Mambo muhimu ya kufanya pindi tu unapopokea taarifa za msiba wa mzazi wako au ndugu yako wa karibu

Mambo muhimu ya kufanya pindi tu unapopokea taarifa za msiba wa mzazi wako au ndugu yako wa karibu

Maandika yanatuasa kuwa tayari ,maana hatujui siku wala saa
Binadamu tunajisau sana tuwapo duniani .Hasa wenye uhakika wa kula na kuvaa ,kulala pazuri na kufanya mambo ya kidunia kama wapendavyo.

Watu husahau kabisa kwamba kuna mauti ,watu wako busy na mishe kila kukicha na malengo mia zaidi,hawajui kabisa kwamba kuna kuondoka siku yoyote.
Watu hawana habari kabisa na Mwenyezi Mungu,watu huishi kama vile walijileta duniani,wana kejeri kwa wenzao,dharau ,wenye kudhihaki,wasio thamini wengine,wenye kiburi,waongo na wasio mtumainia Mwenyezi Mungu.

Mauti yapo na tunatembea nayo.watu tumtumainia mwenyezi Mungu inabidi kujitayarisha kwa yajayo,yawe mema au mabaya.

Mtu mwenye imani thabiti haogopi kifo ,mana tupo ili tufe,na pale jambo baya linapo kufika yabidi umtumainie mwenyezi Mungu mana hauna uwezo wa kubadili kuwa vile unataka wewe.

Mwenye imani hofu na mashaka huwa havipo ,tunahofu na kifo mana hatuna wema ndani yetu.tulishajikatia bima ya uhai wa hapa hapa duniani,watu hawataki kuondoka duniani,na akiona wa karibu yake kaondoka atalia hadi kamasi, kugalagala chini,kufuru kama zote na anamalizia na kuzimia,
Akiamuka tena analia hadi anavua nguo na kutamka maneno yasiyo kuwa na matumaini.

Alichosema mtoa mda yupo sahihi kabisa ,kujiandaa ki roho ni bora zaidi ya yote.Tusiwe kama wasio na imani,
Kama tukiishi twamishia Mungu, na kufa kwetu ni faida.kila kukicha yatupasa kusali na kutambua ya kuwa mauti ipo na hakika ipo siku tutakufa na wapendwa wetu wataondoka .
Basi tufe kifo chema na chenye matumaini,tusiishi kama wanyama wasio na akiri

Wapumzike kwa amani walio tutangulia.
 
Hili suala limekaa kiimani sana Kumuombea marehemu apumzike salama..hii naona haina mantiki yoyote
Ya ni kweli mkuu, wengi wameongea hivi na hata mimi naamini hivyo, lkn hili ni swala la kufarijiana sana.

Kwani mfiwa anapomuombea baba yake, mama yake au ndugu yake fulani huhisi kama amemfanyia flavour fulani ambayo pengine inaweza japo kumsaidia huko alipo.

Ndio pale utasikia watu wanasema RIP, Pumzika kwa amani au ulazwe mahali pema peponi nk.
 
Maandika yanatuasa kuwa tayari ,maana hatujui siku wala saa
Binadamu tunajisau sana tuwapo duniani .Hasa wenye uhakika wa kula na kuvaa ,kulala pazuri na kufanya mambo ya kidunia kama wapendavyo.

Watu husahau kabisa kwamba kuna mauti ,watu wako busy na mishe kila kukicha na malengo mia zaidi,hawajui kabisa kwamba kuna kuondoka siku yoyote.
Watu hawana habari kabisa na Mwenyezi Mungu,watu huishi kama vile walijileta duniani,wana kejeri kwa wenzao,dharau ,wenye kudhihaki,wasio thamini wengine,wenye kiburi,waongo na wasio mtumainia Mwenyezi Mungu.

Mauti yapo na tunatembea nayo.watu tumtumainia mwenyezi Mungu inabidi kujitayarisha kwa yajayo,yawe mema au mabaya.

Mtu mwenye imani thabiti haogopi kifo ,mana tupo ili tufe,na pale jambo baya linapo kufika yabidi umtumainie mwenyezi Mungu mana hauna uwezo wa kubadili kuwa vile unataka wewe.

Mwenye imani hofu na mashaka huwa havipo ,tunahofu na kifo mana hatuna wema ndani yetu.tulishajikatia bima ya uhai wa hapa hapa duniani,watu hawataki kuondoka duniani,na akiona wa karibu yake kaondoka atalia hadi kamasi, kugalagala chini,kufuru kama zote na anamalizia na kuzimia,
Akiamuka tena analia hadi anavua nguo na kutamka maneno yasiyo kuwa na matumaini.

Alichosema mtoa mda yupo sahihi kabisa ,kujiandaa ki roho ni bora zaidi ya yote.Tusiwe kama wasio na imani,
Kama tukiishi twamishia Mungu, na kufa kwetu ni faida.kila kukicha yatupasa kusali na kutambua ya kuwa mauti ipo na hakika ipo siku tutakufa na wapendwa wetu wataondoka .
Basi tufe kifo chema na chenye matumaini,tusiishi kama wanyama wasio na akiri

Wapumzike kwa amani walio tutangulia.
Mkuu umeandika maneno ambayo yamenigusa sana moyo wangu. Hakika ulichoandika kinamantiki kubwa ndani yake, na mwenye akili anapaswa kukizingatia.

Anaeongea maneno ya Mungu kwenye mitandao kama hii anakuwa ameisaidia jamii kubwa iliyomsahau Mungu na kumkumbatia shetani. Huu ni ukumbusho wenye faida kwa kila anaeamini uwepo wa Mungu.

I hope wenye macho wamesoma na kuelewa, na wenye akili wamezingatia na kuyafanyia kazi.
Baraka za Mungu zikushukie popote ulipo.
 
Habari zenu wana JF wenzangu

Bila kupoteza muda ndugu zangu inajulikana wazi kuwa kila binadamu yupo hapa duniani kwa siku zake maalum za kuishi, na baada ya siku hizo kuisha atakufa na kurudi kule alipotokea.

Sasa basi.. ingawa kifo kipo lakini hakuna anaependa kufa au kufiwa. Hii ni kwa sababu kwanza ukishakufa haurudi kuwa hai, pili hakuna anaejua kwa macho yake mwenyewe kwamba baada ya kufa anakwenda wapi, tatu dini zimekuwa zikitueleza kuhusu adhabu iliyopo mbele yetu baada ya vifo vyetu kutokana na matendo yetu.

Kwa vile hakuna binadamu aliekamilika, kwahiyo kila mmoja wetu anajiona ana makosa mbele ya Mungu, hivyo kuogopa kufa mapema na kwenda kukutana na adhabu zake.

Halikadhalika pia hakuna anaependa kufiwa. Hii ni kwa sababu mfiwa anajua kwamba huyo baba yake, mama yake, mtoto wake au ndugu yake aliefariki hatopata tena chance ya kuonana nae katika maisha ya duniani. Yani ndio unakuwa mwisho wao kuongea pamoja, kucheka pamoja, kuishi pamoja, kusaidiana, kupendana, kuonana nk.
Hivyo basi mfiwa huumia kwa namna ambavyo alimpenda au kuwa na ukaribu na marehemu.

Maumivu ya kufiwa, au kufa kwa yule anaekiona kifo chake huwa ni makubwa sana. Mfano mama anapoona kwamba ugonjwa alionao hauwezi kupona, na pengine anakaribia kufa huku akiwaacha watoto wake wakiwa bado wadogo mno wenye kumuhitaji na kuhitaji malezi yake, ni lazima ataumia sana tena sana ila hatokuwa na la kufanya zaidi ya kuomba dua Mungu amsaidie kumlelea watoto wake kupitia mtu fulani, (labda bibi, mamdogo, shangazi nk) pindi tu atapochukua roho yake.

Mimi nimesha experience kufiwa na mzazi ambae tulimpenda sana, na yeye alitupenda mno watoto wake. So i know how it feel kuondokewa ghafla au hata kwa maradhi na mzazi au ndugu, lakini kuna njia ambayo ukiitumia kipindi cha msiba huo mzito itakusaidia kwa kiwango fulani kupunguza maumivu utayopata wewe mfiwa.

Je unatakiwa ufanyaje baada ya kushuhudia kwa macho yako kifo cha baba yako, mama yako, au ndugu yako, au pengine kuletewa habari za kifo chake.

1) Jambo la kwanza kama ni Mkristo unatakiwa hapo hapo useme ama kwa hakika bwana wewe ndio ametoa na wewe ndio umetwaa, jina lako lenye nguvu kuliko majina yote lihimidiwe daima milele AMEN

Kama ni Muislamu unatakiwa kusema Inna lillah Wainna Illayhi rajiun (Hakika sisi wote ni wa kwako Mola wetu mtukufu, na kwako wewe Mola wetu mtukufu sisi sote tutarejea)

Kwa wale wasiofatilia kauli hizi za dini unaweza kusema sisi tulimpenda, lakini wewe Mungu ndio umempenda zaidi.

Hii itakupa faraja kubwa mfiwa kwani itambidi ukubaliane na ukweli kwamba Mungu mwenyewe ameamua kuchukua kilicho chake, kwahiyo huna budi kukubaliana na hali hiyo hata kama hukutarajia au kupendezewa nacho.

2) Jambo la pili unatakiwa umuombe Mungu kwa imani yako akuongoze katika kipindi hiki kigumu kwako, lakini pia akupe subira na ustahamilifu, na pia kukuepusha na kufuru. Hii ni kwa sababu kuna baadhi ya watu wakifiwa na watu wao wa karibu huluzi fasta control na kupelekea wengine kukufuru Mungu kwamba "kwanini umemchukua mama yangu tu na sio mama wa kina Nusrat, Jessica, Abdallah, John nk" sijui "nimekukosea nini Mungu hadi kunipa msiba huu mzito ambao unajua kabisa siwezi kuubeba", "Eeh Mungu wangu kwanini umemchukua mwanangu mkubwa ambae ndio alikuwa tegemeo langu, je maisha yangu yatakuaje baada ya kumchukua mwanangu huyu mwenye msaada mkubwa kwangu nk. Yani inafika kipindi mtu anasahau kwamba kila kiumbe hapa duniani ni cha Mungu, kwahiyo hakuna mwenye uwezo au ruhusa ya kumzuia kukichukua, iwe leo, kesho au siku yoyote aitakayo yeye muumbaji.
Kumbuka Mungu huwa hakosei na wala haonei. Kila analofanya limekamilika tangu enzi na enzi.

3) Jambo la tatu ni kumuomba Mungu akupe muongozo wa maisha yako mapya ambayo utaishi bila kuwa karibu na yule alieondoka.

4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.

Kifupi ya kwangu ni hayo tu, ila kama kuna mungine anayo ya zaidi ya haya basi ruhusa kuyaorodhesha hapo chini kwenye comments.

Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.

Karibuni ndugu zangu.
Huyo Mungu huwezi kuthibitisha kwamba yupo.
 
Huyo Mungu huwezi kuthibitisha kwamba yupo.
Mkuu umesoma vizuri lkn hapo chini ya uzi wangu, au umekimbilia kuandika kabla ya kusoma thread yote?
Hii ni kwa wale tunaoamini uwepo wa Mungu, bila kujali dini ya mtu. Ila wasioamini uwepo wa Mungu naomba wasome tu lakini wasiandike chochote kuharibu uzi huu.

Karibuni ndugu zangu.
Mimi nilijua kama watu kama nyinyi hamkosekani ndio maana nikatoa angalizo mapema.
 
Mkuu umesoma vizuri lkn hapo chini ya uzi wangu, au umekimbilia kuandika kabla ya kusoma thread yote?
Mimi nilijua kama watu kama nyinyi hamkosekani ndio maana nikatoa angalizo mapema.
Imani ni kitu cha faragha yako, fanya kwako, msikitini, kanisani etc.

Ukiileta imani in the public sphere, umealika uchambuzi.

Huko mtu akikuingilia, hata mimi nitatetea haki yako ya kuamini unachotaka bila kuingiliwa.

Ukileta imani yako JF, umeianika ichambuliwe.

Nakwambia hivi, huyo Mungu wako mwenyewe ni wa hadithi tu, hayupo.

Ndiyo maana huwezi kuthibitisha yupo.

Kama unabisha, thibitisha yupo.
 
Umejaza tu Kumuomba Mungu kumuomba Mungu lkn hutoi solution ya maana, kuomba sio solution kma akiki yako bado haijakaa sawa,

Suala la kwanza ni saikolojia yako, hili ndilo jambo la msingi kuliko yote hapo, kuomba Mungu kunafuata baada ya akili yako kutengamaa na kukubaliana na ukweli pia kuwa na uwezo wa kuhandle machungu, usipokuwa vzr kisaikolojia hata uombe/uombewe vipi ni kazi bureeee...
 
Umejaza tu Kumuomba Mungu kumuomba Mungu lkn hutoi solution ya maana, kuomba sio solution kma akiki yako bado haijakaa sawa,

Suala la kwanza ni saikolojia yako, hili ndilo jambo la msingi kuliko yote hapo, kuomba Mungu kunafuata baada ya akili yako kutengamaa na kukubaliana na ukweli pia kuwa na uwezo wa kuhandle machungu, usipokuwa vzr kisaikolojia hata uombe/uombewe vipi ni kazi bureeee...
Mkuu ndomaana nikasema kama kuna mungine anaeweza kujazia jazia kama hivi ajazie ili watu wengi waendelee kujifunza kupitia uzi na comment.
Shukran kwa mchango wako wenye faida na manufaa kwa wasomaji.
 
Dah nimesoma mpaka mwili umesisimka... Eee Mungu naomba uwalinde wazazi wetu 🤔🤔
Ndo hivyo mkuu, hili ni swala ambalo haliepukiki katika maisha yetu.

Mungu awalinde wazazi wetu na atupe mwisho mwema.
 
We umeongelea mambo ya kiroho. Yapo ya kimwili au kidunia. Ukifiwa usipipoteze mwelekeo.
Kwanza funga milango watu wakusanyike nje au kibarazani.

Pili usilielie, angalia nyendo za ndugu zako maana wengine wanatumika kipindi cha msiba kufanya hujuma kwenye familia.

Tatu kama eneo lako kuna utaratibu wa kuendesha misiba na jumuia, ukoo, vyama vya kuzikana n.k waachie wafanye majukumu yao.

Nne hakikisha wasichana na aki na mama wa ndani wanakuwa sehemu moja usiku na mchana ili wasifanye uchafu kipindi cha msiba.
Uchafu gani wakati wa msiba mkuu???
 
4) Jambo la nne tumia muda mwingi kumuombea marehemu ili apate makazi mema au Mungu aipokee roho yake na kuiweka katika roho za walio wema.
Kumuombea marehemu ni kupoteza muda tu. Mtu mwenyewe alipokuwa hai hakurekebisha mambo yake na Mungu afe ndiyo watu baki mumuombee makazi mema na roho yake kupokelewa mbinguni/akhera?

Ukifia dhambini ndiyo imetoka hiyo; na faili lako limefungwa. Tujitahidi kurekebisha mambo yetu na kuwa na mahusiano mema na Mungu tukiwa hai 🙏🏿

Screenshot_20230426_122935_Swahili Bible Offline.jpg
 
Ndo mana tukasema inategemea na mtu. Ila ukiwa unamuomba Mungu kwamba siku likitokea tukio la aina hiyo akuongoze katika haya manne, basi uwezekano wa kuyafanya kupitia Mungu upo.
Mungu atutie nguvu na atuepushe na vifo vyenye maumivu makali.
 
Kumuombea marehemu ni kupoteza muda tu. Mtu mwenyewe alipokuwa hai hakurekebisha mambo yake na Mungu afe ndiyo watu baki mumuombee makazi mema na roho yake kupokelewa mbinguni/akhera?

Ukifia dhambini ndiyo imetoka hiyo; na faili lako limefungwa. Tujitahidi kurekebisha mambo yetu na kuwa na mahusiano mema na Mungu tukiwa hai 🙏🏿

View attachment 2600146
Asante mkuu kwa ujumbe huu kupitia biblia takatifu. Nina imani wengi watajifunza kupitia andiko hili.
 
Omba upate fedha za kutosha kutoka kwa marafiki usitumie akiba Yako isipokuwa kwa mahitaji maalumu
 
Msiba ukikufika hutakumbuka hata moja hapo,tena unaweza shtuka wiki imepita mlishazika ndo wewe unarejewa na utimamu, siku zote 7 unakokotwa tu
 
Msiba ukikufika hutakumbuka hata moja hapo,tena unaweza shtuka wiki imepita mlishazika ndo wewe unarejewa na utimamu, siku zote 7 unakokotwa tu
Wapo ambao wanakumbuka mkuu, inategemea mtu na mtu.
Msiba unauma, lkn ni jambo ambalo huwa haliepukiki na kila mmoja wetu anakubaliana na jambo hilo. Hakuna mtu asiekubali kuwa kuna kufa au kufiwa.
 
Back
Top Bottom