Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Acha kulipua hio sigara ya Urusi Braza [emoji2][emoji2] unaturushia sana...


Hivi unakumbukaje mambo yaliyotokea mwaka 1989 kwa usahihi hivyo???

Halafu malaika na vitu vya kufanana na malaika vyote vipo kwenye ulimwengu wa roho. Watu waache kuchanganya ulimwengu wa Roho na mwili kama wanavyichanganya UNIVERSE na COSMOS .
Hayo unayoona kama uko timamu ni Hallucination tu, labda kama unaona ukilala maana ulimwengu wa roho huwasiliana kwa ndoto pia.
Ila kimwili Malaika na Shetani ni matendo ya watu ikitegemeana na roho ipi iko ndani ya mtu husika (Mungu/Shetani anamtumia nani na kwa wakati gani)
Mfano;
Kuna vitu hutokea kwenye maisha unajikuta hii hio kawaida huyu mtu kama Mungu vile!

Ulimwengu wa roho kwenye mwili hauna nafasi bila mwili unao exist.
 
Acha kulipua hio sigara ya Urusi Braza [emoji2][emoji2] unaturushia sana...


Hivi unakumbukaje mambo yaliyotokea mwaka 1989 kwa usahihi hivyo???

Halafu malaika na vitu vya kufanana na malaika vyote vipo kwenye ulimwengu wa roho. Watu waache kuchanganya ulimwengu wa Roho na mwili kama wanavyichanganya UNIVERSE na COSMOS .
Hayo unayoona kama uko timamu ni Hallucination tu, labda kama unaona ukilala maana ulimwengu wa roho huwasiliana kwa ndoto pia.
Ila kimwili Malaika na Shetani ni matendo ya watu ikitegemeana na roho ipi iko ndani ya mtu husika (Mungu/Shetani anamtumia nani na kwa wakati gani)
Mfano;
Kuna vitu hutokea kwenye maisha unajikuta hii hio kawaida huyu mtu kama Mungu vile!

Ulimwengu wa roho kwenye mwili hauna nafasi bila mwili unao exist.
Asante sana. Kwa maelezo yako mazuri haya. Ulichoongea bado upo kwenye imani kuwa ni hisia. Na ndicho unachokiongea hapa.

Hiki ulichokiongea ni hisia aka Imani na unaamini kuwa aliyeandika bandiko hili anatumia sigara ya urusi. Mimi naheshimu imani yako.
 
Za masaa wana JF.

Leo nimeona ni vyema kuwaletea kisa kilichonitokea mwaka 1987 nikiwa kidato cha tano huko Ilboru secondary school. Nilikuwa nikisikia tu habari za malaika kwenye ibada za kidini.

Siku hiyo niliamka usiku kwenda kusoma darasani kama kawaida yangu, yapata saa nane za usiku. Hakukuwa na mtu yeyote darasani bali mimi tu. Wakati naendelea na kubukua ghafla ukatokea mwanga mkali mbele yangu. Ukaniangazia, niliingiwa na hofu na kuanza kutetemeka. Mara nikasikia sauti ya binadamu ikitoka kwenye mwanga ule. Ikiinita jina langu David, David usiogope tazama hapa.

Nilijawa na nguvu na kukaza macho yangu kuutanzama ule mwanga. Ghafla nimuona kiumbe afananae na mwanadamu rangi yake ya silver inayong'aa sana. Mdomo wangu ulikuwa mzito nilishindwa kuongea. Yule kiumbe alinisogelea na kuniambia "Nimekuja kukupa siri ya ulimwengu" Ndipo kiumve hicho kilinigusa kidevu changu, nilihisi kupigwa shot ya umeme. Akaendelea kusema mimi ni malaika, nimekuja kujidhilisha kwako. Ndipo mwili wangu wote ulianza kutetemeka. Alinishika na nikajikuta nipo katika eneo ambalo sijawahi kuliona ni zuri sana.

Akaniambia hapa ndipo huja watu wanapokufa duniani. Alinionesha watu mbalimbali waliokufa, walikuwa pale wakiwa na furaha. Nilimuona mwalimu wangu wa Hisabati kidato cha pili aliyekufa kwa ajali ya gari. Nilimuona akiwa na furaha.

Malaika huyo aliniambia usiogope kuhusu kifo maana ni sehemu ya ukamilisho.

Ni mambo mengi mno niliyapata siku hiyo. Kwa leo naongelea haya tu. Mpaka sasa malaika mbalimbali huwa wanakuja. Nimeshawazoea na tunaongea nao mambo mengi tu.

Nitakuja kuwaeleza namna yetu sisi tulivyofungwa kwenye kifungo cha hapa duniani. Na namna gani ya kuuona ulimwengu wote.

Asante kwa sasa.
Wenu mtiifu D.
Tayari UZI
 
Asante sana. Kwa maelezo yako mazuri haya. Ulichoongea bado upo kwenye imani kuwa ni hisia. Na ndicho unachokiongea hapa.

Hiki ulichokiongea ni hisia aka Imani na unaamini kuwa aliyeandika bandiko hili anatumia sigara ya urusi. Mimi naheshimu imani yako.
Hisia ni tofauti na imani mkuu..
mfano wa Hisia ni Hasira/furaha
Imani
WAEBRANIA 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

na hili ni tatizo kubwa kushindwa kutofautisha vitu vinavyofanana kimtazamo.
 
Hisia ni tofauti na imani mkuu..
mfano wa Hisia ni Hasira/furaha
Imani
WAEBRANIA 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

na hili ni tatizo kubwa kushindwa kutofautisha vitu vinavyofanana kimtazamo.
Hapa nadhani unaongea tisa na kenda.
Namna gani utakuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo pasipo hisia!?

Unaongelea jambo lilelile tu. Yaani uhakika wa mambo ya tarajiwayo ni kuhisi kuwa kitu kile unacho wakati huna.

Nakusihi tuliza akili kwanza uupitie uzi huu ukiwa upo open minded. Zaidi sana utakuwa unaongelea hicho hicho nilichokiandika.

Imani ipo moyoni(Nafsi), imani ni hisia.
Nikikutukana ukapata hasira ni hisia kuwa unaamini kile nilichokisema kinautwenza utu wako.

Safi kabisa uliposema hasira ni hisia very good.
 
Hisia ni tofauti na imani mkuu..
mfano wa Hisia ni Hasira/furaha
Imani
WAEBRANIA 11:1
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.

na hili ni tatizo kubwa kushindwa kutofautisha vitu vinavyofanana kimtazamo.
Halafu somo la imani haliishii katika tafsiri hiyo moja tu. Imani ni jambo kubwa mno.
Kwa sababu umekuja kwa njia ya biblia. Hebu soma hapa:-
"zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. "
Waefeso 6:16
 
Ulikuwa ushaanza kuvuta bangi au kutumia kilevi chochote ??
 
Back
Top Bottom