Malengo yako ya mwaka huu yametimia?

Malengo yako ya mwaka huu yametimia?

Well ni December, tunaumalizia mwaka! Kila mmoja kwa namna yake kuna malengo alijiwekea, yametimia? Kama ndiyo kwa asilimia ngapi? Na kama bado kwa nini? Wapi ulifeli?

Binafsi niseme malengo hayakutimia kwa 95%, kuna biashara ipo somewhere, vijana wanaharibu mwanzo mwisho. Kwa huu mwaka nimeshawabadilisha kama mara 3, nakosa usimamizi mzuri kutokana na majukumu yangu mengine.

kuna bajaji nilinunua (mkononi) bei poa 3.8m, ilikuwa kwenye mazingira mazuri nikampa kijana. Ni headache, kila siku visingizio mara service, kwa wiki hela naweza kupewa mara 4 au tatu, nikamnyang'anya nikampa ndugu yangu akomae.

Huyu ndiyo kirusi kabisa, hela haleti mara service, mara sijui kanunua nini na hivi sina uzoefu na spare na service, kwa ujumla ananipiga haswa! Nimepanga kuiuza na nishamwambia dalali, najua ndugu hawatanielewa lakini hakuna namna. Kuna ka-plot kako sehemu, nilipanga kujenga lakini nimeishia kuweka tofali tu.

Kuna mtu nilimuazima kiasi kadhaa aiendeleze biashara yake, mambo siyo mambo, niseme ana majanga kuliko mimi, tena hata kumdai nashindwa, naona akinikatia plot kama sehemu ya makubaliano endapo atakwama kunilipa.

Kuna majanga yalitokea kazini, dah, namshukuru Mungu mambo yakaenda powa, ingenigharimu sana.

Kwa kifupi huu mwaka haujawa mzuri kwangu kimalengo, kiuchumi naona niko pale pale nilipokuwa, malengo niliyojiwekea vitu vingi sijatimiza.

Vipi malengo yako yametimia? Kichumi na nyanja nyinginezo? Naamini kuteleza siyo kuanguka, bado tunayo nafasi ya kupambana na kusahihisha tulipokosea.
Hayajatimia, nilipanga kuingiza billion 3, 5 au 7 lakini mpaka tarehe 5 Desemba sijapata hata billion 1. Lakini sijakata tamaa kwa hizi wiki chache zilizobaki na Kama nikishindwa basi 2023 mapemaa kabla ya mwezi wa sita nipate billions zangu zisizopungua 5
 
Hayajatimia, nilipanga kuingiza billion 3, 5 au 7 lakini mpaka tarehe 5 Desemba sijapata hata billion 1. Lakini sijakata tamaa kwa hizi wiki chache zilizobaki na Kama nikishindwa basi 2023 mapemaa kabla ya mwezi wa sita nipate billions zangu zisizopungua 5
Utaiba au? Kama miezi 12 umepata 1b, 1month 5b utatoboaje
 
Bora unywee kwa mangi,,, zile mnakaa bar kampani kubwa,, unapiga round unatumia hela nyingi Sana ! Unaweza tumia 60k ukaishia kunywa bia 4 na mchemsho tu ,,,, kumbe ungekua alone ungepata huduma hio hio kwa gharama kidogo
Acha kabisa, kuna siku kuna mtu alikuwa ananidai 190,000 nikampigia simu mwenyewe kwamba tukutane sehemu fulani nimpe hela yake.
Nilivyofika akawa anatoa visingizio kwamba anamalizia kazi anakuja tu. Mwisho wa siku kuna kampani ikaibuka pale hadi akidi ikatimia, nikajikuta nimemaliza hela yote hadi nakuwa msanii wa kumpiga sound mdai wangu.
Nikajifunza bia zitanyweka kwa mangi tu.
 
Lengo langu mwaka huu 2022 nikimbie(jogging) 1,500km. Mpaka sasa nimekimbia 1,330s km kwa kweli sitoboi Nina wiki mbili tu
Cc Twilumba
View attachment 2436694
Shukrani Mkuu RRONDO kwa kuni tag, na hongera kwa hatua hiyo...si jambo dogo hata tu uamuzi wa kufikisha hizo kms!!

Mimi Bwana Malengo yangu ni kupiga 2400 Kms kwa Jogging lla hadi leo ndo nimefikisha 2100Kms sijui kama nitatoboa ingawa nikikaza natoboa sema huu mwezi nao una mambo mengi, ngoja nijitahidi niweke kando mambo ya Dunia nikomae na Jogging nimalizie hizo Km 300!
 

Attachments

  • Strava To date.png
    Strava To date.png
    82.5 KB · Views: 7
Umeeleza vizuri sana lakini nadhani mwisho ungeweza kujibu hoja kwa kueleza namna ulivyofikia malengo yako kulingana na targets zako za mwaka wako kama ulivyoeleza hapo. Otherwise naona umemjibu kwa kumshambulia huku ukitegemea na yeye afanye hivyo hivyo. Lenho lilikua zuri ila umefeli kufikisha ujumbe ulipoingoza personal attack na pia hujajibu alichouliza

Sent using Jamii Forums mobile app
Jamaa alileta ujuaji kwa personal attack, sikutaka kumjibu panic,,,, alitakiwa ajibu hoja ,,,mfano mwaka wake ulianza January, sa hv tuko dec pengine Bado kidogo mwaka wake uishe VP Yale aliyopanga yametimia ? Watu wako na stress anakuja kuattack tu ,,,,
 
Yangu yametimia maana nilipanga nitembee na wanawake 7.kila mwenzi soo far nimebuluza sana,mpaka sasa nimetembea na wanawake 78 bado 6 nimalize mwaka,thank u God 🙏🙏
 
Shukrani Mkuu RRONDO kwa kuni tag, na hongera kwa hatua hiyo...si jambo dogo hata tu uamuzi wa kufikisha hizo kms!!

Mimi Bwana Malengo yangu ni kupiga 2400 Kms kwa Jogging lla hadi leo ndo nimefikisha 2100Kms sijui kama nitatoboa ingawa nikikaza natoboa sema huu mwezi nao una mambo mengi, ngoja nijitahidi niweke kando mambo ya Dunia nikomae na Jogging nimalizie hizo Km 300!
Amazing
 
Umeeleza vizuri sana lakini nadhani mwisho ungeweza kujibu hoja kwa kueleza namna ulivyofikia malengo yako kulingana na targets zako za mwaka wako kama ulivyoeleza hapo. Otherwise naona umemjibu kwa kumshambulia huku ukitegemea na yeye afanye hivyo hivyo. Lenho lilikua zuri ila umefeli kufikisha ujumbe ulipoingoza personal attack na pia hujajibu alichouliza

Sent using Jamii Forums mobile app
Mie mwaka wangu mpya unaanzaga mwezi wa tano. Nashukuru kwa kunirudisha road
 
Yangu yametimia maana nilipanga nitembee na wanawake 7.kila mwenzi soo far nimebuluza sana,mpaka sasa nimetembea na wanawake 78 bado 6 nimalize mwaka,thank u God [emoji120][emoji120]
Piga hesabu gharama unazozutumia juu yao ! Malaz, chakula, vinywaji na cash ,,,,
 
Back
Top Bottom