Man United kupigania kutoshuka daraja

Man United kupigania kutoshuka daraja

Man United: Kipigo, Matumaini Yanayoyeyuka, na Mvumo wa Mashaka

Usiku wa Desemba 30, 2024, Old Trafford, uwanja uliojaa kumbukumbu za ushindi wa kihistoria ukageuka kuwa kaburi la matumaini ya mashabiki wa Manchester United.

Sauti za shangwe zilizokuwa zinaashiria imani ya mashabiki zilidhoofika, na kuzimwa kabisa baada ya kipenga cha mwisho.

Newcastle United walitembea kwa ushindi wa mabao 2-0, wakiacha wingu zito kwa Man United.

United, Mabingwa wa enzi, sasa wanaingia mwaka mpya wakiwa kwenye nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya England.

Wakiwa na alama 19 baada ya mechi 17, tofauti ya alama 7 tu inawatenganisha na timu zilizo hatarini kushuka daraja.

Hakuna tena miujiza kubadili matokeo ya "Fergie Time." Hakuna tena wachezaji kama Cantona, Ronaldo au Rooney kuokoa timu.

Timu inaenda kwa kasi kwenye hadhi za timu ndogo za EPL. Ni habari mbaya. Jitihada nyingi zimefanyika ili kunusuru timu, lakini bado inazama.

Ni msimu wa giza, msimu ambao historia inapigwa kikumbo na hali halisi isiyosameheka.

Ova
Hata Asernal iliwahi kupitia hali kama hii baada ya Wenger kuondoka, nadhani upepo tu. Hata Makolokwinyo yaliwahi kupitia situatio kama hii ikaokoka kwenye mechi za kufungia ligi tena ni mechi fixing.
 
1000300611.jpg

Leo hii
Lineup
 
Hivi kwann mtu kama rashford ameamua kutokaza kama anavyokaza amad, garnacho??
Aisee sisi united fans tushasema Hadi basi, tatizo si kocha, amorim ni bonge la kocha, shida ni wachezaji. They aren't enough kabisa. Angalia magoli tunayofungwa ni uzembe wa wachezaji wenyewe, hivi kama mchezaji ufundishwe kupiga pasi, kufunga, je intensity pia ufundishwe wakati ni jambo la kuwa na desire tu moyoni ndo huzalisha intensity. Angalia Newcastle ni timu ambayo ina athletes wa kutosha na ni mid table team!, niambie UTD wana wa kufanana na wachezaji kama Gordon, isak, hapo kati Kuna watu kama Tonali, Bruno gumaires sisi tuna casemiro, eriksen haya beki wana Fabian schar, burn sisi tuna maguire, haya angalia benchi Lao wana Harvey Barnes, Miguel almiron halafu kumbuka wana majeruhi nao. Are we serious? Mid table timu ina vyuma kama hivyo haya hebu niambie sisi tunaweza kushindana kweli, mapesa yote Yale lakini hayatusaidii chochote zaidi ya utapeli tu hahaha.

Binafsi naamini Omar berrada anaweza kutufikisha mahali kama akifanikiwa kupata watu sahihi.
 
Mbona ugarte anaonekana kukaza? Mazroul anakaza? Hivi kwa nini Martinez ameacha kukaza? Enzi za fagason hata ukifungua YouTube angalia pambano la timu ya Fergus wanakaza sana?? Hawa wananini?? Fernandez anakaza japo anapoteza poteza ila anakaza??

Ninaamininkuna wakati hernandez anapiga rough makusudi akapunzike. I m sure
 
Hivi kwann mtu kama rashford ameamua kutokaza kama anavyokaza amad, garnacho??
Tumelea upumbavu sisi wenyewe, kipindi kile Kila kitu aliachiwa Ferguson Sasa alivyoondoka hakukuwa na kocha mwenye kaliba kama yake na vile vile mpira ulikuwa unatoka kwenye transition ya kwamba kocha Sasa kazi yake ni kufundisha tu mpira na kutoa ushauri wa hapa na pale, tulijisahau kwenda na timing ya kuweka watu wa mpira badala yake tukaweka watu wa biashara tu. Tatizo ni moja tu ni management basi wengine ni mbuzi wa kafara tu. Timu kama hii si wa kutuletea average players na wastaafu.
 
Back
Top Bottom