Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Fao la kujitoa sio in

Fao la kujitoa sio interest ya mtu mmoja ni suala la kitaifa na kisera zaidi. Vijana wengi walioajiliwa sekta binafsi ni wahanga wa hili na wanapomaliza mikataba yao ni vyema wakapewa pesa zao ili wakajiajili kuimarisha uchumi. Serikali pekee haiwezi kuajili vijana wote hivyo wengi lazima wajiajili na kwa wale wanaoajiliwa sekta binafsi wapate mwendelezo wa kukuza uchumi pindi mikataba yao inapoisha
Wahanga wa mabadiliko wa fao la kujitoa ni wengi. Lakini ukitaka kuelewa maumivu yao - Ni wale wanaofanya kazi migodini. Hivi kweli na nature ya kazi hizo - mfano underground excavator operator au gold room operator akiacha kazi unamsubirisha hadi afikie umri wa kustaafu? Really is it fair? Ilhali tunajua lifespan yake imeshuka mno na huo umri anaweza asiufikie wa kustaafu.

Kama tuna nia njema kwamba tunawajali raia wote uzeeni, basi na wao waheshimiwa wasubirie Pension hadi pale watakuwa wameachia jimbo. OVA.
 
unaongelea interest zako vs interest za taifa.
afanye unachotaka ndio utaona amefanya kitu? since when anafanya mambo kumridhisha mtu fulani?
Mbona kumkamata sabaya ni interest ya chadema na imetekelezwa kwaio na interest ya ndugu yetu hapa itekelezwe tu
 
unaongelea interest zako vs interest za taifa.
afanye unachotaka ndio utaona amefanya kitu? since when anafanya mambo kumridhisha mtu fulani?
Fao la kujitoa ni interest ya wafanyakazi wote wa sekta binafsi. Kazi yangu ina mkataba wa miaka 3 iweje nisipewe hela yangu mpaka nifike miaka 55?


Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Ulaaniwe uzao wa aliyepitisha sheria hii kandamizi huku yeye mwenyewe hausiki katika mateso ya sheria hii
 
Ahhh sawa mama Samia awe mtumwa wa Wananchi lakini akitaka wananchi ndo wawe watumwa wake basi hapa ujue hatafanya lolote miaka yake hii minne tofauti na kudharaulika.

Magufuli kafanya kazi ngumu na yenye manufaa sana kurudisha nchi kwenye mstari inapaswa aendelee huyu mama kuiweka mstari myoofu zaidi ila akiteleza tu tunajikuta tuko maporokoni kama ya awamu ya 4 iliyokuwa imejaa vituko visivyoelezeka hata kidogo.
 
Mifuko hiyo ya hifadhi ya jamii haina hata senti unadhani Mama atalifanikishaje hili within a short time?..

Tuwe realistic bhana.

Kuna mambo mengi zaidi mama anayopaswa kuyatilia mkazo kwani yanarekebeshika fasta..sio hili.
Hiyo hela imeenda wapi? Kama ilichangwa maana yake inatakiwa kuwepo na kama haipo aliyeitumia airudishe watu wapate stahiki zao.

Kuna mambo ya kuyapa muda sio hela ya wavuja jasho. Mbona hela za wabunge na madiwani zipo.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo hela imeenda wapi? Kama ilichangwa maana yake inatakiwa kuwepo na kama haipo aliyeitumia airudishe watu wapate stahiki zao.

Kuna mambo ya kuyapa muda sio hela ya wavuja jasho. Mbona hela za wabunge na madiwani zipo.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Tunajenga kwa fedha zetu za ndani hukuwahi kuisikia?..mixer madege yasiyokuwa na kichwa wala miguu..plus project za majengo ambazo hazirudishi faida.

Mimi nadhani inabidi tumpe mama ili serikali ipeleke fedha kwenye hiyo mifuko..kwani hata ulipaji wa mafao kwa wazee wetu imekuwa ni danadana nyingi coz hamna hela ya kutosha.

Na Mama alisema ataipatia hii mifuko fedha..ninachoamini ni kuwa haliwezi kuwa jambo ya siku mbili.

Fao la kujitoa nakubaliana na wadau kuwa ni zuri hasa kwa vijana wanaofanya kazi za mikataba.
 
Unakuta mbunge anajisifia kusema watu wangu. Huku hao watu wakiteseka, fukara. Shule majengo shida, huduma za afya tabu. Mtu mmoja analipwa mamilioni.

Hakuna haki. Wabunge wenyewe majimboni hawaonekani. Wakienda Bungeni maswali ni yale yale toka nazaliwa hakuna linalo badilika. Utasikia korosho, Pamba, ufugaji, madini, elimu. Hivi haya yote hayajapata ufumbuzi toka wakati wa Nyerere hadi Leo! Miaka 60 tunaongelea jambo lile lile!

Ulaya ya miaka ya hamsini na tisini ilikuwa masikini si kama ya Leo. China, Malyasia, India, Korea na nyinginezo walikuwa masikini.
Je sisi watanzania tumelaniwa nini? Nyerere alitupatia viwanda leo vyote hakuna.

Shida ni nini? Nilibahatika kufanya kazi serikalini, nilipo ingia nilishangaa mengi. Hapo nikajua Tanzania kwendelea ni kazi. Tutapiga mark time.

Tunahitaji kubadili mfumo wa kiutumishi. Tunahitaji kubadili matumizi ya fedha na mshahara. Tunahitaji kubadili mfumo wa utekelezaji wa miradi.

Pia kubadili mfumo wa Bunge. Na kuwa na wabunge wachache. Kufuta viti maalum. Na wabunge wawajibishwe mara wanapokuwa si wawajibikaji.

Hivyo tunahitaji muundo mpya wa serikali. Hata baraza la mawaziri hatuhitaji utitiri wa mawaziri.

Kuna mtaalamu wa ujenzi ni Afisa mkubwa walijenga barabara isiyo na kiwango ktk kumhoji akanambia akijenga ya kiwango yeye na familia yake watakula nini?

Anajua hyo isiyo na kiwango baada ya muda itahitaji matengenezo hivyo atapata fedha. Nilichoka!

Afisa mmoja mkubwa anateuliwa na Rais akanambia usipo kula fedha ya serikali wengine wanakula. Usiangalie kuendeleza nchi. Jiendeleze mwenyewe.

Baada ya muda niliona niache kazi ya serikali na kufanya kazi katika mashirika ya kimataifa.

Tuombeni na kudai Katiba mpya. La sivyo hata vyama shindani vikiingia bado ni yale yale.
 
Ile ndege ndogo ya Rais ile ya jamhuri ya muungano walipewa ATCL na sasa hivi Rais anatumia madege makubwa makubwa ya ATCL katika route zake🐒🐒🐒

Ni mambo ya kijinga sana ambayo hata mtoto mdogo wa chekechea hawezi kufanya.Halafu kama unavyojua kwa sasa hivi Tanzania haina bunge kwa hiyo hakuna wa kuuliza kuhusu hilo suala.
Umeiona hiyo ndege ya Rais huko ATCL mkuu au umeandika tu!
 
MAMA SAMIA; UNAPOTEZA MUDA WAKO KAMA HUTOFANYIA KAZI HILI,

Kwa Mkono wa, Robert Heriel

Miaka mitatu iliyopita niliandika makala yenye ujumbe wa namna hii nikimtonya aliyekuwa Rais wa wakati huo, Hayatti John Magufuli. Nilimwambia JPM kuwa anapoteza muda wake tuu, na nilizifananisha mbio zake kama mbio za sakafuni ambazo hufika ukingoni kwa upesi.

Mhe. Rais, Samia Hassan Suluhu, usijesema ninadharau uyafanyao isipokuwa nakutonya siri ambayo itakurahisishia kazi ya kulifanya taifa hili kuwa taifa tajiri.

Watu wengi walinipinga, na huenda hata leo wakanipinga, sikatai kupingwa lakini kabla sijapingwa naomba utulivu wa fikra zenu katika jambo hili. Kwa yeyote anayetaka kuongoza taifa hili basi aniazime utulivu wa fikra zake kisha badaye tutajadili kwa kina.
Andiko hili halitamhusu Mama Samia Hassan pekeake bali litawahusu viongozi wote ambao wapo kwenye nafasi kubwa za kufanya maamuzi, pia wale wote wenye ndoto za kuongoza nchi hii.

Mama Samia Suluhu ambaye kwa sasa ni Rais wa taifa letu atahesabika kama kiwakilishi cha viongozi wote wakuu mliopo na mtakaokuja kuongoza nchi hii. Aidha mawazo haya kuchukuliwa ama kutokuchukuliwa haitanifanya nilete chuki kwa washauriwa isipokuwa itakuwa ni wajibu wangu kuyasema yale ninayoona ni nafuu kwa taifa.

Mhe. Rais, ninapenda kukupongeza kwa jitihada kadhaa ulizochukua katika kuleta unafuu katika nchi yetu kama vile ulivyonavyo, hata hivyo natambua yakuwa haupo pekeako, kwani Urais ni Taasisi.

Hatuwezi endelea katika nchi yetu pasipo KUFANYA UVAMIZI NA KUNYONYA WENGINE, hili nitalisema kila siku iendayo kwa Mungu dunia ingalipo mimi nikiwepo. Bila UVAMIZI hakuna maendeleo. Binafsi naamini Maendeleo ni Uvamizi wa maeneo mengine duniani na kuyanyonya.

Hatuwezi endelea kwa kutumia Rasilimali zetu pekeake, hatuwezi endelea kwa kutegemea raia wetu pekee. Huo ni uongo wa mchana kweupe. Siku nchi yetu itakapojua kuwa ili tuendelee tunapaswa kuvamia wengine na kuwanyonya vilivyo ndio siku hiyo hiyo tutaweza kuendelea.

Hakuna nchi yoyote duniani iliyoendelea kwa kutumia wananchi wake pekee na rasilimali zake pekee, nchi zote duniani ziliendelea kwa kuvamia mataifa mengine na kuiba kama sio kunyonya mali za nchi zingine.

Taifa la Misri liliendelea kwa biashara ya utumwa ambapo lilichukua watumwa mahali mahali na kuwaleta nchini Misri kufanya kazi za vibarua ambazo Kuwatumikisha wamisri wenzao ingekuwa jau. Hata Waisrael walishawahi kuonja joto la jiwe huko Misri.

WAMEDI, WAAJEMI, WAASHURU, WAGIRIKI, WARUMI wote waliendeleza maeneo yao kwa kuenda kuvamia mataifa mengine na kuiba mali kama madini, mifugo, na watu wenye nguvu kama watumwa.

Wafaransa, waingereza, Wareno, Wajerumani, Wahispania, Waitaliano miongoni mwa wengine walivamia mataifa mengine na kuyageuza makoloni yao, walichuma mali na kunyonya nguvu za makoloni yao mna kujenga nchi zao.

Mataifa kama Japan, Marekani, Uchina, Urusi yamevamia mataifa mengine kwa mtindo wa Uwekezaji na ukoloni mamboleo, teknolojia miongoni mwa mambo mengine.

Mifano hiyo michache inadhihirsha kuwa huwezi endeleza nchi yako kwa level za juu kimataifa pasipo kuvamia wengine na kuwanyonya iwe kwa mabavu au kwa hiyari yao wenyewe.

Taifa letu lazima ifikie hatua tuweke mikakati ya kusaidia watu wetu wapate unafuu na sapoti ya kuweza kuvamia mataifa mengine na kuyanyonya.

Unajua kuchukua kodi kwa raia mwenzako ni noma tofauti na kuchukua kodi kwa raia wa nchi zingine. Kumtumikisha ndugu yako ni kazi zaidi kuliko kumtumikisha mtu baki.

Kanuni inasema, usipovamia unavamiwa, usipokula wenzako basi utaliwa na wenzako. Hiyo ndio kanuni inayoongoza dunia. Usiponyonya utanyonywa. Hakuna nchi iliyoendelea hapa duniani bila kunyonya mataifa mengine, hakuna nchi masikini duniani bila kunyonywa na mataifa mengine. Hakuna.

Nchi yetu imevamiwa kila upande, imezingirwa kila pembe, tumevamiwa kiutamaduni, dini tulizonazo zote ni uvamizi wa kipekee unaozalisha mamilioni kwa mamilioni ya pesa kwenda nchi za dunia ya kwanza. Madhehebu yote makubwa hapa nchini makao yake makuu yapo nchi zilizoendelea. Na sehemu ya kipato cha sadaka huenda huko.

Zile sisi tunaziita Sadaka lakini zile ni pesa na ni mradi ambao ungeweza kuiletea nchi faida. Mapato ya vitabu, vijarida, huduma za kijamii, dhana za muziki nk, hupandisha uchumi wa mataifa hayo.

Ingefaa nchi yetu iwe na dini yake, naamini wapo watu werevu wa kutunga sheria za kimila, desturi, miiko, sala, dua, mavazi, vyakula, ujenzi, kilimo, miuujiza nk ambazo zitaingizwa katika kitabu cha muongoz ndani ya dini yetu. Ili tuwe huru. Nafahamu ni kazi kuanzisha mambo haya lakini hata hizi dini za uvamizi tulizonazo hazikuanzishwa kirahisi, zilianzishwa kwa ugumu tena kwa damu na machozi.

Tayari baadhi ya Watanzania wenzetu washaenda KUVAMIA kwenye mataifa mengine, hawa huitwa walowezi kama sio Diaspora. Serikali inapaswa iwatambua, iwachukulia kama raia wenzetu. Wazalishe huko na kuleta utajiri huku, wakatwe kodi. Mbona wale Ma-explorer, Wamishenari na wafanyabiashara walikuwa wanarejesha mali kwao, kwa nini hawa wetu wasiwekewe utaratibu.

Serikali ipunguze mlolongo katika kuchukua Hati ya kusafiria, iweke utaratibu mzuri wa vijana kuchukua hati hizo na kutafuta pembe za kwenda kusaka maisha. Serikali isiogope ku-take Risk kama kuna vijana wanaotaka kujitoa mhanga. Mbona Kenya, Nigeria wameweza, huu ni muda wa kuvamiana sio kuvamiwa.

Tumeshaona kila uchwao Wachina, Wahindi, mataifa jirani wanavyovamia nchi yetu kung'ang'ania Mali. Serikali isiogope.

Kila siku tunawaona kwenye vyombo vya habari Mamia ya Waethiopia na wasomali wakipita nchi yetu kwenda kuvamia South Africa na maeneo mengine, viongozi wetu hiyo muichukue kama changamoto, changamsheni vijana wetu wawe na hiyo spirit ya kuvamia pasipo woga, unapozima spirit za hivyo ni kuzima maendeleo ya nchi pasipo kujua.

Inafahamika wazi kuwa ni rahisi kufanikiwa ukiwa mbali na nyumbani ukilinganisha na ukiwa nyumbani.

Haya vamia Congo huko, hao vijana wanaojifanya wanapenda upanya road, ujambazi, kusanya wote, peleka jeshini, fundisha mapambano, chukua wote peleka msituni Congo, chukua madini. Imeisha hiyo.

Kila fursa itumiwe ipaswavyo, sio unakamata jambazi unaua, au unafunga unajipa kazi ya kulilinda na kulipa chakula, peleka msituni huko likalete pesa kwa utaratibu maalumu.

Mataifa makubwa yanajua kucheza na mambo ya uvamizi, kuunda vikundi vya waasi au Magaidi makusudically kwa ajili ya kuzalisha uchumi hiyo kwao ni fursa nono wasiotaka iwapite.

Mataifa makubwa hayapotayari kuona fursa yoyote inawapita, mataifa makubwa yanajua ni ngumu kuzuia uovu na mauaji kutoweka duniani hivyo wanaona watumia hao wapenda uovu kujizalishia utajiri.

Mataifa makubwa yanajua kuzuia umalaya ni jambo ambalo lilishashindikana, kama ni hivyo basi wakaona hiyo waigeuze fursa na kuiwekea utaratibu, wakapitisha ikawa ni biashara kama biashara zingine, watu wanalipa kodi, watu wanacheza pono wanauza kwenye mataifa mengine, wanapata pesa.

Sasa lazima tuwe na akili kama ulimwengu huu, ni kweli tunamaadili ila tujue sio wote wenye hayo maadili, na kuyazuia hatuwezi, ndio maana kila mara picha za uchi zinavuja, ingefaa watu wapendao huo mchezo, wachukuliwe wawekewe utaratibu, warekodiwe, ziuzwe nchi zingine watu wajipatie kipato nchi iendelee.

Pengine nikaonekana nimechanganyikiwa lakini ikiwa jambo lolote unalichukia na hulipendi lakini huwezi kulitowesha basi litumie kama fursa kukuzalishia na kukuingizia kipato. Huo huitwa Uvamizi wa kitu usichokipenda.

Wazungu tangu zamani hawatupendi, kutuua wote hawawezi, hivyo kwa sasa wanatutumia kama fursa kwao, na wanajipatia utajiri kupitia sisi wasiotupenda, hiyo ni akili.

Sio kila kitu usichokipenda ukiondoe na kukiangamiza, vingine vitumie kama fursa. Hiyo ndio Akili

Kwa mfano Pombe kidini sio nzuri lakini kuiondoa pombe duniani ni Uongo, yaani haiwezekani kwa sababu wapo wanaoipenda, hivyo serikali zenye akili zikaona kuzuia pombe tumeshindwa sasa tuifanye kuwa fursa, hiyo ni akili

Naweza andika mambo mengi, andiko likawa refu jambo ambalo watu wengi hawapendi,

Lakini lengo langu ni kuwatonya viongozi kuwa nchi hii hatuwezi endelea kwa kutegemea wananchi wa ndani, huko ni kuumizana tuu na kufanya watu wasiwe wazalendo.

Ziundwe kamati zenye watu wenye akili, wanamikakati, wanausalama, wenye roho ngumu, wanataaluma waunde mipango ya kuvamia mataifa mengine.

Kumbuka; Tusipovamia tutavamiwa. Hata hivyo tusipovamia sasa bado itatupasa tuvamie baadaye. Kuvamia hakuepukiki. Tusiwe na aibu ya macho.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
 
MAMA SAMIA; UNAPOTEZA MUDA WAKO KAMA HUTOFANYIA KAZI HILI,

Kwa Mkono wa, Robert Heriel...
Umeandika wazo fikirishi, lakini likitekelezwa kwa umakini na watu makini linatekelezeka na linatoa matokeo chanya.

Naomba weka katika inbox yangu nitakuita tulijadili na kuliwakilisha. Na kuomba sana tena sana usikumbatie wazo lako tuu.
Kubali kuchukua mawazo bora ya wenzake yanayo weza kufanyiwa kazi.

This is pure imperialism and it is how the world runned. It can be mutually transfered to normal business undertakings. A serious contribution for the second time from JF within my entire period of membership in this platform.

Thanks so much for this piece of divine contribution.
 
Kayafa alipoipeleka ATCL ulipitwa na habari hizo?
Usiishi kwa theory mkuu. Nakuuliza tena, hiyo ndege umewahi kuipanda au kuiona huko Atcl au umeng’ang’ania na aliyosema uliyemwita Kayafa! Fanya utafiti.
 
Usiishi kwa theory mkuu. Nakuuliza tena, hiyo ndege umewahi kuipanda au kuiona huko Atcl au umeng’ang’ania na aliyosema uliyemwita Kayafa! Fanya utafiti.
Nifanye utafiti wa nini wakati Kayafa aliagiza ndege ipelekwe ATCL?
 
Wakaribishwe wawekezaji kweny usafirishaji turakufa na korona na mbanano huu wa daladala..tusaidieni
 
Back
Top Bottom