Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Mimi hii ilinikuta tena kama njia hii ya TAIDUME ilifikia natembea naongea mwenyewe hadi watu wananistukia..hiyo taasisi niliichukia sana lakini kuna mtu akaniambia njia pekee ni kukubali na kuamua kuachia kutochukia..kusema kweli nilijua ndio mwisho wa dunia kwa yale maumivu….maana sikutegemea!
Hii hakika asikie kwa mtu tuu huwa sitaki kabisa imkute mtu…..

Bahati mbaya tena kwangu ikaja kumkuta mdogo wangu tena yeye alishariport kituo cha kazi kwaajili ya kusaini mkataba …jumatatu inayofata anaambiwa kuwa wameshitisha mkataba watamjuza yani akarudi na mizigo yake toka mkoani ….hakika ule mwaka sitousahau …. Nilikuwa nashinda geto nalia tuu asikwambie mtu kama si Mungu sujui kwakweli…

Namshukuru sana Mama yangu kwakweli ndio wakati yeye alilia na mimi wakati wote na tukawa tunaongozana kwenye maombi na alikuwa na imani ambayo nisingekuwa kuwa nayo…alikuwa ananiambia kwa sababu kazuia hii ataleta nyingine…Mama alikuwa analia lakini nilikuwa sijawai kumuona..lakini siku moja nakwenda kumtembelea ndio namkuta anasali uku anaongea analia na Mungu wake ,wakati huo hajajua kama mimi nimefika nasikiliza ..hakika tuwaheshimu wazazi na tuwatunze jamani…. Mimi ilinibidi kutoka nje kwa uchungu nilijikuta natoka machozi kuona na mliza kiasi kile Mama yangu..
Lakini hakika Mungu ni mwema sana yalipita na tukasahau na kila mtu akapata kwingine!

Mungu ni mwema sana sana….hii situations kusema kweli ndio ilinifunza kusali, kutenga muda wa kanisani….yaani wee acha..Jamani tujifunze kuwa karibu na Mungu kila wakati tusijidanganye mambo hubadilika wakati wowote….hata serikalini kufukuzwa kupo pia….
Mungu awabariki wazazi
Hakika wanatuwazia mema.

Mama yangu huwa anaumia sana ninapopita magumu kibaruani.
Katika harakati za kutafuta ajira,Mama ni mtu ambaye anafuatilia sana ,yaani ni anauliza matokeo ya interview kuliko hata mimi mwenyewe niliyefanya interview Hahaha..Kila siku atauliza,vipi kule wamesemaje?hawajatoa tu majibu?
Na ikitokea matokeo yakatoka nikakosa,mama huwa anaumia sana.
Hadi imefika kipindi simfahamishi chochote kuhusu kuitwa interview maana maumivu anayoyapata mimi kukosa ajira ni Makubwa kuliko hata yangu mwenyewe...
Bado muda huo huo sapoti yake kifedha,kimaombi yaani katika kila kitu haijawahi kupungua.

Yaani hapa duniani hakuna watu Wana Upendo wa dhati kama wazazi.


.......
Katika kila jambo kuna kusudi la Mungu.
Mungu akiamua kukupitisha huko,pengine ili ujue ukuu wake,ujue msaada wake
Lakini zaidi sana ujue kuheshimu na kuthamini kazi utakayopata.


....
Mtu aliyepata kazi kimteremko bila changamoto,kwa namna moja au nyingine hawezi jua nini watu wanapitia,
Ataona ni normal tu....ila yule aliyestruggle ,ups&down yaani huyo anaelewa maisha vizuri kwa vitendo.
 
EPISODE 12: Wacha kudharau watu kwa muonekano wao, heshimu kila mtu maana huwezi jua

Hapa naomba nitilie mkazo kwamba kama ulikuwa na hiyo tabia please stop despising people based on their appearance at once and for all. Respect everyone because you never know. I emphasize the importance of treating everyone with respect and avoiding judgment based solely on outward appearances.

Point ya msingi hapa ni kwamba, one should not underestimate or look down upon others based on how they look, as appearances can be deceiving, and you may not fully understand someone's worth or capabilities without getting to know them. The call for respect underscores the idea that showing kindness and consideration to everyone, regardless of their appearance, is a more just and equitable approach. Unaweza kutumia google translator kupata maana kwa kugha ya kwenu hata Kingoni.

Iko hivi, maisha ya hapo ofsini kwa walemavu yaliendelea kama kawaida as time ilivosonga na mimi nikaendelea kupata uzoefu. Aisee nilikuwa deep sana kwenye issues za disability pamoja na mikakati mbali mbali ambayo ipo kisheria, kisera na kiprogramu ambayo ipo katika utekekelezwaji ili kutetea haki za watu wenye ulemavu. Niliongeza uzoefu mkubwa sana kwenye CV hususani mwasala ya disability inclusion into developmental programs. Nimeenda sana bungeni kufanya lobbying and advocacy sessions na kamati mbalimbali za kudumu za bunge na kuwapa madini wabunge mambo gani ya kwenda kuongea bungeni yakuwezesha watu wenye ulemavu. Hapa niwamegee siri moja, michango mingi ya wabunge wakati wa vikao vya bunge mara nyingi inakuwa ni madini wanayopewa na wadau mbali mbali husussani hizi NGOs kwenye sekta husika. Kama wiki hiyo yatajadiliwa matahalani maswala ya ukatili wa kijinsia basi NGOs zinazodili na maswala ya kijinsia wataandaa vikao na wabunge na kuwapa madini ya nini sheria, sera na mikakati ya kimataifa inataka ili kumlinda mtoto au mwanamke dhidi ya ukatili wa kijinsia. Hivyo hivyo kwenye mijadala ya maswala ya uchumi, usafirishaji, nishati nk. So hata sisi tulitumia fursa hiyo vizuri fursa, na waheshimiwa wabunge hawana baya mkikaa nao na kuwaelimisha vizuri basi wanaibeba ajenda yenu vizuri tuu, ila angalizo isiwe tuu hoja ambazo zinamwelekeo wa kukiaibisha chama watakukataeni mcha kweupe, hahahaa.

Kwakweli namshukuru Mungu niliiva sana kwenye maswala ya disability inclusion na mpaka leo nina uzoefu mkubwa sana whent it comes to disability inclusion and empowerment. Nimesema hapo juu kwamba tuwache kudharau watu kisa nafasi zetu au mwonekano wa mtu maana huwezi kujua huyo mtu au watu tunaowadharau watatufaa vipi. Najua hii sio hoja ngeni kwenu na mmeshaisikia mara nyingi sana. Hapa nitakupeni uzoefu wangu kwa mfano hai kabisa.

Pale kwa walemavu nilimkuta sisat duu mmoja hivi ameajiriwa kwenye nafasi ya maswala ya M&E. Alikuwa ni professional kweli kweli kwenye M&E. Sasa kwenye kuhangaika hangaika na ajira akajikuta ameajiriwa pale. Kiukweli yule dada sijui niseme alikuwa na nyodo au ni dharau au ni kujiskia sana, maana sijui hata mimuweke kundi gani. Ni dizaini ya vile visista duu vya kuvaaga mawani za macho si mnajuaga vijitabia vyao (sio wote jamani ila ni most of them). Any way tumuite tu sista duu.

Basi bhana, sista duu wetu yule kiukweli hakuwa mtu wa kuchangamana sana na watu alikuwa very selective, na mara kwa mara alikuwa anasema pale ofisini yeye hapakuwa sehemu yake target zake ni kufanya kazi na internationa NGOs yaani yeye alijiona ni wakimataifa zaidi. Haikuwa kitu kibaya kutamanai kufanya kazi na international organizations lakini alikuwa anabeza sana ile ofisi as if yeye hakuwa anafanya kazi. Kiukweli yule dada alikuwa mzuri sana kwenye maswala ya M&E nampa respect kwa hilo hata mimi alibrash vitu sana ambavyo niliviapply katika kazi zangu. Sista duu I still salute you kwa hilo, ulinifaa sanaaa.

Basi sista duu ilikuwa asione kazi kwenye international NGO anaomba na alikuwa ananyenyekea sana wageni kutoka kwenye international NGOs wanaokuja pale ofisini. Kule hakukuwa kujichanganya bali ilikuwa ni kujishobosha, any way kila mtu ana mbinu zake hata mimi nilishawahi kulamba viatu vya Dr KJ kama mnakumbuka ili mradi tuu kupata ninachotaka. Na hata hapa still bado nawalamba watu miguu wakivutiwa na CV yangu wanipe connection ahahahaa. Unashangaa nini unaambiwa hata viongozi wengi wa Kiafrika wanalamba viatu vya wakubwa wa magharibi ili waendelee kupata misaada na wengine kusalia madarakani – sembuse mimi na sista duu? Habari ndio hiyo.

Kama nilivosema pale ofsini kulikuwa na wageni wa aina tofauti tofauti sana wanaokuja. Kwa kuwa tunadili na watu wenye ulemavu basi ilikuwa ni kawaida watu wenye ulemavu kuja pale wengine kuomba misaada, wengine kutafuta kazi lakini pia wafadhili wengi sana au mashirika ya kimataifa walikuwa wanakija pale kuangalia namna ya kufanya kazi na sisi. Na hao wafadhili na mashirika ya kimataifa ndio ilikuwa target ya sista duu. Na vile alikuwa na kingereza kilichonyooka basi aliwaentertain vizuri sana ilia pate connection.

Sasa nakumbuka wakati Fulani wakati nina miaka kama mitatu pale ofsini ilikuwa ni kipindi cha mvua. Siku hiyo ofsini tulikuwa mimi na sista du utu ofsini kwa sababu kuna safari tulkikuwa tunaandaa ili tusafiri. Gafla akaingia ofsini jamaa mmoja kwa mwonekano tuu alikuwa yupo kama rafu rafu kimtindo, alikuwa amevaa pensi yake halafu amelowana chepechepe. Sasa ile anaingia pale reception hakuna mtu akaanza kuita sista duu akatoka. Sijui kaongea naye nini mara karudi akaniambia nitoke nikamsaidie kuna mtu anamletea ubishi hataki kuondoka.

Mimi nikatoka nikiwa na tahadhari zote nikijua labda ni kibaka na kweli kwa muonekano tuu yule jamaa uanaweza ukamuitia ukibaka kwanza alikuwa na dreads hizi fupi ila nilipozichunguza nikagundua zina matunzo hizi ni vile tuu zimelowa na mvua. Basi nikamsalimia pale jamaa akasema anataka kuongea na uongozi ila yule sista duu hampi ushirikiano wa kutosha. Nikamsikiliza pale jamaa akasema hana muda sana ni muhimu aongee na uongozi kama vipi tumpe namba za simu ya mkuu wetu pale.

Kiukweli jamaa ilikuwa ngumu sana kumwelewa, sista duu akawa analazimisha jamaa aondoke. Ila mimi kiubinadamu tuu nikamwambia sistaduu hebu mwache jamaa asubiri basi hata mvua ikate maana ilikuwa inanyesha balaa. Sista duu akasema kama utakaa naye hapo reception sawa maana hamwamini mwani kumuacha mwenyewe. Anaenda kuendelea na kazi zake ofsini kwake. Basi mimi nikaenda kuchukua laptop yangu nikawa nimekaa na yule jamaa pale reception huku na endelea na shughuli zangu na huku numdodosa mdogo mdogo. Nikampa na kikombe cha gahawa pale ili walau mwili upate joto.

Sasa yule jamaa alikuja na dereva wake ila alikuwa amemwacha mbali kidogo maana walipotea potea sana kwenye kuitafuta ile ofisi ilipo. Yule jamaa alivokuja pale simu na kila kitu chake alikuwa ameacha kwenye gari hivyo akaniomba amfate dereva wake ili kama anishirikishe kilichomleta pale. Basi akaenda baada ya muda mfupi nikaona m-prado unapaki pale nje jamaa akashuka na begi lake la laptop. Then akanaimbia kama mimi mwenyeji pale na nipo kitengo gani. Nikamwambia, basi akaniambia kwakuwa menejiment haipo basi atanishirikisha mimi kilichomleta na majibu yanatakiwa ndani ya wiki moja so mimi nilitakiwa niijulishe menejiment proposal yake. Nikamwambia basi ngoja nimuite na yule sista duu jamaa akagoma kabisa akasema kama siwezi kufanya naye mimi kikao basi wacha aende.

Nikamwambia basi tuendelee. Jamaa akawasha kompyuta yake na akaanza kunipitisha kwenye program ambayo wanataka kufanya na sisi pale ofisini ambayo itawanufaisha watu wenye ulemavu. Asee yule jamaa alikuwa na anawakilisha shirika moja la ulaya ambao walikuwa wanajishughulisha na maswala ya afya sasa yeye alikuwa amehamishiwa Kenya ambako ndio makao makuu ya East Africa ya hilo shirika. Na ni yeye ndio alieandika hiyo proposal ya kufanya kazi na watu wenye ulemavu Tz na ilikuwa ni proposal kubwa tuu yenye pesa mingi. Kwa kweli nivutiwa na ile proposal sasa pale ikawa ishu ni menejiment ya ofisi yetu wakiiridhia tupige kazi. Ndio mana alikuwa anafosi sana kuonana na menejiment.

Nikamwambia mimi na yule sistaduu ni sehemu pia ya menejiment ila hilo swala ni bodi ya wakurugenzi sio CEO peke yake. Ila nikamhahakikishia atapewa jibu ndani ya hiyo wiki moja. Basi akanishukuru pale tukabadilishana biz cards. Pia akaniachia na ile proposal ili niipitie vizuri ili nitakapoiwasilisha kwa wakubwa iwe rahisi. Aliniachia full proposal yenye mpaka bajeti, ilikuwa ni kubwa mno. Ile project ilikuwa ina nafasi nyingi tuu za kazi kwa wale watakaobase pale ofsini na watakaohitajika kule kwenye shirika lao. Nikaisoma pale then nikamshirikisha sista duu. Unaambiwa alipagawa sana baada ya kuiona ile proposal. Nikamuonyesha na biz card ya yule rasta alipagawa zaidi mana jamaa alikuwa ni partnership advisor wa hilo shirika so ni cheo kikubwa sana. Basi kwenye kuzicheki zile positions mimi nikaona moja ambayo inafaa kubase kule kwenye shirika nikasema hapa lazima nifanye jambo. Na sista duu nay eye aliiona ya mkuu wa kitengo cha M&E ipo akasema nay eye lazima afanye jambo. Sikutaka kumakatisha tama pale na pia sikutaka kumwambia jinsi yule rasta alivomkataa wakati tunafanya nae kikao kile.

Basi mimi nikampigia simu CEO na kumpatia ile taarifa akasema ataitisha kikao cha menejiment na bodi kesho yake. Kweli siku ya pili mimi nikapresent ile proposal utafikiri mimi ndio niliyeiandaa. Basi huku na huku nikapewa jukumu la kumjibu yule jamaa kwamba menejiment na bodi ya wakurugenzi imeridhia kufanya ule mradi in partnership na shirika lao. Basi siku hiyo hiyo nikamu-email rasta na akarespond promptly kwamba wataorganize a skype meeting baina yao na sisi. Baada ya kama siku tatu tukafanya skype meeting pale na deal was closed kwamba tuanze maandalizi ikiwemo kutafuta wafanyakazi.

Basi tukatoa matangazo pale. Binafsi nikamcheki rasta kwa wasapu kumwambia kuwa nina interest na ile position niliyoiona kwenye proposal ambayo ipo kule upande wao. Pale pale akanicall na akanifanyia interview kwa njia ya simu ambayo sikujiandaa kabisa. Akaniambia japo sijaona CV yako lakini nitakuinterview technical questions basi tukafanya interview tukamaliza. Ila akaniambia atanitumia email ya mwajiri wa ofisi yao wa Nairobi ili nitume CV na cover letter. Alivonitumia email address na mimi nikaandaa CV yangu na cover letter faster nikamtumia yule mwajiri. Akanijibu nijianda kesho nitafanyiwa interview kwa video call. Kweli kesho yake tukanya interview, walikuwa panelist wawili nakumbuka rasta hakushiriki. Pale pale wakaniambia nimepata Kazi so nisubiri offer letter. It was simple like that.

Basi wiki iliyofata kweli nikapokea offer letter na contact ambao nilitakiwa nisign na kuwarudishia immediately. Siku ya pili nikapokea simu kutoka kwenye ofisi yao ya hapa Dar ambapo ndio ingekuwa ofisi yangu mpya ya kufanyia kazi. Nikatakiwa nipeleke testimonials zangu kwa uthibitisho, basi nikafanya hivyo na nikawaomba wanipe mwezi mmoja ili niweze kumalizana na huku kwa walemavu. Ujue sio vizuri kuondoka mahali ukiwa na vimeo vimeo, clear kwanza vimeo vyako ndio uondoke na huo ndio uprefessional.

Baada ya wiki wakati tangazo la kazi limetoka sista duu akaniuliza taidume tunafanyaje sasa maana chansi ndio hii mimi nikamjibu mwenzio hapa nilipo naandika resignation letter naenda kujoin na shirika la rasta. Akashtuka sana akaniuliza mbona muda bado mpa briefing pale akashangaa sana. Akaniambai nayeye atamcheki. Ikabidi nimwambie tuu ukweli pale kwa situation yake itakuwa ngumu maana rasta hataki hata kumuona na hata mpa ushirikiano wa kutosha na anawza akamuharibia kabisa.

Nikamshauri kwa kuwa rasta hamjui kwa jina ni bora tuu akafanya procedures za kawaida anaweza akapata maana una CV nzuri. Akanijubu wewe niconnect basi, msaada wako utakuwa umeishia hapo kuhusu hayo mengine niachie mimi hakuna mkate mkate mgumu mbele ya chai. Nikasema poa. Pale pale nikamcall rasta na kumweleza interest za sista duu. Sasa rasta akataka kujua huyo sista ni nani nikamwambia subiri nampa namba yako atakupigia. Kweli nikampa sista duu akasema atampigia jioni akiwa off.

Basi tukaendelea na majukum na mimi nikasubmitt ile resignation letter kwa mkono kwa CEO. Kiufupi alisikitika sana lakini kwa kuwa alikuwa mwelew akaniruhusu kwa moyo mmoja. Usiku kwenye saa mbili hivi wakati nipo home napiga msosi mara nikaona rasta ananipigia. Nikajiuliza kuna nini tena? Kupokea pale akaniambia tuu kifupi ofisi yao haiwezi kufanya kazi na sista duu. Akaniamba wewe umepata ile kazi sio kwa sababu una vigezo vikubwa kuliko watu wengine bali additional value was the respect you showed when we first met. Basi akaniongea sana pale akasema wao katika ofisi yao wanasisitiza sana kuheshimu na kujitoa kwa ajili ya watu wengi. Akanianbia hata sista duu amemweleza maneno hayohayo na kumwambia wazi kwamba hawawezi kufanya nae kazi. Basi tukagana pale na mimi nikamcall sista duu kumuuliza imekuwaje maana jamaa kanipigia. Alichoniambia tu niachane na mambo hayo ahikuwa rizki yake na rizki anatoa Mungu. Kwa yale majivuno yake sikutaka kumshauri chochote.

Ndio ikawa hivyo hivyo ndugu zanguni. See you next episode.
Visistaa duu vya hivi huwa ata kuolewa inakuwa shida .. natamani ata ungetupia picha yake, ila acha tu
 
Mungu awabariki wazazi
Hakika wanatuwazia mema.

Mama yangu huwa anaumia sana ninapopita magumu kibaruani.
Katika harakati za kutafuta ajira,Mama ni mtu ambaye anafuatilia sana ,yaani ni anauliza matokeo ya interview kuliko hata mimi mwenyewe niliyefanya interview Hahaha..Kila siku atauliza,vipi kule wamesemaje?hawajatoa tu majibu?
Na ikitokea matokeo yakatoka nikakosa,mama huwa anaumia sana.
Hadi imefika kipindi simfahamishi chochote kuhusu kuitwa interview maana maumivu anayoyapata mimi kukosa ajira ni Makubwa kuliko hata yangu mwenyewe...
Bado muda huo huo sapoti yake kifedha,kimaombi yaani katika kila kitu haijawahi kupungua.

Yaani hapa duniani hakuna watu Wana Upendo wa dhati kama wazazi.


.......
Katika kila jambo kuna kusudi la Mungu.
Mungu akiamua kukupitisha huko,pengine ili ujue ukuu wake,ujue msaada wake
Lakini zaidi sana ujue kuheshimu na kuthamini kazi utakayopata.


....
Mtu aliyepata kazi kimteremko bila changamoto,kwa namna moja au nyingine hawezi jua nini watu wanapitia,
Ataona ni normal tu....ila yule aliyestruggle ,ups&down yaani huyo anaelewa maisha vizuri kwa vitendo.
Hakika Mkuu! Wazazi hasa Mama wanaumizwa sana sana mimi ilifika kipindi nikawa simwambii Mama kama nimefanya interview maana alikuwa anateseka sana nikawa namwambia tuu niombee!
Alikuwa akisikia kwenye habari kuwa serikali itaajiri au kuna kazi sehemu lazima atanipigia kuniambia yani alikuwa anateseka kama vile ndiyo yeye hadi mimi nikawa naumia!
Hata baada ya kusitishwa gafla kile kibarua kwenye ile taasisi yani Mama alihangaika sana mara naambiwa amekwenda wizarani ,mara amekwenda kutafuta namba ya mtu fulani serikalini ili mradi tuu anajua atapata msaada ,alihangaika sana na alitafuta kila mtu ambaye alijua atasaidia lakini aligonga mwamba akaambiwa ni maelekezo toka juu kwa hiyo hizo ajira zimesitishwa!

Kuna siku alikuja akaniambia kuwa amejihakikishia kuwa hizi ajira hazipo tena akasema tujipange upya ilikuwa kwenye simu lakini nilikuwa nasikia uchungu alionao ….
 
Hakika Mkuu! Wazazi hasa Mama wanaumizwa sana sana mimi ilifika kipindi nikawa simwambii Mama kama nimefanya interview maana alikuwa anateseka sana nikawa namwambia tuu niombee!
Alikuwa akisikia kwenye habari kuwa serikali itaajiri au kuna kazi sehemu lazima atanipigia kuniambia yani alikuwa anateseka kama vile ndiyo yeye hadi mimi nikawa naumia!
Hata baada ya kusitishwa gafla kile kibarua kwenye ile taasisi yani Mama alihangaika sana mara naambiwa amekwenda wizarani ,mara amekwenda kutafuta namba ya mtu fulani serikalini ili mradi tuu anajua atapata msaada ,alihangaika sana na alitafuta kila mtu ambaye alijua atasaidia lakini aligonga mwamba akaambiwa ni maelekezo toka juu kwa hiyo hizo ajira zimesitishwa!

Kuna siku alikuja akaniambia kuwa amejihakikishia kuwa hizi ajira hazipo tena akasema tujipange upya ilikuwa kwenye simu lakini nilikuwa nasikia uchungu alionao ….
Wamama Wana huruma sana
Yaani kwa hayo maelezo uliyotoa namuona Mama yangu kabisa🙌

Hicho uulichoelezea ndicho kipindi anachokipitia mama yangu.
Siku hizi huwa simwambii chochote kuhusu kazi maana ni kumtesa.

Yaani Upendo wa mama ni mkubwa sana...huwa namuomba sana Mungu ampe maisha marefu mama yangu,hadi aone mafanikio yangu na kuyafaidi...achilia mbali hivi vibarua vya wahindi vya kausha damu ambazo hakuna chochote tunapata.
 
Wamama Wana huruma sana
Yaani kwa hayo maelezo uliyotoa namuona Mama yangu kabisa🙌

Hicho uulichoelezea ndicho kipindi anachokipitia mama yangu.
Siku hizi huwa simwambii chochote kuhusu kazi maana ni kumtesa.

Yaani Upendo wa mama ni mkubwa sana...huwa namuomba sana Mungu ampe maisha marefu mama yangu,hadi aone mafanikio yangu na kuyafaidi...achilia mbali hivi vibarua vya wahindi vya kausha damu ambazo hakuna chochote tunapata.
Yaani misoto inafunza sana yani Mama yako anafikia hatua anakupiga tafu ya kodi hakuna anayejua …watu wanakuona unatoka kwako Geto kumbe kibarua hakikufanyi ulipe kodi zaidi ya kula ..kumbe mlipa kodi ni mama yako na anakufichia siri hakuna ndugu anajua yaani!

Mkuu Nakuhakikishia ni swala la muda tuu! Mungu ni mwema sana hatomuacha Mama alie na kuumia milele….mara nyingi tukiwa katika hali hii tunakuwa hatuoni kama kuna pakutokea na hata mimi sikuwai ona kama kunapakutoke lakini nina hakika hata wewe utatoka tuu! Huyu Mungu ni wetu sote !
 
Yaani misoto inafunza sana yani Mama yako anafikia hatua anakupiga tafu ya kodi hakuna anayejua …watu wanakuona unatoka kwako Geto kumbe kibarua hakikufanyi ulipe kodi zaidi ya kula ..kumbe mlipa kodi ni mama yako na anakufichia siri hakuna ndugu anajua yaani!

Mkuu Nakuhakikishia ni swala la muda tuu! Mungu ni mwema sana hatomuacha Mama alie na kuumia milele….mara nyingi tukiwa katika hali hii tunakuwa hatuoni kama kuna pakutokea na hata mimi sikuwai ona kama kunapakutoke lakini nina hakika hata wewe utatoka tuu! Huyu Mungu ni wetu sote !
Wamama wanakuwa frustrated sana hasa watoto wa kiume mkikwama..
Hapo usiombe ndo uwe first born[emoji119]

Heri hata sisi wa kike tunakaa nyumbani


Amin Mkuu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu ambaye ajapitia maisha magumu hawezi kuelewa lyfe ndo kama wanafunzi wa chuo wanajali sana mavai na simu Kali sababu pesa ya boom wanakua hawajaitolea jasho wanasahau kwamba Kuna maisha baada ya chuo.shukrani za dhati ni kwa wazazi wetu wetu ambao hawapendi kuona tunapitia changamoto#

Sent from my Pixel 4a (5G) using JamiiForums mobile app
 
Mimi hii ilinikuta tena kama njia hii ya TAIDUME ilifikia natembea naongea mwenyewe hadi watu wananistukia..hiyo taasisi niliichukia sana lakini kuna mtu akaniambia njia pekee ni kukubali na kuamua kuachia kutochukia..kusema kweli nilijua ndio mwisho wa dunia kwa yale maumivu….maana sikutegemea!
Hii hakika asikie kwa mtu tuu huwa sitaki kabisa imkute mtu…..

Bahati mbaya tena kwangu ikaja kumkuta mdogo wangu tena yeye alishariport kituo cha kazi kwaajili ya kusaini mkataba …jumatatu inayofata anaambiwa kuwa wameshitisha mkataba watamjuza yani akarudi na mizigo yake toka mkoani ….hakika ule mwaka sitousahau …. Nilikuwa nashinda geto nalia tuu asikwambie mtu kama si Mungu sujui kwakweli…

Namshukuru sana Mama yangu kwakweli ndio wakati yeye alilia na mimi wakati wote na tukawa tunaongozana kwenye maombi na alikuwa na imani ambayo nisingekuwa kuwa nayo…alikuwa ananiambia kwa sababu kazuia hii ataleta nyingine…Mama alikuwa analia lakini nilikuwa sijawai kumuona..lakini siku moja nakwenda kumtembelea ndio namkuta anasali uku anaongea analia na Mungu wake ,wakati huo hajajua kama mimi nimefika nasikiliza ..hakika tuwaheshimu wazazi na tuwatunze jamani…. Mimi ilinibidi kutoka nje kwa uchungu nilijikuta natoka machozi kuona na mliza kiasi kile Mama yangu..
Lakini hakika Mungu ni mwema sana yalipita na tukasahau na kila mtu akapata kwingine!

Mungu ni mwema sana sana….hii situations kusema kweli ndio ilinifunza kusali, kutenga muda wa kanisani….yaani wee acha..Jamani tujifunze kuwa karibu na Mungu kila wakati tusijidanganye mambo hubadilika wakati wowote….hata serikalini kufukuzwa kupo pia….
Wachache wataelewa hii kitu!! Lakini Mungu still mwaminifu.....
 
Mungu awabariki wazazi
Hakika wanatuwazia mema.

Mama yangu huwa anaumia sana ninapopita magumu kibaruani.
Katika harakati za kutafuta ajira,Mama ni mtu ambaye anafuatilia sana ,yaani ni anauliza matokeo ya interview kuliko hata mimi mwenyewe niliyefanya interview Hahaha..Kila siku atauliza,vipi kule wamesemaje?hawajatoa tu majibu?
Na ikitokea matokeo yakatoka nikakosa,mama huwa anaumia sana.
Hadi imefika kipindi simfahamishi chochote kuhusu kuitwa interview maana maumivu anayoyapata mimi kukosa ajira ni Makubwa kuliko hata yangu mwenyewe...
Bado muda huo huo sapoti yake kifedha,kimaombi yaani katika kila kitu haijawahi kupungua.

Yaani hapa duniani hakuna watu Wana Upendo wa dhati kama wazazi.


.......
Katika kila jambo kuna kusudi la Mungu.
Mungu akiamua kukupitisha huko,pengine ili ujue ukuu wake,ujue msaada wake
Lakini zaidi sana ujue kuheshimu na kuthamini kazi utakayopata.


....
Mtu aliyepata kazi kimteremko bila changamoto,kwa namna moja au nyingine hawezi jua nini watu wanapitia,
Ataona ni normal tu....ila yule aliyestruggle ,ups&down yaani huyo anaelewa maisha vizuri kwa vitendo.
Pole sana! Sa zingine sijui ni better kufanya interview bila kuwapata taarifa maana wanaumia sana ukiwaambia hujapita interview!
 
Ni kweli hakuna ambapo niliondoka kwa ubaya kama ambavyo utaendelea kuona katika segments za mbele ila mambo sio rahisi kama unavofikiria. Mashirika niliyofanya mimi sio rahisi kurudi ukiwa hauna mchongo maana nafasi zinakuwa tayari zina watui Ila unaweza kurudi endapo kazi zitatangazwa upya, hayo mambo ya parttime ni nadra sana ktokea.
Ila mara nyingi nimekuwa nawaibukia kama nina shughuli zangu labda zinazohitaji proper office environment, strong internet, printing na vitu vingine vidogo vidogo. Mzee ishu ya ajira ni changamoto sana imagine mimi nina uzoefu usiopungua miaka saba napata changamoto vipi kwa fresh graduate?

Bravoo
 
EPISODE 13: Never outshine or outsmart your boss. Sikuwa makini na ilinicost

Natumaini wengi mmeshawahi kuusikia huu msemo. Ofcourse kama wewe ni bookworm utakuwa umeshakutana mara nyingi tuu hii phrase ya try never to outshine your boss in working invironment, hata bwana Robert Greene katika buku lake la The 48 Laws of Power ameongelea kwa kirefu sana hii ishu. That is to say, in a professional setting, it's generally advisable to be mindful of how you present your achievements and capabilities in relation to your supervisor or manager.

The idea behind this statement is that while it's important to excel in your work and contribute to the success of the team or organization, doing so in a way that makes your boss feel threatened or overshadowed (watoto wa mjini wanasema KUFUNIKWA) can potentially have negative consequences. If you appear to be too competent or ambitious, it might create discomfort or insecurity in your supervisor, leading to a tensioned relationship. Mtaanza kuwindana kama chui na sungura. This doesn't mean you should hide your skills or not strive for excellence. Instead, it suggests that you should be aware of the dynamics in your workplace and navigate them diplomatically. It may involve giving credit to your boss for your accomplishments, seeking their guidance, and being sensitive to their leadership style. Kwa hiyo this is another skills or experience that I would live to share with you kwani ilinitokea mimi mwenyewe na kuna kitu ilinicost maana sikuwa makini.

Sasa trudi nyuma kidogo wakati nakabidhi ile barua ya kuacha kazi pale kwa walemavu. Sasa wakati nampa ile resignation letter yule CEO kuna kitu akaniambia ambacho kilinikumbusha mbali sana. Aliniambia “hivi Taidume unajua bila wewe mimi nisingekuwa hapa kwenye hii nafasi?” akaendelea kusema, “naomba hata huko uendako ukaendelee kusimamia weledi wako na ukawe balozi mzuri wa taasisi yetu”.

Nikavuta kumbukumbu nyuma nikakumbuka miaka miwili nyuma wakati ndio kwanza nina miezi saba kazini pale ofisi ya watu wenye ulemavu. Nakumbuka wakati huo kulikuwa na wageni flani kutoka Uingereza walikuwa wanakuja pale ofsini kufanya kitu kinaitwa Organization Capacity Assessment (OCA). Kama n ilivodokeza kwamba pale kwa walemavu donors wengi wana interest sana ya kupeleka projects pale kwahiyo mara nyingi kabla hawaleta hizo project huwa wanafanya hiyo kitu ya kuitwa OCA, ambapo wanaassess uwezo wa taasisi husika kwenye angle mbali mbali kama vile muundo wa taasisi, mifumo ya fedha, ufuatiliaji, mifumo ya kutunza na kutoa taarifa, uwezo wa kutekeleza miradi kama weledi wa uongozi na staff na makolokolo mengine mengine mengi sana ili mradi wajiridhishe fedha yao haitopotea bure, ambayo kwao ni risk kubwa. OCA pia ilikuwa inasaidia to identify the gaps and areas for performance improvement. By evaluating internal processes, systems, and structures, organizations can pinpoint inefficiencies and bottlenecks and implement changes to enhance overall performance. Fani za watu hizo na wengi wanaishi hapa mjini kwa ajili ya kazi hizo, pia nina uzoefu wa kutosha kwenye hili eneo.

Basi bwana nakumbuka wale wageni walitoa taarifa kwamba watakuja siku flani basi mimi kwa akili ya kawaida tu nikajua inatakiwa tuainishe maeneo ambayo kama taasisi tunafanya vizuri nay ale ambayo hatufanyi vizuri ikiwemo kuangalia fursa na changamoto zilizopo, hiyo inaitwa SWOT analysis. Lakini nikaona hakuna msisitizo wowote kutoka kwa top leaders pale na siku zinasogea. Basi siku moja kwenye meeting nikawauliza tunajiandaaje na ugeni unaokuja? Maana mimi ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kushuhudia ugeni unaokuja kutufanyia OCA. Nikajibiwa tu kwamba mnisijali wao (top leaders) wanauzoefu wa kutosha na watalihandle hilo so nisiwe na wasi wasi.

Nikaona ni sawa basi nikaliacha lipite. Kwa structure ya ile ofisi ilikuwa kuna bodi ambao waote ni watu wenye ulemavu, then top leaders pia wote wana ulemavu, then ndio sisi waajiriwa ambao sio lazima uwe na ulemavu. Nadhani hili walifanya makusudi ili kuonesha representation na inclusion. Basi ikafika wiki ya kufanyawa OCA ambapo wale wazungu walikuwa wanaongea na idara mbali mbali kabla ya kufanya majumuisho kwenye mkutano wa mwisho na kufikia mwafaka maeneo gani tuboreshe au tuendelee nayo ili waweke mzigo. Kwa kweli nilipata experience mpya kabisa hapo ndipo niliewa vizuri sana mifumo na miundo ya ofisi the way zinatakiwa kuwekwa na kufuatwa.

Sasa nakumbuka siku ya mwisho wale wazungu walitualika wote yaani board members, top leaders na sisi staff kwenye kikao cha majumuisho. Sasa unajua wazungu wana tabia moja ambayo nimeiexperience sana kwenye kufanya nao kazi. Hawataki kuonekana wanakupangia kitu huwa wanataka wewe mwenyewe muhusika useme unataka nini na upendekeze njia za kukuwezesha ili kuwezesha kufanya unachokitaka. Yaani wana ile diplomatic approach kwamba hata kama unaongea pumba slowly watakurudisha kwenye mstari na wakiona unang’ang’ania sana wataachana na wewe kwa mtindo ambao utakuja kujua badae kwamba kumbe nilichemka pale.

Ushawahi kunyimwa mchongo namzungu? Atakupa feedback ambayo wewe mwenyewe ukikaa utasema kweli wamenitendea haki. Mathalani mzungu anakuambia "Thank you for taking the time to interview with us. We appreciate your interest in the position. During the interview, we observed some areas where there could be room for improvement in your responses to certain questions. Specifically, when asked about …………., we were hoping to hear more details about that. Please next time tell us more about that area”. Japo umekosa dili lakini angalau utajiskia faraja si ndio? Sasa kutana na hawa wabongo sijui ni bongo moonsearch au bongo sunsearch wanavyotoa feedback kwa madogo wanaojitokeza kwenye mashindano yao ya kuimba, yaani mara nyingi ni kukatishana tamaa tu na kebehi ambazo hazimjengi mtu. Kwanza watakucheka halafu wakikuhurumia sana watakwambia katafute kazi nyingine. Kukuambia tokaaa ni kawaida, sasa hiyo ndio nini? Key note hapa sisifii wazungu, bali nasema tujifunze weledi kutoka kwa wazungu huku nikitambua fika kuna watanzania ni weledi wazuri tuu kuliko hao wazungu.

Basi kwenye kile kikao nakumbuka wale wazungu wakatoa shukrani pale kwa ushirikiano tuliwapatia na wakasema wamepata uzoefu wa kutosha wa kutosha kutoka kwetu. Baada ya hapo wakauliza swali pale je nini ambacho sisi kama taasisi tunakuhitaji ili watufanyie? Binafsi nikaona hili ni swala la msingi sana maana uwanja ulikuwa ni wetu na wale jamaa wana financial capacity kubwa sana ya kweza kutusapoti.

Basi wakaanza pale wazoefu kuongea ambao ni wale board members na top leaders. Wakawa wanatoa hoja zao pale somethings like tufanyiwe trainings za maswala maswala ya uendeshaji wa ofisi, sijui uandishi wa miradi, maswala ya usimamizi wa fedha nk. Yaani kwangu mimi nilikuwa naona wanaongelea very pet issues ukicompare na changamoto zilizopo pale ofsini. Basi wao wakawa wanajimwaga mwaga pale wakiwashawishi wale wazungu watusapoti kwenye maeneo hayo ambapo mengi yalilenga kwenye kufanyiwa seminar nk ambapo walipendekeza tuzunguke kote mikoani kuwatrain watu wenye ulemavu. Basi wale wazungu wakawa wanachukua notes pale. Mwisho wakauliza wale viongozi kama wanadhani hayo ndio ya muhimu kuliko yooote kwa mustakabali shirika. Cha ajabu nikaona wanakubali.

Asee mimi nikanyoosha mkono kutaka kuchangia nikaruhusiwa. Nikaanza kwa kusema mimi tangu nimejiunga na shirika lile ni kama miezi sita tu lakini kama staff nimeshapata hizo training wanazosema zaidi zaidi ya mara mbili kutoka kwa wadau tofauti tofauti. Nikawaambia hizo trainigs au kujengeana uwezo sio tiba ya muda mrefu kwenye sustainability ya shirika na hata mstakabali wa watu wenye ulemavu. Nikawaambia kwahilo mimi nitakuwa tofauti kidogo.

Basi nikaona wale wazungu wanakaa vizuri na kunigeukia huku wakinisikiliza kwa makini sana na wote wakitoa notebooks zao kujiandaa kunukuu nitakavyoongea. Wakati huo huo nikawaona wale viongozi wangu wananitolea macho yale ya kusema unataka kufanya nini tena taidume hahaa lakini sikujali. Basi nikaanza kuorodhoshesha na kufafanua maeneo ambayo mimi binafsi kwa uzoefu niliokaa pale ndio yanapaswa kufanyiwa kazi na kupewa sapoti. Nikatiririka pale nikigusia maeneo yafuatayo.

Moja, structure ya ofisi haiwezi kuleta matokea chanya. Maana pale watu tulikuwa tunaajiriwa kwa project zilizopo so hakukuwa na Secretariat ya kudumu ya kutekeleza majukumu ya kila siku kwani project ikiisha na staff wanaondoka. Wale bodi members na wale top leaders ndio walikuwa wanaact as program secretariat. Kumbuka wale bodi members na top leaders kigezo ilikuwa ni kuwa na ushawishi kwa watu wenye ulemavu nasio weledi wa kuendesha ofisi.

kwahiyo nikapendekeza kwamba structure ya ofisi iwe na bodi ya wakurugenzi ambao itakuwa inazingatia weledi kwa kujumuisha makundi ya watu mbali mbali wakiwemo watu wenye ulemavu wenye weledi. Then kuwe na office program secretariat ambapo nikapendekeza kwa kuanzia kuwe na nafasi nne ambazo ni Mkurugenzi Mtendaji (CEO), Meneja w utawala, fedha na rasilimali watu (Finance and Admn manager), Resource Mobilization & Head of Programs na mtu wa ufuatiliaji na tathmini (M&E Manager).

Nakapendekeza kuwa hizo nafasi ziwe za kudumu pale shirikani ambapo wahusika watasimamia shighuli za kila siku za utendaji wa ofisi ikiwemo pamoja na kutafuta wafadhili na kuandika miradi mbali ili kuendelelea kuwanufaisha watu wenye ulemavu. Nikapendekeza secretariat hii itawajibia moja kwa moja kwa bodi ya wakurugenzi ambayo bodi nayo itawajibika kwa mkutano mkuu wa shirika ambao unajumuisha vyama vyote vya watu wenye ulemavu nchini na ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho juu ya mstakabali wao.

Na support niliyoiomba kufaniukisha hilo kutoka kwa wale wazungu ilikuwa ni kuwezesha vitendea kazi vya ofisi kwa ajili ya watakaoajiriwa kwenye hizo nafasi, kusupport walau mishara ya miaka mitatu ya kuanzia na pia kuwezesha fedha kidogo kwa ajili ya kufanya zoezi la kureview na kuimprove baadhi y avipengere vya kwenye katiba ili kufit kwenye mabadiliko hayo, maana hii ishu yamapendekezo niliyotoa yalikuwa yanagusa katiba ya shirika.

Nikawaambia hayo mambo ya trainings za kujengeana uwezo na mambo mengine itakuw ni assignment ya hao watakaoajiriwa kama program secretariat kuja na mikakati mbali mbali ya kuweza kutatua changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuboresha mifumo ya uendeshaji wa ofisi. Nikamaliza.

Basi wale wazungu walikuwa imporessed sana na recommendation zangu hiyo walionesha na kuisema wazi wazi ambapo automatically wale viongozi wangu hawakuweza kunipinga. Uzuri na sista duu naye akakazia mule mule nilimopitamo maana nay eye kuna fursa aliiona palekwenye mapendekezo yangu. Basi wale wazungu wakaniambia yale yote niliyoongea niyaweke kwenye maandishi na niwatumie ndani ya siku mbili ili wayafanyie kazi na wayaweke kwenye report yao. Tukaagana pale huku wakinipa email contact zao ili niwasiliane nao nikashacompile mapendekezo yangu.

basi kila mtu akwa anaendelea na majukumu yake huku minikiwa ndio naanza kufanyia kazi yale mapendekezo. Mara nasikia naitwa kwa ukali na mmoja wa wale viongozi – taidume tonane board room sasa hivi. Dah, nikajua tu teyari kushwaka huko. Kweli nikaenda kufika nawakuta viongozi wangu wamekaa tayari kwa kutoa mashambulizi. Swali la kwanza kuulizwa lilikuwa “ni lini umeanza kuwa msemaji wa shirika letu?” Duu hapo kiroho kikapiga paap! Lakini nikawajibu mimi sio msemaji wa shirika kwani sio kiongozi. Wakaniuliza sasa ilikuwa utuseme kwa wale wageni bila kutuconsult? Basi kila mmoja akawa anatoa shutuma zake pale kwamba navuka mipaka na kabla sikuzungumza ilipaswa niwashirikishe wao. Wale wazee walipamba moto sana.

Ikabidi niwaache waongee mpaka wamalize kisha nikawambia. Kwanza naombasana mnisamehe sikujua kama mngekwazika hovyo. Pili mimi nilitumia nafasi ile kama mjumbe wa kikao na kile kilikuwa ni kikao kazi ambapo kila mjumbe alikuwa na haki ya kutoa maoni au kukataa maoni au mapendekezo mbayo aliona hayajengi. Kisha nikawauliza je kuna baya lolote ambalo nililifanya au kuongea kwenye kikao? Kwa noma noma hivyo hibyo wakajoibu hakuna baya nililolifanya isipokuwa hoja kazi zile nilipaswa kuwaeleza mapema. Basi nikawajibu tyu kwamba wote tulikuwa pale na hakukuwa na muda wa kuanza kuelekezana ila kama mnaona nilivoongea ni vibaya basi mlipaswa kuvikataa pale pale au kama vipi nitaandika email kwaambia wale wazungu kwamba basi waachane na mapendekezo yangu kwa sababu viongozi hajaridhia. Wakawa wapole wakaniambia lengo sio kukataa wewe endelea lkn siku nyingine utujulishe befor haujasema kwani wewe sio msemaji wa shirika. Tukaachana kivyo.

Basi baada ya wiki wale wazungu wakanijibu kwamba wameridhia mapendekezo yangu yoote. Kwamba watasupport vitendea kazi vya ofisi, watasapoti mishahara na oia watasapoti mchakato wa mabadiliko ya katiba ya shirika letu. Ila wao walikuwa na mapendekezo yao, kwamba eti ile nafasi ya CEO niikaimu mimi kwa muda na niutumie muda huo pamoja na viongozi kurecruit watu wengine kadiri ya mapendekezo yangu. Baadae uongozi ukiridhia wani indorse kuwa the CEO au pale tuliita Executive Director (ED) kabisa na sio kukaimu tena. Kwanza nilikuwa shocked sikujua kama wangefikiria kwamba mimi ndio niwe ED pale. Lakini nilichowaambia badala ya kunijibu mimi personally nikawaomba wawaandikie viongozi. Maana nikaona hii ya kunijibu mimi kisha mimi ndio nipeleke yale majibu kwa uongozi ingeleta balaa jingine tena, yani ingeonekanika kumbe yote yale yalikuwa mipango ya kujimilikisha nafasi. Kweli wawaandika viongozi kuwataarifu maamuzi waliyofikia [pamoja na mapendekezo waliyotoa.

Ile email ilipowafikia viongozi ilileta shida sana. Ilikuwa exactly ni kama nilivotarajia wale viongozi waliichukulia mpoja kwa moja kama figisu hivo ikaamsha hasira zao upya. Vikao vikakaliwa wakakubalina kwamba maamuzi mengine yote ya wale wazungu wanayakubali isipokuwa lilke swala la mimi kuwa kaimu ED ili kuongoza mchakato wa mabadiliko. Nakumbuka yule dada sista duu alinitetea sana na kunitaka niipiganie ile nafasi ila mimi sikutaka kwa kutotaka kuleta conflict of interest. Yeye pia alikuwa anaitaka ile nafasi ya Head of M&E. Alijua njia ikiwa nyepesi yakwakwe itakuwa rahisi.

Basi wale viongozi wakajibu kwamba wamekubaliana na maamuzo na wanaikubaki support ya wale wazungu isipokuwa swal la mimi kuwa kaimu ED kwa muda. Basi wale wazungu kishingo upande wakakubaliana na viongozi na hivyo ukafanyika mchakato wa kupata wafanyakazi. Ili kusimamia weledi kwenye kuwapata wafanyakazi wale wazungu nao waliomba wawe sehemu ya panelist ili kufanya kitu kinaitwa joint recruitment. Tangazo likatoka na mimi nikaaply nafasi ya Resource mobilization & Head of programs ili kuondoa sintofaham na uongozi wangu maana ile nafasi ya ED iliwatoa macho sana.

Kweli mchakato ulikamilika nakumbuka tukapata ED Mpya ambae ndio huyo nimemrefer kama CEO kwenye hii stori, akapatikana mtu wa uatawala na fedha, mimi nikapata ile nafasi ya Heads of programs, Fundraising and Advocacy manager, pamoja na mkuu wa M&E ambaye ni sista duu wetu wa kwenye hii stori. Basi maisha yakaendelea kama kawaida na sasa ikawa pale ofsini ni kazi kazi na mabadiliko kweli yalionekana kitu ambacho najivunia mpaka kesho. Badae yule ED aks CEO akaja kujua mlolongo mzima ulivokuwa na pale kama ningekaza basi mimi ni=dio ningekalia kile kiti, basi akazidi kunikubali na tukawa tunashirikiana kwa mambo mengi sana. Chini ya uongozi wake na mimi nikiwa nina jukumu la kuandika na kusimamia miradi tulifanikiwa kupata miradi mingi sana kuhusiana na maswala ya haki za watu wenye ulemavu. Basi kwenye ile moment wakati namkabidhi ile barua ya kuresign alinikumbusha kitu ambacho kilinifanya nikumbuke matukio mengi yaliyopita.​

Kiufupi, my position involves a diverse set of responsibilities that contribute to both organizational success and societal impact. Individually, through this position I acquired a range of valuable skills and experiences, including:

Strategic decision making Skills
Lobbying and advocacy skills
Leadership and Team Management
Program Planning and Implementation
Networking and Relationship Building
Capacity Building
Fundraising and Financial Management
Monitoring, Evaluation, Accountability, and Learning (MEAL)
Communication and Representation
Policy Development and Implementation
Organization Capacity Assessment (OCA)


WADAU KAZI KWENU, CV NDIO HIYO, see you in next episode

Muendelezo soma Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa
 
EPISODE 13: Never outshine or outsmart your boss. Sikuwa makini na ilinicost

Natumaini wengi mmeshawahi kuusikia huu msemo. Ofcourse kama wewe ni bookworm utakuwa umeshakutana mara nyingi tuu hii phrase ya try never to outshine your boss in working invironment, hata bwana Robert Greene katika buku lake la The 48 Laws of Power ameongelea kwa kirefu sana hii ishu. That is to say, in a professional setting, it's generally advisable to be mindful of how you present your achievements and capabilities in relation to your supervisor or manager.

The idea behind this statement is that while it's important to excel in your work and contribute to the success of the team or organization, doing so in a way that makes your boss feel threatened or overshadowed (watoto wa mjini wanasema KUFUNIKWA) can potentially have negative consequences. If you appear to be too competent or ambitious, it might create discomfort or insecurity in your supervisor, leading to a tensioned relationship. Mtaanza kuwindana kama chui na sungura. This doesn't mean you should hide your skills or not strive for excellence. Instead, it suggests that you should be aware of the dynamics in your workplace and navigate them diplomatically. It may involve giving credit to your boss for your accomplishments, seeking their guidance, and being sensitive to their leadership style. Kwa hiyo this is another skills or experience that I would live to share with you kwani ilinitokea mimi mwenyewe na kuna kitu ilinicost maana sikuwa makini.

Sasa trudi nyuma kidogo wakati nakabidhi ile barua ya kuacha kazi pale kwa walemavu. Sasa wakati nampa ile resignation letter yule CEO kuna kitu akaniambia ambacho kilinikumbusha mbali sana. Aliniambia “hivi Taidume unajua bila wewe mimi nisingekuwa hapa kwenye hii nafasi?” akaendelea kusema, “naomba hata huko uendako ukaendelee kusimamia weledi wako na ukawe balozi mzuri wa taasisi yetu”.

Nikavuta kumbukumbu nyuma nikakumbuka miaka miwili nyuma wakati ndio kwanza nina miezi saba kazini pale ofisi ya watu wenye ulemavu. Nakumbuka wakati huo kulikuwa na wageni flani kutoka Uingereza walikuwa wanakuja pale ofsini kufanya kitu kinaitwa Organization Capacity Assessment (OCA). Kama n ilivodokeza kwamba pale kwa walemavu donors wengi wana interest sana ya kupeleka projects pale kwahiyo mara nyingi kabla hawaleta hizo project huwa wanafanya hiyo kitu ya kuitwa OCA, ambapo wanaassess uwezo wa taasisi husika kwenye angle mbali mbali kama vile muundo wa taasisi, mifumo ya fedha, ufuatiliaji, mifumo ya kutunza na kutoa taarifa, uwezo wa kutekeleza miradi kama weledi wa uongozi na staff na makolokolo mengine mengine mengi sana ili mradi wajiridhishe fedha yao haitopotea bure, ambayo kwao ni risk kubwa. OCA pia ilikuwa inasaidia to identify the gaps and areas for performance improvement. By evaluating internal processes, systems, and structures, organizations can pinpoint inefficiencies and bottlenecks and implement changes to enhance overall performance. Fani za watu hizo na wengi wanaishi hapa mjini kwa ajili ya kazi hizo, pia nina uzoefu wa kutosha kwenye hili eneo.

Basi bwana nakumbuka wale wageni walitoa taarifa kwamba watakuja siku flani basi mimi kwa akili ya kawaida tu nikajua inatakiwa tuainishe maeneo ambayo kama taasisi tunafanya vizuri nay ale ambayo hatufanyi vizuri ikiwemo kuangalia fursa na changamoto zilizopo, hiyo inaitwa SWOT analysis. Lakini nikaona hakuna msisitizo wowote kutoka kwa top leaders pale na siku zinasogea. Basi siku moja kwenye meeting nikawauliza tunajiandaaje na ugeni unaokuja? Maana mimi ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kushuhudia ugeni unaokuja kutufanyia OCA. Nikajibiwa tu kwamba mnisijali wao (top leaders) wanauzoefu wa kutosha na watalihandle hilo so nisiwe na wasi wasi.

Nikaona ni sawa basi nikaliacha lipite. Kwa structure ya ile ofisi ilikuwa kuna bodi ambao waote ni watu wenye ulemavu, then top leaders pia wote wana ulemavu, then ndio sisi waajiriwa ambao sio lazima uwe na ulemavu. Nadhani hili walifanya makusudi ili kuonesha representation na inclusion. Basi ikafika wiki ya kufanyawa OCA ambapo wale wazungu walikuwa wanaongea na idara mbali mbali kabla ya kufanya majumuisho kwenye mkutano wa mwisho na kufikia mwafaka maeneo gani tuboreshe au tuendelee nayo ili waweke mzigo. Kwa kweli nilipata experience mpya kabisa hapo ndipo niliewa vizuri sana mifumo na miundo ya ofisi the way zinatakiwa kuwekwa na kufuatwa.

Sasa nakumbuka siku ya mwisho wale wazungu walitualika wote yaani board members, top leaders na sisi staff kwenye kikao cha majumuisho. Sasa unajua wazungu wana tabia moja ambayo nimeiexperience sana kwenye kufanya nao kazi. Hawataki kuonekana wanakupangia kitu huwa wanataka wewe mwenyewe muhusika useme unataka nini na upendekeze njia za kukuwezesha ili kuwezesha kufanya unachokitaka. Yaani wana ile diplomatic approach kwamba hata kama unaongea pumba slowly watakurudisha kwenye mstari na wakiona unang’ang’ania sana wataachana na wewe kwa mtindo ambao utakuja kujua badae kwamba kumbe nilichemka pale.

Ushawahi kunyimwa mchongo namzungu? Atakupa feedback ambayo wewe mwenyewe ukikaa utasema kweli wamenitendea haki. Mathalani mzungu anakuambia "Thank you for taking the time to interview with us. We appreciate your interest in the position. During the interview, we observed some areas where there could be room for improvement in your responses to certain questions. Specifically, when asked about …………., we were hoping to hear more details about that. Please next time tell us more about that area”. Japo umekosa dili lakini angalau utajiskia faraja si ndio? Sasa kutana na hawa wabongo sijui ni bongo moonsearch au bongo sunsearch wanavyotoa feedback kwa madogo wanaojitokeza kwenye mashindano yao ya kuimba, yaani mara nyingi ni kukatishana tamaa tu na kebehi ambazo hazimjengi mtu. Kwanza watakucheka halafu wakikuhurumia sana watakwambia katafute kazi nyingine. Kukuambia tokaaa ni kawaida, sasa hiyo ndio nini? Key note hapa sisifii wazungu, bali nasema tujifunze weledi kutoka kwa wazungu huku nikitambua fika kuna watanzania ni weledi wazuri tuu kuliko hao wazungu.

Basi kwenye kile kikao nakumbuka wale wazungu wakatoa shukrani pale kwa ushirikiano tuliwapatia na wakasema wamepata uzoefu wa kutosha wa kutosha kutoka kwetu. Baada ya hapo wakauliza swali pale je nini ambacho sisi kama taasisi tunakuhitaji ili watufanyie? Binafsi nikaona hili ni swala la msingi sana maana uwanja ulikuwa ni wetu na wale jamaa wana financial capacity kubwa sana ya kweza kutusapoti.

Basi wakaanza pale wazoefu kuongea ambao ni wale board members na top leaders. Wakawa wanatoa hoja zao pale somethings like tufanyiwe trainings za maswala maswala ya uendeshaji wa ofisi, sijui uandishi wa miradi, maswala ya usimamizi wa fedha nk. Yaani kwangu mimi nilikuwa naona wanaongelea very pet issues ukicompare na changamoto zilizopo pale ofsini. Basi wao wakawa wanajimwaga mwaga pale wakiwashawishi wale wazungu watusapoti kwenye maeneo hayo ambapo mengi yalilenga kwenye kufanyiwa seminar nk ambapo walipendekeza tuzunguke kote mikoani kuwatrain watu wenye ulemavu. Basi wale wazungu wakawa wanachukua notes pale. Mwisho wakauliza wale viongozi kama wanadhani hayo ndio ya muhimu kuliko yooote kwa mustakabali shirika. Cha ajabu nikaona wanakubali.

Asee mimi nikanyoosha mkono kutaka kuchangia nikaruhusiwa. Nikaanza kwa kusema mimi tangu nimejiunga na shirika lile ni kama miezi sita tu lakini kama staff nimeshapata hizo training wanazosema zaidi zaidi ya mara mbili kutoka kwa wadau tofauti tofauti. Nikawaambia hizo trainigs au kujengeana uwezo sio tiba ya muda mrefu kwenye sustainability ya shirika na hata mstakabali wa watu wenye ulemavu. Nikawaambia kwahilo mimi nitakuwa tofauti kidogo.

Basi nikaona wale wazungu wanakaa vizuri na kunigeukia huku wakinisikiliza kwa makini sana na wote wakitoa notebooks zao kujiandaa kunukuu nitakavyoongea. Wakati huo huo nikawaona wale viongozi wangu wananitolea macho yale ya kusema unataka kufanya nini tena taidume hahaa lakini sikujali. Basi nikaanza kuorodhoshesha na kufafanua maeneo ambayo mimi binafsi kwa uzoefu niliokaa pale ndio yanapaswa kufanyiwa kazi na kupewa sapoti. Nikatiririka pale nikigusia maeneo yafuatayo.

Moja, structure ya ofisi haiwezi kuleta matokea chanya. Maana pale watu tulikuwa tunaajiriwa kwa project zilizopo so hakukuwa na Secretariat ya kudumu ya kutekeleza majukumu ya kila siku kwani project ikiisha na staff wanaondoka. Wale bodi members na wale top leaders ndio walikuwa wanaact as program secretariat. Kumbuka wale bodi members na top leaders kigezo ilikuwa ni kuwa na ushawishi kwa watu wenye ulemavu nasio weledi wa kuendesha ofisi.

kwahiyo nikapendekeza kwamba structure ya ofisi iwe na bodi ya wakurugenzi ambao itakuwa inazingatia weledi kwa kujumuisha makundi ya watu mbali mbali wakiwemo watu wenye ulemavu wenye weledi. Then kuwe na office program secretariat ambapo nikapendekeza kwa kuanzia kuwe na nafasi nne ambazo ni Mkurugenzi Mtendaji (CEO), Meneja w utawala, fedha na rasilimali watu (Finance and Admn manager), Resource Mobilization & Head of Programs na mtu wa ufuatiliaji na tathmini (M&E Manager).

Nakapendekeza kuwa hizo nafasi ziwe za kudumu pale shirikani ambapo wahusika watasimamia shighuli za kila siku za utendaji wa ofisi ikiwemo pamoja na kutafuta wafadhili na kuandika miradi mbali ili kuendelelea kuwanufaisha watu wenye ulemavu. Nikapendekeza secretariat hii itawajibia moja kwa moja kwa bodi ya wakurugenzi ambayo bodi nayo itawajibika kwa mkutano mkuu wa shirika ambao unajumuisha vyama vyote vya watu wenye ulemavu nchini na ambao ndio wenye maamuzi ya mwisho juu ya mstakabali wao.

Na support niliyoiomba kufaniukisha hilo kutoka kwa wale wazungu ilikuwa ni kuwezesha vitendea kazi vya ofisi kwa ajili ya watakaoajiriwa kwenye hizo nafasi, kusupport walau mishara ya miaka mitatu ya kuanzia na pia kuwezesha fedha kidogo kwa ajili ya kufanya zoezi la kureview na kuimprove baadhi y avipengere vya kwenye katiba ili kufit kwenye mabadiliko hayo, maana hii ishu yamapendekezo niliyotoa yalikuwa yanagusa katiba ya shirika.

Nikawaambia hayo mambo ya trainings za kujengeana uwezo na mambo mengine itakuw ni assignment ya hao watakaoajiriwa kama program secretariat kuja na mikakati mbali mbali ya kuweza kutatua changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuboresha mifumo ya uendeshaji wa ofisi. Nikamaliza.

Basi wale wazungu walikuwa imporessed sana na recommendation zangu hiyo walionesha na kuisema wazi wazi ambapo automatically wale viongozi wangu hawakuweza kunipinga. Uzuri na sista duu naye akakazia mule mule nilimopitamo maana nay eye kuna fursa aliiona palekwenye mapendekezo yangu. Basi wale wazungu wakaniambia yale yote niliyoongea niyaweke kwenye maandishi na niwatumie ndani ya siku mbili ili wayafanyie kazi na wayaweke kwenye report yao. Tukaagana pale huku wakinipa email contact zao ili niwasiliane nao nikashacompile mapendekezo yangu.

basi kila mtu akwa anaendelea na majukumu yake huku minikiwa ndio naanza kufanyia kazi yale mapendekezo. Mara nasikia naitwa kwa ukali na mmoja wa wale viongozi – taidume tonane board room sasa hivi. Dah, nikajua tu teyari kushwaka huko. Kweli nikaenda kufika nawakuta viongozi wangu wamekaa tayari kwa kutoa mashambulizi. Swali la kwanza kuulizwa lilikuwa “ni lini umeanza kuwa msemaji wa shirika letu?” Duu hapo kiroho kikapiga paap! Lakini nikawajibu mimi sio msemaji wa shirika kwani sio kiongozi. Wakaniuliza sasa ilikuwa utuseme kwa wale wageni bila kutuconsult? Basi kila mmoja akawa anatoa shutuma zake pale kwamba navuka mipaka na kabla sikuzungumza ilipaswa niwashirikishe wao. Wale wazee walipamba moto sana.

Ikabidi niwaache waongee mpaka wamalize kisha nikawambia. Kwanza naombasana mnisamehe sikujua kama mngekwazika hovyo. Pili mimi nilitumia nafasi ile kama mjumbe wa kikao na kile kilikuwa ni kikao kazi ambapo kila mjumbe alikuwa na haki ya kutoa maoni au kukataa maoni au mapendekezo mbayo aliona hayajengi. Kisha nikawauliza je kuna baya lolote ambalo nililifanya au kuongea kwenye kikao? Kwa noma noma hivyo hibyo wakajoibu hakuna baya nililolifanya isipokuwa hoja kazi zile nilipaswa kuwaeleza mapema. Basi nikawajibu tyu kwamba wote tulikuwa pale na hakukuwa na muda wa kuanza kuelekezana ila kama mnaona nilivoongea ni vibaya basi mlipaswa kuvikataa pale pale au kama vipi nitaandika email kwaambia wale wazungu kwamba basi waachane na mapendekezo yangu kwa sababu viongozi hajaridhia. Wakawa wapole wakaniambia lengo sio kukataa wewe endelea lkn siku nyingine utujulishe befor haujasema kwani wewe sio msemaji wa shirika. Tukaachana kivyo.

Basi baada ya wiki wale wazungu wakanijibu kwamba wameridhia mapendekezo yangu yoote. Kwamba watasupport vitendea kazi vya ofisi, watasapoti mishahara na oia watasapoti mchakato wa mabadiliko ya katiba ya shirika letu. Ila wao walikuwa na mapendekezo yao, kwamba eti ile nafasi ya CEO niikaimu mimi kwa muda na niutumie muda huo pamoja na viongozi kurecruit watu wengine kadiri ya mapendekezo yangu. Baadae uongozi ukiridhia wani indorse kuwa the CEO au pale tuliita Executive Director (ED) kabisa na sio kukaimu tena. Kwanza nilikuwa shocked sikujua kama wangefikiria kwamba mimi ndio niwe ED pale. Lakini nilichowaambia badala ya kunijibu mimi personally nikawaomba wawaandikie viongozi. Maana nikaona hii ya kunijibu mimi kisha mimi ndio nipeleke yale majibu kwa uongozi ingeleta balaa jingine tena, yani ingeonekanika kumbe yote yale yalikuwa mipango ya kujimilikisha nafasi. Kweli wawaandika viongozi kuwataarifu maamuzi waliyofikia [pamoja na mapendekezo waliyotoa.

Ile email ilipowafikia viongozi ilileta shida sana. Ilikuwa exactly ni kama nilivotarajia wale viongozi waliichukulia mpoja kwa moja kama figisu hivo ikaamsha hasira zao upya. Vikao vikakaliwa wakakubalina kwamba maamuzi mengine yote ya wale wazungu wanayakubali isipokuwa lilke swala la mimi kuwa kaimu ED ili kuongoza mchakato wa mabadiliko. Nakumbuka yule dada sista duu alinitetea sana na kunitaka niipiganie ile nafasi ila mimi sikutaka kwa kutotaka kuleta conflict of interest. Yeye pia alikuwa anaitaka ile nafasi ya Head of M&E. Alijua njia ikiwa nyepesi yakwakwe itakuwa rahisi.

Basi wale viongozi wakajibu kwamba wamekubaliana na maamuzo na wanaikubaki support ya wale wazungu isipokuwa swal la mimi kuwa kaimu ED kwa muda. Basi wale wazungu kishingo upande wakakubaliana na viongozi na hivyo ukafanyika mchakato wa kupata wafanyakazi. Ili kusimamia weledi kwenye kuwapata wafanyakazi wale wazungu nao waliomba wawe sehemu ya panelist ili kufanya kitu kinaitwa joint recruitment. Tangazo likatoka na mimi nikaaply nafasi ya Resource mobilization & Head of programs ili kuondoa sintofaham na uongozi wangu maana ile nafasi ya ED iliwatoa macho sana.

Kweli mchakato ulikamilika nakumbuka tukapata ED Mpya ambae ndio huyo nimemrefer kama CEO kwenye hii stori, akapatikana mtu wa uatawala na fedha, mimi nikapata ile nafasi ya Heads of programs, Fundraising and Advocacy manager, pamoja na mkuu wa M&E ambaye ni sista duu wetu wa kwenye hii stori. Basi maisha yakaendelea kama kawaida na sasa ikawa pale ofsini ni kazi kazi na mabadiliko kweli yalionekana kitu ambacho najivunia mpaka kesho. Badae yule ED aks CEO akaja kujua mlolongo mzima ulivokuwa na pale kama ningekaza basi mimi ni=dio ningekalia kile kiti, basi akazidi kunikubali na tukawa tunashirikiana kwa mambo mengi sana. Chini ya uongozi wake na mimi nikiwa nina jukumu la kuandika na kusimamia miradi tulifanikiwa kupata miradi mingi sana kuhusiana na maswala ya haki za watu wenye ulemavu. Basi kwenye ile moment wakati namkabidhi ile barua ya kuresign alinikumbusha kitu ambacho kilinifanya nikumbuke matukio mengi yaliyopita.​

Kiufupi, my position involves a diverse set of responsibilities that contribute to both organizational success and societal impact. Individually, through this position I acquired a range of valuable skills and experiences, including:

Strategic decision making Skills
Lobbying and advocacy skills
Leadership and Team Management
Program Planning and Implementation
Networking and Relationship Building
Capacity Building
Fundraising and Financial Management
Monitoring, Evaluation, Accountability, and Learning (MEAL)
Communication and Representation
Policy Development and Implementation
Organization Capacity Assessment (OCA)


WADAU KAZI KWENU, CV NDIO HIYO, see you in next episode
Naam [emoji91]
 
Back
Top Bottom