Man United kupigania kutoshuka daraja

Man United kupigania kutoshuka daraja

Mdakuzi

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
4,294
Reaction score
6,872
Man United: Kipigo, Matumaini Yanayoyeyuka, na Mvumo wa Mashaka

Usiku wa Desemba 30, 2024, Old Trafford, uwanja uliojaa kumbukumbu za ushindi wa kihistoria ukageuka kuwa kaburi la matumaini ya mashabiki wa Manchester United.

Sauti za shangwe zilizokuwa zinaashiria imani ya mashabiki zilidhoofika, na kuzimwa kabisa baada ya kipenga cha mwisho.

Newcastle United walitembea kwa ushindi wa mabao 2-0, wakiacha wingu zito kwa Man United.

United, Mabingwa wa enzi, sasa wanaingia mwaka mpya wakiwa kwenye nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England.

Wakiwa na alama 19 baada ya mechi 17, tofauti ya alama 7 tu inawatenganisha na timu zilizo hatarini kushuka daraja.

Hakuna tena miujiza kubadili matokeo ya "Fergie Time." Hakuna tena wachezaji kama Cantona, Ronaldo au Rooney kuokoa timu.

Timu inaenda kwa kasi kwenye hadhi za timu ndogo za EPL. Ni habari mbaya. Jitihada nyingi zimefanyika ili kunusuru timu, lakini bado inazama.

Ni msimu wa giza, msimu ambao historia inapigwa kikumbo na hali halisi isiyosameheka.

Ova
 
Masikini Man United inanitesea mpenzi wangu, hapa tulishaagana kumbe mtu anachapa uzi wa majonzi!

Lakini, ni kama nilivyokuambia sikuona uharaka wa RA kuanza kazi badala yake mngemuachia msimu huu aumalize RVN kwa maana alishaanza na upepo mzuri na timu ilirudi kuwa na ari.

Amorim ni kocha mzuri, sana. Ila ilifaa aanze msimu wake mwenyewe na mipango yake mwenyewe na sio kumalizia msimu uliokwisha kuanza kwa kusuasua.

Poleni sana, sie Arsenal wala hatuna shida na nyie tena. Mbaya wetu ni Liverpool, basi.
 
Masikini Man United inanitesea mpenzi wangu, hapa tulishaagana kumbe mtu anachapa uzi wa majonzi!

Lakini, ni kama nilivyokuambia sikuona uharaka wa RA kuanza kazi badala yake mngemuachia msimu huu aumalize RVN kwa maana alishaanza na upepo mzuri na timu ilirudi kuwa na ari.

Amorim ni kocha mzuri, sana. Ila ilifaa aanze msimu wake mwenyewe na mipango yake mwenyewe na sio kumalizia msimu uliokwisha kuanza kwa kusuasua.

Poleni sana, sie Arsenal wala hatuna shida na nyie tena. Mbaya wetu ni Liverpool, basi.
We nimwanaume vua hio hijabu uliovaa
 
Ha haaa.
Nampa pole Mdakuzi sie
Liverpool tunajipigia tu makolobwanji wote.
Huku Yanga kule Liverpool raha tupu mwendo wa 5G.
Sijui kwanini Mimi na Mhandisi Hersi Saidii wote tunashabikia timu mbili zinazo fanana!?
Masikini Man United inanitesea mpenzi wangu, hapa tulishaagana kumbe mtu anachapa uzi wa majonzi!

Lakini, ni kama nilivyokuambia sikuona uharaka wa RA kuanza kazi badala yake mngemuachia msimu huu aumalize RVN kwa maana alishaanza na upepo mzuri na timu ilirudi kuwa na ari.

Amorim ni kocha mzuri, sana. Ila ilifaa aanze msimu wake mwenyewe na mipango yake mwenyewe na sio kumalizia msimu uliokwisha kuanza kwa kusuasua.

Poleni sana, sie Arsenal wala hatuna shida na nyie tena. Mbaya wetu ni Liverpool, basi.
 
Ha haaa.
Nampa pole Mdakuzi sie
Liverpool tunajipigia tu makolobwanji wote.
Huku Yanga kule Liverpool raha tupu mwendo wa 5G.
Sijui kwanini Mimi na Mhandisi Hersi Saidii wote tunashabikia timu mbili zinazo fanana!?
Hana maana huyo nae ameshaiharibu timu (Yanga) tumepoteza matumaini klabu bingwa.

Ila nini, Liverpool mnanikosesha raha sana. City ameshatoka kwenye ramani nyie ndio mnakiwasha hampoi.
 
Man u wanahitaji: kipa mwenye kiwango; viungo 4 (jamii ya salah) na washambuliaji wawili Wenye viwango.
Man u tatizo la ukabaji hskuna wanatakiwa wasajili namba 6, 5, 4, 3 , 2 na na mawinga wenye kasi. Mfano Madrid wanabebwa na wachezaji wenye kasi mbele bila hivyo Madrid wangekua kama Man u, Madrid wahitajika wasajili namba 6, 4 na 3.
 
Ha haaa.
Nampa pole Mdakuzi sie
Liverpool tunajipigia tu makolobwanji wote.
Huku Yanga kule Liverpool raha tupu mwendo wa 5G.
Sijui kwanini Mimi na Mhandisi Hersi Saidii wote tunashabikia timu mbili zinazo fanana!?
Nyie livakuku hakika mpeteseka sana enzi za fagie time ilikua ninadra enz zile kumkuta shabik waliva kijana bora saiv mpate raha nanyie
 
Back
Top Bottom