EPISODE 10: Get ready for unexpected
Story Interlude…….
Before sijaendelea na stori yangu naomba kusema hili. Kuna baadhi ya watu wananiuliza hapa jukwaani na wengine kunijia PM kutaka kujua kwamba inaonekana niliwahi kupata pesa nyingi kwanini sikufikiria au sifikirii kujiajiri? Najua wapo wengine wengi ambao wanajiuliza hilo swali ila wameamua tu kupita kimya kimya.
Sasa ipo hivi, kwanza kabisa katika watu ambao wanaoamini katika “be employed with a plan B” mimi ni mmoja wao. Siwezi kuzungumzia hapa kuhusu kushika pesa au kutoshika pesa lakini nitazungumzia mtazamo na uzoefu wangu katika hiyo be employed with a plan B. Kipindi nipo ajira tofauti tofauti nilishajaribu sana hizo plan B, kwamba kutengeneza kipato nje ya kazi yangu. Kama nilivoeleza na nitakavyoendelea kuelezea huko mbele kazi zangu kwa asilimia 60 zilikuwa ni za kusafiri safari sana, So fursa niliyoiona kwanza kwa haraka ni kulima kwa kukodisha au kununua mashamba huko vijijini. Naweza kusema nimelimisha sana mazao tofauti tofauti lakini kwakweli kazi ya kulima au kulimisha inataka kwanza usimamizi wa madhubuti sana. Sasa kwangu mimi ilikuwa ngumu sana kwa sababu leo nipo kesho sipo unaacha wasimamizi unaowaamini kule shamba lkn mwisho wa siku hasara tuu.
Lakini pia nilijaribu baadhi ya biashara kwa hapa mjini lakini pia usimamizi ulinigharimu. Kingine nilichogundua asee hakuna mtu anafanikiwa kwa kusomea au kuiga kuwa mfanyabiashara isipokuwa bishara ni inner motive ambayo mtu anakuwa nayo. Labda mtu akose option kabisa ya kuajiriwa ndio anaweza akaforce akawa mfanya biashara mzuri maana hana option.
Ukiwa na inner motive ya kufanya biashara hakuna kitakachokuzuia hata kusafiri kikazi hakuwezi kuwa tatizo sana lakini kwa mimi vingi nilivyojaribu vilikufa au ilikuwa ni loss tuu. Kwahiyo kama wewe umejaaliwa hiyo inner motive na umeajiriwa unaweza kuwa na mafanikio sana kwa sababu kipato unachopata kwenye kuajiriwa kinabust biashara zakko.
Kwahiyo ndugu zangu this is not an excuse lakini tunakumbushana tu binadamu tumeumbwa tofauti sana lakini pia tumelelewa kwenye mazingira tofauti. Nyie wenyewe mashahidi, hata humu ndani kuna nyuzi zinaanzishwa mtu ana milioni 100 lkni hajui afanye biashara gani wakati huo huo kuna watu wana nyuzi humu wanatafuta laki2 mtaji ili waimplement project zao watoboe maisha. Pia Hapa JF nyuzi kibao zimeanzishwa kushangaa hao viongozi wanaotuimbia mahuburi kila siku watu wafikirie kujiajiri na wakati wenyewe wakitumbuliwa hawajiari ila wanatega kunyenyekea teuzi zingine. Hapo utaona kwamba sio kwamba watu hawajui umuhimu wa kuwa na plan B lkini ile inner motive ni tatizo. Ni mtazamo tuu huu jamani. Kwa hiyo wandugu bado natafuta ajira hahahaa
OK, The chill time's interlude done, let's switch it up and get down to business. Nilisema hapo juu expect the unexpected eeh? Yes, ujue kwenye haya maisha sometimes mtu unakuwa unapanga mipango yako na kuwa namategemeo makubwa sana lakini unachokuja kukutana ni kinyume kabisa na matarajio yako. Wewe unapanga hili lakini unapigwa na kitu kizito ambacho huku tarajia kabisa.
Kama nilivodokeza huko juu kwenye maelezo yangu kwamba pale ofsini ukifauru probation unapewa mkataba wa miaka miwili ambao unaweza kurenewkila baada ya miaka miwili kulingana na uhitaji wa ofisi. Mashirika mengi tu haya makubwa yasiyo ya kiserikali wanafanya hivi hata haya international. Na kwa taratibu za pale ofisini ilikuwa ukifauru kurenew mkataba mara mbili yaani ufanye nao kazi kwa miaka minne na kuendelea huwa wanakupa zawadi nzuri tuu ya fedha nadhani ilikuwa ni motivation ya kuwafanya watu wabaki pale kwa muda mrefu japo kutimuana kulikua nje nje kama usipoenda sawa na taratibu za ofisi.
Basi mimi nashukuru Mungu nilipiga mzigo kwa muda wa miaka minne yaani nilifanikiwa kurenew mkataba mara moja. Sasa kuna kipindi nikaona huku kwenye ma NGO ni kama job security inakuwa ndogo sana, maana unaweza mwenyewe ukajidamka asubuhi, ukanyoosha, ukafika job ukakuta barua kutoka kwa HR kwamba kazi basi. Kwahiyo nikaanza kufikiria kutafuta kazi serkalini kwa kuamini kwamba kule kuna pensionable employment yaani ajira ya kudumu. Halafu yale mazingira very hectic ya kazi nikawa naona kama watu wa government wanakula sana shushu basi nikawa nawatamani sana. Maana mtu unakosa hata muda wa kusimamia mambo yako muhimu hata ujenzi unawea ukajikuta kwa sehemu kubwa ubawaacha mafundi wanajenga bila uwepo wako. Basi bhana Kwa kuwa sikuwa na presha basi nikawa natafuta kazi huku sina haraka kihivyo nikawa navizia zile nafasi ambazo naona nazihitaji ndio naaply.
Mungu wa mbinguni asivyo Athumani na wala haishi Kigamboni, ikatokea kwamba miezi miwili kabla ya kurenew mkataba wangu yaani nimalize miaka minne ili kama menejiment wataridhika na mimi basi nindelee nitimize miaka sita nikapata mchongo serikalini tena kwenye hizi idara ambazo zinajiendesha zenyewe mfano wa TRA, TPDC, TCRA, TBS, BRELA etc. Kuna moja hapo ndio nilipata tena ilikuwa ni kitengo cha elimu kwa umma ni shavu ambalo lilikuwa na safari nyingi maana ilikuwa ni kuzunguka mikoani kuelimisha watu maswala yanayohusiana na idara husika. Kwakweli ilikuwa na nafasi nzuri sana ambayo sikujiuliza mara mbili.
Nikaitaarfu menejimenti kwamba sitarenew tena mkataba. Nakumbuka line meneja wangu alisikitika sana maana mimi nilikuwa ni kati ya majembe yake aliyokuwa anayategemea katika kurescue challenged situation. Hapa nimekumbuka ishu moja nakumbuka kuna siku nililala au nilitoka ofsini saa kumi alfajiri kisa kurescue situation.
Ilikuwa hivi, boss kubwa la pale ofsini alienda Canada kweny meeting na donors sasa kwa kuwa ile ofisi yetu ilikuwa ni moja ya shirika linalofanya vizuri basi wakamwalika boss kubwa aende huko kutoa presentation namna gani tuanvofanya kazi mpaka kutoa matokeo makubwa. Sasa boss kubwa yeye alikuwa amejiandaa zile issue strategic zaidi kumbe wale donors walikuwa wanataka vitu ambavyo kwa boss kubwa vilikuwa ni minor sana nap engine vingempa shida kuvijibia kikamilifu labda kama angesoma maripoti ya miaka ya nyuma.
Sasa alipomaliza presentation yake inaonekana nwakamshooti maswali ambayo yalihitaji zaidi mtu anaeenda sana field ili kutoa majibu ya uhakika. Bosikubwa akamcheki line meneja kama vipi amwandalie baadhi ya majibu. Sasa muda huo ilikuwa ni muda wa kama saa moja ousiku watu ndio tunajiandaa kutoka ofsini na wengine wameshaondoka. Nadhani kwa kule Canada ilikuwa ndio asubuhi watu ndio wanaaza majukumu yao ya kikazi. Mara line manager akanipa simu niongee na bosskubwa jamaa akanielekeza pale ishu anazozitaka nimwandalie then nimtumie kwa email. Mimi nikamtumia fasta nikawa naondoka. Wakati nimshafika nje ya ofisi mara naona bosskubwa ananipigia wasapu kupokea ananiomba nimtafutie tena baadi ya taarifa. Nikalaani sana kwanini nilikuwa hewani wasapu hahaaa ila nikageuza sikuwa na jinsi. Sasa ile nitumie taarifa hii mara ile ikawa haiishi uzuri zile data mimi nilikuwa nazo. Basi nikamwambia bosskubwa kama vipi waniunge mimi kwa skype nikiwa pale ofsini ili tusaidie kuwajibu. Boss kubwa akaniuliza kama nina uhakika sita mwangusha, nikamwambia kwani hizo info si ndio mimi ambazo ninampatia, lakini nikashindwa tu kumwambia mbona wewe unajikanyaga kanyaga tuu huko hahaha. (Jokes, ofcourse I respect the na amekuwa role model wangu sana na alishalamba uteuzi serikalini mda mrefu tuu) kwenye ministerial level)
Basi akanicoonect pale yale majamaa meupe yakaanza kunishoot maswali pale nikawa nawajibu, wakawa wanataka kueleshwa kwa undani sana maana walikuwa ni wawakilishi wa wafadhili ambao ilikuwa walete mpunga mrafu sana ofisini. Basi pale nikajikuta naenda nao mpaka session yote aliyopangiwa bosskubwa ni kama bosskubwa alitumia akili kuwaambia kuwa kuna ofisa alimwandaa kutoka Tanzania (yaani mimi eti) kushiriki ule mkutano kwani alitaka kuonyesha pale ofsini tunacollective working style, basi ile pia ilimpa crediti sana. Basi mimi nikajikuta natoka pale saa nane yaani kama inaenda inaenda saa kumi. Uzuri ile ofisi ilikuwa karibu na breakpoint pale posta basi mda wa wao wakibreak kula mimi naingizia zangu breakpint nagonga msosi. Basi mwisho bosskubwa akanipa likizo ya sikumbili nipumzike kufidia ile kazi ya kutoboza usiku.
Basi wakati naaga menejiment wakanishawishi sana nibaki lakini ikashindikana na nikawapa sababu naenda serikalini basi ikabidi tuu waelewe na kunitakia kila lenye heri. Kwakuwa nilimaliza miaka mine pale basi nikapewa mshiko wangu wa pongezi na wiki ya mwisho wakandaa farewell cake tukatata pale ofisi nzima then nikamalizia vimeo vyangu kisha nikakabidhi ofisi nikaondoka kuanza majukumu mapaya.
Sasa kule serikalini baada ya kupokea offer letter kilichobaki ni kusaini tu mkataba. Kwa kuwa tulikuwa watu kama 10 hivi tuliopata ajira pale kwenye hiyo position ilibidi tusubiriane ili wote tuanze siku moja. Kwa hiyo mimi tangu nilipoacha kazi nilikuwa na kama mwezi mmoja hivi wa kupumzika ndio nikaanze kazi serikalini. Niliona afadhali na nilifurahi kupata hilo gap kwa sababu huo muda niliutumia kupumzika na familia nyumbani kwa sababu kipindi hicho ndio kwanza nilikuwa nimetoka kuoa na nina katoto ka kwanza. Basi maisha yakawa poa tuu huku nikiendelea kusikilizie muda ufike nikaanze mzigo serikalini.
Sasa kipindi kile ilikuwa ndio kipindi Magufuli ameingia ofisini, nadhani wote mnakumbuka speed aliyoingia nayo madarakani. Advertise ya kwanza Mkurugenzi wa ile idara ambayo nilipata kazi akatumbuliwa. Hiyo haikuwa big ishu kwangu sana maana ilikuwa hainiathiri moja kwa moja. Advertise ya pili mzee baba akastopisha ajira zote mpya serikalini until further directives. Hapo ndo nilipopigwa na kitu kizito, askwambie mtu ile taarifa uliifurahia au kuona ya kawaida kama tu ilikuwa haikugusi moja kwa moja ila kwa sisi ambao ilitugusa asee!!!
Sasa nikajipa moyo sisi tayari tunaofa letter so itakuwa haituhusu. Nikatamani kuwapigia wengine ambaop nao walikuwa wamepata iyo kazi lakini binafsi nikawa siwajui kwani nilisikia tu pale idarani wanasema nitakuwa na wenzangu wengine kama 10 hivyo tunasubiriana ili tuanze wote pamoja. Basi nikatimba pale idarani kwenda kuulizia mstakabalim utakuweje. Niliulizwa tuu umekuja na ile barua ya ofa? Nikajibu ndio, wakaniambia iache hapo kwa sekretari mpaka utakapopewa taarifa nyingine kwa muda ule maelekezo yalikwa ndio hayo. Daa pale pale nihisi nguvu zinaniishia lkn nikajikaza basi nikaiacha ile barua pale kwa secretary lakini nikaitoa kopi, na nikamuomba namba yule sekretari ili niwe nafatilia. Katika kipindi ambacho nilikuwa nafatilia taarifa ya nabari basi ni kipindi kile maana nilikuwa nataka kujua mzee baba ataruhusu lini kuendelea na michakato ya ajira pale ilipoishia.
Hahaaa ni kama ilikuwa kusubiria mawe yanayochemshwa eti yataiva, mzee baba alikaza. Nilikuwa nampigia simu yule sekretari wa pale serikalini kufatilia maendeleo nadhani mpaka alinichoka maana kuna siku akaniambia kaka sasa naona tu nikutafutie namba ya katibu wa ikulu ili uwe unampigia mwenyewe moja kwa moja. Dah nikaona hapa nishachokwa sasa, lakini nikasema hata kama ningekuwa mimi ningefanyaje. Kwakweli Nilikuwa frustrategy sana kipindi hiki ila sikujilaumu kuacha kazi kule nilikokuwepo maana sikukurupuka ni vile mipango imekwenda ndivyo sivyo. Basi ikabidi nikubaliane na hali halisi. Siku moja line manager akanipigia simu kuniuliza kama lile sekeseke limenikuta na mimi nikamweleza pale na mimi miongoni mwao akaishia tu kuniambia yaani mwezi uliofata tu baada ya mimi kuondoka walikuwa wameshapata mtu mwingine. Nilichomwambia tu asjali ila nitamweka awe referee wangu kwenye CV yangu maana niko mbioni sasa kutafuta sehemu ningine.
Hivi ndivyo ilivyokuwa na msala wangu wa kuhamia serikalini. Hapo nilijifunza kitu kikubwa sana wakati mungine sio kila plan unayoitegemea inakuja kama ilivyo, therefore, you better get ready for the unexpeceted outcomes. Ila badae nikaja kumwelewa na nikamkubali sana Rais Magufuli, ilikuwa ni nadra sana kutomfatilia hotuba zake kwenye vyombo vya habari labda niwe sina nafasi.
See you to the next episode tuone ilikuwaje. Thank you.