Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Ushauri awafute kazi Mwigulu, Bashiru, Olesabaya, DPP, Mkumbo, Ndalichako, Jafo, Kabudi, Gwajima na timu yake yote wizara ya afya, RC Mbeya, Mambosasa, RPC Dom n.k
Umemsahau, Doto James Katibu mkuu hazina, gavana wa bank kuu, engineer Nyamuhanga katibu mkuu Tamisemi, engineer Patrick Mfugale , RC Njombe, RC Iringa, mkurugenzi wa ATCL, TBS,TCRA, doto Biteko.
 
Karibu mama Samia na ninakuombea kwa msaada wa Mwenyezi Mungu akuongoze ktk njia ya haki,hekima na utu vitu vilivyokuwa vimepotea ktk Tanzania kwa miaka mitano iliyopita. Umtangulize Mungu ktk kazi zako zote!

Natambua umerithi taifa lililogawanyika sana lakini nikuombee uliunganishe tena taifa wananchi wapendane bila kujali itikadi,ukabila,rangi,dini na tofauti zetu za maoni.

Mama pambana kuinua tena uchumi wetu na biashara zifufuke tena! Pambana ktk mapambano ya haki kutokomeza rushwa na wizi serikalini. Pambana kusafisha serikali yako kwa kujitenga na kuwachukulia hatua za kisheria wakubwa serikalini ambao walikaa kimya au walishiriki ktk mauaji na kuwatesa raia!

Iangalie upya Idara yetu nyeti ya Usalama wa Taifa kama inakidhi mahitaji yetu ya sasa. Isafishe Polisi kwa kuwaondoa makada wa CCM wabakie ktk kunadi sera za CCM kwa magwanda ya kijani. Safishi safu yako ya ma RC,DC na Wakurugenzi wa Miji,Manispaa na Majiji.

Rudisha demokrasia na haki za kiraia kwa kuruhusu mchakato huru wa Katiba mpya! Utakumbukwa kwa miaka mingi na Watanzania watakao zaliwa miaka ijayo. Itakuwa njia ya kuwafungulia akina mama kuongoza nchi hii. Jihadhari sana na wanasiasa wanafiki,wezi,wauaji na waongo! Jihadhari na team ya mtangulizi wako kwasababu wamelitia taifa aibu kubwa!

Safisha miji yetu mikubwa kwa kuondoa biashara ktk barabara na baraza za watembea kwa miguu! Wajengee wamachinga maeneo mazuri ya kufanya biashara na usafiri wa kuaminika ktk maeneo yao. Haiwrzekani miji yetu mikuu iendelee na holela kama tunavyo shuhudia.

Mwisho mama saidia ktk mapambano ya corona na upatikanaji chanjo mapema uweze kuirudisha mapema sekta ya utalii ktk ushindani na kulinda maisha ya Watanzania. Wagonjwa wenye matatizo ambayo yanahitaji utaalamu ambao haupo nchini wasaidie wapate tiba nje!
 
Kwanza nitoe pongezi kwa Mama yetu mpendwa, Rais Samia Hassan Suluhu. Mama kilio chetu kikubwa kipo kwenye biashara na kilimo. Mama bora umekuja utufungulie mipaka tukauze mazao nje ya nchi jamani hali ni mbaya mchele super umefika 1200.

Watu magunia yanawaozea ndani. Lingine mama ni hawa TRA. Mama naomba ondoa taskforce kwenye swala la ukusanyaji kodi tunateseka Mama. Pia tazameni upya mienendo na hizo kanuni mama tunatetekea watoto wenu mliotutuma tukajiajiri. Naimani mwaka huu wengi watafungua biashara badala ya kufunga.

Mama ukigusa hapo mbona burudani🙏🏽 Ni hayo tu mama. Asante.
 
Mh Rais Mama Samia, ombi kubwa kwako ni kutoa tamko la kudhibiti ugonjwa wa covid19 (Corona) na pia kukubali kuagiza chanjo (Vaccine).

Mh. Rais, mahospitali yote nchini yamejaa,wengi ni wale wanaougua ugonjwa wa kushindwa kupumua na tatizo ni ukosefu wa vifaa vya upimaji kama huu ugonjwa ni upi haswa.

Lakini madaktari wengi wanatudokeza kuwa wapendwa wetu wanaogua wana kila dalili za covid 19.

Tunaomba tuige wenzetu kwa kuweka hatua za kudhibiti ugonjwa huu na kuwaruhusu mahospitali yote, hasa ya binafsi kuingiza nchini chanjo,chini ya uangalizi wa Wizara ya Afya na Vyombo Vingine Husika.

Tuhamasishe kuvaa barakoa,kupiga marufuku mikusanyiko,maharusini,misibani,mpirani n.k,kunawa mikono,sehemu za ibada za Wakristo na Waislamu ziwe na utaratibu wa Waumini kukaa mita 2 kati yao(Distancing)n.k.

Sie Mh Rais tunaishi duniani kama nchi nyingine. Sote kwa pamoja tuupige vita ugonjwa huu hatari.
 
Salimia ni.moja tu Korona Ipo.au Haipo Tanzania.Kama ipo jibu tifuate Nokia za Kisayansi na Kama.

Haipo tuendelee Kujifukiza na Kumwomba Mungu.as of Mumgu Makao take makuu ni Tanzania.

Wait wangu wanaangamia kwa Kukosa Maarifa...Joseph.
 
Waanyakazi wa afya wapimwe kila baada ya wiki tatu, nani anajua kama wao pia wanaeneza igonjwa kwa wagonjwa wengine.

wanunuliwe PPE za kutosha.
 
Seconded, najua Raisi mama yetu atalibeba na hili mwanzo mzuri sana bandali,hope wizara ya fedha ,BoT nk wataguswa na magereza wenye kesi siso isha bravo kwa maelekezo yako juzi wakati wa mapokezi ya CAG report
 
Waanyakazi wa afya wapimwe kila baada ya wiki tatu, nani anajua kama wao pia wanaeneza igonjwa kwa wagonjwa wengine.

wanunuliwe PPE za kutosha.
Washauri UK huko dada huku sisi hatuna habari na Corona tunaendelea na mambo yetu tu.
 
Consiparation theory ivi Tz hakuna corona hata mtamuua kila mtu ninyi makuwadi na vibaraka wa mabeberu,tunaendele kuikataa corona kama tulivo ikataa chadema
 
Mh Rais Mama Samia, ombi kubwa kwako ni kutoa tamko la kudhibiti ugonjwa wa covid19 (Corona) na pia kukubali kuagiza chanjo (Vaccine).

Mh. Rais, mahospitali yote nchini yamejaa,wengi ni wale wanaougua ugonjwa wa kushindwa kupumua na tatizo ni ukosefu wa vifaa vya upimaji kama huu ugonjwa ni upi haswa.

Lakini madaktari wengi wanatudokeza kuwa wapendwa wetu wanaogua wana kila dalili za covid 19.

Tunaomba tuige wenzetu kwa kuweka hatua za kudhibiti ugonjwa huu na kuwaruhusu mahospitali yote, hasa ya binafsi kuingiza nchini chanjo,chini ya uangalizi wa Wizara ya Afya na Vyombo Vingine Husika.

Tuhamasishe kuvaa barakoa,kupiga marufuku mikusanyiko,maharusini,misibani,mpirani n.k,kunawa mikono,sehemu za ibada za Wakristo na Waislamu ziwe na utaratibu wa Waumini kukaa mita 2 kati yao(Distancing)n.k.

Sie Mh Rais tunaishi duniani kama nchi nyingine. Sote kwa pamoja tuupige vita ugonjwa huu hatari.


Jaribu ku tafuta video ya Dr Colman Vernom anasema matumizi ya vaccine ni mauwaji

PolitiFact › feb › d...

Doctors administering COVID-19 vaccines aren't guilty of ... - PolitiFact

Claim: Doctors and nurses who administer the coronavirus vaccine can be "tried as war criminals."
Claimed by: Bloggers
Fact check by PolitiFact: Pants on Fire
 
Nyie vihere here mnaotangaza kuwa corona ipo Tanzania ndio mnafanya nchi ijawe na hofu, kama hao wanaowapa chanjo ya corona kwanini wasiwape chanjo ya Ukimwi na maralia au wawapeni dawa kabisa ya kuponya ukimwi, mbona mnausahau ugonjwa wenye miaka dahari,
 
Kwanini mnalazimisha kila mtu kuwa muoga!?... Umeshawahi kupanda mwendokasi asubuhi au jioni!?.., hakuna cha balakoa wala nini na watu wanajaa vibaya, hiyo Corona ingekuwa hatari Kimara wote wangekuwa wanauguza. Tanzania imechagua njia iliyoichagua ku deal na Corona. Uliwahi muona Samia na barakoa!?,hujiulizi kwanini!?, Kama unataka jifungie na familia yako,wahimize wavae barakoa, wasiende popote wajifungie tu. Mwende Kenya mkachanjwe halafu mrudi. Wengine mtuache maana mmechagua kufata njia hizo. Wazungu kibao wanapinga hizo chanjo.
 
Back
Top Bottom