Mambo matano aliyosema Rais Samia jana yaliyonisikitisha

Mambo matano aliyosema Rais Samia jana yaliyonisikitisha

..Samia amedai Dr.Kijaji ameshindwa majukumu yake ya Uwaziri wa biashara kwasababu ni mwanamke.

..pia amesema moja ya sifa iliyomfanya amteue Dr.Jafo Waziri wa biashara ni kuwa na " mdomo mwingi. "
haaaaaaaaa haaaaaaaaa haaaaa!
 
..pia Samia alisema amemteua Kamishna mpya wa Tra kwasababu anajua vichochoro vya wizi ktk Tra, na huenda hata yeye Kamishna mpya aliwahi kushiriki wizi alipokuwa mtumishi wa Tra huko nyuma.
Aiseeeh! Kwa hivyo Rais hajui vichochoro ila Kamishna ndio anajua vichochoro vyote.
 
..huyu Mama hapaswi kuzungumza chochote tofauti na alichoandikiwa na wasaidizi wake.

..mambo aliyoyaongea jana yanadhihirisha kwamba hana upeo na uelewa wa kuwa ktk nafasi ya Mkuu wa nchi.
Alijivua nguo Jana. Hasa kwenye mikopo ya IMF alionesha kwamba serikali haina plan.
 
Kama ulimsikiliza alisema jana kwamba kidata mpaka baadhi ya watumishi wa ikulu na viongozi wa serikali walikuwa hawampendi itafakari vizuri hyo kauli.
Kweli mkuu. Kuna jambo limejificha.
 
Job Ndugai aombwe TU samahani hadharani. Manake kila siku mnademka na kauli yake kwa style tofauti tofauti, lakini mantiki ni ile ile
Tatizo la ndugai alifanya ujinga mwingi kabla ya kauli yake. Hivyo anaonekana mnafiki tu.
 
Wakati Rais Samiah akiwaapisha Viongozi Jana , Kuna mambo matano aliyasema kwenye hotuba yake ambayo yalinisikitisha.

1. Jambo la kwanza Rais kadai mikopo inaifanya Tanzania inyayasike

Nimehuzunika Rais anapokiri ya kwamba mikopo tunayokopa inatufanya tunyanyasike. Huyu ni udhaifu mkubwa wa Rais wa Nchi kukiri hadharani ya kwamba anapoenda kukopa huko nje huwa ananyanyasika. Kwa maana nyingine Rais amekiri kwamba hii mikopo Ina masharti magumu kabla ya kukopa na hata baada ya kukopa yanayoifanya nchi inyanyasike Kama alivyosema Rais.

Pia kwenye muktadha huo, Rais kadai tunakopa nje na kunyanyasika kwa sababu watu hawalipi Kodi. Kwa maana nyingine Rais alikuwa anajua Kodi hazilipwi ila akawa anafidia kwa kukopa mikopo huko kwa wanyanyasaji, Sasa unyanyasaji umekidhiri kaamua kudai Kodi ilipwe.

Swali langu kwa Rais kwanini unakubali nchi inyanyasike kwa mikopo mnayokopa?. Na hayo manyanyaso ni yepi tuyajue, isije kuwa Kuna masharti magumu yanayoingilia uhuru wa Taifa wa kiuchumi, kisiasa, kisheria na hata kitamaduni. Tuweke wazi kwenye hili.

2. Jambo la pili Rais kadai Pale Kariakoo kuna siasa nyingi.
Rais amedai ya kwamba alituma wajumbe wake kwa Siri kule kariakoo na kugundua ya kwamba Kuna wafanyabiashara wengi walikuwa wanafungua maduka au kuingia kwenye mgomo bila ya kujua sababu ya mgomo.

Nimeshangaa kwa kauli hii ya Rais. Maana mwaka Jana wafanyabiashara wa Kariakoo walifanya mgomo na mwisho wanafanya kikao na Waziri Mkuu pamoja na Waziri wa Fedha, na walieleza sababu nyingi Sana za kwanini wanagoma Tena live kwenye vyombo vya habari.

Inakuwaje Tena hao hao wafanyabiashara ndani ya muda mfupi wadai hawajui kwanini wanagoma? Ok, tufanye hawajui wanachogomea, ni kwanini Serikali ilisitisha baadhi ya kanuni kwa muda? Kama vile matumizi ya EFD na Faini ya kutotumia receipt kwa wafanya biashara wa Kariakoo?. Ina maana Rais pamoja na kupata taarifa ya wafanyabiashara kutojua wanagomea nini bado aliendelea na kusimamisha kanuni?.

Naona Kama Rais amejichanganya au anatuchanganya kwenye hili eneo, au yeye ndio analeta siasa kwa kudai wanaogoma hapo kariakoo hawajui sababu kwanini wanagoma na bado serikali ikasimamisha kanuni hapo kariakoo.

Swali langu ni kwamba je wale wafanyabiashara hawakuwa na sababu za kugoma? Na ni kwanini Serikali imeukubali kutii baadhi ya malalamiko ya watu ambao inajua hawajui wanachogomea?.

3. Jambo la tatu, Rais kaingiza mambo ya jinsia kwenye kazi za Serikali
Wakati anamtambulisha Waziri mpya wa viwanda na biashara, Ndugu Suleiman Jaffo, Rais kadai amaemua kumteua Jaffo maana pale kariakoo Kuna mikikimikiki mingi ambayo Dr Ashatu Kijaji asingeiweza kwa sababu ni mwanamke. Nikajiuliza kwanini alimteua kwenye nafasi hiyo Kama alijua kwa mikiki iliyopo kwa Waziri mwanamke hataiweza?.

Rais akaendela kudai ya kwamba ameamua kumteua Dr Ashatu Kijaji kuwa Waziri wa Mazingira na Muungano, ili ashughurikie mambo ya nishati ya gesi ya kupikia. Akadai amemteua yeye pamoja na Naibu Katibu Mkuu mawanamke maalim kwaajili ya kushughulikia gesi ya kupikia. Na akadai kwasababu wao ni wanawake amewateua makusudi na wakishindwa atashangaa wanashindwaje na wao ni wanawake.

Swali langu la msingi ni je Kuna Wizara zinazowafaa wanawake tu? na Kuna Wizara zinazowafaa wanaume tu?. Na Kama zipo ni Wizara zipi hizo?. Na kwanini Rais anazijua na bado amateua jinsia tofauti kwenye Wizara husika?

4. Jambo la nne Rais kadai kuwa Wafanyakazi wa TRA walifanya sherehe Kidata alipohamishwa TRA
Rais kwenye hotuba yake kadai kwamba taarifa za kuhamishiwa zilipofika TRA, wafanyakazi wengi walifurahia Sana na kuamua kufanya sherehe. Kwa maana nyingine Kidata alikuwa very strict kwenye kazi yake lakini bado Rais akamuondoa.

Kwenye muktadha huo huo Rais kadai Kidata hakuoendwa na TRA na pia hakuoendwa na Ikulu maana alikuwa mchapa kazi Sana na amenyooka. Sasa ikamwa najiuliza Kama una Kamishna mkuu wa TRA anayejituma na kusimamia taratibu, inakuwaje unamtoa hapo?. Unadai atakuwa mshauri wako, kwanini awe mshauri wako ilhali alikuwa anasimamia taratibu na anajua kazi?.

Swali langu ni kwamba Kama Kidata alikuwa amenyooka mpaka kuchukiwa na Ikulu pamoja na wengine , inakuwaje Rais kamtoa? Rais anahitaji mtu wa aina gani mwingine?. Kama Kidata hakuwa Mtendaji mzuri kwanini Rais adanganye?.

5. Jambo la mwisho, Rais kamuomba Kamishna Mkuu wa TRA kutoshirikiana na TRA kuiba
Kwenye hili Rais kakosea Sana kuliweka alivyoliweka. Maana kauli yake ni kwamba anathibitisha ya kwamba TRA Kuna wezi. Sasa Kama kiongozi wa nchi unajua Kuna wezi ndani ya TRA kwanini huchukui hatua?. Na kwanini umewaacha wezi qanaendelea kuiba na Wala huwa kamati mpaka unamshauri Kamishna mpya wa TRA asishirikiane na wezi waliopo ndani ya TRA.

Swali langu ni kwamba hawa wezi ndani ya TRA ni akina nani?

By Econonist.
Tatizo kubwa la Tanzania ni matumizi ya hela au kodi wanazokusanya. Kuna watu wanakula ruzuku kubwa sana. Na hao watu wanajificha nyuma ya uraia wa Tanzania. Hawa wafanyabiashara wengi wakubwa wenye asili ya Asia wanachota sana ruzuku zetu. Mfanyabiashara au Mwekezaji mzawa hawezi kupewa hizo nafasi kwa sababu wazawa hawatoi gawio kubwa kwa walio kwenye Mamlaka. Wapo wanaomiliki mashamba ya. Mkonge, wanao-agiza mafuta na wanaosambaza mbolea ruzuku wanazokula hawa jamaa aisee. Ukizunguka mitaani na mitandaoni kutwa tunajadili Simba na Hanga. Bongo fleva na Bongo movie . Halafu unakuta mtu ana kiwanda huku amepanga apartment upanga. Ukienda Pakistani,India na U.A.E ana mahekalu utadhani anafanya biashara Marekani. Kusumbuana kote huku ni uhaba wa dola. Mikopo inabidi ulipe kwa Dola .Dola itakaaaje hapa nyumbani wakati Biashara kubwa zinazohitaji dola zinamilikiwa na watu wenye prime interest nje ya Tanzania. Unataka dola iwepo wakati uagizaji wa mafuta, bandari kavu, uagizaji wa mbolea n.k tenda umewapa watu wenye asili ya nje. Kumbuka hizi bishara hazizalishi dola bali zinahitaji dola toka ndani iende nje. Mimi sio mbaguzi ila jamani tujionee huruma kuna bilionea kahamisha familia U.A.E na huyu ndio ana tenda ya kusambaza mbolea nchi nzima na ni mwekezaji wa mkonge. Unadhani faida kubwa anayopata inabaki Tanzania au anaiwekeza nje ?
 
Alijivua nguo Jana. Hasa kwenye mikopo ya IMF alionesha kwamba serikali haina plan.

..hata suala la kusema Dr.Kijaji aliishindwa wizara ya biashara kwa sababu ya jinsia yake ni kauli ya kudhalilisha wanawake. Kumbuka kwamba Ashatu Kijaji ni Daktari wa falsafa, sasa mwanamke aliyeelimika mpaka ngazi hiyo bado ananyanyapaliwa kwa jinsia yake. Bado anaambiwa kuna kitu amepungukiwa ktk kutumikia serikali kwasababu ya jinsia.
 
Hizo tafsiri zako umejitungia kwa ujuha wako tu. Hapo Rais mama Samia Suluhu katumia falsafa ya "mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini" ambayo wewe huifaham.
Punguza matusi wewe mwanamke usiye na adabu. Kama huna la kusema Kaa kimya. Kuna ujuha zaidi ya kumuhamisha Waziri Wizara kisa ni mwanamke?
 
Wakati Rais Samiah akiwaapisha Viongozi Jana , Kuna mambo matano aliyasema kwenye hotuba yake ambayo yalinisikitisha.

1. Jambo la kwanza Rais kadai mikopo inaifanya Tanzania inyayasike

Nimehuzunika Rais anapokiri ya kwamba mikopo tunayokopa inatufanya tunyanyasike. Huyu ni udhaifu mkubwa wa Rais wa Nchi kukiri hadharani ya kwamba anapoenda kukopa huko nje huwa ananyanyasika. Kwa maana nyingine Rais amekiri kwamba hii mikopo Ina masharti magumu kabla ya kukopa na hata baada ya kukopa yanayoifanya nchi inyanyasike Kama alivyosema Rais.

Pia kwenye muktadha huo, Rais kadai tunakopa nje na kunyanyasika kwa sababu watu hawalipi Kodi. Kwa maana nyingine Rais alikuwa anajua Kodi hazilipwi ila akawa anafidia kwa kukopa mikopo huko kwa wanyanyasaji, Sasa unyanyasaji umekidhiri kaamua kudai Kodi ilipwe.

Swali langu kwa Rais kwanini unakubali nchi inyanyasike kwa mikopo mnayokopa?. Na hayo manyanyaso ni yepi tuyajue, isije kuwa Kuna masharti magumu yanayoingilia uhuru wa Taifa wa kiuchumi, kisiasa, kisheria na hata kitamaduni. Tuweke wazi kwenye hili.

2. Jambo la pili Rais kadai Pale Kariakoo kuna siasa nyingi.
Rais amedai ya kwamba alituma wajumbe wake kwa Siri kule kariakoo na kugundua ya kwamba Kuna wafanyabiashara wengi walikuwa wanafungua maduka au kuingia kwenye mgomo bila ya kujua sababu ya mgomo.

Nimeshangaa kwa kauli hii ya Rais. Maana mwaka Jana wafanyabiashara wa Kariakoo walifanya mgomo na mwisho wanafanya kikao na Waziri Mkuu pamoja na Waziri wa Fedha, na walieleza sababu nyingi Sana za kwanini wanagoma Tena live kwenye vyombo vya habari.

Inakuwaje Tena hao hao wafanyabiashara ndani ya muda mfupi wadai hawajui kwanini wanagoma? Ok, tufanye hawajui wanachogomea, ni kwanini Serikali ilisitisha baadhi ya kanuni kwa muda? Kama vile matumizi ya EFD na Faini ya kutotumia receipt kwa wafanya biashara wa Kariakoo?. Ina maana Rais pamoja na kupata taarifa ya wafanyabiashara kutojua wanagomea nini bado aliendelea na kusimamisha kanuni?.

Naona Kama Rais amejichanganya au anatuchanganya kwenye hili eneo, au yeye ndio analeta siasa kwa kudai wanaogoma hapo kariakoo hawajui sababu kwanini wanagoma na bado serikali ikasimamisha kanuni hapo kariakoo.

Swali langu ni kwamba je wale wafanyabiashara hawakuwa na sababu za kugoma? Na ni kwanini Serikali imeukubali kutii baadhi ya malalamiko ya watu ambao inajua hawajui wanachogomea?.

3. Jambo la tatu, Rais kaingiza mambo ya jinsia kwenye kazi za Serikali
Wakati anamtambulisha Waziri mpya wa viwanda na biashara, Ndugu Suleiman Jaffo, Rais kadai amaemua kumteua Jaffo maana pale kariakoo Kuna mikikimikiki mingi ambayo Dr Ashatu Kijaji asingeiweza kwa sababu ni mwanamke. Nikajiuliza kwanini alimteua kwenye nafasi hiyo Kama alijua kwa mikiki iliyopo kwa Waziri mwanamke hataiweza?.

Rais akaendela kudai ya kwamba ameamua kumteua Dr Ashatu Kijaji kuwa Waziri wa Mazingira na Muungano, ili ashughurikie mambo ya nishati ya gesi ya kupikia. Akadai amemteua yeye pamoja na Naibu Katibu Mkuu mawanamke maalim kwaajili ya kushughulikia gesi ya kupikia. Na akadai kwasababu wao ni wanawake amewateua makusudi na wakishindwa atashangaa wanashindwaje na wao ni wanawake.

Swali langu la msingi ni je Kuna Wizara zinazowafaa wanawake tu? na Kuna Wizara zinazowafaa wanaume tu?. Na Kama zipo ni Wizara zipi hizo?. Na kwanini Rais anazijua na bado amateua jinsia tofauti kwenye Wizara husika?

4. Jambo la nne Rais kadai kuwa Wafanyakazi wa TRA walifanya sherehe Kidata alipohamishwa TRA
Rais kwenye hotuba yake kadai kwamba taarifa za kuhamishiwa zilipofika TRA, wafanyakazi wengi walifurahia Sana na kuamua kufanya sherehe. Kwa maana nyingine Kidata alikuwa very strict kwenye kazi yake lakini bado Rais akamuondoa.

Kwenye muktadha huo huo Rais kadai Kidata hakuoendwa na TRA na pia hakuoendwa na Ikulu maana alikuwa mchapa kazi Sana na amenyooka. Sasa ikamwa najiuliza Kama una Kamishna mkuu wa TRA anayejituma na kusimamia taratibu, inakuwaje unamtoa hapo?. Unadai atakuwa mshauri wako, kwanini awe mshauri wako ilhali alikuwa anasimamia taratibu na anajua kazi?.

Swali langu ni kwamba Kama Kidata alikuwa amenyooka mpaka kuchukiwa na Ikulu pamoja na wengine , inakuwaje Rais kamtoa? Rais anahitaji mtu wa aina gani mwingine?. Kama Kidata hakuwa Mtendaji mzuri kwanini Rais adanganye?.

5. Jambo la mwisho, Rais kamuomba Kamishna Mkuu wa TRA kutoshirikiana na TRA kuiba
Kwenye hili Rais kakosea Sana kuliweka alivyoliweka. Maana kauli yake ni kwamba anathibitisha ya kwamba TRA Kuna wezi. Sasa Kama kiongozi wa nchi unajua Kuna wezi ndani ya TRA kwanini huchukui hatua?. Na kwanini umewaacha wezi qanaendelea kuiba na Wala huwa kamati mpaka unamshauri Kamishna mpya wa TRA asishirikiane na wezi waliopo ndani ya TRA.

Swali langu ni kwamba hawa wezi ndani ya TRA ni akina nani?

By Econonist.
Mikikimikiki ya Kariakoo imemuondoa mwanamke kwakua haiwezi na kumuweka mwanaume sasa niseme hivi hiyo ni midogo zaidi ya ile iliyopo hapa Nchini Tanzania.
Kwahiyo nishauri hivi kama Nchi tunahitaji mtu anaeweza kumudu mikikimikiki pia [emoji123]

Sent from my SM-G970U using JamiiForums mobile app
 
Ni kama vile mheshimiwa hajajua kuwa yeye ndio anahitajika kutoa majibu ya hoja anazoziibua mwenyewe.

Inaoneka kuna mambo mengi hoja zinaamuliwa kwa ushauri wa watu kadhaa na sio yeye peke yake which is good kushirikidha taasisi. Je hao wanaoshirikishwa hawana maslahi binafsi
Kweli mkuu. Kwa kauli yake ya Jana ni kama Hana maamuzi kwenye mambo mengi. Kwa mfano kwenye suala la Kariakoo alikaa kimya ila Jana ndio kaka kuongea huku maamuzi yaliyotolewa yako kinyume na kauli yake.
 
Back
Top Bottom