CHADEMA hawajasema wanataka vikao vya bunge vipunguzwe wala malipo yapunguzwe. Wamesema, kwenye submission yao ya John Mnyika leo, wanataka kila jimbo liwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa, mmoja mwanamke mmoja mwanamme.
Kwa hio, kwa mapendekezo ya CHADEMA, bunge hili la sasa la watu 400 linaenda kuwa na watu 800!
Tuwe na Rais wa kike na kiume basi! Na diwani mwanamke na mwanamke. Mana tunatafuta jozi za wawili wawili wa kwenda kuchumbiana kwenye vikao!
Ni mtu gani mwenye akili kichwani, wa chama cha upinzani cha nchi ya dunia ya tatu, ya watu masikini wa kutupwa, wachafu wenye njaa, wanaoshindia mihogo na maji machafu ya mitoni, biashara za masinia ya ndizi vichwani, boda boda na mama ntilie, anaependekeza kuongeza gharama za kutajirisha viongozi ???