Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

Mambo muhimu niliyojifunza katika maisha yangu ya kuajiriwa

EPISODE 4: Avoiding taking sides amongst staff conflicts made me a hero and profesional

Maisha ya kazi pale ofisini yaliendelea huku nikiendelea kuzoeana na watu pale ofisini. Ofisi ile ilikuwa na only 5 employed staff yaani Mr KJ the boss, mimi, Mhasibu, PS na dereva. But most of the tasks involved external outsourcing. Maisha yaliendelea miezi ikakatika na ndipo nilipozidi kuzijua pia tabia za watu pale ofsini, na uhakika hata tabia zangu pia zilianza kufahamika na wengine.

Sasa nikaja kuthibitisha kwamba PS na Mhasibu ni paka na panya. Hili nilihisi siku nyingi lakini nilikuwa bado kuthibitisha. Basi wale madada kila mmoja kwa wakati wake akipata time ya kuongea na mimi basi ni kumkandia mwenzake. Kiufupi wale madada walikuwa kila mmoja anataka niwe upande wake. Yaani nilikuwa siulizi jambo la mtu ila najikuta nimeambiwa, at first nikajua ni mambo ya wanawake tu lakini as time went on nikarialize wale wadada wana biff kubwa sana. Therefore I was finding the proper moment to make it clear that I was there to work and I didn’t want to get involved in office politics.

Nilipofanya upelelezi nikaja kugundua kwamba wale watu kila mtu alikuwa na strength anazoringia pale ofisini hivyo kujiona anaweza kumvimbia mwenzake. Nilikuja kugundua kwamba yule PS alikuwa ni zaidi ya boss pale ofisini kwani maamuzi mengi ya uendeshaji wa ofisi yeye alitia mkono wake. Siku niliyokuja kujua kumbe hata ule mshahara wangu ambao ni nusu ya mshahara wa boss yeye ndio aliyemtaka boss anipatie nilipigwa ganzi ya mwili. Yaani yule PS akitaka ubaki ofsini unabaki, akitaka utimuliwe kazi unatimuliwa. Unaambiwa wengi waliopita pale kwenye position yangu na madereva waliondoka kwa sababu PS hakuwapenda hususani madada nilivosikia. Kuna hawa service providers kama ishu za internet, usafi, stationaries nk ilikuwa ili wapate kazi pale ofsini basi kwanza walimridhishe PS ndio wanapata tender.

Kwanza yule PS alikuwa PS kweli, ile pisi ilikuwa inafanana na toto za Kinyarwanda zenye mibinuko maridadi kwa nyuma halafu mavazi yake ya ofisini ukikutana nae usiku unaweza sema anaenda kujiuza. Sijui alimpa nini bosi wangu mpaka akawa ni mshauri wake mkuu unaambiwa, bora ukosane na boss unaweza kusavaivu kuliko ukosane na PS, imekula kwako.

Kwa upande wa yule Mhasibu nikaja kujua kwamba anabond kubwa sana na asilimia kubwa ya donors wa pale ofisini na aliaminika sana na board members. Yaani yule dada alikuwa ameiva kwenye kazi yake na akajijengea uaminifu mkubwa sana kwa wafadhili kiasi kwamba linapokuja swala la finance wafadhili na board members huwaambii kitu kwake yaani kauli yake ni kama sheria kwenye kusimamia mambo ya fedha. Nilisikia kuna kipindi alipigwa zengwe na PS aondoke, wafadhili baadhi wakatishia kusitisha kuprovide fedha zao endapo mhasibu yule angeondoka mpaka watakapopewa sababu genuine za kueleweka. Ngoma ikawa nzito ikabidi abakishwe. Sema yule dada hakuwaga na vinyongo na watu wengine waliopita kwenye position yangu au watu wa tendering labda uwe mbadhilifu wa fedha anakuchoma moja kwa moja sio kwa boss bali kwa wafadhili. Kifupi yule mhasibu ni kama aliwekwa pale na wafadhili ili kusimamia upigaji, so there was no way majungu ya PS yangeweza kumfukuzisha kazi.

Imagine upo kwenye situation kama iyo ambapo kila upande unataka uungane nao ili kuimarisha kambi yake. Hii niliichukulia kama changamoto kubwa sana kwangu na ukiangalia ilikuwa ni ajira yangu ya kwanza na mimi lengo langu pale lilikuwa ni kugrow ili kupata weledi wa kazi. Nikajiapiza siwezi pale kwamba siwezi haribu carrier future yangu kisa hawa madada wawili. Pale ilikuwa nikichoose upande wa PS basin ni wazi Mhasibu atanifanya adui napengine kuniharibia hata kwa wafadhili kwa mbinu yoyote maana hili nililiona liko wazi japo yeye hakuwahi kunitamkia. And viceversa, nikichagua kambi ya Mhasibu basi automatically nitamjua PS ni nani maana nitapigiwa zengwe kwa boss mpaka niseme.

I remember one day ilikuwa ijumaa, ofsini siku hiyo nilikuwa mimi na PS tu, boss na mhasibu walienda kwenye meeting wakatawanyikia huko huko. Sasa hiyo siku kuna washkaji zangu flani watatu nilipiga nao Olevel wakawa wananipigia sana tukutane maeneo ya breakpoint sio mbali na ofisi. Kipindi hicho pale breakpoint ya posta ilikuwa inabamba sana siku za ijumaa kwa sababu wafanya kazi wengi wa posta ilikuwa ni sehemu yao ya kula bata., wenyewe wakidai kusubiria foleni isogee kabla hawajarejea makwao cha ajabu wengi wanajikuta wanarejea makwao asubuhi kabisa hahaha. Basi PS akaniambia nay eye anataka kwenda akale ili asepe. Mimi nilikuwa sipendi kabisa mazoea kama hayo ya kufatana fatana naye ila aling’ang’ania sana nikaona sio kesi wacha twende.

Nakumbuka vizuri sikuhiyo PS alikuwa amevaa kijigauni kifupi ambacho kilimbana na kilichora umbo lake matata sana. Wakati tunashuka pale breakpoint (PS alikuwa anadrive jamani hahahaa nilisahau kuwaambia) kwenda kule ndani nikawa aibu naona mimi maana watu walikuwa wanatukodolea balaa nahisi mafisi ya mjini yalisema hichi kibwamdogo kinapata wapi uwezo wa kula ile mashine. Na kweli kimuonekano PS alikuwa ni wa level za juu sana ukilinganisha na mimi hahaaa.

Basi tukajoin na washkaji pale wale jamaa zangu walishoboka sana na PS. Uzuri pia PS ni mtu wa kujichanganya sana yaani dakika 0 tu ugeni umeisha na anazigida pombe vizuri tuu. Kile kikao kimeenda mpaka kama saa mbili hivi usiku ikaja proposal watu tuhame. Sasa mimi nilivoona PS amewaka kimtindo nikaona hawezi kuendesha huyu hivyo nikamshauri ndinga akaache ofisini ili tutumie usafiri wa wale jamaa zangu maana sio salama. Akanipa key nikapeleka gari yake kisha tukasepa. Kiufupi siku ile wale jamaa zangu wa mgodini walikuwa na pesa sana walikuja mjini kula bata.

Kufika mida ya saa nane usiku mimi nimechoka sasa nikawa namlazimisha PS achukue bajaji aende kwake wale jamaa wakawa bado wanataka kampani yake na PS ndio haelewi anataka aendelee kula bata. Japo alikuwa ni mtu mzima lakini nikaona siwezi kumwacha na wale majamaa ya mgodini imani yangu sikui iliwaza nini kutowaamini. Sasa PS kuna namba za nyummbani kwake ilikuwa inampigia mara kwa mara nahisi ni dada wa kazi yule alikuwa anampa maelekezo kuhusu mtoto. Lkn kuna namba nyingine ilikuwa ikimpigia anasogea pembeni anaongea kisha anarudi tunaendelea na mambo. Sasa kuna muda akawa ametoka kuongea na simu akanipa mimi nimshikie simu zake yeye akawa bize na story. Kidogo mimi nikaanza kumlazimisha tuondoke nikampandishe bajaji akalale. Kweli nikafanikiwa sasa wakati nampa zile simu zake kuna moja nikaona ipo hewani yaani alipomaliza kuongea haikukatwa na zilikuwa zimepita kama dk 40 hivi. Basi nikaikata na kila mtu akashika njia yake.

Asubuhi ya saa 12 Jumamos nikiwa nina mausingizi kibao maana nilichelewa sana kulala nikasikia simu ya boss ikiita. Kucheki nikakuta missed 3 za boss nikampigia. Alichoniambia ni maneno matano tu – Tukutane Ofisini Leo Saa2 Asubuhi. Akakata simu. Baada kama ya nusu saa PS ananipigia simu kuniambia boss kasema tukutane ofisini asubuhi na wewe ila mimi nimemwambia siendi nimechoka. Nikamwambia mimi pia kaniambia ila wewe unapata wapi ujasiri wa kumkatalia boss wako bila sababu. Nikamshawishi akakubali maana nilimwambia pia inabidi akachukue usafiri wake. Basi ikawa hivyo mimi nikajiandaa faster nikaanza kuelekea ofsini. Kwa kuwa ilikuwa Jumamosi nikapiga zangu pensi, sendo na Tshirt tu sikuwaza sana kutoka kioficial na nikajisemea some times its better to expose your few characters.

Pale ofsini kama tulitanguzana tuu na PS coinsidencily na yeye alikuwa amevaa kipensi kipedo cha blue kama pensi yangu ila juu alivaa zile makenzie enzi hizo ndio zinatoka toka tuu. PS alikuwa ni mtu wa kwenda sana na fasheni. Basi ile tunaingia tuu ofsini tunamkuta boss amekaa kwenye ofisi yangu anatafuta tafuta sijui nini kwenye desk yangu. Alipotuona tuu akakasirika sana na kutuuliza kwa hiyo mmeona kulala pamoja haitoshi mkaona mmechishe na nguo kabisa halafu mnakuja ofsini kama ofisi ya babaenu sindio? Kwanza sikumuelewa lkn ikabidi kwa nijiangalie mavazi ndio kujua wote tumevaa shorts na zote za jinsi za bluu. Nikaona leo hapa wahaya wamepanda kichwani.

Siku hiyo boss alinifokea sana kwa nini namuingilia kwenye anga zake. Kiufupi zile simu ambazo PS alikuwa anaenda kupokelea pembeni zilikuwa ni za boss. Sasa sijui alikuwa anamdanganya yupo wapi mana alikuwa alikuwa anapokelea kwenye ukimya. Sasa ile simu ambayo PS hakuikata kumbe ilikuwa ni ya boss na alivorudi palena kunipa mimi nimshikie boss alisikia na kurekodi kila kitu. Mpaka mimi navomwambia tuondoke mpaka nilivokuwa nabagain bajaj bos anasikia, so alijiaminisha mimi naingilia anga zake na jana nimekula mzigo. Duuh unajua nilipagawa sana. So akaniambia ameshaniandalia barua ya kuachishwa kazi nilipomuuliza ana hoja gani akasema wazi eti nimeshindwa kushawishi menejeiment kipindi nipo kwenye probation.

Kipindi hicho chote boss anafoka PS yupo kimya. Mimi namwangalia kwa yale macho ya kuuliza mbona upo kimya si umueleze ilivokuwa? Ni kama alinisikia. PS akamwambia tena kwa kumuita kwa jina lake huku akimlegezea sauti “KJ njoo ofsini kwako mara”. Boss wangu masikini ukali wote ukaisha akaelekea ofsini kwake kama ngamia anavoelekezwa kibla. Basi mimi nikawa nimekaa tu nimejiinamia reception wao wapo ofsini kwa boss. Wamekaa huko kama dakika 40 nzima mara PS akatoka akaniita. Nikaingia kwa hofu sana. Chaajabu boss alikuwa mpole sana na akaniomba msamaha kwa kunifikiria vibaya na eti ananishukuru kwa kuwa muungwana kwa PS wake. Akaongea mambo mengi lakini kubwa na msisitizo alinipiga mkwara mzito kwamba hawezi hata siku moja kukubali pusi yoyote (alitumia neon hilo hilo pusi) kuingia kwenye 18 zake kwa huyo PS. Na akasema tuongee tu kama wanaume yeye huyo PS wake amemgharimia vitu vingi sana ikiwemo mjengo (ambao umeshakamilika lkn PS bado hajaamia), usafiri na bills zote za mjini. Na akanambia ananiambia hayo kwa sababu anaamini mimi nipo smart kichwani hivyo hataki kuniopoteza na anamini nitakuwa na msaada kwenye ile ofisi. Ingekuwa mimi ni kama pusi wengine asingesubiri hata tuonane ofisini kunipa nafasi ya kujitetea angenitimua job kwenye simu tuu kama alivowafanyia wengi tuu waliopita.

Basi kikao kikaisha hivyo sasa sijuiPS alimwambia nini kule ndani wakati mimi sipo. Mimi nikaaga pale nikaondoka zangu wao nikawaacha. Ila nilikuwa na mawazo sana kwa sababu nikaona pale ofsini panatakiwa uishi kwa akili sana yaani vibiff vya ajabu ajabu sana na kila mtu anataka uwe upande wake. Maana wakati nimetoka boss alinitumia meseji iliyosomeka “nimekusamehe wewe endelea kufanya kazi kwa bidii na kama sipo ofisini nataka umchunguze …….. (PS) mienendo yake kisha unijulise”. Nikaona huu sasa sio weledi I have to do something about this.

Kwa kawaida pale ofsini kunakuwaga na Monday briefing sessions ambapo kama boss akiwepo tunapeana updates za wiki iiyopita na plan for the due week. Bahati nzuri next Monday since hiyo saga yangu ya PS na boss itokee tulifanya hiyo meeting. Tulipeana updates pale na plan za wiki then kwenye ile session ya mengineyo nikanyoosha mkono nikaruhusiwa, Nikasema leo liwalo na liwe.

Kwanza niliwashukuru kwa kunipokea pale kazini na ushirikiano walionipa kwa kipindi chote hapo kazini. Boss aliposikia hiyo hiyo intro akashtuka sana akaniuliza “Taidume unataka kuacha kazi sababu ya mambo yale ya jana?” ni kama aliropoka. Hii kauli ilimfanya mhasibu ashangae na kuuliza kwani jana kilitokea nini boss? Kabla hajajibu boss mimi nikaendelea. Hapana boss siwezi kuacha kazi kwa sasa kwani bado napenda kufanya kazi hapa ila nataka tu kuweka msimamo wangu sawa ili kuweka mazingira yangu ya kazi mazuri. Boss akaniuliza una maana gani? Nikamjibu, kwanza boss jana nimefurahi sana kwa kunielewesha ukweli na hii imenifanya kuwa huru. Haya maneno niliyaongea makusudi mbele ya mhasibu kwa sababu ni zaidi ya mara tatu aliwahi kuniambia anatafuta timing nzuri awachane PS na boss waache kuchanganya mambo ya mahusiano yao na kazi, yaani kama wanamahusiano wawe na mipaka kwani imefikia hatua PS ana maamuzi unprofessional yanayoathiri shirika.

Basi nikaendelea. “Najua mhasibu wewe unafahamu mahusiano ya PS na boss, najua pia boss unafahamu biff la chini chini lililopo baina ya PS na Mhasibu, lakini pia najua wote PS na Mhasibu mnajaribu kunishawishi ili niwe upande wake, na pia najua ni kwa nanmna gani PS alivo na ushawishi kwako bosi. Sasa haya mazingira kwakweli yananifanya mimi kufanya kazi kwenye mazingira magumu mno. Natamani kufanya kazi kwenye mazingira ambayo yatawezesha mimi kuendelea kujifunza na kufanya kazi kwa kushirikiana.

Nikaanza kumsifia mmoja mmoja pale mchango wake katika ufanyaji kazi wangu pale. Nikaanza na boss. Nikamwambia boss wewe unajua ulikonitoa nilikua hapa nikiwa sina skills zozote lakini leo hii angalau ninaweza kujimudu katika majukumu yangu na CV yangu imeboreka. Bado nahitaji kujifunza vitu vingi sana kutoka kwako kwani wewe umekuwa role model wangu kwa vitu vingi sana professionally. Kwa mHasibu nikamwambia napenda sana jinsi anavopangilia mambo yake ya kazi kwani uko very smart. Kwako wewe A ni A na B ni B umenifundisha kunyooka na kusimamia weledi kwenye kila jambo hata likiwa dogo. PS naye nikamwambia asione yeye kama hana msaada kwangu may be hajui tuu. Nikamwambia impression aliyonipa siku ya kwanza jinsi alivonipokea ilinifanya njione pale ni nyumbani. Nikamwambia ule muda anaotumia kunisaidia kuchakua chakua kule kwenye mafaili kama kuna taarifa nazitafuta unaiokolea mambo mengi sana na muda. Niliongea kwa hisia sana siku ile vitu vinavyonikwaza mpaka kupelekea mhasibu na PS kulengwa lengwa na machozi. Mwisho nikawaambia as for me I will never choose any side for personal interest, but I will always be cooperative to the team for organization interests.

Boss akaniangaliaaa mwisho akasema mwingine mwenye dukuduku. Asee yule mhasibu alivunja ukimya alifunguka mambo mengi sana mpaka alilia sana tukaanza kubembeleza. Tena aliyembembeleza sana alikuwa ni PS walikuambatiana wakalia hapo huku mimi na boss tunawaangalia tuu. Badae wakaombana misamaha pale, sasa sijui ilitoka moyoni au midomoni. Mwisho boss aliuliza nini kifanyike ili kuboresha utendaji wa ofisi. Tukatoa toa proposal pale tukakubaliana tufanyie kazi mikakati tuliyojiwekea. Kwenye kufunga kikao boss alinishukuru sana kwa kuibua hoja hiyo na kwa kuwa kikao kikao kilitumia muda mrafu mpaka mchana boss akaoendekeza tukale lunch nje ya office. Iilkuwa poa sana maisha baada ya hapo kama kulikuwa na usnitch basi ni ule wa chini chini sana.

Don’t miss episode 5, to see how honesty na kutokuwa na tamaa kulivonipa another job connection
Oyaa wee
 
Kujishusha ni kujinyenyekeza ili uweze kufanikisha mambo flani katika maisha. Hii inasaidia maana wengi waliofanikiwa wanapenda kunyenyekewa so ni rahisi ku linki nao ukiwa mnyenyekevu.

Kujidhalilisha ni kujitoa ufahamu ili kufanikisha mambo katika maisha. Hii ni kwenda extra mile kufanya jambo lolote linaloweza hata kutweza utu wako ilimradi ufurahishe nafsi ya mtu aliyekuzidi ili akusaidie kwa mambo flani katika maisha.
Big up sana hapa
 
Tofautisha Arrogance na emotions intelligence , watu wanaojishusha wanakuaga na emotions intelligence ukiwa na akili Ila hauna emotions intelligence basi huwezi kuwa MTU mwenye mafanikio makubwa maana maisha yanahitaji Sana kiwango kikubwa cha emotions intelligence na sio akili tu
Kwa utaalamu wangu mdogo wa sailolojia, huyu mtoa mada ana adversorial intelligence, yaani uwezo wa kupambana katika hali zote za kimaisha.
 
Mkuu TAI DUME story yako ni nzuri sana na imejaa mafundisho kwa watu wa aina mbalimbali. Ila nakushauri kwamba ongea yote ila usisahau kipengele cha kula tunda kimasihara, ni kipengele muhimu sana kwa story zinazobamba hapa Jf. Ongelea hata mahusiano ya boss na PS au unda story ya aina hiyo wewe na demu wako wa kitaa au wateja wenu hapo kazini ilimradi kisikosekane tu.
Asante.
Mnawaza kugegedana tu [emoji23][emoji23]. stori inaweza kuwa nzuri bila ya mambo ya kugegedana mkuu TAI DUME baki kwenye kiini cha uzi
 
EPISODE 4: Avoiding taking sides amongst staff conflicts made me a hero and profesional

Maisha ya kazi pale ofisini yaliendelea huku nikiendelea kuzoeana na watu pale ofisini. Ofisi ile ilikuwa na only 5 employed staff yaani Mr KJ the boss, mimi, Mhasibu, PS na dereva. But most of the tasks involved external outsourcing. Maisha yaliendelea miezi ikakatika na ndipo nilipozidi kuzijua pia tabia za watu pale ofsini, na uhakika hata tabia zangu pia zilianza kufahamika na wengine.

Sasa nikaja kuthibitisha kwamba PS na Mhasibu ni paka na panya. Hili nilihisi siku nyingi lakini nilikuwa bado kuthibitisha. Basi wale madada kila mmoja kwa wakati wake akipata time ya kuongea na mimi basi ni kumkandia mwenzake. Kiufupi wale madada walikuwa kila mmoja anataka niwe upande wake. Yaani nilikuwa siulizi jambo la mtu ila najikuta nimeambiwa, at first nikajua ni mambo ya wanawake tu lakini as time went on nikarialize wale wadada wana biff kubwa sana. Therefore I was finding the proper moment to make it clear that I was there to work and I didn’t want to get involved in office politics.

Nilipofanya upelelezi nikaja kugundua kwamba wale watu kila mtu alikuwa na strength anazoringia pale ofisini hivyo kujiona anaweza kumvimbia mwenzake. Nilikuja kugundua kwamba yule PS alikuwa ni zaidi ya boss pale ofisini kwani maamuzi mengi ya uendeshaji wa ofisi yeye alitia mkono wake. Siku niliyokuja kujua kumbe hata ule mshahara wangu ambao ni nusu ya mshahara wa boss yeye ndio aliyemtaka boss anipatie nilipigwa ganzi ya mwili. Yaani yule PS akitaka ubaki ofsini unabaki, akitaka utimuliwe kazi unatimuliwa. Unaambiwa wengi waliopita pale kwenye position yangu na madereva waliondoka kwa sababu PS hakuwapenda hususani madada nilivosikia. Kuna hawa service providers kama ishu za internet, usafi, stationaries nk ilikuwa ili wapate kazi pale ofsini basi kwanza walimridhishe PS ndio wanapata tender.

Kwanza yule PS alikuwa PS kweli, ile pisi ilikuwa inafanana na toto za Kinyarwanda zenye mibinuko maridadi kwa nyuma halafu mavazi yake ya ofisini ukikutana nae usiku unaweza sema anaenda kujiuza. Sijui alimpa nini bosi wangu mpaka akawa ni mshauri wake mkuu unaambiwa, bora ukosane na boss unaweza kusavaivu kuliko ukosane na PS, imekula kwako.

Kwa upande wa yule Mhasibu nikaja kujua kwamba anabond kubwa sana na asilimia kubwa ya donors wa pale ofisini na aliaminika sana na board members. Yaani yule dada alikuwa ameiva kwenye kazi yake na akajijengea uaminifu mkubwa sana kwa wafadhili kiasi kwamba linapokuja swala la finance wafadhili na board members huwaambii kitu kwake yaani kauli yake ni kama sheria kwenye kusimamia mambo ya fedha. Nilisikia kuna kipindi alipigwa zengwe na PS aondoke, wafadhili baadhi wakatishia kusitisha kuprovide fedha zao endapo mhasibu yule angeondoka mpaka watakapopewa sababu genuine za kueleweka. Ngoma ikawa nzito ikabidi abakishwe. Sema yule dada hakuwaga na vinyongo na watu wengine waliopita kwenye position yangu au watu wa tendering labda uwe mbadhilifu wa fedha anakuchoma moja kwa moja sio kwa boss bali kwa wafadhili. Kifupi yule mhasibu ni kama aliwekwa pale na wafadhili ili kusimamia upigaji, so there was no way majungu ya PS yangeweza kumfukuzisha kazi.

Imagine upo kwenye situation kama iyo ambapo kila upande unataka uungane nao ili kuimarisha kambi yake. Hii niliichukulia kama changamoto kubwa sana kwangu na ukiangalia ilikuwa ni ajira yangu ya kwanza na mimi lengo langu pale lilikuwa ni kugrow ili kupata weledi wa kazi. Nikajiapiza siwezi pale kwamba siwezi haribu carrier future yangu kisa hawa madada wawili. Pale ilikuwa nikichoose upande wa PS basin ni wazi Mhasibu atanifanya adui napengine kuniharibia hata kwa wafadhili kwa mbinu yoyote maana hili nililiona liko wazi japo yeye hakuwahi kunitamkia. And viceversa, nikichagua kambi ya Mhasibu basi automatically nitamjua PS ni nani maana nitapigiwa zengwe kwa boss mpaka niseme.

I remember one day ilikuwa ijumaa, ofsini siku hiyo nilikuwa mimi na PS tu, boss na mhasibu walienda kwenye meeting wakatawanyikia huko huko. Sasa hiyo siku kuna washkaji zangu flani watatu nilipiga nao Olevel wakawa wananipigia sana tukutane maeneo ya breakpoint sio mbali na ofisi. Kipindi hicho pale breakpoint ya posta ilikuwa inabamba sana siku za ijumaa kwa sababu wafanya kazi wengi wa posta ilikuwa ni sehemu yao ya kula bata., wenyewe wakidai kusubiria foleni isogee kabla hawajarejea makwao cha ajabu wengi wanajikuta wanarejea makwao asubuhi kabisa hahaha. Basi PS akaniambia nay eye anataka kwenda akale ili asepe. Mimi nilikuwa sipendi kabisa mazoea kama hayo ya kufatana fatana naye ila aling’ang’ania sana nikaona sio kesi wacha twende.

Nakumbuka vizuri sikuhiyo PS alikuwa amevaa kijigauni kifupi ambacho kilimbana na kilichora umbo lake matata sana. Wakati tunashuka pale breakpoint (PS alikuwa anadrive jamani hahahaa nilisahau kuwaambia) kwenda kule ndani nikawa aibu naona mimi maana watu walikuwa wanatukodolea balaa nahisi mafisi ya mjini yalisema hichi kibwamdogo kinapata wapi uwezo wa kula ile mashine. Na kweli kimuonekano PS alikuwa ni wa level za juu sana ukilinganisha na mimi hahaaa.

Basi tukajoin na washkaji pale wale jamaa zangu walishoboka sana na PS. Uzuri pia PS ni mtu wa kujichanganya sana yaani dakika 0 tu ugeni umeisha na anazigida pombe vizuri tuu. Kile kikao kimeenda mpaka kama saa mbili hivi usiku ikaja proposal watu tuhame. Sasa mimi nilivoona PS amewaka kimtindo nikaona hawezi kuendesha huyu hivyo nikamshauri ndinga akaache ofisini ili tutumie usafiri wa wale jamaa zangu maana sio salama. Akanipa key nikapeleka gari yake kisha tukasepa. Kiufupi siku ile wale jamaa zangu wa mgodini walikuwa na pesa sana walikuja mjini kula bata.

Kufika mida ya saa nane usiku mimi nimechoka sasa nikawa namlazimisha PS achukue bajaji aende kwake wale jamaa wakawa bado wanataka kampani yake na PS ndio haelewi anataka aendelee kula bata. Japo alikuwa ni mtu mzima lakini nikaona siwezi kumwacha na wale majamaa ya mgodini imani yangu sikui iliwaza nini kutowaamini. Sasa PS kuna namba za nyummbani kwake ilikuwa inampigia mara kwa mara nahisi ni dada wa kazi yule alikuwa anampa maelekezo kuhusu mtoto. Lkn kuna namba nyingine ilikuwa ikimpigia anasogea pembeni anaongea kisha anarudi tunaendelea na mambo. Sasa kuna muda akawa ametoka kuongea na simu akanipa mimi nimshikie simu zake yeye akawa bize na story. Kidogo mimi nikaanza kumlazimisha tuondoke nikampandishe bajaji akalale. Kweli nikafanikiwa sasa wakati nampa zile simu zake kuna moja nikaona ipo hewani yaani alipomaliza kuongea haikukatwa na zilikuwa zimepita kama dk 40 hivi. Basi nikaikata na kila mtu akashika njia yake.

Asubuhi ya saa 12 Jumamos nikiwa nina mausingizi kibao maana nilichelewa sana kulala nikasikia simu ya boss ikiita. Kucheki nikakuta missed 3 za boss nikampigia. Alichoniambia ni maneno matano tu – Tukutane Ofisini Leo Saa2 Asubuhi. Akakata simu. Baada kama ya nusu saa PS ananipigia simu kuniambia boss kasema tukutane ofisini asubuhi na wewe ila mimi nimemwambia siendi nimechoka. Nikamwambia mimi pia kaniambia ila wewe unapata wapi ujasiri wa kumkatalia boss wako bila sababu. Nikamshawishi akakubali maana nilimwambia pia inabidi akachukue usafiri wake. Basi ikawa hivyo mimi nikajiandaa faster nikaanza kuelekea ofsini. Kwa kuwa ilikuwa Jumamosi nikapiga zangu pensi, sendo na Tshirt tu sikuwaza sana kutoka kioficial na nikajisemea some times its better to expose your few characters.

Pale ofsini kama tulitanguzana tuu na PS coinsidencily na yeye alikuwa amevaa kipensi kipedo cha blue kama pensi yangu ila juu alivaa zile makenzie enzi hizo ndio zinatoka toka tuu. PS alikuwa ni mtu wa kwenda sana na fasheni. Basi ile tunaingia tuu ofsini tunamkuta boss amekaa kwenye ofisi yangu anatafuta tafuta sijui nini kwenye desk yangu. Alipotuona tuu akakasirika sana na kutuuliza kwa hiyo mmeona kulala pamoja haitoshi mkaona mmechishe na nguo kabisa halafu mnakuja ofsini kama ofisi ya babaenu sindio? Kwanza sikumuelewa lkn ikabidi kwa nijiangalie mavazi ndio kujua wote tumevaa shorts na zote za jinsi za bluu. Nikaona leo hapa wahaya wamepanda kichwani.

Siku hiyo boss alinifokea sana kwa nini namuingilia kwenye anga zake. Kiufupi zile simu ambazo PS alikuwa anaenda kupokelea pembeni zilikuwa ni za boss. Sasa sijui alikuwa anamdanganya yupo wapi mana alikuwa alikuwa anapokelea kwenye ukimya. Sasa ile simu ambayo PS hakuikata kumbe ilikuwa ni ya boss na alivorudi palena kunipa mimi nimshikie boss alisikia na kurekodi kila kitu. Mpaka mimi navomwambia tuondoke mpaka nilivokuwa nabagain bajaj bos anasikia, so alijiaminisha mimi naingilia anga zake na jana nimekula mzigo. Duuh unajua nilipagawa sana. So akaniambia ameshaniandalia barua ya kuachishwa kazi nilipomuuliza ana hoja gani akasema wazi eti nimeshindwa kushawishi menejeiment kipindi nipo kwenye probation.

Kipindi hicho chote boss anafoka PS yupo kimya. Mimi namwangalia kwa yale macho ya kuuliza mbona upo kimya si umueleze ilivokuwa? Ni kama alinisikia. PS akamwambia tena kwa kumuita kwa jina lake huku akimlegezea sauti “KJ njoo ofsini kwako mara”. Boss wangu masikini ukali wote ukaisha akaelekea ofsini kwake kama ngamia anavoelekezwa kibla. Basi mimi nikawa nimekaa tu nimejiinamia reception wao wapo ofsini kwa boss. Wamekaa huko kama dakika 40 nzima mara PS akatoka akaniita. Nikaingia kwa hofu sana. Chaajabu boss alikuwa mpole sana na akaniomba msamaha kwa kunifikiria vibaya na eti ananishukuru kwa kuwa muungwana kwa PS wake. Akaongea mambo mengi lakini kubwa na msisitizo alinipiga mkwara mzito kwamba hawezi hata siku moja kukubali pusi yoyote (alitumia neon hilo hilo pusi) kuingia kwenye 18 zake kwa huyo PS. Na akasema tuongee tu kama wanaume yeye huyo PS wake amemgharimia vitu vingi sana ikiwemo mjengo (ambao umeshakamilika lkn PS bado hajaamia), usafiri na bills zote za mjini. Na akanambia ananiambia hayo kwa sababu anaamini mimi nipo smart kichwani hivyo hataki kuniopoteza na anamini nitakuwa na msaada kwenye ile ofisi. Ingekuwa mimi ni kama pusi wengine asingesubiri hata tuonane ofisini kunipa nafasi ya kujitetea angenitimua job kwenye simu tuu kama alivowafanyia wengi tuu waliopita.

Basi kikao kikaisha hivyo sasa sijuiPS alimwambia nini kule ndani wakati mimi sipo. Mimi nikaaga pale nikaondoka zangu wao nikawaacha. Ila nilikuwa na mawazo sana kwa sababu nikaona pale ofsini panatakiwa uishi kwa akili sana yaani vibiff vya ajabu ajabu sana na kila mtu anataka uwe upande wake. Maana wakati nimetoka boss alinitumia meseji iliyosomeka “nimekusamehe wewe endelea kufanya kazi kwa bidii na kama sipo ofisini nataka umchunguze …….. (PS) mienendo yake kisha unijulise”. Nikaona huu sasa sio weledi I have to do something about this.

Kwa kawaida pale ofsini kunakuwaga na Monday briefing sessions ambapo kama boss akiwepo tunapeana updates za wiki iiyopita na plan for the due week. Bahati nzuri next Monday since hiyo saga yangu ya PS na boss itokee tulifanya hiyo meeting. Tulipeana updates pale na plan za wiki then kwenye ile session ya mengineyo nikanyoosha mkono nikaruhusiwa, Nikasema leo liwalo na liwe.

Kwanza niliwashukuru kwa kunipokea pale kazini na ushirikiano walionipa kwa kipindi chote hapo kazini. Boss aliposikia hiyo hiyo intro akashtuka sana akaniuliza “Taidume unataka kuacha kazi sababu ya mambo yale ya juzi?” ni kama aliropoka. Hii kauli ilimfanya mhasibu ashangae na kuuliza kwani juzi kilitokea nini boss? Kabla hajajibu boss mimi nikaendelea. Hapana boss siwezi kuacha kazi kwa sasa kwani bado napenda kufanya kazi hapa ila nataka tu kuweka msimamo wangu sawa ili kuweka mazingira yangu ya kazi mazuri. Boss akaniuliza una maana gani? Nikamjibu, kwanza boss juzi nimefurahi sana kwa kunielewesha ukweli na hii imenifanya kuwa huru. Haya maneno niliyaongea makusudi mbele ya mhasibu kwa sababu ni zaidi ya mara tatu aliwahi kuniambia anatafuta timing nzuri awachane PS na boss waache kuchanganya mambo ya mahusiano yao na kazi, yaani kama wanamahusiano wawe na mipaka kwani imefikia hatua PS ana maamuzi unprofessional yanayoathiri shirika.

Basi nikaendelea. “Najua mhasibu wewe unafahamu mahusiano ya PS na boss, najua pia boss unafahamu biff la chini chini lililopo baina ya PS na Mhasibu, lakini pia najua wote PS na Mhasibu mnajaribu kunishawishi ili niwe upande wake, na pia najua ni kwa nanmna gani PS alivo na ushawishi kwako bosi. Sasa haya mazingira kwakweli yananifanya mimi kufanya kazi kwenye mazingira magumu mno. Natamani kufanya kazi kwenye mazingira ambayo yatawezesha mimi kuendelea kujifunza na kufanya kazi kwa kushirikiana.

Nikaanza kumsifia mmoja mmoja pale mchango wake katika ufanyaji kazi wangu pale. Nikaanza na boss. Nikamwambia boss wewe unajua ulikonitoa nilikua hapa nikiwa sina skills zozote lakini leo hii angalau ninaweza kujimudu katika majukumu yangu na CV yangu imeboreka. Bado nahitaji kujifunza vitu vingi sana kutoka kwako kwani wewe umekuwa role model wangu kwa vitu vingi sana professionally. Kwa mHasibu nikamwambia napenda sana jinsi anavopangilia mambo yake ya kazi kwani uko very smart. Kwako wewe A ni A na B ni B umenifundisha kunyooka na kusimamia weledi kwenye kila jambo hata likiwa dogo. PS naye nikamwambia asione yeye kama hana msaada kwangu may be hajui tuu. Nikamwambia impression aliyonipa siku ya kwanza jinsi alivonipokea ilinifanya njione pale ni nyumbani. Nikamwambia ule muda anaotumia kunisaidia kuchakua chakua kule kwenye mafaili kama kuna taarifa nazitafuta unaiokolea mambo mengi sana na muda. Niliongea kwa hisia sana siku ile vitu vinavyonikwaza mpaka kupelekea mhasibu na PS kulengwa lengwa na machozi. Mwisho nikawaambia as for me I will never choose any side for personal interest, but I will always be cooperative to the team for organization interests.

Boss akaniangaliaaa mwisho akasema mwingine mwenye dukuduku. Asee yule mhasibu alivunja ukimya alifunguka mambo mengi sana mpaka alilia sana tukaanza kubembeleza. Tena aliyembembeleza sana alikuwa ni PS walikuambatiana wakalia hapo huku mimi na boss tunawaangalia tuu. Badae wakaombana misamaha pale, sasa sijui ilitoka moyoni au midomoni. Mwisho boss aliuliza nini kifanyike ili kuboresha utendaji wa ofisi. Tukatoa toa proposal pale tukakubaliana tufanyie kazi mikakati tuliyojiwekea. Kwenye kufunga kikao boss alinishukuru sana kwa kuibua hoja hiyo na kwa kuwa kikao kikao kilitumia muda mrafu mpaka mchana boss akaoendekeza tukale lunch nje ya office. Iilkuwa poa sana maisha baada ya hapo kama kulikuwa na usnitch basi ni ule wa chini chini sana.

Don’t miss episode 5, to see how honesty na kutokuwa na tamaa kulivonipa another job connection
Very interesting
 
Here i stand

Hapo kwenye training upewe wewe tena kwa kustukiza unaweza kuomba sala moja hiyo ukahisi hii sala/dua Mungu pekee ndiye aliye sikia hata masikio yako unaweza kusema hayajui chochote.

Tuzidi kupambana
 
giphy (1).gif
 
Nakuomba usiweke kula tunda kimasiahara,usiwape watu sex emotion vibration frequency please utaonekana wa tofauti kidogo. Mana maisha yetu sio kuwa tunahitaji ngono Bali how to survive during dangerous situation,how to bear with stressful situation like uliyoyapitia
 
Mkuu mimi nimepata mawaidha ya tajiri maarufu Ali Mufuruki akiwaasa graduates kujishusha ili kupata angalau sehemu ya kuanzia.

Aliwaambia graduates wafanye kazi, hata kama ni kuosha magari mjini, ilimradi wanajua mpango wao ni kufanya nini kuitoa katika maisha. Wasione aibu kufanya kazi yenye maslahi kwa sababu wao ni graduates.

Na nishaishi maisha ya aina zote ya kwetu ushuani na Uswahilini nilikojitosa tu kuona maisha, nikafunga mkanda mpaka New York City kutafuta maisha bila kumjua mtu.

Kwa hivyo, somo la kujishusha katika maisha ili kupata pa kuanzia, nalielewa sana.

Nishawahi kukaa sehemu ambazo wale watu wa pale wangejua mimi ni nani wangenichukulia tofauti kabisa, lakini mimi hata sikutoa credentials zangu nilikuwa nimejishusha tu, na hata hapo kuna watu walikuwa wananiangalia kimagutu magutu wanaona huyu mbona kama hapa kajiegesha tu lakini si wa hapa?

Kumbe nilikuwa nasoma tu katika darasa la maisha.[emoji16][emoji16]
Ee bana mkuu nime kuelewa sana kwa ushauri huu.

Noted..[emoji3578][emoji119]
 
Back
Top Bottom