View: https://youtu.be/9ebMOVI87h0?si=sJm0h1XJPQDVVuaQ
Jana nimetumiwa hiyo link na rafiki zangu ambao sio watanzania wakishtushwa na kukasirishwa na huyo mzungu akiwadhalilisha Watanzania hasa Wanawake,
Kwenye comments nimesikitishwa na baadhi ya wanaume wa Kitanzania wakimsapoti na kujichekesha chekesha kama fisi limeona fupa, mtu anaonesha ubaguzi wazi wazi kwa kuwaita Maskini, mna magonjwa ya zinaa, mnaomba omba, mnafake furaha na maisha bora n.k jitu linafurahi kisa hayo maneno kasema mzungu dah! naimagine huyo mzungu angekua amewasema hivyo Wasouth au Wanigeria sijui kama angekua anapumua sasa hivi,
Serikali inatumia billions of money kuita watalii Tanzania halafu watu kama huyu mzungu wanaongea uzushi na uongo ili kukimbiza watalii Tanzania, mtu kama huyu kwanini asifunzwe ili iwe fundisho kwa wageni wengine wakiwa nchini wafanye kilichowapeleka na sio kuongea uzushi na uongo kwenye mitandao?
(Hii tunaongea wenyewe kama familia) dada zetu wa Dar muwe na stara sisi tushawazoea kutuomba omba hela sasa akitokea mgeni mjikaze basi, wazungu hawajazoea kuombana ombana hela, tulia akupe mwenyewe, sio umekutana na mtu leo kesho unampa mkeka wa matatizo yako, kodi, bills, hospital, mama, wadogo zangu, acheni hizo mjishughulishe kama wenzenu wa mikoa mingine, mnawaponza wengine kwa makosa yenu, kadhalika kaka zetu ukitoka na mzungu usijibweteke bills zote alipe yeye jitutumie angalau hata mgawane nusu kwa nusu, unaweza ukasema nalipia vinywaji, lipia chakula au nalipia usafiri lipia chakula na vinywaji sio unajichekesha kesha tu ikija bill unavizia mwanaume mwenzio alipe haipendezi mbadilike!
Haya twendeni tukamshambulie huyo mzungu kwenye comments atukome waTZ.