Uchaguzi 2020 Mapingamizi halali kisheria dhidi ya mgombea nafasi ya Urais

Uchaguzi 2020 Mapingamizi halali kisheria dhidi ya mgombea nafasi ya Urais

Mbona mnatia huruma hivyo! Lissu tunamkatafunua kwenye sanduku mapema sana ili azidi kuchanganyikiwa! TL hawezi kuwa Raisi wa Tanzania, labda awe raisi wa Twitter.
Mkate kwenye sanduku kwa haki..no problem ndio demokrasia hiyo..nini povu sasa?

Kama unatumia demokrasia kumkata kwenye sanduku,then it is right!

Mengine ni ya uungu mtu mnatuletea hapa....yaani Tume ipo chini yenu,hakuna nchi hapo!
 
So na ujanja wako wote huo unasubiri hayo yatokee kisha ukakojoe ukalale badala ya kuja na mechanism ya kukabiliana na huo uhuni.
Mkuu

Mawe yupo juu ya sheria

Tume iko chini yake.....Mahakama iko chini yake....

Huyu dikteta alipokua anaua hizi institutions kua chini yake watu wazima nchi hii walikua wanapiga makofi...

Ujanja wa ku-overcome hili ni hizi kelele zinazopigwa na Amsterdam,pia lazima elders wa hii nchi waongee wazi wazi na mengine mengi
 
Mapingamizi namba 4 na 5 yanavunja misingi ya haki ya Watanzania kuchaguliwa uongozi.

Nafikiri hata Ripoti ya Jaji Nyalali ilishauri tuondoe sharti la wagombea kuwa wanachama wa vyama vya siasa.
Serikali ilishashindwa kesi na walipewa muda kurekebisha hicho kipengele ila hatuna watu kama mtikila kwa sasa
 
Mahakama ya Rufaa ilitengua uamuzi wa Mahakama Kuu, hivyo, Mtikila alipoteza kesi.
Mahakama ya afrika ilimpa ushindi na ikaipa muda serikali kutekeleza wakati huo tulikuwa na bunge la katiba wakasingizia kipengele hicho kimewekwa lakini tunajua mwisho wa bunge la katiba kwani hakuna kinachotekelezwa
 
Mahakama ya afrika ilimpa ushindi na ikaipa muda serikali kutekeleza wakati huo tulikuwa na bunge la katiba wakasingizia kipengele hicho kimewekwa lakini tunajua mwisho wa bunge la katiba kwani hakuna kinachotekelezwa
Mahakama ya Haki za binadamu ya Afrika haina meno ni toothless dogo.
 
Mkuu

Mawe yupo juu ya sheria

Tume iko chini yake.....Mahakama iko chini yake....

Huyu dikteta alipokua anaua hizi institutions kua chini yake watu wazima nchi hii walikua wanapiga makofi...

Ujanja wa ku-overcome hili ni hizi kelele zinazopigwa na Amsterdam,pia lazima elders wa hii nchi waongee wazi wazi na mengine mengi
Elder aliyekuwa anasikilizwa na Magufuli ni Mkapa peke yake, wengine wote walishaambiwa wanawashwawashwa.
 
Mkuu

Election Commision ipo ndani ya mifuko ya mwenye enzi kuu duniani....

Itapigwa simu au text msg atakatwa mtu.....ni lazima...

Dictator yeyote duniani ni muoga kupita maelezo kuona kwenye sanduku la kura kuna jina la worthy challenger.....

Taasisi zote zipo held by the balls na mwenye enzi duniani na mbinguni....

Utaona vituko sana...just wait and seee!

Electoral Commision itakua weaponized to delete the threatening candidate to the dictator.....
Watamkata na Hashimu Rungwe ili kuonyesha sio Lisu pekee
 
Nasikia CCM wameongezea la kwao kwamba
1. Lissu kaanza kampeni mapema
2. Lissu katoa maneno ya uchochezi wakati wa kutafuta wadhamini...
3. Kufanya maandamano na mikutano ya hadhara bila mufuata taratibu za kisheria.

Haya ndiyo makosa ya Lissu according to Lumbumba yanayomuondolea sifa ya kugombea Urais wa Jamhuri yetu.
 
MAPINGAMIZI HALALI KISHERIA DHIDI YA MGOMBEA NAFASI YA URAIS.

Wiki ijayo tarehe 26 August, 2020 itakuwa ni siku ya wagombea kuwasilisha mapingamizi dhidi ya wagombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mapingamizi halali kisheria anayoweza kuwekewa mgombea wa nafasi ya Urais kwa mujibu wa masharti ya ya Kifungu cha 35 D na 40 (1) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 yakisomeka kwa pamoja na (read in tendem with) masharti ya Kanuni ya 39 (4) ya Kanuni za Uchaguzi wa Rais na Wabunge, 2020 (Tangazo la Serikali Na. 402 la 2020) ni haya yafuatayo;

(1) Mgombea Urais sio raia wa Tanzania.

(2) Mgombea Urais hajafikisha umri wa miaka 40.

(3) Mgombea Urais hajui kusoma na kuandika Kiswahili au Kiingereza.

(4) Mgombea Urais sio mwanachama wa chama cha siasa.

(5) Mgombea Urais hajadhaminiwa na chama cha siasa kugombea.

(6) Mgombea Urais amekutwa na hatia ya kosa la jinai la kukwepa kodi katika kipindi cha miaka 5 kabla ya siku ya Uchaguzi.

(7) Mgombea Urais hajadhaminiwa na wapiga kura 200 kutoka mikoa 10 ya Tanzania ikiwemo mikoa 2 kutoka Zanzibar.

(8) Mgombea Urais hajadhaminiwa na idadi ya kutosha ya wapiga kura.

(9) Mgombea Urais hakulipa dhamana ya Tshs 1, 000, 000/=

(10) Mgombea Urais hakuwasilisha au hakuambatinisha picha kwenye Fomu ya Uteuzi.

(11) Mgombea Urais ameshindwa kuambatanisha Tangazo la Kisheria (statutory declaration) kwenye Fomu ya uteuzi ambalo limesainiwa na mgombea na limefanywa mbele ya Jaji kudhibitisha kuwa mgombea anayo nia na anazo sifa za kugombea Urais.

(12) Mgombea Urais ameshindwa kuweka wazi pesa ambazo atazitumia katika uchaguzi.

(13) Mgombea Urais hakusaini kukubali kutii Maadili ya Uchaguzi.

(14) Mgombea Urais hakujaza au hakurudisha Fomu ya Uteuzi kwa Tume ya Taifa Uchaguzi kwa mujibu wa matakwa ya sheria.

(15) Mgombea Urais amefanya makosa ambayo yamezuhiwa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010.

(16) Kutokana na taarifa ambazo ziko kwenye Fomu yake ya Uteuzi, mgombea hana sifa za kuwa mgombea wa nafasi ya Ubunge au mjumbe wa baraza la wawakilishi la Zanzibar zilizoainishwa na Katiba husika.

(17) Taarifa ambazo mgombea Urais amewasilisha kwa Tume ya Taifa uchaguzi hazijitoshelezi kumtambua mgombea.

(18) Kutokana na taarifa ambazo ziko kwenye Fomu yake ya Uteuzi, hana sifa za kuwa mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizoainishwa na Katiba.

Haya ndo mapingamizi 18 pekee ambayo anaweza kuwekewa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio vinginevyo.
#15! Utawekaje pingamizi wakati hajaanza kuzitumia gharama za uchaguzi!
 
Kiwekwe kipengele cha kuwapima Mental health wagombea
Madikteta wengi huwa wanamatatizo hayo na ni vigumu wao kuyakubali kuwa ni matatizo

Mathalan huyu anaeondoka madarakani
 
Hapo namba 15 inaondoka na lisu.
Si mlisema Lisu hana pesa za kampeni CHDEMA imteuwe Nyalandu?! Au ameshapata pesa? Alafu muulize Lijualipole, si Mbowe amekula ile pesa ya kampeni bilion ngapi sijui!! Number 15 haiwezi, na wala mboga mboga yeyote mwenye akili kisude tu, hatadhubutu kuitumia kumwekea Lisu pingamizi! Kwanini msiseme ni Mkenya, aliongezewa damu na Wakenya!!
 
Tatizo lako ni mtu wa matukio hukui nini kilifata baada ya mahakama ya rufani kutengua uamuzi huo ingia hata google tafuta hukumu ya mgombea binafsi Tanzania utapata mwendelezo

Mimi sijui naomba unielimishe kuhusu bindingness nature na execution ya hukumu ya Mahakama ya Haki za binadamu ya Afrika.

Je serikali ya Tanzania ikikataa kuheshimu hukumu ya Mahakama ya Haki za binadamu inaweza kuchukuliwa hatua gani za kisheria?

Naomba unielimishe kuhusu haya maswala mawili.
 
Tunataka vifungu vya sheria Kama hivi. Hongera sana mleta maada. Sio watu mnabishana Mambo ya kisheria halafu hamna kifungu chochote mlicho note
 
Back
Top Bottom