Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Maoni, Ushauri na Mapendekezo kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Status
Not open for further replies.
-Njia ambazo zinatumika kuwakabili wanaokujaribu, zinakuingiza zaidi majaribuni. Hii tabia ya kukamatakamata watu hovyo, ndiyo inakufanya ujaribiwe zaidi na zaidi.
-Mimi kama raia mtiifu, lazima niishauri serikali ; Tabia ya kuwakamata akina Lissu, Zitto, Mbowe na wapinzani wengine, haiwafanyi wakuogope, bali unawajenga kitofauti.
-Na wewe si umesema ni wa tofauti? Basi na wenyewe unawafanya wawe wa tofauti. Unawakamata na kuwaweka mahabusu, wakiachiwa wanaongea yaleyale yasiyokupendeza. Unawakamata tena, mwisho wanazoea, wanaona ni sehemu ya maisha yao.UNAJARIBIWA NA UNASHINDWA ZAIDI
-Ogopa sana wapinzani, wakiona jela ni sehemu ya maisha yao watakusumbua mpaka maisha ya Ikulu utayaona yamejaa presha. Si presha za kazi ya kuwahudumia wananchi, ni presha ya usalama.UTAJARIBIWA KAMA HUTOBADILIKA
-Wapinzani wamezowea vurugu mechi za dola. Wakiona virungu hawaogopi, ukiwaonesha bunduki wanasogea kidogo tu. Ukiwapiga mabomu ya machozi, utapita muda yatakauka, ukiwamwagia maji ya kuwasha, wanawashwa, baadaye muwasho unaisha, maisha yanaendelea.
-Wapinzani wanapokuwa sugu baada ya kusumbuliwa muda mrefu na serikali, wanakuwa hawana tofauti na magaidi wanaodai haki zao bila kuogopa kifo. Wanaweza kufanya chochote bila kuhofia dola, maana kwao dola huona ni adui yao. Hiyo ni hatua mbaya sana.
-Naomba nikuulize swali MAGUFULI, ni wapi wapinzani wamewahi kunyamazishwa kwa nguvu za dola hadi wakatulia ? UMESHARUSHUSU KUJARIBIWA
-Binadamu ameumbwa kuzoea mazingira. Akiwa anasikia sana milio ya risasi, inafikia wakati anazoea. Akizoea mabomu, akisikia tu, anakimbilia kulala chini. Hata mfungwa wa muda mrefu, wakati mwingine hushangaa uraiani watu wanaishije.
-Ingekuwa matumizi makubwa ya dola yanasaidia watawala kuwanyamazisha wapinzani, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekata tamaa na kwenda Butiama, akawe Chifu wa Wazanaki na habari za kudai uhuru wa Tanganyika angeachana nazo.
-Hata hivyo, kadiri walivyokuwa wakimwandama ndivyo naye alivyozidisha harakati. Utawala wa Kiingereza, ulimfanya Mwalimu Nyerere awe sugu, akaendelea kupambana mpaka uhuru ulipopatikana.Vyama vya upinzani navyo havitonyamaza hadi wapate kile kinachotakiwa.
-Nguvu kubwa ya dola ingekuwa inasaidia kunyamazisha upinzani, Nelson Mandela ‘Madiba’, angenywea tangu miaka ya 1960. Akina Jacob Zuma, wasingeukwaa urais. Makaburu wangeendelea kutawala na ubaguzi wa rangi ungetamalaki hadi leo.
-Ni kwa sababu nguvu kubwa ya dola huwa hainyamazishi upinzani, ndiyo maana Sani Abacha hakuwahi kuifanya Nigeria itulie. Joseph Kabila, hajamudu kuiweka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) katika utulivu, vilevile Paul Kagame na utulivu wa Rwanda ni magirini tu.
-Unadhani miaka 27 ambayo Mandela aliishi jela, siku zote hizo zilikuwa za mateso? Ukifikiria hivyo utajidanganya kabisa, vipo vipindi ambavyo alifurahia maisha hata kama alinyimwa uhuru kwa kukaa gerezani.Lakini alijua kuna siku atapata ushindi na alipata.
-Tazama sasa, wakati Mandela akizoea maisha ya jela na kuona ni sehemu ya kawaida katika maisha yake, nje, Serikali ya Kikaburu ikawa kwenye mateso makubwa kutokana na presha ya kumfunga jela Mandela pamoja na wanaharakati wengine.
-Chukua hii; Matumizi makubwa ya nguvu ya dola dhidi ya wapinzani, kwa kawaida huifanya serikali yenyewe iteseke kuliko hata wapinzani wenye kukamatwa na kufungwa.
-Kwa maana kwamba serikali hukosa utulivu kwa sababu wapinzani ni viongozi, kwa hiyo wanakuwa na kundi kubwa la wafuasi, ukiwakamata inabidi shughuli nyingi zisimame na gharama za kukamata ni kubwa mno. Hayo ni mateso makubwa.
-Fikiria kumsafirisha Lissu kutoka Singida mpaka Dar es Salaam, kumsaka Zitto usiku na mchana ikiwa ni pamoja na kuizingira nyumba yake kwa siku tatu. Kisha Lissu anapewa dhamana anaondoka akiwa anatabasamu, Zitto anajitokeza mwenyewe halafu anasema “siogopi.” MAJARIBU GANI UNAYOYATAKA ZAIDI YA HAYA
-Tuachane na mateso kwa serikali, akina Lissu wakizoea jela, watakuwa wanaona kama vile wako ofisini kwako pale UFIPA. Kule kuna watu, siasa zinaweza kuendelea hukohuko ndani.
Ninakukumbusha kuwa kuna kipindi Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, alikataa kutoka jela, alitaka aishi hukohuko baada ya kuona anaonewa sana polisi uraiani.
Ujumbe wangu ni kwamba MAGUFULI afanye kazi zake inavyotakiwa. Awaache akina Lissu, Zitto, Mbowe na wapinzani wengine wafanye siasa zao, yeye ajikite kujenga nchi.
Ikiwa anaona wapinzani wanataka kulifanya suala la Bunge Live kuwa ni ajenda yao, yeye anamwambia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye aruhusu bunge lionekane moja kwa moja.BILA HIYO TUNAKUJARIBU NA TUTAKUSHINDA
Kama ni bajeti ipangwe vizuri na iwe kweli, sio yenye chumvi kibao na majigambo mengi wakati ni hewa tupu.HAPA LAZIMA UJARIBIWE
Kuwafukuza bungeni wabunge haisaidii, mwisho wataona ni sehemu ya maisha yao. Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwakomoa wapinzani, haisaidii, watajenga chuki tu. HAPA LAZIMA TUTAKUSHINDA Umejenga majaribu mwenyewe
Dawa ya kuwanyamazisha wapinzani sio kuzuia mikutano ya kisiasa,bunge live,kupitisha bajeti kwa nguvu na kejeli kibao,kuwatukana wapinzani majukwaani,kutumia polisi kila siku,kuwafukuza bungeni, HAPA LAZIMA TUKUJARIBU NA TUTASHINDA.
Nimkumbushe Rais Magufuli kuwa enzi ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa, Chama cha Wananchi (Cuf), kama chama kikuu cha upinzani wakati huo, kilitangaza siasa za kimapambano kwa kauli mbiu ya jino kwa jino.
Mapambano yalikuwepo makali kweli na wapinzani hawakunyamza. Ni kipindi ambacho Cuf walijitangaza kuwa wao wapo Ngangari, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Omar Mahita, akasema polisi nao ni Ngunguri. Ikawa mapambano ya Ngangari na Ngunguri.
Kipindi cha utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Dk Jakaya Kikwete, mambo ya Ngangari na Ngunguri hayakusikika, mapambano ya jino kwa jino, hayakuwepo. Ni kwa sababu kulikuwa na uhuru wa wanasiasa wa upinzani kufanya siasa zao.
Pamoja na uhuru uliokuwepo, matukio machache yalipotokea kati ya upinzani na dola, athari yake ilionekana. Rejea mauaji ya Arusha kama somo la karibu zaidi katika nyakati za machafuko wakati wa JK.
Vitisho vya “sijaribiwi” na “mimi nipo tofauti”, vinaweza kurejesha jino kwa jino na Ngangari, matokeo yake yakakutesa wewe MAGUFULI zaidi kuliko kujenga utulivu wa kitaifa.
#UKUTA NI LAZIMA September 1
 
Mmeshaambiwa kuwa tangulieni na wake zenu mkione cha mtema kuni. Sasa mbona mnalia lia humu?
 
-Njia ambazo zinatumika kuwakabili wanaokujaribu, zinakuingiza zaidi majaribuni. Hii tabia ya kukamatakamata watu hovyo, ndiyo inakufanya ujaribiwe zaidi na zaidi.
-Mimi kama raia mtiifu, lazima niishauri serikali ; Tabia ya kuwakamata akina Lissu, Zitto, Mbowe na wapinzani wengine, haiwafanyi wakuogope, bali unawajenga kitofauti.
-Na wewe si umesema ni wa tofauti? Basi na wenyewe unawafanya wawe wa tofauti. Unawakamata na kuwaweka mahabusu, wakiachiwa wanaongea yaleyale yasiyokupendeza. Unawakamata tena, mwisho wanazoea, wanaona ni sehemu ya maisha yao.UNAJARIBIWA NA UNASHINDWA ZAIDI
-Ogopa sana wapinzani, wakiona jela ni sehemu ya maisha yao watakusumbua mpaka maisha ya Ikulu utayaona yamejaa presha. Si presha za kazi ya kuwahudumia wananchi, ni presha ya usalama.UTAJARIBIWA KAMA HUTOBADILIKA
-Wapinzani wamezowea vurugu mechi za dola. Wakiona virungu hawaogopi, ukiwaonesha bunduki wanasogea kidogo tu. Ukiwapiga mabomu ya machozi, utapita muda yatakauka, ukiwamwagia maji ya kuwasha, wanawashwa, baadaye muwasho unaisha, maisha yanaendelea.
-Wapinzani wanapokuwa sugu baada ya kusumbuliwa muda mrefu na serikali, wanakuwa hawana tofauti na magaidi wanaodai haki zao bila kuogopa kifo. Wanaweza kufanya chochote bila kuhofia dola, maana kwao dola huona ni adui yao. Hiyo ni hatua mbaya sana.
-Naomba nikuulize swali MAGUFULI, ni wapi wapinzani wamewahi kunyamazishwa kwa nguvu za dola hadi wakatulia ? UMESHARUSHUSU KUJARIBIWA
-Binadamu ameumbwa kuzoea mazingira. Akiwa anasikia sana milio ya risasi, inafikia wakati anazoea. Akizoea mabomu, akisikia tu, anakimbilia kulala chini. Hata mfungwa wa muda mrefu, wakati mwingine hushangaa uraiani watu wanaishije.
-Ingekuwa matumizi makubwa ya dola yanasaidia watawala kuwanyamazisha wapinzani, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekata tamaa na kwenda Butiama, akawe Chifu wa Wazanaki na habari za kudai uhuru wa Tanganyika angeachana nazo.
-Hata hivyo, kadiri walivyokuwa wakimwandama ndivyo naye alivyozidisha harakati. Utawala wa Kiingereza, ulimfanya Mwalimu Nyerere awe sugu, akaendelea kupambana mpaka uhuru ulipopatikana.Vyama vya upinzani navyo havitonyamaza hadi wapate kile kinachotakiwa.
-Nguvu kubwa ya dola ingekuwa inasaidia kunyamazisha upinzani, Nelson Mandela ‘Madiba’, angenywea tangu miaka ya 1960. Akina Jacob Zuma, wasingeukwaa urais. Makaburu wangeendelea kutawala na ubaguzi wa rangi ungetamalaki hadi leo.
-Ni kwa sababu nguvu kubwa ya dola huwa hainyamazishi upinzani, ndiyo maana Sani Abacha hakuwahi kuifanya Nigeria itulie. Joseph Kabila, hajamudu kuiweka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) katika utulivu, vilevile Paul Kagame na utulivu wa Rwanda ni magirini tu.
-Unadhani miaka 27 ambayo Mandela aliishi jela, siku zote hizo zilikuwa za mateso? Ukifikiria hivyo utajidanganya kabisa, vipo vipindi ambavyo alifurahia maisha hata kama alinyimwa uhuru kwa kukaa gerezani.Lakini alijua kuna siku atapata ushindi na alipata.
-Tazama sasa, wakati Mandela akizoea maisha ya jela na kuona ni sehemu ya kawaida katika maisha yake, nje, Serikali ya Kikaburu ikawa kwenye mateso makubwa kutokana na presha ya kumfunga jela Mandela pamoja na wanaharakati wengine.
-Chukua hii; Matumizi makubwa ya nguvu ya dola dhidi ya wapinzani, kwa kawaida huifanya serikali yenyewe iteseke kuliko hata wapinzani wenye kukamatwa na kufungwa.
-Kwa maana kwamba serikali hukosa utulivu kwa sababu wapinzani ni viongozi, kwa hiyo wanakuwa na kundi kubwa la wafuasi, ukiwakamata inabidi shughuli nyingi zisimame na gharama za kukamata ni kubwa mno. Hayo ni mateso makubwa.
-Fikiria kumsafirisha Lissu kutoka Singida mpaka Dar es Salaam, kumsaka Zitto usiku na mchana ikiwa ni pamoja na kuizingira nyumba yake kwa siku tatu. Kisha Lissu anapewa dhamana anaondoka akiwa anatabasamu, Zitto anajitokeza mwenyewe halafu anasema “siogopi.” MAJARIBU GANI UNAYOYATAKA ZAIDI YA HAYA
-Tuachane na mateso kwa serikali, akina Lissu wakizoea jela, watakuwa wanaona kama vile wako ofisini kwako pale UFIPA. Kule kuna watu, siasa zinaweza kuendelea hukohuko ndani.
Ninakukumbusha kuwa kuna kipindi Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, alikataa kutoka jela, alitaka aishi hukohuko baada ya kuona anaonewa sana polisi uraiani.
Ujumbe wangu ni kwamba MAGUFULI afanye kazi zake inavyotakiwa. Awaache akina Lissu, Zitto, Mbowe na wapinzani wengine wafanye siasa zao, yeye ajikite kujenga nchi.
Ikiwa anaona wapinzani wanataka kulifanya suala la Bunge Live kuwa ni ajenda yao, yeye anamwambia Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye aruhusu bunge lionekane moja kwa moja.BILA HIYO TUNAKUJARIBU NA TUTAKUSHINDA
Kama ni bajeti ipangwe vizuri na iwe kweli, sio yenye chumvi kibao na majigambo mengi wakati ni hewa tupu.HAPA LAZIMA UJARIBIWE
Kuwafukuza bungeni wabunge haisaidii, mwisho wataona ni sehemu ya maisha yao. Naibu Spika, Dk Tulia Ackson kuwakomoa wapinzani, haisaidii, watajenga chuki tu. HAPA LAZIMA TUTAKUSHINDA Umejenga majaribu mwenyewe
Dawa ya kuwanyamazisha wapinzani sio kuzuia mikutano ya kisiasa,bunge live,kupitisha bajeti kwa nguvu na kejeli kibao,kuwatukana wapinzani majukwaani,kutumia polisi kila siku,kuwafukuza bungeni, HAPA LAZIMA TUKUJARIBU NA TUTASHINDA.
Nimkumbushe Rais Magufuli kuwa enzi ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa, Chama cha Wananchi (Cuf), kama chama kikuu cha upinzani wakati huo, kilitangaza siasa za kimapambano kwa kauli mbiu ya jino kwa jino.
Mapambano yalikuwepo makali kweli na wapinzani hawakunyamza. Ni kipindi ambacho Cuf walijitangaza kuwa wao wapo Ngangari, aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Omar Mahita, akasema polisi nao ni Ngunguri. Ikawa mapambano ya Ngangari na Ngunguri.
Kipindi cha utawala wa Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Dk Jakaya Kikwete, mambo ya Ngangari na Ngunguri hayakusikika, mapambano ya jino kwa jino, hayakuwepo. Ni kwa sababu kulikuwa na uhuru wa wanasiasa wa upinzani kufanya siasa zao.
Pamoja na uhuru uliokuwepo, matukio machache yalipotokea kati ya upinzani na dola, athari yake ilionekana. Rejea mauaji ya Arusha kama somo la karibu zaidi katika nyakati za machafuko wakati wa JK.
Vitisho vya “sijaribiwi” na “mimi nipo tofauti”, vinaweza kurejesha jino kwa jino na Ngangari, matokeo yake yakakutesa wewe MAGUFULI zaidi kuliko kujenga utulivu wa kitaifa.
#UKUTA NI LAZIMA September 1
Acha maneno mengi.. Njia hizi zitaendelea kutumika na hiyo tarehe 1 mnasubiriwa.
 
Ngoja nimalizie kusoma kitabu changu cha A Man of The People then ntarudi kucomment
 
Huyu mkuu wetu kwakweli cjamuelewa coz ni jambo la kushangaza eti wapinzani wasifanye siasa sasa kazi yao itakuwa ni nini hasa manake cpati jibu hadi sasa lakini yy mkuu anafanya hata juzi juzi alikuwa Tabora na Shinyanga. Mimi kwa mtizamo wangu wapinzani hawawezi zuia wananchi wasipate huduma coz ya mikutano au siasa za wapinzani. Na hivyo basi namsihi huyu mkuu wetu awaache wapinzani wafanye kazi yao kama katiba inavyoelekeza
 
Mmeshaambiwa kuwa tangulieni na wake zenu mkione cha mtema kuni. Sasa mbona mnalia lia humu?
Wewe Lizaboni, what if what you want happen? Utawaua kwa kuwa ni wake na watoto wa wanaume wa vyama pinzani? Au una njia mbadala? Ina maana ccm inatekeleza sera za makaburu zilizoua familia za watoto wa wapinzani kule soweto? Usichochee vurugu kwa maslahi ya tumbo lako. Niwashangae watu wa ccm na viongozi wenu kwa kuwaandaa polisi kukabiliana na watu wanaofanya yao kwa mujibu wa katiba yao. Au ndio kusema katiba ya jmt ni ya ccm? Makonda usome uzi huu ili ubadilike kwa yale uliyoyafanya jana kule ukonga na ukaliondoe tamko lako la kuwataka ffu waingie mtaani kuwasambaratisha watakaoandamana badala ya kufanya kazi yao kwa mujibu wa sheria ya kuwalinda watu na mali zao wakiwamo wanaoandamana. Ni kwanini utendaji wa viongozi na vyombo vya ulinzi vya nchi hii ni tofauti na nchi nyingine? Igeni basi namna ya kuyalinda maandamano yoyote ili kuepusha vurugu zinazoweza kuzuilika! Tunakotaka kufikishwa siko tulikokutarajia, tuna nafasi ya kuyatable na muafaka ukafikiwa na siyo kutishana na kutegeana kwa marungu ili mtuumize.
 
Rais Mtukufu Isombo la Sahoyo wakwa! Mtukufu ni Mungu Peke yake. Huyo Rais Unayemtaja Simjui Ila Utukufu alio nao ni Nini? Nahisi Rais Unayemtaja ni Wa Nchi ya Afrika na Marais Mengi wa Afrika wamejaa Ushetani, Ninauhakika na Unayemtaja hali kadhalika
auyo ambulia vatanebarebare vimamayafo...utaneue mwana vaita.hai na hai mmeku.
 
Maoni yngu katiba ya warioba irudi tna ili viongzi wanaojiona wao ndo wao 2umlize ili kla mtanznia afaidke na mawazo yke
 
Napongeza kwa maamzi ya kuhamishia Serikali Dodoma. Ninachoshauri akumbuke kuwa Dar es salaam ndio chanzo cha uchumi wa Tanzania. Si lazima ahamishe idala zote za Serikali hasa zinazofanya biashara. Kuhamisha taaaisi mhimu zinazotegemewa kwenye viwanda na uchumi kwa ujumla ni kosa na naamini hatafanya hivyo. Vilevile namshauri asiuze nyumba za Serikali kama alivyotamka siku chache zilizopita na badala yake majengo hayo yatumike kama sub office za wizara au kanda. Kama kanda hazihitajiki basi majengo hayo wapewe vyuo vya umma yatumike kama hostel au hata madara. Kuna vyuo mhimu sana na havina hostel za kutosha na vipo katikati ya mji mfano DIT IFM,CBE n.k
 
Kwanza napenda kuweza wazi mimi si mwanachama wa chama chochote, chama changu ni chama mbacho kitaleta maendeleo ya Watanzania. Binafsi napenda kumpongeza Rais Magufuli kwa hatua zake nyingi za kupambana na watu ambao walipenda kuwanyonya wenzao. Mhe.Rais achana kupambana na wapinzani fanya yafuatayo:

1.Hakikisha vijijini maisha yao yainuke wasiishi kwa ndoto huku wakisema ipo siku na sisi tutakuja kuwa na Zahanati nzuri kama mjini. Mhe.Rais unaweza kabisa kufanya kijiji kikawa kama mjini huduma za kijamii zikapatikana kama mjini najua ndio dhamira yako, wanaopambana na kuweka operation UKUTA hawatafanikiwa kamwe.

2.Wananchi wanahitaji maendeleo sana lakini hawapo tayari ku support UKUTA kama mijini mahitaji ya msingi kama Dawa hospital zikapatikana kwa wakati, Maji bila mgao nchi nzima, Umeme pia, watu wa mabondeni ukawajengea mitaro ya maji bila kugusa nyumba zao ambazo walijenga kwa kujinyima sana. Kwa vitu hivyo ukiwafanyia hawata support UKUTA kamwe lakini kama utaendeleza siasa ambazo tulizizoea watu hawa kuna uwezekano mkubwa sana wakajiunga.

3.Ajira ni shida maana kwenye barua yako ya tarehe 13 Juni, 2016 ulisitisha vibali vya ajira Serikalini na kupanda kwa mishahara kwa watumishi wa UMMA. Naamini ulikuwa na wazo zuri la ku control wage bill kwa miezi miwili na muda wa miezi miwili imefika tayari lakini unazidi kuongeza jobless mtaani maana ukitaka kujua haya kumbuka interview iliyoitwa na Uhamiaji pale uwanja wa Taifa watu zaidi 20,000 walikuja na vyeti vyao.

4.Wewe ndie mwenye kila kitu hao wenye UKUTA ni njia tu za kukuchelewesha kufikia malengo yako ili ikifika 2020 wajifanye wanakukumbushia ahadi ulizoshindwa kuzitekeleza, achana na UKUTA Mhe.Rais pambana na wasiolipa kodi upate pesa za kujenga nchi yetu.

5.Naamini bado watanzania wanaku support sana ndio maana baadhi ya wake wa wenye UKUTA wanalia wakiwasii waume zao wasiende tarehe 1, Septemba kwenye UKUTA wanajua kitakachofuata.

6.Waachie waendeleze Propaganda zao za UKUTA wakija shtuka wewe umeshajenga zahanati kila kijiji na Daktari yupo tayari.

7.Wapinzani fanyeni kazi tujenge nchi yetu.
 
Kwanza napenda kuweza wazi mimi si mwanachama wa chama chochote, chama changu ni chama mbacho kitaleta maendeleo ya Watanzania. Binafsi napenda kumpongeza Rais Magufuli kwa hatua zake nyingi za kupambana na watu ambao walipenda kuwanyonya wenzao. Mhe.Rais achana kupambana na wapinzani fanya yafuatayo:

1.Hakikisha vijijini maisha yao yainuke wasiishi kwa ndoto huku wakisema ipo siku na sisi tutakuja kuwa na Zahanati nzuri kama mjini. Mhe.Rais unaweza kabisa kufanya kijiji kikawa kama mjini huduma za kijamii zikapatikana kama mjini najua ndio dhamira yako, wanaopambana na kuweka operation UKUTA hawatafanikiwa kamwe.

2.Wananchi wanahitaji maendeleo sana lakini hawapo tayari ku support UKUTA kama mijini mahitaji ya msingi kama Dawa hospital zikapatikana kwa wakati, Maji bila mgao nchi nzima, Umeme pia, watu wa mabondeni ukawajengea mitaro ya maji bila kugusa nyumba zao ambazo walijenga kwa kujinyima sana. Kwa vitu hivyo ukiwafanyia hawata support UKUTA kamwe lakini kama utaendeleza siasa ambazo tulizizoea watu hawa kuna uwezekano mkubwa sana wakajiunga.

3.Ajira ni shida maana kwenye barua yako ya tarehe 13 Juni, 2016 ulisitisha vibali vya ajira Serikalini na kupanda kwa mishahara kwa watumishi wa UMMA. Naamini ulikuwa na wazo zuri la ku control wage bill kwa miezi miwili na muda wa miezi miwili imefika tayari lakini unazidi kuongeza jobless mtaani maana ukitaka kujua haya kumbuka interview iliyoitwa na Uhamiaji pale uwanja wa Taifa watu zaidi 20,000 walikuja na vyeti vyao.

4.Wewe ndie mwenye kila kitu hao wenye UKUTA ni njia tu za kukuchelewesha kufikia malengo yako ili ikifika 2020 wajifanye wanakukumbushia ahadi ulizoshindwa kuzitekeleza, achana na UKUTA Mhe.Rais pambana na wasiolipa kodi upate pesa za kujenga nchi yetu.

5.Naamini bado watanzania wanaku support sana ndio maana baadhi ya wake wa wenye UKUTA wanalia wakiwasii waume zao wasiende tarehe 1, Septemba kwenye UKUTA wanajua kitakachofuata.

6.Waachie waendeleze Propaganda zao za UKUTA wakija shtuka wewe umeshajenga zahanati kila kijiji na Daktari yupo tayari.

7.Wapinzani fanyeni kazi tujenge nchi yetu.
Ushauri wako utafanyiwa kazi baada ya 1st sept
 
ni ushauri mzuri kwa mheshimiwa rais nadhan akizingatia hayo basi tutapiga hatua na si kupambana na hawa jamaa maana walishandikana
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom