Manjagata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 13,942
- 15,371
Mimi siyo chawa wa mama! Wewe ni chawa wa mama wa maeneo gani?Kwani wewe hutaki u DC?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mimi siyo chawa wa mama! Wewe ni chawa wa mama wa maeneo gani?Kwani wewe hutaki u DC?
Panga na rungu tu vingetosha kwa mimi kuingia vitani.Wewe peleka moyo wako vitani bila silaha halafu utuletee mrejesho hapa
Halafu ukute unatembea kwa miguuNdugu zangu Watanzania,
Tembeeni vifua mbele,tembeeni kwa maringo,tembeeni kwa Madaha,tembeeni bila hofu,tembeeni bila wasiwasi,tazameni mbele kwa matumaini ,tazameni mbele kwa furaha kwa sababu kwa hakika na kiukweli Tanzania tuna Rais kwelikweli.
Tuna kiongozi mbele yetu Watanzania,tuna Amiri Jeshi Mkuu wa Viwango vya Kidunia katika Mzani wa uzito wa Juu,Tuna Mzalendo wa kweli mbele yetu,Tuna Mama hodari Mwenye kiapo cha kuitetea,kulinda na kulipigania Taifa Letu kwa Jasho na Damu.Tuna Mama wa Nguvu , shupavu, imara na madhubuti kwelikweli.
Nimepita katika ukurasa wa Twitter wa Rais wetu na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan na kukuta ameandika ujumbe wake kwenda kwa Jeshi letu lenye uzalendo wa hali ya juu kabisa. Maneno ambayo nilipokuwa nayasoma nimejikuta nikibubujikwa na machozi ya furaha kuwahi kutokea .
Nimejikuta Moyo wangu ukijawa na Morali ya hali ya juu kiasi kwamba Hata vita itokee Leo naweza hata kubeba panga na rungu begani kwenda kupambana na adui mwenye silaha nzito na vifaru vya kivita na ndege za kivita angani. Lakini kwa maneno ya Rais wetu mpendwa mimi naweza kusonga mbele katika uwanja wa Mapambano uwakao Moto Pasipo kurudi Nyuma.
Rais Samia siyo Binadamu wa kawaida.ni mtu na nusu,ni zaidi ya kiongozi.Amenijaza ujasiri sana leo hii zaidi ya ule niliokuwa nao. Katika andiko lake katika siku hii ya kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi letu la JWTZ tangia kuasisiwa kwake amenukuu maneno ya Hayati Baba wa Taifa yasemayo "Moyo Kwanza kabla ya silaha" yaliyotolewa na Mwalimu Nyerere wakati huo kama sehemu ya hotuba yake.
Rais wetu mpendwa ameendelea kusema ya kuwa Kwa moyo wa waliotangulia mbele za haki na Moyo wa Makamanda na wapiganaji Wetu Taifa letu limeendelea kuwa imara,mipaka yetu imeendelea kuwa salama na watanzania wameendelea kuishi kwa amani katika Nchi yao.
Akamalizia kwa kusema ya kuwa Utii wenu ,nidhamu yenu na utayari wenu kwa Nchi yetu ndio Msingi wa watanzania kuendelea kuwaamini na kuwa na matarajio makubwa nanyi.lindeni imani hiyo kwa nguvu kubwa tena nguvu kubwa sana.Endeleeni kufanya kazi zenu Mkijuwa ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu nipo pamoja Nanyi kwa Hali zote.
Ndugu zangu maneno aliyomaliza hapo mwishoni Rais wetu ndiyo yamenitoa na kunibubujisha machozi kuwahi kutokea.Maneni ya kwamba Endeleeni kufanya kazi zenu Mkijuwa Amiri Jeshi Mkuu Nipo Nanyi kwa Hali zote .ni maneno yenye kujawa na uzalendo wa hali ya juu sanaaaaaaa Kwa Taifa letu.
Ni Maneno yenye kuonyesha ni namna gani Rais wetu amelitanguliza mbele Taifa letu na kuwa tayari kulipigania,kulitetea na kulilinda katika hali zote na kwa gharama yoyote ile iwayo. Mama ni zawadi kutoka kwa Mungu Mwenyewe tunayopaswa kujivunia na kuitunza kwa wivu mkubwa sana.View attachment 3084305View attachment 3084306
Kazi iendelee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kila ukibubujikwa na machozi unaanzisha thread si utajaza server bila sababu za msingi?
Hawa ndiyo viongozi wa CCMBado kidogo tuu uchumi wetu utalingana na China..
Shetani kabisa hiliVua chupi haraka Sana akuweke nyuma cha moto. Jinga wewe. Mungu chukua hili lishetani haraka Sana lichome moto liteketee
Ni jitu halina akili limelaaniwaHuwa unavuta bhangi?🤔
NakubaliKazi nzuri na za kupendeza anazofanya Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan,ni ngumu sana kukaa kimya pasipo kuzungumza.tukikaa kimya hata mawe yatazungumza