Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Mwendazake ametuathiri wengi hasa Sisi watumishi, naingia mwaka wa6 sijui nyongeza ya mshahara wala daraja jipya.
Mshahara umezidi kupungua kwa makato ya Loan Board
 
Nikusalimu kwa jina la Jamhuri. Ikumbukwe huyu mama (Janeth) alikuwa bado ni Mtumishi wa Umma hivyo akachukua likizo bila malipo.

Ni muda sasa umrudishe katika utumishi wa Umma amalizie muda wake wa kustaafu.
 
Ikimpendeza ukimaanisha kwa utashi wake, hapo siwezi kuingilia maamuzi yake.

Ila kwa ushauri wangu tu, huyo mama vyema akatulia nyumbani au aendelee na majukumu yake ya mwanzo, yale makelele ya kule bungeni na zile kambi zilizoibuka yatamrudishia maumivu tu,

Hata akipewe hiyo nafasi vyema aikatae apumzishe akili yake.
 
Nikusalimu kwa jina la Jamhuri....ikumbukwe huyu mama (Janeth) alikuwa bado ni Mtumishi wa Umma hivyo akachukua likizo bila malipo...

Ni muda sasa umrudishe katika utumishi wa Umma amalizie muda wake wa kustaafu
Dooh..
Kwa hiyo nafasi ya ubunge itolewe tu kama rambi rambi, au?!!!
 
Bado tunasafari ndefu sana kama TAIFA katika kupiga hatua. Inabidi tuondokane na watu wa kujikomba kwenye system na tuondokane na maprofesa waliogushi elimu.
 
Hahaaaaa mhishimiwa supika kwanza nikurudishe nyuma mme wangu angekuwepo hii hoja msingeileta hapa yaani wooote sukuma ndani kabla hahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Nikusalimu kwa jina la Jamhuri....ikumbukwe huyu mama (Janeth) alikuwa bado ni Mtumishi wa Umma hivyo akachukua likizo bila malipo...

Ni muda sasa umrudishe katika utumishi wa Umma amalizie muda wake wa kustaafu
kwamba hiyo nafasi inatolewa kama shukurani? hongo au kujipendekeza?
hakuna cheo cha asante.
 
Hongera sana mama kwa kuapishwa kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.

Sasa baada ya Tanzania kupata uzoefu wa kutosha kutokana na awamu zake za uongozi, na tukaona mazuri na mapungufu yake, na wewe pia kupata uzoefu wa kutosha chini ya Mzee Magufuli ninakuomba haya yafuatayo:

Kwanza, usiturudishe nyuma tena. Awamu ya tano imetuonyesha nini maana ya uhuru na kujitegemea. Tanzania haina mjomba wala shangazi huko nje. Maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe. Jukumu lako ni kutupanga, kutuvuvia, kutushawishi na kutuonyesha kwa mfano wako wewe mwenyewe kwamba inawezekana, tunaweza, tusonge mbele.

Pili, Mzee Magufuli kafa, lakini spirit yake haijafa. Ni askari aliyefia vitani akiwa mstari wa mbele, katika kupambania uhuru wetu na kujitegemea kwetu. Usije kufanya kosa kufanya mapungufu ya style ya Magufuli ya uongozi iwe kigezo cha wewe kubadili uelekeo wa nchi yetu, katika kujiamini na kuthubutu. Magufuli kafa lakini kaacha alama na kaacha spirit. Wenye hiyo spirit wamo ndani ya chama tawala, vyama vya upinzani, serikalini, sekta binafsi, na kwa wakulima na wafanyakazi. Hili ni jeshi kubwa sana usicheze nalo.

Tatu, tutakusikiliza kwa umakini, tutakuangalia sana mienendo yako, tutatizama sana namna zako kama zinaturudisha nyuma au zinatupeleka mbele. Nisiseme sana katika hili lakini itoshe tu kwamba spirit ya Mzee Magufuli haijafa. Tukiona tu dalili kwamba unakotupeleka siko hatutakuvumilia. Tushaonjeshwa uhuru hatutarudi tena kwenye utumwa. Tushaonjeshwa kujitegemea hatutarudi kwenye utegemezi tena.

Mwisho, Mungu akupe hekima ya kuongoza watu milioni 60, kwa akili na ujasiri. Ninaamini utatuvusha salama, karama ya uongozi unayo, itendee haki. Tegemea ushirikano wetu.

Pia soma: Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli
Hiyo familia haijikwezi kwa fadhila hizo na naamini hauwezi kukubali mambo ya siasa tena. Hata watoto wake usitarajie wakajiingiza huko
 
Tunajitaji kiongozi ambaye ndiye bora katika wale wanaozungumza.
Kiongozi ambaye Hana lawama, kiongozi ambaye vitivo vyake(faculties)vimetulia.
Kiongozi ambaye watu wote wanaompinga hawawezi kumfanya atetereke, kiongozi mwenye kuelewa upeo wa juu kabisa wa ukweli.
Kiongozi wa Chama ambaye mwenendo wake ni mkamilifu na dhamira zake ni kamilifu.
Kiongozi ambaye amejikita katika kutafakari.
Kiongozi ambaye Hana tabia ya kuona uchungu au kukata tamaa, ambaye Hana hofu wala uchovu.
Kiongozi ambaye ana uvumili u kwa watu; ambaye hagandamani na watu lakini pia hagombani nao.
Kiongozi wa Chama anapaswa kuwa na akili ya wema wakati wote.
Katika kila uwanja maarifa yake yanapaswa kuwa mengi.

Tunataka kiongozi ambaye anaweza kuwaunganisha watu, ambaye akizungumza watu wanakuwa na utengamano,furaha na utulivu.
Kiongozi ambaye anazungumza maneno matamu,yenye hoja na dhahiri.
Kiongozi ambaye hashirikiani na wapumbavu,wenye maoni yasiyofaa,ambao ni waongo,wanaozungumza maneno ya kashfa,ya ukali au wanadanganya.
Kiongozi ambaye anashirikiana na wote ambao wamenyooka,hawada nganyi,ambao kila wakati hufanya kazi baada ya kuzingatia athari ya matendo yao.
 
^Ndugu zangu, najua mtanikumbuka^ Kiongozi ambaye anaogopa lawana amepoteza sifa ya uongozi. Bi Mkubwa ametuangusha sana sisi Watanzania
 
Panueni vizuri dawa ipenye vizuri 😁😁 Nyie ni vibaraka wa mabeberu ambao mnatumika kwajili ya maslahi ya mabeberu ili kujaribu kuiweka nchi hatarini kwa kukosa amani, acheni uchochezi na kuwatumikia mabeberu
 
Tumuombee mama na tumuunge mkono. Mwendazake ilibidi afe tu taifa lipone la sivyo angeendelea kuishi zaidi ya mwezi tungekuwa kama Haiti.
 
Back
Top Bottom