The Sunk Cost Fallacy
JF-Expert Member
- Dec 1, 2021
- 19,582
- 14,167
Naunga mkono hoja, upuuzi aliokuwa anafanya Jiwe Kisa kutafuta kupendwa kwa lazima haiwezekani kwa sasa.Biblia inasema 'mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru kwelikweli ' kumradhi kwa watu wa imani nyingine lakini kwa sisi wakristo tunaoamini maandiko ya Biblia Takatifu tunaona sasa ni wakati wa watu kuijua kweli. Kwa nini?
i) Uelewa wa watu ni mdogo sana juu kinachoendelea kwenye uchumi. Kukaa kimya kwa serikali kunatafsirika kwamba nao ni sehemu ya vitu kupanda bei.
ii) Samia hajatafuta ushujaa ila amaekuweka tayari kwa ajili ya kufunga mkanda kwa hali inayokuja. Inabidi watu wajue mzalishaji mkubwa duniani wa nishati, madini, nafaka na sunflower yupo vitani na uzalishaji na usambazaji lazima utikiswe.
iii) Nampongeza kutoa taarifa ya hali ilivyo na kwa jinsi ilivyo huo ndio ushujaa.
Wale mnaojifariji kumchukia Rais Kisa kawaambia ukweli ndio kwanza mna mpa baraka.
Shikilia hapo hapo