Marais Bora wa muda wote wa Tanzania ni Nyerere halafu Kikwete

Ni kweli kama Baba wa taifa alifanya vile kwa wakati ule kwa nini sisi tusifanye changes kulingana na wakati huu tuliopo
Miaka aliyotawala baba wa Taifa ni michache kuliko utawala alipoishia kutwala

Swali
Kwa nini bado tunaendelea kumnanga Mzee wa watu wakati nafasi ya kurekebisha upungufu wote uliopo Kwa sasa upo chini yetu?

Tuache ujinga Jk,Kikwete,Mkapa,Mawiny,Magufuli wamepita nini tunafanya kwa sasa kupambana na utawala uliopo

Raisi Samia
Kandamiza hapo hapo hakuna cha bure kwa sasa tufanye kazi mkono uende kinywani
 
Ni mawazo yako na binafsi ninayaheshimu. Ila mimi nina mtazamo tofauti.
 
Kumbe eeeh
 
Bado hajatokea. Hadi siku 50% ya Watanzania wamudu kula milo miwili tu kwa siku bila taabu.
 
Naona unaanza kufilisika kisiasa Mkuu, JK huyu anayenuka rundo la damu la marais wenzie ama JK yupi?

JK huyu bwanyenye ama JK yupi?

JK huyu dalali wa nchi na kuhani Mkuu ama JK yupi Mkuu?

Huyu huyu wa IPTL, Richmond na Dowans, ama JK yupi Mkuu?
 
Na kwa kukuhakikishia, huyu bwege siku kadondoka chali watu watalala na kushinda misikitini na makanisani wakimshukuru Mungu kwa kumalizana na mtu wake japo tayati katuachia makovu yasiyoisha kuanzia kwa Baba wa Taifa, Mzee Ben na Mwamba JPM.

Na ni kwasababu yake leo taifa halina mwenyewe, halina mkubwa wala mdogo wote ni kambale
 
Acheni kumfananisha Nyerere na Wapuuzi Wengine Afrika Mashariki au hata Afrika nzima sawa?

Kidogo ungesema anayeelekea Kufanana nae Kiuongozi na Kiakili ni Rais wa Rwanda Paul Kagame ningekupongeza na siyo Watu Wengine wa hovyo hovyo, Wezi na Wanafiki.

Na ambaye ndiyo nitakuja kuwa 100% kama alivyokuwa Hayati Mwalimu Nyerere ni Mimi Mwalimu GENTAMYCINE na niombeeni tu Afya Njema na Uhai mrefu ili Watanzania wote mumuone Nyerere mliyempenda na mliyemlilia sana ndani yangu.
 
Kikwete Kama asingekuwa Samia, Sita na Mkapa now toka 2015 tungekuwa na Katiba mpya.

Acha porojo zako, Kikwete si ndio aliyeiweka rasimu ya Katiba ya Warioba kwapani akiogopa kama ingepita angeswekwa lupamgo kama Zuma? Ufisadi wake na HOME SHOPPING CENTRE!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…