Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Huijui njaa wewe....

Njaa haina baunsa
Hustling nilizopitia/ninazopitia njaa haikuwahi kuwa obstacle kwangu
Nishapiga Sana pasi ndefu, halafu nipo happy na watu bize na mishe zangu

Kulalia maji ndio Sana tu, asubuhi naamka Kama usiku nimekula birian

Baada ya kufanikiwa kwa hiki kidogo nilichonacho, nikaja kugundua watu waliofanikiwa wanawapenda Sana watu wabishi/wakazaji
 
moja kati ya silaha kubwa sana kwenye safari ya maisha ni kujishusha, tofauti na hapo umekwisha’ watu watakuwa wanakupita wasema tu yule anakuburi sana achaneni nae.
Matokeo yake tunapata viongozi incompetent. Kwa sababu asilimia kubwa ya watu wanapoenda kujishusha(of which ni unafiki kwani wakishasogea nao ni viburi tu) ni wale wenye uwezo mdogo sana kiakili.

Watu wengi wenye akili naturally ni arrogant, hawapendi kuburuzwa na kupelekwa pelekwa na wanajiamini kitu ambacho mara nyingi hutafsiriwa kama kiburi.

Mwisho wa siku nchi tumejaza viongozi na decision makers incompetent sana. Hadi mtu unajiuliza huyu alifikaje hapa. Kumbe katumia silaha ya kujishusha a.k.a unafiki!
 
Matokeo yake tunapata viongozi incompetent. Kwa sababu asilimia kubwa ya watu wanapoenda kujishusha( of which ni unafiki kwani wakishasogea nao ni viburi tu) ni wale wenye uwezo mdogo sana kiakiri.
Watu wengi wenye akili naturally ni arrogant, hawapendi kuburuzwa na kupelekwa pelekwa na wanajiamini kitu ambacho mara nyingi hutafsiriwa kama kiburi.
Mwisho wa siku nchi tumejaza viongozi na decision makers incompetent sana. Hadi mtu unajiuliza huyu alifikaje hapa. Kumbe katumia silaha ya kujishusha a.k.a unafiki!
Uzi uishie hapa

Asante
 
Graduate kukataa kazi Uliyosemea kisa mshahara mdogo na huna Ajira yoyote pengine ndo kwanza Umemaliza chuo ni Suala la Ovyooo sanaaaaa...!! Hakuna fala anaeajiri mtu sababu ya degreee yake hapana experience inakupa hela ya maana ila degree yako inakupa kazi...!!
 
Mkuu mimi nimepata mawaidha ya tajiri maarufu Ali Mufuruki akiwaasa graduates kujishusha ili kupata angalau sehemu ya kuanzia.

Aliwaambia graduates wafanye kazi, hata kama ni kuosha magari mjini, ilimradi wanajua mpango wao ni kufanya nini kuitoa katika maisha. Wasione aibu kufanya kazi yenye maslahi kwa sababu wao ni graduates.

Na nishaishi maisha ya aina zote ya kwetu ushuani na Uswahilini nilikojitosa tu kuona maisha, nikafunga mkanda mpaka New York City kutafuta maisha bila kumjua mtu.

Kwa hivyo, somo la kujishusha katika maisha ili kupata pa kuanzia, nalielewa sana.

Nishawahi kukaa sehemu ambazo wale watu wa pale wangejua mimi ni nani wangenichukulia tofauti kabisa, lakini mimi hata sikutoa credentials zangu nilikuwa nimejishusha tu, na hata hapo kuna watu walikuwa wananiangalia kimagutu magutu wanaona huyu mbona kama hapa kajiegesha tu lakini si wa hapa?

Kumbe nilikuwa nasoma tu katika darasa la maisha.😁😁
Mkuu Kiranga,
Hiyo signature yako imekuwa misattributed kwa Plato.

Source: Famous Misquotations: We Can Easily Forgive a Child Who is Afraid of the Dark, the Real Tragedy…
 
EPISODE 2: Kwenye mazingira mapya ya kazi, JIONGEZE. Ugeni mwisho wiki ya kwanza

Here I am talking abouth the ability to adapt to new situations and learn quickly. Demonstrate a willingness to learn and take on new responsibilities kwa uharaka. Employers value employees who can quickly acquire new skills and knowledge to keep up with evolving job environment and requirements.

Bhasi bana nikaenda kwenye ofisi yangu niliyoichagua na kuanza kuupitia ule mkataba. Nakumbuka mchecheto mkubwa kwenye kuusoma ule mkataba ulikuwa kwenye salali kuliko hata vipengele vingine. Chaajabu kwenye mkataba ule hakukuwa na kipengele cha “remuneration” ambapo ndio utaona maswala ya salali yako na benefits mbalimbali kama vile bima ya afya, posho za likizo nk. Ila kulikuwa na kipengele cha majukumu tuu tu ya kazi na blabla nyinginezo.

Kichwa iliwaka sana moto nakumbuka. Nikajiuliza maswali mengi sana sasa hii inakuwaje, its my first job contract – yes, but how can it miss such a crucial contract segment!! Ahahaaa. Nikaskuti pale je nikamuulize boss au yule dada mhasibu? Maana yule dada Mhasibu alikuwa ana act pia as HR wa shirika. Nilichoamua kufanya kwa muda ule ni kutousaini ule mkataba, kwanza sikupewa time frame ya kuusoma na kuurudisha kwa boss ukiwa umesainiwa.

Japo sikuwa nimesettle kiakili ila niliamua niendelee kujisomea vipengele vingine vilivyoainisha majukumu yako as a Program Officer – Advocacy. Yaani hata hiyo the meaning and approaches to advocacy nilikuwa sijui, kaazi kwelikweli. Hapo nikagundua kwamba nilikuwa empty kabisa kwenye ile position kwa maana ya kukosa uzoefu na hata baadhi ya majukumu sikuelewa kabisa yanataka nifanye nini. I missed the technical know.

Kiufupi nilijifanyia a quick self assessment of my knowledge, skills and experience related to the job responsibility, nikajiona labda nina qualify kwa not more than 15%. Kwanza niliogopa, pili nikajicheka, tatu nikaona hata kile kipengele cha salali nikisema niulizie na nikiulizwa unataka ulipwe sh ngapi na shughuli ipi utakazofanya nitajibu nini? Anyway nikajipa moyo lazima kutakuwa na job orientation kutoka kwa mzoefu hususan Dr KJ mwenyewe ili nipate uelewa wa kazi.

Basi wakati nasubiri utaratibu mwingine, nikaenda kwa yule secretary nikamuomba anipe docs zinazohusiana na projects za pale ofisini hususani kama kuna reports zozote. Nikapewa pale madocs kibao nikaendelea kujisomea. Hii at least ilinipa mwanga zaidi wa nini kinachofanyika pale ofisini. Ilipofika muda wa mchana kabla ya lunch nikamsikia Dr KJ akimuaga (kwa sasa nitakuwa natumia neno boss) secretary wake kwamba anaondoka nyumbani hajisikii vizuri. Mimi hakuja kuniaga sikujali sana nikajua labda ni kutojisikia vizuri kwake. Nikaendelea kujisomea zile docs mpaka muda wa kufunga ofisi ulipofika. Nikaondoka. Hiyo ilikuwa ni first day officially employed in my entire life. Kwakweli Nilisali sala ndeeeefuu sana ya kumshukuru Mungu nilipofika magetoni kwangu.

Kwa ile wiki nzima boss hakuja kabisa ofsini. Nakumbuka siku ya tatu nikaomba namba yake kwa secretary nikampigia boss wangu kumjulia hali. Hakupokea zaidi ya mara tatu so nikamtext kumjulia hali lakini hakujibu. Ila yule secretary akimpigia simu anazipokea na boss alikuwa anampigia mara kwa mara yule Mhasibu kumpa maelekezo ya flani flani kwenye department yake. Nikaona sio kesi madam nimeshamtext tena kwa kujitambulisha basi atajuwa mwenyewe. Hakuja ofisini wiki nzima.

Sasa mimi zile docs za report na programs mbali mbali nilimaliza kuzipitia na kuna baadhi ya mambo nikawa siyaelewi na nikijaribu kumuuliza secretary au mhasibu hakuna wanalolijua. Uzuri pale ofisini kama zilivyo ofisi nyingi nyingine kulikuwa na strong internet you connect through wi-fi. Basi kwa zile mambo ambazo nilikuwa sizielewi nikajiongeza kuingia youtube ili kupata tips. Asee pale ndio nilijua kumbe youtube ukiitumia vizuri inaweza kuwa chuo kikuu ada yake ni bando lako tuu.

Kwa ile wiki ambayo boss hakuja ofsini nilikula shule ya kutosha youtube, na nilikuza uelewa wa majukumu yangu walau kwa 60%. Kwa kuwa kulikuwa na projector pale ofisini kuna wakati nikuwa naproject zile youtube lectures ili nisichoke kitu ambacho kiliwafanya hata wale madada wengine wa ofisini nao kujiunga na mm kufatilia, hususani yule secretary, maana yeye ukiacha kupokea wageni na kusoma emails zinazotumwa Info, majukumu yake mengi alikuwa nayo boss anapokuwa ofisini (Kumbuka yule alikuwa ni Personal Secretary wa boss, kuanzia sasa nitamwita PS)

Nakumbuka Ijumaa wakati tunajiandaa kuondoka ofisini boss alinipigia simu kunitaka niandae training manual kuhusiana na training flani ambayo inatakiwa akatrain watu weekend hiyo (kesho yake Jumamosi). Uzuri nilishapitia youtube maana moja ya majukumu yangu ilikuwa ni kutrain raia wa huko vijijini kuhusiana na maswala ya PETS na SAM – Kama huyajui hayo mambo zama you tube. Bai kwa reference za you tube na kureview mariport ya pale ofisini nikatengeza ile manual fasta tuu then kwenye saa 11 nikamtumia. Nikampigia simu kumueleza kwamba nishamtumia kazi, hakupokea ila akanitext tuu weekend njema. Basi nikafunga ofisi pale nikasepa maana walinipa copy ya funguo za ofisi.

Wiki ya pili ofisini ilianza Jumatatu kama kawaida. Bosi alifika ofisini mapema sana angalau nikajua may be anaweza kunielekeza maswala ya kazi na pengine kupata muda wa kudiscuss kuhusiana na salali maana ishu ilikuwa bado pending. Baada ya muda akaniita ofsini kwake, akaniambia nijiandae kwa safari kesho tunaenda Tanga (Handeni na Kilindi) kutrain watu maswala ya PETS na SAM. Hakuongelea chochote kuhusiana na ile kazi aliyonipa ila nikamuuliza tu natakiwa kuandaa nini kwenye hiyo safari?

Asee gafla tu boss alinichenjia kinoma noma akafoka kwa sauti mpka ofisi nzima ikawa inasikia. “Yaani officer mzima hujui majukumu yako kwenye safari, mbona unakuwa mzembe mzembe sana, unashindwa hata kutumia akili kidogo tuu kujiongeza? Hii ndio shida ya kusaidia watu wasiojielewa” aling’aka boss KJ. Kisha akaanza kukohoa mfululizo kikohozi kile kama cha TB sugu mpaka PS akaja kumpetipeti na kumtuliza. Nakweli boss akawa calm kisha akatuambia tuondoke ofsini kwake anataka kupumzika, ila mimi niandae safari.

Unajua nilipigwa butwaa ambalo sikuwahi kupigwa nalo kwenye maisha yangu yoote hapa duniani. Nikajiuliza pale nimekosea kipi hasa mpaka bosi kukasirika mpaka anakohoa kama anataka kukata utepe wa kifo? Uzuri nikamkumbuka yule dereva wake basi nikaenda parking kumtafuta (yule dereva huwa haingii ofsini labda akiitwa nilikuja kujua badae kwamba boss alimwambia yeye ofisi yake ni kwenye gari hivyo akae ofisini kwake. Na ole boss ashuke chini ili waondoke na asimkute atawashiwa moto balaa).

Unajua hawa madereva wa maboss wanakuwa wanajua mambo mengi sana ukiwatumia vizuri utafaidika sana. Basi nikamuuliza driver bosi huwa anafanyaje fanyaje mnapoendaga kutain watu vijijini? Kwa kweli alinisaidia sana kunipa hints na vingine akaniambia nikamuulize muhasibu hususani namna ya kuandaa bajeti. Wakati naondoka nirudi juu dereva akaniambia huku akijichekesha “bwana Taidume karibu kwenye ofisi yetu bwana hapa kazi zako itabidi uzijue kwa kufosi hakuna wa kukuelekeza” Na mimi nikajichekesha pale nikamshuru.

Kwa msaada wa yule dreva na muhasibu nikaweza kuandaa safari ile vizuri tu tuu kama vile kuandaa bajeti ya mafuta, malipo ya ukumbi, chakula, nauli za washiriki pamoja na posho zetu za safari. Kuhusiana na notes za kufundishia yule PS alinipa training manuals pale zenye kila kitu, nilichoshangaa tuu iweje boss last week aliniambia nimwandalie training manual wakati zilikuwepo. Badae nikaja kujua alikuwa ananipima tuu na uzuri nilitembelea karibu mule mule isipokuwa vitu vichache sana.

Kumbuka ile safari ilikuwa ni very short note binafsi hata sikujiandaa lkn kwa kuwa nilikuwa naishi mwenyewe kininja nilifurahia sana tuu na hivi Tanga nilikuwa siifahamu. Wakati nasubmitt budget kwa boss for his approaval akaniambia niongeze na bajeti ya PS wake, kwahiyo tulitakiwa kuondoka watu wanne yaani Boss, mimi, PS na dereva. Na pia akanipa orodha ya coordinators wa kule field niwasiliane nao ili kufatilia maandalizi.

Kesho yake tulianza safari ya Handeni tukafika mapema tu na moja kwa moja tukaenda kuonana na wenyeji wetu pamoja na kukagua maandalizi ya semina kama vile ukumbi, mtu wa chakula nk. Ila kwenye kutafuta lodge za kulala nikagundua PS na Boss wameshafanya booking hivyo tulivyowaacha lodge kwao mimi na dereva tuakatafuta logde nyingine. Sikutaka kuhoji sana na pia nikajiongeza. Jioni ile PS akanicheki twende kula so tukakutana nae sehemu ila boss hakuwepo. Nikamuuliza akasema boss hali yake sio nzuri na sio mtokaji tokaji sana wa usiku na ameshakula. Basi tukapata msosi pale na drinks mbili tatu then tukamrudisha kwake na sisi tukarudisha majeshi logde kwetu.

Asubuhi nilitakiwa kuwahi ukumbini boss alinipigia akaniambia angekuja badae kidogo. Kwahiyo nilihakikisha logistics zote zipo sawa pale watu wameshajiregister, stationaries zimegawiwa, projector iko connected n.k. Boss alipofika alianza moja kwa moja kuendesha ile training huku mimi nikichukue key notes kwa ajili ya report. Ile session ilikuwa ni ya siku tatu pale Handeni then tukamailizie Kilindi siku tatu zingine kisha tugeuze. Boss alikuwa ni trainer mzuri sana na mcheshi sana kwa washiriki kitu ambacho nilikipenda na alikuwa tofauti sana na yule anayefoka foka ofsini. Nilimfatilia kwa makini sana na kujifunza mengi kwake.

Kiukweli hali ya boss kiafya haikuwa nzuri nakumbuka siku ya mwisho ya ile training pale Handeni asubuhi aliniita kule lodge kwake akanipa zile notes akaniambia nipitie session ya siku hiyo kwani mimi ndio nitaanza kufundisha siku hiyo yeye atakuwa anaintervine atakapoona panafaa. Kidogo nilishtuka na kawoga kaliniingia lkn nikasema nitaogopa mpaka lini? Nikamwambia sawa, nikarudi lodge kujiandaa maana ilikuwa ni saa moja na session zinaanza saa tatu.

Muda wa semina ulipowadia nikaanza kuwatrain pale. Sitaisahau hii siku kwani nilitumia akili mingi sana ili kuendana na hiyo kazi. Ujue kuna vitu vingi sana vya kuzingatia ambavyo boss nilimwona anafanya. Mfano inatakiwa ubalance speed yako, uwe very interactive and allow members participation, toa mifano mingi sana iwezekanavo, fahamu tabia za trainees wako kwani wana upeo na behavior tofauti tofauti, kingine mimi nilikuwa very junior kwa umri halafu wengi wao pale walikuwa ni watu wazima hivyo ilitakiwa kuwa makini sana na lugha. Mpaka unafika muda wa lunch boss hakuintervene popote na wala na sikuweza kuisoma sura yake kama nafanya sawa au nimeenda OP.

Niliendelea na ile session mpaka mwisho kwa siku hiyo, boss aliniachia nimalize yeye alifanya ile session ya kufunga tuu na hivyo tukawa tumemaliza pale Handeni. Jioni kama kawaida mimi na PS tulijumuika kupata msosi na drinks. Yule dereva alikuwa hakai na sisi kabisa nikajua labda ni very introvert au misingi yake ya kazi haimruhusu, sikuweza kupata majibu maana hiyo ilikuwa ni wiki ya pili tuu ofsini. Basi kwenye kupiga piga story na PS pale akaniambia;

PS: Unajua Taidume unaweza ukaenda mwenyewe Kilindi?

Mimi: Kivipi mbona sikuelewi

PS: Ndio hivyo, maana jamaa amekuelewa sana yaani leo amekusifia sana tulipokuwa lodge kwamba umepiga mzigo fresh.

Mimi: Aisee! Sasa mbona itakuwa mtihani, huko Kilindi mimi simjui yeyote, basi at least tungeenda wote walau siku moja halafu nyie mgeuze.

PS: Mh sidhani maana kwanza boss ameshukuru wewe upo kwa kuwa hali yake kiafya sio nzuri so amesema atakuacha wewe umalizie. Lakini kaka Taidume mbona umepiga mzigo fresh tuu boss anaumwa wacha tu arudi Dar.

Mimi: Dah poa ila sio mbaya kwahiyo mnaondoka kesho?

PS: Nafikiri hivyo, ila atakupigia.

Basi tukaachana pale kama kwenye saa 4 hivi usiku. Na kweli ile nafika tu chumbani boss akanipigia huku akikohoa mfulizo kwamba kesho asubuhi saa moja niende pale kwake kuna maagizo. Nikajifanya sijui lolote nikamwitikia tu sawa. Asubuhi nikaenda kwake pale akaniita chumbani nikakuta wameshafungasha mabegi. Basi akanipa maagizo pale kwamba wao wanageuza Dar hivyo mimi nitamalizia Kilindi.

Sikubisha wala kuhoji chochote maana PS alishanitonya jana yake. Basi nikaachiwa mpunga pale wa kufacilitate session za kule Kilindi. Dereva alikuwa hajui kama watageuza kurudi Dar na mimi sikutaka kumwambia, hivyo ikabidi tutoke pale wote ili wapitie mzigo wa dereva wasepe. Hiyo ilikuwa Jumamosi, Session ya Kilindi ilikuwa inaanza Jumatatu ya next week. Hivyo niliamua mchana nianze safari ya kwenda Kilindi ili nipafahamu na Jumapili niweze kufanya maandalizi.

Jumapili nilifanya maandalizi muhimu ikiwemo kuonana na coodinators wa kule hivyo kila kitu kilienda sawa. Jumatatu nikapiga session zangu na nilifanikiwa kumaliza salama Jumatano Mchana wa saba. Siku hiyo hiyo nikabatika kupata usafiri mpaka Tanga mjini maana Kilindi kulichosha sana nikaona bora nikalale Tanga town. Alhamis niligeuza zangu Dar ambapo ijumaa nilienda ofisini. Boss hakuwepo ila nilimpigia simu kwamba nimerudi na akaniambia tuu tutaonana Jumatatu na akanipa ruhusa ya kwenda kupumzika nyumbani. Basi mimi nikafanya retirement pale na kukabidhi madocuments na some change kwa muhasibu nikasepa zangu. Nakumbuka ile weekend ilikuwa mujarabu sana, wacha tuu. Jumatatu yake nikaandaa report na kumtumia boss kwenye email yake. Aliireview huko huko alipokuwepo maana hakuja ofsini siku hiyo. Aliweka some few inputs akaniambia niiprint na kuifile.

See you soon guys kuna mengi yanakuja!!!!!!!
Muendelezo soma Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa
 
Matokeo yake tunapata viongozi incompetent. Kwa sababu asilimia kubwa ya watu wanapoenda kujishusha( of which ni unafiki kwani wakishasogea nao ni viburi tu) ni wale wenye uwezo mdogo sana kiakiri.
Watu wengi wenye akili naturally ni arrogant, hawapendi kuburuzwa na kupelekwa pelekwa na wanajiamini kitu ambacho mara nyingi hutafsiriwa kama kiburi.
Mwisho wa siku nchi tumejaza viongozi na decision makers incompetent sana. Hadi mtu unajiuliza huyu alifikaje hapa. Kumbe katumia silaha ya kujishusha a.k.a unafiki!
Tofautisha Arrogance na emotions intelligence, watu wanaojishusha wanakuaga na emotions intelligence ukiwa na akili Ila hauna emotions intelligence basi huwezi kuwa MTU mwenye mafanikio makubwa maana maisha yanahitaji Sana kiwango kikubwa cha emotions intelligence na sio akili tu.
 
UTANGULIZI
Wakuu habari.

Naandika hii story yangu ikiwa ni mwaka sasa nipo mtaani nikiendelea na harakati za kusaka ajira mpya toka mkataba wangu wa ajira ulipoisha mnamo Desemba 2022. Nimeamua kushea uzoefu wangu kwa mtindo wa Masimulizi (katika episodes) kwa kuamini pengine inaweza kuwa na mafunzo kwa waajiri, waajiriwa au wanaotegemewa kuajiriwa. Naomba moderatoes wa JF wauache huu uzi wangu hapa hapa kwenye Jukwa la Ajira kwani muktadha wa simulizi hii maswala ya kubadilishana uzoefu katika swala la ajira na sio mambo ya entertainment. Twende kazi.

Episode 1: Sikuogopa kujidhalilisha ili kupata reliable connection

Mwaka 2011 nilipomaliza my 1st degree kama ilivo kwa wanachuo wengine, nilikuwa na expectation kubwa sana ya kupata ajira nzuri ndani ya muda mfupi. Hii ilijengwa na kiburi kwamba mwaka mmoja before sijamaliza niliwaaproach ndugu na wadau kwenye network yangu kwamba mwakani namaliza. Kila mmoja alinipromise kunisaidia kupata job au kuniconnect na waajiri mbali mbali. Swala likawa ni kwamba wewe maliza tu chuo then utuambie ili tukafanyie mipango.

Kimbebe kilikuja baada ya kumaliza. Nilitulia kwanza mwezi mmoja then nikaanza kucheki walionipromise job kwamba I am available. Asee nilipigwa dana dana za kutisha na mwishowe wengine wakawa hata hawapokei simu zangu. Nikiwaibukia nyumbani au maeneo yao ya kazi wanaishia kunipa nauli ya kurudia na kuniambia ajira ngumu cha muhimu wewe endelea kumuomba Mungu. It was very disappointing situation at that time na nikafikia hatua ya kuanza kuwachukia bila sababu as if wao ndio wanaonisababishia ugumu wa kuajiriwa, hahahaaa.

Basi nikaanza kuumiza kichwa how to go about finding the job. Nikaaply sana kazi kupitia job adverts za mtandaoni lkn mimi mwenyewe nikaona as a fresh graduate I didn’t have the skills and required experiences. Nikaanza kuona hata elimu yenyewe may be course niliyosoma haina maana bora lile boom ningelitumia kwa kuanzisha hata kimradi cha kuchoma popcorn mtaani.

Hali ilikuwa mbaya to most of the graduates mana kila nikiwacheki wana nao wanalalamika kama mm tuu isipokuwa wachache sana wenye connection tena za familia zao za kuzaliwa. Hapo nikakumbuka wakati naenda kuanza form 5 way back bro wangu aliwahi kuniambia “dogo huko shule nenda kawe na marafiki wa aina mbili, either wenye akili sana darasani au wale wanaotoka kwenye familia bora”. Nilikuja kumwelewa kipindi hiki ni nini bro alichomaanisha. Kwamba wale wenye akili sana darasani watakuinfluence kufauru na wale wanaotoka maisha bora ni future asset katika connection za ajira. Sasa mimi kutoka na usela wangu mavi wa teenager sikuwa na hata mmoja kati ya hao. Roho ilikuja kuniuma zaidi nilipogundua nilipokuwa advance niligombana na jamaa mmoja ambaye kwao walikuwa wapo poa sana wa kutokea mkoa wa Iringa, nilipooulizia habari zake nikasikia kwa kipindi kile natafuta ajira alikuwa ni msimamizi wa kampuni ya usafirishaji mizogo(malori) na walikuwa na ofidi zao bandarini (clearing and forwarding). Laiti yule jamaa ningemfanya best friend ukute ingekuwa rahisi kwa yeye kunipa mchongo. Anyway, les forget about him.

Nakumbuka siku moja nikiendelea kusaga visigino katika harakati zangu za kutembeza bahasha, kwenye foleni mikamwona lecturer wangu mmoja hivi, tumuite Dr KJ (PhD ya kihaya hiyo) kwenye shangingi lake akiendeshwa na dereva wake kama kawaida. Huyu lecturer nilimkumbuka kwa sababu alikuwa na sifa sana kwenye vipindi vyake na alikuwa anafundisha somo la project Management.

Yaani huyu Muhaya alikuwa anatumia nusu ya muda wake kwenye lecture kujisifia. Ataanza kuwananga maprof kwamba japo yeye ana PhD ila hakuna prof anaemzidi akili na pesa chuo kizima, kwanza yeye anaendeshwa na mshahara anaimlipa dereva wake ni sawa na wa tutorial assistant wa pale chuo. Alikuwa mdhalilishaji sana kwa wanafunzi hususani watoto wa kike au wanaofeli somo lake. Ila watu walichompendea jamaa alikuwa sometimes anagawa sana maokoto akiwakuta wanafunzi njiani ila ndio mjue mtadhalilishwa. Jamaa alikuwa anatembea na dola au Euro akidai pesa za madafu ni nzito, hatukujua anapata wapi zile dola dola. Nakumbuka kuna semester alimlipia ada jamaa mmoja alikuwa anasoma kwa shida sana alikuwa hana boom. Alimlipia ada ya semester ya mwisho ila yule jamaa cha moto alikiona maana Dr KJ kwenye kila kipindi alichofundisha kwenye madarasa yake lazima amtolee mfano yule jamaa mpaka mlipiwa ada akawa famous chuo hahahaaa.

Basi bhana nilipomwona kwenye foleni Dr KJ vitu vingi vingi vikapita kama mshale kwenye mawazo yangu. Kwamba huyu jamaa anaweza akawa asset lkn anaweza akanidhalilisha vibaya sana na nitamuanzanje yupo kwenye gari. Je atanikumbuka maana wanafunzi tulikuwa wengi sana. Lkn nikifikiria pale geto nadaiwa kodi mwenye nyumba keshanivumilia kama two months (nilamua kukomaa mjini sikutaka kwenda mkoani). Wakati naendelea kuwaza foleni ikaanza kutembea, asee sijui ni nini kilinikuta nikajikuta naikimbilia ile gari na kwenda kuisimamia kwa mbele nikiizuia isiende huku nikimwonyeshea ishara dereva apaki pembeni. Dereva alipoona anaweka foleni akamuuliza bosi wake wafanyeje hahaaa maana nacheka kama ni mazuri. Basi Dr KJ kwa wasiwasi akamwambia aweke pembeni.

Basi nikasogea upande wa Dr KJ akawa hataki kushusha kioo, akanielekeza niende upande upande wa dereva. Nikajua tuu boss anaogopa labda nitamdhuru so he decided to sacrifice his driver- hahahaa. Basi nikaenda upande wa dereva aliposhusha kioo nikamsalimia.

Mimi: shikamoo Dr KJ

Yeye: Unanifaham?

Mimi: Ndio wewe ni mwalimu wangu wa somo flani nimemaliza mwaka jana.

Yeye: (Bado akiwa na wasiwasi) Nitaamini vipi na kwanini unanisimamisha kama jambazi?

Mimi: (Bila kujiuma uma) Naomba unisamehe sana Dr, ni kuvurugwa na hapa nimeopna kama bahati
kukuona. Dr mimi nipo katika harakati za kutafuta kazi, nimekusimamisha ili nikuacjie CV yangu maana naamini wewe network yako ni kubwa pengine unaweza ukaniconnect na wadau wako.
Yeye: (Akacheka sana huku akiniita niende upande wake). Kwa hiyo unatafuta kazi gani?

Mimi: Kwa sasa nahitaji sehemu yoyote ya kujishikiza ili nipate uzoefu, lakini uzuri wewe ni mwalimu wangu wa PM so unaweza ukaona ni wapi zile theory wapi naweza kuziapply.

Akaniangalia sana kisha akaniuliza unajua nini kuhusu project management na principles for effective project management? Nikamshushia madude kwa style ambayo nadhani ilimkamata kisawa sawa. nIkamsisitizia kwamba mimi sijawahi kushikwa kwenye somo lake. Baada ya kumjibu pale akaniambia. Mbona unaonekana una njaa sana? Shika hii nenda kale mimi nina mambo mengi sana na hapa unanichelewesha tuu. Sikupokea kwanza ile pesa ila nikamwambia Sir please just take my CV may you can see how you can help. Akaniuliza, sasa CV yako umeandika nini wakati hujawahi kufanya kazi popote? Halafu sina mda wa kutembea na makaratazi kwa gari yangu. Akawa anafunga kioo, asee nikaking’anga’ania. Akaniambia unataka nini sasa pesa nimekupa umekataa. Nikamwambia, kama huwezi kutembea na makaratasi basi naomba email address yako ili nikutumie. Akaniangaliaa, kisha akatoa business card akanipa. Mimi nikaicheki nikaona ile biz card sio yake ni ya mdada. Nikamwambia mbona sio yako. Akaniambia “vizuri sana upo makini, mpigie huyo dada simu kesho muda kama huu”. Hiyo ilikuwa ni kama saa tisa hivi. Kisha akanipa ile pesa, akasepa zake.

Mwendelezo #15
Very interesting story nipo na wewe mpaka pale utakapoweka nukta maana na mimi Jobless promax.
 
Back
Top Bottom