Marealle afungua kesi kutaka bibi yake afukuliwe mahala alipoishi miaka 80

Marealle afungua kesi kutaka bibi yake afukuliwe mahala alipoishi miaka 80

Mali ya Baba inanitoa roho,....Bora nikae peembeni, niinusuru roho yangu mimi, niinusustu Babaa...oiho yangu mimi......Harunaaaa

Mtu amepumzika kaburini, watoto wanataka kuuana kama vile wao wataishi milele
Wayahudi na wapalestina wanauana huko... Kwa taarifa yako hamna kitu kinaleta ugomvi kama ardhi. Sentimita 20 tu inaweza kukutoa roho.
 
Hao ni watu masikini na hawana lolote!
Ndugu kugombea akari 2 hadi kufikia hatua ya Kutaka kufukua mwili wa Marehemu mama yao mdogo!
Chuki, wivu na akili ndogo zimejaa kwenye hiyo familia kwa sasa!
Wajinga hao wanatumia vibaya jina la Chief Marealle!
 
Hawa ni ndugu tena nawajua nini kushindwa kuelewana ? au mmekumbuka kuwa dada yenu alizkwa na dhahabu zake?

Hizi ndizo laana za ukoo, wataacha ukoo unaandamwa na kesi milele.
 
Hawa ni ndugu tena nawajua nini kushindwa kuelewana ? au mmekumbuka kuwa dada yenu alizkwa na dhahabu zake?

Hizi ndizo laana za ukoo, wataacha ukoo unaandamwa na kesi milele.
Wana utajiri wa fedha ila wana umasikini wa akili
 
Ardhi ya uchagan ni dhahabu
Elezea. Unafahamu potentiality ya ardhi inapimwaje?

Ardhi potential inatakiwa iwe na rutuba, iwe karibu na mji wenye mzunguko mkubwa wa fedha, iwe jirani na bandari, barabara kubwa, lakini pia isiwe na makaburi kila kona.

Moshi Vijijini kila shamba pamezikwa mtu. Hili peke yake ni kikwazo katika soko. Makaburi yanashusha thamani ya ardhi kuliko unavyofikiri.

Ndiyo maana hata kwenye hii kesi ya hawa Wamarangu, upande mmoja unataka kaburi lifukuliwe, ni kwa sababu anaona kwamba kaburi lile ni kikwazo katika thamani ya eneo linalo zozaniwa.

Leo hii nenda kwa mtu mjini mwambie unauza ardhi Moshi Vijijini; kwanza atakushangaa kwa sababu hapauziki.

Wizara husika imeshawashauri kwamba Halmashauri husika ianzishe eneo maalum la makaburi ili viwanja vipimwe, Mji wa Moshi uongezewe eneo halafu utangazwe Jiji, ila bado mafuvu yao yamekakamaa tu.

Vishoiya!
 
Utajiri uliopindukia ni utajiri wa aina gani. Wachaga kwa sifa za kijinga?
Watanzania wenye asili ya hapa kwetu wapo wanne tu

Hans Macha
Ernest Massawe
Arnold B.S Kilewo
Harold Temu
Wilfred Tarimo


/...........................................................

1. Patrick Schegg

Net worth on the DSE: $23.5-million / 57,598,500,000 Tshs/=

Holdings: NMB Bank PLC, CRDB Bank PLC


2. Aunali Rajabali

Net worth on the DSE: $23.4-million / 57,353,400,000 Tshs/=

Holdings: NMB Bank PLC


3. Sajjad Rajabali

Net worth on the DSE: $23.4-million / 57,353,400,000 Tshs/=

Holdings: NMB Bank PLC


4. Hans Macha

Net worth on the DSE: $6.4-million / 15,686,400,000 Tshs/=

Holdings: CRDB Bank


5. Ernest Massawe

Net worth on the DSE: $5.3-million / 12,990,300,000 Tshs/=

Holdings: TOL Gases Limited

6. Murtaza Nasser

Net worth on the DSE: $2.7-million / 6,617,700,000 Tshs/=

Holdings: Tanzania Portland Cement
.

7. Sayed Kadri

Net worth on the DSE: $2.1-million / 5,147,100,000 Tshs/=

Holdings: Tanzania Portland Cement, Swissport Tanzania, Tanzania Cigarette Public Limited


8. Said Bakhresa

Net worth on the DSE: $1.5-million / 3,676,500,000 Tshs/=

Holdings: Tanzania Portland Cement

9. Arnold B.S Kilewo

Net worth on the DSE: $1.1-million / 2,696,100,000 Tshs/=

Holdings: 5.68-percent of TOL Gases, 0.013-percent in Tanzania Breweries

10. Harold Temu

Net worth on the DSE: $$720,000
1,764,720,000 Tshs/=

11. Wilfred Tarimo
Net Worth at DSE USD 980,000.

Holdings: TBL.
 
kuna watu wengine wakitaka kudhulumu mali wanakimbilia kuzika mtu, anachodai Frank Mareale ni sahihi , baraza la ardhi litambue mipaka na si kutoa maamuzi kwa hisia
Kwa nini Mahakama Kuu isingemaliza hiyo kesi ya mipaka na badala yake imeaamuru kesi ianze tena upya baraza la Aridhi!? Hii kesi haishi leo wala kesho, mtakuja niambia siku moja!!
 

Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro,imeliamuru baraza la Ardhi wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro,kurejea upya mgogoro wa Ardhi wa familia maarufu ya chifu Marealle kwa kutembelea eneo linalobishaniwa na wanandugu hao na kurekodi upya mipaka na kisha kutoa maamuzi chini ya mwenyekiti mwingine wa baraza hilo

Jaji kuu,Lilian Mongella katika kesi namba 51/2023 ya mrufani Frank Mareale dhidi ya Ackley Mareale ambao wote ni wanandugu, Jaji Mongella alisema mahakama imepitia ushahidi na maamuzi ya Baraza la Nyumba na Makazi la Mji wa Moshi chini ya Uenyekiti wa Reginald Mtei yaliyotolewa mei 5 mwaka huu na kusema kuwa maamuzi hayo yalikuwa na kasoro za kisheria.

"Nimeamua kesi hii ya wanafamilia wa Mareale isikilizwe upya kwa sababu Baraza la Ardhi lilikosea kisheria kwa kushindwa kuonyesha mipaka ya ekari mbili inayogombaniwa"

Katika kesi ya awali iliyofunguliwa na Frank Mareale katika Baraza la Ardhi Nyumba na Makazi katika Mji wa Moshi, alikuwa na madai matatu moja wapo ni ombi la Baraza hilo litamke kuwa eneo la ekari mbili yeye ni mmiliki halali, Pili Baraza litoe amri ya kufukuliwa kwa mwili wa mama yake mdogo marehemu Veronica Mareale aliyeishi katika eneo hilo miaka 80 na kufariki mwaka 2020 na pia alitaka alipwe gharama za kesi.

Akizungumza nje ya Mahakama,Wakili wa Ackley Mareale,Julius Semali alisema kuwa hana pingamizi na uamuzi wa Mahakama kwani ana uhakika kuwa mteja wake ni mmiliki halali wa eneo hilo kwa kuwa mama yake alipata kihalali na alizikwa katika eneo lake.

Naye Wakili wa frank Mareale,Modest Njau aliishukuru Mahakama Kuu kwa uamuzi wake wa kuiagiza Baraza la Ardhi Nyumba na MakaziMoshi kusikiliza upya kesi hiyo na aliamuru Mwenyekiti wa Baraza na wajumbe wake wabadilishwe.

Njau alidai Mahakama Kuu iliona jinsi haki ilivyokuwa ikitaka kuchezewa katika usikilizwaji wa awali nayeye na mteja wake wameridhika na maamuzi hayo

Mei 5 mwaka huu chini ya mwenyekiti wa Baraza hilo la Ardhi Nyumba na Makazi ,Reginald Mtei lilitupilia mbali madai hayo ya Frank Mareale na kusema kuwa Ackley Mareale ni mmiliki halali wa eneo hilo na sio vinginevyo
.
Ardhi tumeikuta tutaiacha ya nini kumsumbua marehemu kwa kipande cha futi 6x6 tu katika eneo la ekari mbili!
 
Ardhi tumeikuta tutaiacha ya nini kumsumbua marehemu kwa kipande cha futi 6x6 tu katika eneo la ekari mbili!
Hiki kizazi msichopita mafunzo ya JKT likitokea la kutokea mnaweza kuacha wake zenu kwenye baridi na kutetea mipaka kweli?

Nina wasiwasi sana na sera za CCM kutowapeleka JKT au kama hakuna namna basi mpelekwe GAZA na UKRAINE mkapate kujua namna ya kutetea ardhi.
 
Huwa ninawashangaa hawa ndugu zangu ni kipi haswa kinawafanya kuzozania vipande vidogo vya ardhi ya Kilimanjaro wakati nchi yetu ina maeneo mengi yasiyotumika.

Kilimanjaro pamejaa na ni eneo lenye population pressure kwa sasa.
Hayo maeneo mengi yanapatikana bure bure Kama enzi hizoo,
pesa pesa ndugu, maeneo yamepanda Bei.
 
Hiki kizazi msichopita mafunzo ya JKT likitokea la kutokea mnaweza kuacha wake zenu kwenye baridi na kutetea mipaka kweli?

Nina wasiwasi sana na sera za CCM kutowapeleka JKT au kama hakuna namna basi mpelekwe GAZA na UKRAINE mkapate kujua namna ya kutetea ardhi.
Uliyepita JKT umejitoa kiasi gani kutetea ardhi waliyopewa waarabu Loliondo, Ngorongoro nk
 
Back
Top Bottom