tweenty4seven
JF-Expert Member
- Sep 21, 2013
- 15,863
- 19,626
Huko nikienda nakula nyama ya digidigi tuHuko kunafaa kuzuru[emoji39]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huko nikienda nakula nyama ya digidigi tuHuko kunafaa kuzuru[emoji39]
Hawakuona kwamba Hali ni mbaya wauze waje kununua baadae? Ngoja zipukutike ndio akili zikae sawa.View attachment 2080443
Mifugo 62,593 imekufa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame. Kati ya mifugo hiyo;
Ng'ombe - 35,746
Kondoo - 15,136
Mbuzi - 10,033
Punda - 1,670
======
Hali ya ukame inayoendelea wilayani Simanjiro mkoani Manyara imesababisha mifugo mbalimbali ikiwemo ng'ombe, kondoo, mbuzi na punda kufa.
Simanjiro. Mifugo 62,593 imekufa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kutokana kukosa maji na malisho baada ya ukame kuvikumba vijiji mbalimbali katika wilaya hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Sendeu Laizer ameyasema hayo Januari 13 kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo.
Sendeu ameitaja mifugo hiyo iliyokufa kuwa ni ng'ombe 35,746, kondoo 15,136, mbuzi 10,033 na punda 1,670.
Amesema katika kipindi hiki hali ya mifugo katika maeneo mengi ya Simanjiro siyo ya kuridhisha kutokana na uhaba wa maji na malisho.
Amesema ufuatiliaji na ukusanyaji wa taarifa za vifo vya mifugo kutokana na athari za ukame unaendelea katika vijiji vyote.
"Hali hii imesababisha baadhi ya mifugo kufa na wafugaji wengi kuhama na kurundika katika maeneo machache yenye maji na malisho," amesema Sendeu.
Mbunge wa jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka amesema kutokana na ukame huo jamii nyingi zimeingia kwenye umaskini kutokana na mifugo yao kufa.
Ole Sendeka amesema kwa sababu ya ukame uliopo nchini baadhi ya wafugaji wamehamisha mifugo yao nje ya nchi ili zipate malisho.
Diwani wa kata ya Naisinyai, Taiko Kurian ametoa ombi kwa Serikali kuruhusu mifugo kuingia ndani ya ukuta wa madini ya Tanzanite ili kupata malisho.
"Mifugo ni benki ya jamii za kifugaji sasa inapokufa kwa ukame inakuwa tatizo tunaiomba Serikali iruhusu mifugo kuingia ndani ya ukuta wa madini ya Tanzanite kwani haitadhiriana," amesema Taiko.
Simanjiro yapitisha Sh25.2 bilioni
Wakati huo, madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro wamepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya Sh25.2 bilioni kwa ajili ya mwaka wa fedha wa 2022/2023.
Ofisa mipango wa halmashauri hiyo, Heri Kuria amesema bajeti hiyo imelenga kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya elimu, afya, maji na miundombinu.
Amesema katika bajeti ya 2022/2023 halmashauri hiyo itatekekeleza miradi mbalimbali na katika bajeti hiyo itaongeza ujenzi wa madarasa ya shule za msingi 20, shule mpya ya sekondar na kituo cha afya.
Ofisi ya Makamu wa Rais na Jafo wapo tuu hakuna anaehangaika wala kupiga kelele kutunza mazingira.Serkali iweke mipango mahususi kila kijiji kila mtaa kwa mwaka walau kila kijiji kipande miti laki moja la sivyo tutakuwa km somalia
Yaani tumekariri kwamba kila leo ndio itakuwa kesho.Hizi nchi za dunia ya tatu tunaishi kwa mazoea na kudra za Mungu.
Shida ya mvua ya mwaka huu imekaa kiswahili Swahili na inanyesha kimafungu.Kuna baadhi ya mkoa wa manyara leo usiku nimeapata taarifa imenyesha mvua ya kutosha...
Kwa pesa gani? Njia rahisi ni kuvuna maji ya mvuaIpeleke maji toka ziwa victoria
Serikali ilisema itsnunua mitambo ya kuchimba maji kila mkoa kwa pesa za uviko,Aweso aje atuambie kama mitambo imekujaYale mahela anayolipwa Ndungai yangeweza kuchimba visima vya maji kuokoa uhai wa raia na hii mifugo.
Mzilankende MnyagoMagufuli kaondoka na mvua yake
Mmasai yupo radhi ng'ombe afe sio kuchinja au kuuza
mkuu Serikali ndo imeleta ukame? Kwamba unataka serikali iagize mahindi ya msaada ili hao mifugo wawe wanapikiwa ugali?Hali ya ukame inayoendelea Baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Manyara inatisha !HaI Sasa Simanjiro pekee ng'ombe 35,000 + wamekufa,mbuzi 10,000,kondoo 15,000 !
Hili ni janga!
Hivi Serikali imekosa mbinu za kuwaokoa wanyama Hawa!
Mkuu mbona uneteseka saana na hii kauli?Serikali ambayo inahamasisha ufisadi bila aibu tena kupitia TV ya Taifa haiwezi kuona janga lolote lile katika nchi.
View attachment 2080730
🤡🤡🤡Mkuu mbona uneteseka saana na hii kauli?View attachment 2081947
Mkuu Kwahiyo malalamiko yako ndo yatafanyiwa kazi?hata nikitoa pendekezo halitofanyiwa kazi maana sio kipaumbele chao kwa sasa wamasai nawapa pole tu wakomae hivyo hivyo
Mkuu Umeambiwa hata nyasi hakuna, Kwahiyo ngombe atashindia maji?Serikali inapaswa kuchimba mabwawa kadhaa yatakayohifadhi maji ya mvua ili kusaidia mifugo isife wakati wankiangazi maana kwa wakati wa jua ng'ombe hunywa maji hata ndoo nne hadi tano kwa siku.
HahahShushia na K-Vant hapo dawa wa moto ni moto
Hao ni ukoo Mollel..wanakaa na ng'ombe hadi anazeeka na kufa..ukoo wa Laizer wajanja, wanauza na kununua mifugo na viwanja pale inapobidi...ndio maana wana mpunga..mara chache utakuta kachoka sanamasai anaona fahari yaan yeye fahari yake n kuwa na ng'ombe nyingi hapo analala kwenye kijumba kilichokandikwa kwa mavi ya ng'ombe yaan utajiri anaulalia [emoji848][emoji848]
umasain ukiwa na ng'ombe nyingi unajeshimika sana