Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naamini Tutajifunza the hard way. Tuwe na mipango mahususi kila mwaka wa kupanda Mamilioni ya Miti kila wilaya. Hii sio dalili nzuri kabisa kwa siku zijazo.Serkali iweke mipango mahususi kila kijiji kila mtaa kwa mwaka walau kila kijiji kipande miti laki moja la sivyo tutakuwa km somalia
Vipi kuhusu Bwawa la Mwl. Nyerere?? Miri mingapi imekatwa namingapi iliyooteshwa??Miti Miti tujenge utamaduni wa kupanda miti iwe ni mpango endelevu Simanjiro ipo kma jagwa sasa hv
hao mbona wachache aisee wamasai wana ng'ombe acha kabisa kule umasaini kuleHiyo ni ishu aisee wafundishwe kufuga kisasa ng'ombe wanaweza kuwahudumia hata kwa mapumba wakati kama huu. Sasa mtu unakuta ana ng'ombe 3000-5000 atawezaje kuwahudumia pumba??? Na wanakufa anaona heri wage hata kuuza hataki achilia kuchinja wale nyama.
Dubai walitengenezaga mvua kama ni mfuatiliaji mzuriIlete mvua mkuu. Hali mbaya sana watu hawajaanza kulima wakati saa hii watu wangekuwa wanavuna mazao ya mwanzo... Nasikia malaysia zipo mvua za kutengeeza,, tufuate wataalamu huko waje kutuletea mvua[emoji125][emoji125][emoji125]
Nimeitoa(Delete) kabisa Mkuu.🙏pw pw ila hiyo inabid uweke tahadhari kabisa maana sio poa kabisa
Siyo Simanjiro pekee hata Longido, Monduli na baadhi ya maeneo ya jirani. Hali ni mbaya Kwa ujumla.Hali ya ukame inayoendelea Baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Manyara inatisha !HaI Sasa Simanjiro pekee ng'ombe 35,000 + wamekufa,mbuzi 10,000,kondoo 15,000 !
Hili ni janga!
Hivi Serikali imekosa mbinu za kuwaokoa wanyama Hawa!
Ukame upo tangu enzi za mababu kenge weweVipi kuhusu Bwawa la Mwl. Nyerere?? Miri mingapi imekatwa namingapi iliyooteshwa??
Hata v8 moja tu ya mkuregenzi wa simanjiro inatosha kuchimba visima 150 wilaya nzimaYale mahela anayolipwa Ndungai yangeweza kuchimba visima vya maji kuokoa uhai wa raia na hii mifugo.
Asante mkuu kwa kutujuza hii habari ya kusikitisha. Jua ni kali. Upepo mkali. Na Watu wanalia njaa. Na mifugo inakufa. Na bei za vitu zimepanda bei maradufu. Mungu ibariki TanzaniaView attachment 2080443
Mifugo 62,593 imekufa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame. Kati ya mifugo hiyo;
Ng'ombe - 35,746
Kondoo - 15,136
Mbuzi - 10,033
Punda - 1,670
======
Hali ya ukame inayoendelea wilayani Simanjiro mkoani Manyara imesababisha mifugo mbalimbali ikiwemo ng'ombe, kondoo, mbuzi na punda kufa.
Simanjiro. Mifugo 62,593 imekufa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kutokana kukosa maji na malisho baada ya ukame kuvikumba vijiji mbalimbali katika wilaya hiyo.
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Sendeu Laizer ameyasema hayo Januari 13 kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo.
Sendeu ameitaja mifugo hiyo iliyokufa kuwa ni ng'ombe 35,746, kondoo 15,136, mbuzi 10,033 na punda 1,670.
Amesema katika kipindi hiki hali ya mifugo katika maeneo mengi ya Simanjiro siyo ya kuridhisha kutokana na uhaba wa maji na malisho.
Amesema ufuatiliaji na ukusanyaji wa taarifa za vifo vya mifugo kutokana na athari za ukame unaendelea katika vijiji vyote.
"Hali hii imesababisha baadhi ya mifugo kufa na wafugaji wengi kuhama na kurundika katika maeneo machache yenye maji na malisho," amesema Sendeu.
Mbunge wa jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka amesema kutokana na ukame huo jamii nyingi zimeingia kwenye umaskini kutokana na mifugo yao kufa.
Ole Sendeka amesema kwa sababu ya ukame uliopo nchini baadhi ya wafugaji wamehamisha mifugo yao nje ya nchi ili zipate malisho.
Diwani wa kata ya Naisinyai, Taiko Kurian ametoa ombi kwa Serikali kuruhusu mifugo kuingia ndani ya ukuta wa madini ya Tanzanite ili kupata malisho.
"Mifugo ni benki ya jamii za kifugaji sasa inapokufa kwa ukame inakuwa tatizo tunaiomba Serikali iruhusu mifugo kuingia ndani ya ukuta wa madini ya Tanzanite kwani haitadhiriana," amesema Taiko.
Simanjiro yapitisha Sh25.2 bilioni
Wakati huo, madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro wamepitisha rasimu ya mpango wa bajeti ya Sh25.2 bilioni kwa ajili ya mwaka wa fedha wa 2022/2023.
Ofisa mipango wa halmashauri hiyo, Heri Kuria amesema bajeti hiyo imelenga kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya elimu, afya, maji na miundombinu.
Amesema katika bajeti ya 2022/2023 halmashauri hiyo itatekekeleza miradi mbalimbali na katika bajeti hiyo itaongeza ujenzi wa madarasa ya shule za msingi 20, shule mpya ya sekondar na kituo cha afya.
Itoshe tu kusema hali ni mbaya kuliko maelezo😭Asante mkuu kwa kutujuza hii habari ta kusikitisha. Jua ni kali. Upepo mkali. Na Watu wanalia njaa. Na mifugo inakufa. Na bei za vitu zimepanda bei maradufu. Mungu ibariki Tanzania
Naamini Tutajifunza the hard way. Tuwe na mipango mahususi kila mwaka wa kupanda Mamilioni ya Miti kila wilaya. Hii sio dalili nzuri kabisa kwa siku zijazo.
Vipi kuhusu Bwawa la Mwl. Nyerere?? Miri mingapi imekatwa namingapi iliyooteshwa??
Ninyi wenye akili timamu mmeotesha mingapi baada ya uharibifu ule??? Hata Kwa maeneo mengine basi mmefanya compensation yeyote ile??Kama miti ilikatwa kwa ajili ya mradi tuache km ilivyo tusipande miti? Hivi mkuu unaakili timamu?
Mmekata miti 2.6mNinyi wenye akili timamu mmeotesha mingapi baada ya uharibifu ule??? Hata Kwa maeneo mengine basi mmefanya compensation yeyote ile??