Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Maoni, Ushauri, Mapendekezo na Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan

Uko sahihi sana mkuu tena bora Hangaya angeenseleaga kukaa kimya tu kuliko alivyoanza kuongea.
Mara tunamwona jobo chamwino eti kaitwa na mama.

Mara anaaza kuchonganisha aliowatumbua na mawaziri, hivi unamweka Lukuvi ofisini kwa waziri mkuu ili afanye nini sasa, Kabudi wa watu eti anasaidia kazi flani flani.
Aisee hata sielewi.
Ukitaka kufurahisha wote, hutomfurahisha mtu.
Unamtumbua halafu unampetipeti. Ndiyo maana 90% ya budget inaishia kwenye uendeshaji maendeleo 10%
 
Hivi karibuni mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia ameonekana kuchukua maamuzi na kutoa kauli zenye kuyumba na kuchanganya umma kwa kiwango kikubwa kiasi cha kuacha gumzo kubwa kwa wananchi mitaani na mitandaoni.

Wachambuzi wa mambo wanaelezea kuwa ugumu wa mambo unaomfikia rais samia leo hii ni kwa sababu ya mambo yafuatayo:

1. Rais alianza madaraka yake kwa mguu mbaya
Wachambuzi wanasema kwa mujibu wa ibara ya 51 kipenge cha 2 cha katiba ya Jamhuri ya muungano, Mara tu baada ya kuapishwa kuwa rais, rais alitakiwa ndani ya siku 14 apeleke jina la waziri mkuu bungeni likapigiwe kura, wachambuzi hao wanasema hata kama angetaka angeweza kulirudisha jina la waziri mkuu huyuhuyu aliyeko sasa, lakini kwa bahati mbaya hakufanya hivyo kitu kinachowafanya watu wahoji hata uhalali wa serikali yake mwenyewe kwa mujibu wa katiba

2. Mgongano wake na Spika Ndugai umeugawa umma
Kiufupi asilimia kubwa ya wananchi wanasapoti kauli ya Ndugai kuwa deni la Taifa linazidi kukua kwa kasi na wananchi wanahofu licha ya wataalamu kujaribu kulielezea kuwa bado ni himilivu. Hata hivyo hasira na vicheko vya wananchi kutokana na kadhia iliyomkumba Ndugai imetokana na madhambi ya Ndugai ya nyuma na wala si kauli yake ya kuonyesha kutopendezwa na nchi kukopa.

3. Kubadili baraza kisha kujaribu kuwafurahisha aliowatumbua barazani
Mwanzo rais aliwaambia wananchi kuwa anakusudia kubadili baraza jwa sababu kuna watu wana ambition za 2025, mara tu baada ya kuwatumbua akaanza kutafuna maneno yake mwenyewe kuwa baadhi ya aliowatumbua ni watu muhimu sana anawahitaji afanye nao kazi, Wananchi wakashikwa mshangao kuwa ina maana wale watatu waliobaki, wawili wakiwa wahamiaji kutoka vyama vya upinzani ndo walitaka kumng'oa 2025?-wananchi wamegoma kukubaliana na hii kitu

4. Kesi ya Mbowe
Wananchi bado wanafuatilia kwa umakini kesi ya Mbowe, hii kesi ugumu wake wanaihusisha na rais kumhukumu Mbowe jinai wakati wa Interview yake na BBC kabla hata mahakama haijatoa hukumu. Kwa hiyo wananchi wanaichululia kesi ya Mbowe kama "Jambo la Rais"

5. Kauli tata ya kuwaambia wateule wake kuwa hata kama wanakula lakini wasivimbiwe ilimradi tu wajipimie.
Hii kauli imechukiza wananchi mno, ile hasira ya wananchi dhidi ya ufisadi imewaka tena. Watu walitaka kusikia kauli yenye mamlaka ya rais ikikemea ulaji na siyo kuwaambia kuwa walaji anawajua, na kwamba anajua wanakula ila sasa wajipimie, wasivimbewe. Wananchi wanahisi rais hana zeal, au mkazo wa kupiga vita ufisadi

6. Ishu ya katiba mpya
Kuna concensus ya kijamii inajengeka kwa kasi nchini kuwa sababu kubwa ya matatizo yetu nchini ya kiuongozi na hata maendeleo yanapata sababu ndani ya katiba ya sasa. Na kuna kutokuamini hatua za kisiasa za raisi kutumia chombo cha msajili wa vyama cha timu ya kuchakata maazimio ya kikao baina yake na baadhi ya vyama. Raia wengi wana amini suala la katiba mpya kwa asilimia kubwa linahitaji utashi wa rais na wanangoja wauone, kwa hiyo rais alitambue hili.

7. Conclusion
Wananchi wanataka rais arudi ktk. njia kuu, yaani arekebishe mambo na makosa ya kimaamuzi, kikauli aliyoyafanya, otherwise imani yao kwake inapungua siku baada ya siku
Kifupi hatuna mtu hapo, tumepigwa vibaya sana. Aliyeweka kipengele cha kuwa rais lazima awe angalau na degree moja aliona mbali sana., mtu ameinga unga elimu kweli awe rais. Yaami ukimsikilia maamuzi yake ni kama anapata ushauri kwa wake wenza very strange.!
 
Bila katiba mpya na tume huru ya uchaguzi hatutaenda mahali popote, tutapiga mark time tu.
 
Tangu ile Machi aliposema, ^Taifa litakuwa kwenye maombolezo ya siku 14,^ wenye akili tukajua hapa tumepigwa si kidogo!

#KilaMbuziAleUrefuWaKambaYake!
 
Hii nchi tulishapigwa tayari hatuna namna acha waendelee kujipimia.
Hivi Madelu na kiparangoto uwaambie wale ila wajipimie si utakuta sufuria zima halipo matokeo yake wazee wangu wanaostaafu NSSF na PSSF watajuta kuzaliwa kwa kipindi hiki.
Samia ameishashauriwa kuwa Madelu hapo wizara ya fedha hafai, lakini hasikii. “ Sikio la kufa halisikii dawa”
 
Mh Rais nakusabahi kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ndugu na Mh Rais, Nina hakika utakuwa umeskia kauli ya kijana wako Patrobas Katambi, dhidi ya vijana wa Kitanzania.

Mh Rais nina hakika utaungana na mimi sifi leo kuamini yakuwa hiyo ni kauli ya kijana aliyeshiba na kuvimbiwa na urefu wa kamba yake.

Hii ni kauli ya mtu aliye vimbiwa sasa anatapata kupata wapi abeue Ili arufu chafu itoke tumboni mwake, au ni mithili ya aliyevimbiwa Sasa anatapata Ili ewa chafu itoke tumboni mwake tatizo hataki kuchagua harufu hiyo aitolee wapi? Hajui mazingira lakini pia hajui ajibane, itoke taratibu au ajiachie itoke kwa nguvu na mbele ya vijana wenzake.

Silalamiki kwani ruhusu ya kula kwa urefu wa kamba zao uliiitoa wewe, tafadhali waelekeze vijana wako baada ya kuvimbiwa wachague wapi pa kupitisha uchafu wa kuvimbiwa kwao ila kwa staili hii 2025 wenye nchi ni wananchi wataamua kama akuvyosema Spika aliyejiuzuru baada ya kuvimbiwa na kushindwa kuchagua uchafu autoeje tumboni.
 
Kwa mara yangu ya kwanza kwa kipindi cha miaka 40 niliyo tumia barabara ya Arusha Moshi, leo imekuwa njem sana kwangu,
Vile vijiwe vya trafiki kusimamishwa kila baada ya mita 500 kuulizwa una kwenda wapi umetoka wapi as if hujitambui lro havipo.

Kuombwa hela za kupiga rangi viatu leo hakuna.

Happy birthday Mama Samia. Long live.

Kumbe ina wezekana polisi kujitathmini.
 
Kwahiyo unapiga mkwara mwenyewe?!!!!!

Nje ya mada kidogo, hivi kale kajamaa kalikokuwa kanapinga kuwa hii siyo awamu ya sita kapo wapi vileee? Na kale alikokuwa anakaita 'shule' mwenyewe bado kapo?!!!!!!
 
Kifupi hatuna mtu hapo, tumepigwa vibaya sana. Aliyeweka kipengele cha kuwa rais lazima awe angalau na degree moja aliona mbali sana., mtu ameinga unga elimu kweli awe rais. Yaami ukimsikilia maamuzi yake ni kama anapata ushauri kwa wake wenza very strange.!
Hadi 2030 mtafika mkiwa mmechoka sana kwa chuki.
 
photo_2022-02-04_12-12-24.jpg


Watanzania tupate wapi Rais kama huyu?

1. Rais mwenye hofu ya Mungu

2. Rais mnyenyekevu kwa anaowaongoza

3. Rais mpenda watu wake wote

4. Rais mpole na mwenye huruma

5. Rais Mtulivu wa roho na nafsi

6. Rais mzuri wa sura na nafsi

7. Rais msikivu kwa wote

8. Rais mvumilivu na mkarimu kwa wote

9. Rais Mzalendo wa kweli kwa Taifa

10. Rais Mkweli kwa Mungu na wanadamu

11. Rais asiyependa sifa wala kujisifia

12. Rais mwenye moyo mweupe pee

Nauliza tena, Watanzania tupate wapi mtu kama huyu ambae Mungu yuko ndani yake?
 
Mambo yanavyokwenda huku chini siyo mazuri kabisa. Tabia za uzembe rushwa na ufisadi zimerudi kwa kasi kubwa kwenye tahasisi za SERIKALI.

Watu wengi hawakumwelewa mh magufuli jinsi alivyokua anafukuza watendaji wazembe.

Mama chukua hatua haraka maana nyani wanamaliza maindi ya Watoto shambani hali siyo nzuri.
 
Back
Top Bottom