Tz baada ya kukaa miongo kadhaa katika ombwe la uongozi, lilitokea jiwe/mwamba ambalo lilichotamka ndicho kilitekelezwa kwa spidi ya mwanga! Kabla yake alikuwepo John Walker, wengine wakimuita Vasco da gama, huyu alitamka mengi lakini hayakufuatwa na vitendo!
Kipindi cha jiwe ilikuwa ukilishawishi jiwe likaelewa na kusema ndio basi unashangilia kuwa imepita hiyo, na kinyume chake ni sawa!
Tumemsikia Mama yetu mpendwa SSH akiongeaongea sana na mara nyingine anajinukuu mwenyewe na mpaka kufikia kujisemea kuwa yeye na jiwe ni kitu kimoja!
Mama hayo maneno yako yote, kwa watz waliozoea vitendo vikifuatia maneno ya mfalme jiwe, hayana maana yoyote kama hutajifunga nguo vizuri na kusimama kidete kuhakikisha yote mazuri ya Magu yanaendelezwa kwa kasi ya mwanga na kamwe usijichanganye na lile kundi nyemelezi likakuondoa mureli!
Mungu tunakuomba uzidi kuilinda na kuibariki nchi yetu Tanzania, amen🙏!