote utakachofanya nitasapoti...... Tupe muongozo
 
Napata jf Kwa freemode inatosha sikumbuki Mara ya mwisho kuweka vocha lini
share ujuzi ndugu maana huyu Hayati(Mungu ilaze roho yake mahali pema peponi) aliacha katukomoa
 
Hii meseji ya kuhamashisha mgomo wa kununua vocha umetumia kifurushi (vocha) au umetumia hewa kuituma humu ndani??!!
Kama una amini njia pekee ya kutuma meseji ni kifurushi (vocha) itabidi uongeze mwendo una achwa kwa kuwa dunia imefika mbali.
 
Kuuchuna haisaidii..ingekua tunajielewa muda huu tupo barabarani kudai haki yetu kutoka kwa serikali hii isiyojali wananchi zaidi ya kodi tu.
Wabongo ni macoward sana muda mwingine.....

Nasema sisi wanunua vocha tukiuchuna japo kwa siku 30 tu..... Utakuja kuona hiyo simu kama ndani ya wiki moja hawatakaa kurekebisha vifurushi na kurejesha vile tunataka....
 
Yaani nisiweke vocha kuchati na demu wangu pumbafu utanipa wewe
 
Back
Top Bottom