Maoni: Dkt. Batilda Buriani ameshushwa mno kuteuliwa kuwa Katibu Tawala

Maoni: Dkt. Batilda Buriani ameshushwa mno kuteuliwa kuwa Katibu Tawala

Dkt. Batilda Buriani alikuwa Balozi Kenya na Japan, Leo kateuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa!! Ni kudhalilishwa mno, ni mawazo yangu.

Angepewa hata ukuu wa Mkoa.
Wadhifa na malipo ya RAS ni sawa sawa na Katibu Mkuu wa Wizara, marupu rupu ndio inakuwa tofauti, waziri anakuwa na uwanja mpana wa kutengrneza marupurupu kuliko RAS.
 
..mbona Rashidi Kawawa alishuka toka Waziri Mkuu mpaka kuwa Waziri asiye na wizara maalum.

..baada ya uhuru Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu na Mzee Kawawa akashika usukani wa nchi.

..Mzee Kawawa alishuka toka kuwa kiongozi mwenye walinzi na msafara, mpaka kuwa kiongozi wa kawaida ambaye gari yake inabidi isukumwe kwanza ndio iwake.

..Pia yupo Mzee Msuya ambaye alikuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Raisi baadae akashuka akawa Katibu wa Uchumi CCM wilaya ya Mwanga.
shallow analysis
 
Anakaataaje uteuzi wakati alikua hana kazi anapika na kumpakulia mzee tu, hakuna cha kushushwa wala nini RAS ni mtu mkubwa sana pia msichukulie poa
 
Taja majina matano
Mfano hukumbuki Hemedi Msangi alikuwa Zanzibar kama kamanda wa polisi. Pia kumbuka Zanzibar ni ndogo hata nafasi zake za uteuzi ni chache hivyo ni kweli utaona kama wengi wanateuliwa huku kwakuwa huku kuna keki kubwa.
 
Mfano hukumbuki Hemedi Msangi alikuwa Zanzibar kama kamanda wa polisi. Pia kumbuka Zanzibar ni ndogo hata nafasi zake za uteuzi ni chache hivyo ni kweli utaona kama wengi wanateuliwa huku kwakuwa huku kuna keki kubwa.
Huku kuna wahudumu wa afya, polisi, manesi, madakteri, Ma-RAS, mawaziri, n.k bona umetaja mmoja tu? kuna tatizo kubwa tunanyonywa muungano uvunjwe haraka
 
Huku kuna wahudumu wa afya, polisi, manesi, madakteri, Ma-RAS, mawaziri, n.k bona umetaja mmoja tu? kuna tatizo kubwa tunanyonywa muungano uvunjwe haraka

Kuhusu Muungano ni kweli kuwa Muungano ulio sawa ni wa Serikali tatu tu. Kama tunakubaliana na huu wa sasa, hatuna namna ya kupinga haya yanayotokea.
 
Dkt. Batilda Buriani alikuwa Balozi Kenya na Japan, Leo kateuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa!! Ni kudhalilishwa mno, ni mawazo yangu.

Angepewa hata ukuu wa Mkoa.
Hana Tija Batlida. Ni mswahili tu kama Bashiru
 
Huyu ndio alikomaa na kesi ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa Lema pale Arusha mjini. Kama alikuwa mbunge, kuwa Katibu Tawala wa mkoa ni sawa tu, na ubalozi si ni hadhi tu kama udaktari au uhandisi (japo hizo nyingine ni za kielimu)

View attachment 1803239
Hajawahi kuwa Mbunge Arusha weeeee hili haliingii wazembe
 
Dkt. Batilda Buriani alikuwa Balozi Kenya na Japan, Leo kateuliwa kuwa Katibu Tawala mkoa!! Ni kudhalilishwa mno, ni mawazo yangu.

Angepewa hata ukuu wa Mkoa.
Ww ndio unaona ameshushwa lakini yeye mwenyewe kashukuru vibaya sana, maana hana ujanja wa kuendesha maisha nje ya madaraka. Kwa taarifa yako hivyo vyeo alivipata sio kwa uwezo bali kwa mbeleko. Kama angekuwa na uwezo, huu ndio ulikuwa wakati sahihi wa yeye kutumia huo uwezo wake kufanya mambo yake, na sio kusubiri hisani ili kuendesha maisha yake.
 
Huyo ni team JK hivyo hicho cheo ni kama njia tu ya kurudishwa matawi ya juu. Isingewezekana atoke alipo halafu ghafla tu apewe cheo kikubwa.
 
Back
Top Bottom