Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Wacha Mungu aitwe Mungi, tulikokuwa tunaelekea Mungu ndiye anaejuwa.
 
mama naomba uangalie wizara ya ardhi, hii wizara ni ngumu mno, ofisi za ardhi zina uozo mkubwa mama.

Kagua kuanzia ofisi za ardhi ngazi ya wilaya yaani hapa ndo kuna balaa la uozo, tunateseka.

Rushwa rushwa yaani ni balaa

Nchi hii kubwa sana, Tumuombee Mama Yetu.
 
JK was far way better president kuliko marais wengi sio Tz tu bali Afrika nzima.
Nitaomba kukupinga hapa mkuu.

Kumbukua ni awamu iliyomwaga pesa mtaani kama awamu ya pili! Ikawafanya ninyi wenye access ya upigaji na mbeleko mtembee juu ya ardhi, watu wakaua kabisa sekta ya kilimo kwa ike KILIMO KWANZA ambayo ilizalisha mapapaa wale, TASAF ikazalisha mapapaa fulani. Tumeshuhudia tambo za hao mapapaa wakimwaga manoti hadharani, TRA na Polisi wakiangalia, kodi ikikusanywa kwa wafanyakazi wanyonge tu, n.k

Hakika haya ndio yalikuwa maendeleo ya mtu na si watu kama mlivyosema chini ya raisi aliyetukanwa kila kona.

Ukimpa mtu pesa mtaani, atajenga St Mary's schools, watasoma watoto wa wenye uwezo, wale wanaopiga na kulindwa, 80% watasoma kayumba, ukiboresha vitu na mifumo, tutarudi kwenye kile kipindi cha kuona shule za serikali ni bora na fahari kubwa mtoto akisoma huko. Ni awamu gani haya mambo yalikufa?
 
Taifa zima limekuwa la kushangaa kuanzia mwananchi wa kawaida hadi mkuu wa nchi, sijui tunaelekea wapi...!!!
 
Kuna watu hufanya mambo kimya kimya, lakini matokeo huwa ndiyo yanazungumza kwa sauti kubwa.

Bado hatujui kama Rais Samia Suluhu Hassan ni kiongozi wa aina hii.

Ngoja, wakati ndio mwamuzi sahihi. Matokeo yataonekana au hayataonekana.

Kama hayataonekana, atakuwa ni rais wa maneno matamu tu basi!
 
Being a leader, an individual needs to be creative on various issues concerning with national development in different angles, and then if it comes to a time a national leader is wandering to various state on going manners it is a stressing state to the national correspondent citizen(s). This implies that she is not creative for any thing in fact she is only waiting for abroad states aids and not to look for solutions on different state matters.

The death of Hon. Magufuli is a threat to our nation, since he used his position effectively to solve different social matters to some instances though he had his own weaknesses as all other human beings we are too.

We have been sold under a lowest price in fact. Tunahitaji kujitathmin kama taifa.

# 666 sir 100
 
Habari wanabodi..!
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu .Jana kwenye mkutano wa viongozi wa CCM na waandishi wa habari moja ya swali lililoulizwa na mwandishi wa habari ni kwamba,je kama CCM wapo pamoja?

Kiukweli ni swali ambalo unaweza ukaona la kizushi lakini mwenye kuuliza swali sio mjinga ,inawezekana kuna kitu amekiona ndani ya Chama cha Mapinduzi hakipo sawa.

Ila bila shaka Mh Daniel Chongolo alilijibu kama ilivyotakiwa kujibu kwamba tupo sawa kabisa .

Ila kwa maoni yangu binafsi naona kama ndani ya CCM kumeibuka waumini wa imani au nadharia mbili kuna wale waliokuwa wanaamini nadharia ya Hayati JPM na kuna wale walio amua kubadilika na kukubaliana na nadharia mpya ya uongozi ya mheshimiwa Samia Hassani.

Hawa wanaoshikiria nadharia ya JPM ndio wale waliogoma kumzika JPM katika mioyo yao,hivyo basi mwenyekiti wa chama,Shaka,Chongolo wanatakiwa wajipe assignment ya kuhakikisha kwamba wanaishi katika kivuli na maono ya JPM kwa sana kuendeleza yale yalio mazuri ili wale ambao hawaja mzika hayati JPM kwenye mioyo yao waendelee kuona kama bado JPM yupo madarakani mpaka pale atakapozikwa.Maana hawa ambao bado hawajamzika JPM mioyoni mwao ndio wale wanaoamini JPM bado ni rais wa JMT.

Sijuhia naeleweka hapa kweli,kam haujaelewa bora tu utulie maana uta mix madesa?
 
Itachukua muda sana mama kumfuta JPM mioyoni mwa watu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…