Marehemu Ayubu Kiguru: Shabiki mkubwa wa Sunderland football club miaka ya 1960

Marehemu Ayubu Kiguru: Shabiki mkubwa wa Sunderland football club miaka ya 1960

Myaya...
Zamani kulikuwa kila mwaka hizi club zinafanya khitma ya
kuwarehemu waliotangulia mbele ya haki.

Siku hizi sijasikia.

Club iliyobaki na utaratibu huu ni Saigon peke yao ambao
kila mwaka wao husoma khitma na kufanya karamu watu
wakaalikwa pamoja na viongozi wa serikali.

Hii shughuli kila mwaka inazidi ukubwa na watu wengi sana
wanahudhuria:

AcA3LUTqtgLOHRvM7L47DtjoJg9_E4t2JWOOMwuJ5EuXdvSyXU2hUZfi6ka4OAbGx1TeBm6VrIVB9kmeTtTHhBJUo7X6nUEpu5jHIwjcnBnQEqMZvYVX6Lps2DhWSXEmGW_sjbT2rdvoFd731TBM2zq1nqwYMng59VXPHWCb5zpnxXWjTzEKhim4JvKYt0XN9UiS-uQkgYODMQiFZt8fBMBAPvZbtQikjt4CZR_dAJYtObdpypwbqhlvAQAHRj9KLRqTfPaBBCc9N_iPOPBWRub_9i9kZHkV4d_BxAQmq2lAQ8JR0FGmGCuYuct07Mq10nJZzF0nC0Rl3_mF2CMVV9ONckFc_DbHiPamH_IMFW_vmJSLxWwsE5FON10m-TJHF9l2FvhlcGIMjKhrmfN0Q7Xf4-MW-BE8e2je2U6NCGnFgEcvRNBPmyl_mJ0dh2WoNH12YG0PF4LX9yBlNxhBwl8V3bFDlV4ZAahWFpqzhEsg1rKZalJadwUWgD8U522rSGHrsdFWP1OX_czL3Je_LCyfr7N5FigZ-nuMeLcAUOhFxgtXXeEj5AizgD6vBcuFbQ1PrFPhdFk2vum_DGFMDGD9AasxeK9Z=w876-h657-no

Aliyekuwa Makamo wa Rais Ghalib Bilal katika khitma ya Saigon 2010

2HyQQKyBfjl6iV9knEG3G8mY1ZYw-kDcLcvOdIsKbXw2L1EpksUSutWDbFaHNljQPvGl1j2ZXIZxIs5SKSaRee3llTqDuZrib2N1ehl8xkkJdodinlKzDFjn2vR8GFBBfLSV80rjqfZdjZBIKoJu7-sl1O-iWy5jxMgV9_Z_WsTbTrbfrjsVO-8K7_spkc66EQ_5TW4Hewdv_HrbcS0KrZgnTAphB-w3W6KwJsBaBSE4D7z0xG5PaPPTu1Q8tqdzrx55ergM3uPzEuKOnqqZh-bigqj26sJNoUZOJN9CwNu4IYO9wsv-Huy-m79NSJT9fOfmlyNg1B5Ap5_VnWABY-r3_vA96mXpX5M6uwzqV-4Qngh200t3CZEaSFrDUijnjhcjUnYqSMyFgwvPw1lcQoKJ11mJ-AWBpMVnMJvd6edXH3cSGyL1ltfYF4eUAUehQ-xVjgORRtHEX1f51ROObXqiFvwm4jUgRm_YQOsSP97uIdw2RyfrB8pprg1Hs7BK4fnPa4BE6qjCWoILTZQrAS5CEW-OF_9mNQ-arF-G8n_EJEgIL0Ubo3K5Xc6DKclg6cNYxSGNS13ZUWUqaD2Ql8XKpTBwFuEG=w876-h657-no

Sheikh Rocket

Zm6moXuc7xOvVLqtJUO3RSqVEkOxoZ2vxR30rRwmDsCYAUHC1lcwN1-f0pEScDo91d8vhjtl2gZv65AYSJYyHb_j1NfqPNn6xr70aoYK1hMPybtnGovmvvcEJM5CkeQTHM4oy1AqruSjuIPuxxx1DnRhp6tDMcrNHqlZ6U3RSi0sFAbTwKq31DwZ01ALOnulpX9bTT9qSLw7e8bua16jSQqVYVKYM5mWu9SC5EKgq_6vU7yK53B3QWyXUeKtEJVUcWqIFFcdTGr2QUxD8kgAT0Q74L6YlATVbxS7UxiCMy0UCCk5moaAw9GUQ0TUiDt43mPfzSgaDdkxqCvW-18Jelg-34XS_GSbrZH9Re7qekN2XAg2xkvEXNeFKkVIMxO2WMICXU3OzVVwNkL1OslnxXVvWL9yZqji40SLLicBGriKkYN6S59CRumhs6yhyP5Df9Bd47VXDwdm5vcDKwWEkmsqKxeLzKcdBOiKGwtAGt3VEs8Z9aZwrOqz-Mh5W92Q60DNRPycY6xAYKR_SY3u2nU5Zy8cSC-snHV2ObFlOIxZt9s_oWSnLZCRmVWrI7vPHHCUA0qR0xDON7tzSIYtYWLuOEinhP54=w876-h657-no

Marehemu Athmani Kilambo aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa miaka ya 1960 - 1970

V_sMAJswn7REGIzfvDX-rNKneH231yguCE9i-YbklbDIjae4i3bvERTXXsXAfSZrNbcHBg7rjkBs1QJf6HmAxMJMLdDlVgqtJXaomy0to_QNh4S_cWzj_jbnIHsEbU3wp_iNPQhW4oJTl1jNcT3S8YVrb63rlXc8v2r3cP-5wB4tQRhzHwzAe7ha9ZWtRXdrrBvlqe_vl28y4jE5VD9jhEw8CxJzCNa1nKg267YqdMFPFF6weJOmLhYIvCQadQrdrY_bJebcCoMykI0CgKK60XMzPva0K5ts8d_nVJ6UZ1jEqf0dxBxT4Qc5Ix2OBBBZvndtVf1qANzswocqKOMgF_DBer75vX531xFRamv8y3t4qfAwEd84Qypdiy6q3jcGtrJTfIRk1cqfFrHjxrNTzmX39vyjRDqeScRUbDnCN22pC5Tq7krVPM0luTy0UgjDF5Ex8LlzspXpGv1PfWsvo12B9VgIbO4Y_9dTRL1Jmz9tkXaAU5rZztbmXpMn6XzSV6IJaDW87Cycab7LF6xxyKG5eNCnuMLdVEd6bD9OMdstrlCfVN9DhIkONvAWqXcm23SSKS3V19y8Sc5ONgHrbHu2k1nBuI_n=w876-h657-no

Marehemu Mohamed Mwita aliyekuwa Mhandisi wa Ndege za Serikali
Mzee Mwita alishafariki kumbe! Oooh namfahamu alikuwa akiishi Magomeni Mikumi. R. I. P.

Kaka ...
 
Unaweza kutukumbusha kisa cha kitwana kucheza nafasi mbili yaani mshambuliaji na golikipa nafasi ambazo alizimudu vyema ilikuwaje?
 
Ok Shukran
Wanamajlis,
Kwa wale wanaopenda kusoma historia ya soka la zamani nimeongeza vitu
katika makala ya Athmani Kilambo.

Nashukuru kuwa JF imenipa nafasi ya kumkumbuka Kilambo ambae yeye
siku zote akiniita kwa nickname yangu ya ''Sidney,'' lakini yeye akitamka,
''Signal.''

Ichukulieni hii kama taazia yake:
Mimi sikuzote nikimuita, ''Kaka Kilambo:''
Mohamed Said: KUTOKA JF: MAREHEMU ATHMAN KILAMBO: YOUNG AFRICANS NA TIMU YA TAIFA MSHINDI WA GOSSAGE CUP 1964 NA 1965

Jumapili iliyopita nilikuwa na Captain Malik kwa kipindi kirefu.

mEOhxVC2Q9uDHfYDI9LEDby5Lr9xRmniP6z3Y2hDOTDI8zf1REeJb1NoIWeTRCSbHOEeEncPKx3G-OqglU46ooz0BtyS2KSJOC0nZFthuUNKolPTMRnorID4HQm5rQ0jkG5kDYJGDJI-mw2nIxVAbX8bflgBbd4LpRhZkLg6tV_HmZjHekddgMvPOCJknM233HC6Zi749dxNkMoaTBIDks1mjl_3L3OBch_WLL_sPQN7xu97xQyhx7G61nA_de6Rw7dVT2vUa04KdgrxrTD3-xwZS60pId38VSKeXl2A0BNTq0A-3_NKZxaxjuK1qWxYP3l0g_VkzQTFhhtupjA123etbrOw2TeOAktSb_2YxKJhi4n05kP20jTKl_2qIvLQYrJblaJjCDo9O2PkzzIBMWUsj36P229caAGB9BF66G74Gkm8FHn-1CXQU0vga6S5Ds-pZUd-_edHjmP2wKJOqoYJAtp6LA6_ve4o5lkIe-qt4NQYZZJoAG6OVxWoMJTx93VNLuWckhUz5W19uNizqdu0ehC6LxAf5WaVR6K_wXWYGiZ7AVoTpbzBSPsFq0scTtkYzWkEjiWz96RAu0uVFCnnhz8PUU0i=w624-h657-no

Wakwanza kulia ni Captain Malik

Captain Malik alikuwa Captain wa Yanga nadhani katika miaka
ya awali ya 1960 na ndiye aliyempokea Kilambo Yanga akitokea
Bagamoyo na kumtia moyo kuwa anaweza kupata nafasi kikosi cha
kwanza.

Juzi alinihadithia mkasa uliotokea Ilala Stadium.

Yanga walikuwa na mechi na wachezaji wote walikuwa weshaingia
uwanjani lakini Kilambo alikuwa kachelewa.

Hakuna aliyekuwa anamjua Kilambo wakati ule hivyo akazuiwa lango
kuu ikabidi Captain Malik aende akampitishe mlangoni.

Sifa moja kubwa ya Captain Malik ni kuwa yeye ni Encyclopedia ya
historia ya mpira Tanzania.
 
2016%2B-%2B1

Mchango wa kujenga club ya Sunderland Msimbazi Street katika miaka ya 1970

Majuzi hapa kulikuwa na Simba Day.
Nimekaa leo asubuhi na kuwaza vipi Simba ilikotokea.

Sijui kama Simba walifanya kisomo, yaani khitma ya kuwarehemu
viongozi, wachezaji na wapenzi wa club toka enzi za Sunderland.

Ikiwa walifanya kisomo naamini kabisa katika majina ambayo
yaliyotajwa moja litakuwa la Ayubu Kiguru.

Aliitwa Ayubu Kiguru kwa kuwa mguu wake mmoja ulikuwa na
athari.

Hii ilikuwa miaka ya 1960.

Mimi bado mtoto na nikipenda Sunderland na nikimjua Ayubu kwa
karibu sana na sababu ni kuwa Ayubu alikuwa na ubao wa biashara
Soko la Kariakoo na mjomba wangu Bwana Khamis Salum na yeye
alikuwa na ubao wake si mbali na ubao wa Ayubu Kiguru.

Ayubu alikuwa na sura jamil na alikuwa mweupe wa rangi.
Mungu alimjaalia Ayubu kipaji cha kuongea na kubishana.

Soko la Kariakoo enzi hizo lilikuwa moja ya vituo vya ushabiki wa mpira
Dar es Salaam.

Yanga na Sunderland walitawala soko na Yanga washabiki wao wengi
walikuwa na biashara ya kuuza samaki kiasi ikawa watani wao wakiwaita
Yanga, ''Wauza Samaki.''

Siku ya mechi ya Sunderland na Yanga moto ulikuwa unawaka sokoni pale
toka mapema asubuhi.

Ushabiki huo utaendelea kwa juma zima takriban baada ya mechi.

Sasa ikitokea kuwa Yanga imefungwa na Sunderland washabiki wa Yanga
walikuwa tabuni kwa juma zima pale sokoni wakipigwa makombora na
Ayubu Kiguru.

Ayubu alikuwa na uwezo wa yeye peke yake kuwanyamazisha Yanga wote
pale sokoni kwa maneno yake, kejeli na kebehi lakini katika namna ambayo
mtu hawezi kughadhibika bali ni kucheka tu.

Enzi zile za Ilala Stadium kelele za kuzomea zikizidi kutoka uoande wa Yanga
Ayubu atasimama kuwaelekea Yanga na atatoa maneno watu watacheka.

Yanga maneno yakiwaingia kisawasawa na sasa wamepwelewa hawana la
kusema basi watamwambia, ''Wewe Ayubu nani atakuweza bwana kiwete
wewe nyie mlojaaliwa na Allah ni mdomo tu.''

Ayubu alikuwa pia ni bingwa wa matusi.

Jibu litakalotoka litamaliza ubishi wote watu watatawanyika watamuacha
Ayubu anapanga nyanya zake huku amevaa jezi ya Hamisi Kilomoni.

Ilikuwa Sunderland ikishinda Ayubu anachukua kikombe anakujanacho
sokoni anakiweka mbele ya ubao wake watu wanapita wanatunza.

Ayubu alikuwa akitukana lakini si kutokana na hamaki wala hasad ya nafsi.

Ilikuwa ndiyo kusherehesha ushabiki wa Yanga na Sunderlaand wala mtu
haendi Msimbazi Polisi kushitaki kuwa katukanwa na Ayubu Kiguru.

ZOKqAPBmC8q1UbYrbXg59vBZeKzVpKf9Wu3ZBQKJRK8buK7jqXPlZbnYiXjFt74XQ95hda2vVKX8R6peFY-wpn-fcDMOHFgIl6E8IILuYKsSINjCYUQt9iTkttnzb96_Gz-kGjuTQyy2goQtOIFcx5H86rcRP7f1gI96PLk5FD3LudGalWSABrYM2TlVEf7v5sMXVRuyEFYPy8oKsHENjt-CvWIlXP7Yr8eGvaVgegBMHw7mlMwNYRqVdpzD0GSQr_lTQCEk2wSU7j_mxzJ5XcXBYDl31GPx2-CotchSWa5l2sBqVP18o-SRCZexCjWF4v_0ncn0zY0qyT-y3Io2XnxUvG194A9Mdr0BSKhb9XtlayuO5EqMA-0YlAqwkiWOXh3AJ6v4b8M9iPSAiNtIAO-Qj3gI9GcO59NapGKis4a395qK1xm_x4vOsICU4-o3dlqxzBii5aU9roRF6xMwac-dxeiD4spNY01V0JWdp8kLhoqk2aQHG_qArAKpKtmDnqJddC5fHD7flU8Z3q_UWDLGDJfQHe_lFEMbEcnkO_elbaKmiZ67UNQQ-hnMFANgHEpOqN8ySCSs11GQeubtFBzv7ehL7q8l=w596-h657-no


Ilikuwa ''ambition,'' yangu siku moja nivae jezi ya Sunderland lakini kipaji kilikuwa
kidogo nikaishia mchangani.

Rafiki yangu marehemu Jumanne Masimenti (Cosmopolitan FC, Simba na
National Team) siku moja tushakuwa wakubwa kanambia, ''Wee ungecheza
mpira gani bwana uko mazoezini sisi tunapiga danadana, wewe uko pembeni
ushavaa jezi unasoma kitabu. Mchezaji mpira gani anakwenda mazoezini na
vitabu?''

Matokeo ndiyo haya leo niko JF hapa nadarsisha historia.
Umesema ulikuwa unaenda mazoezini na vitabu vya kusoma wakati wenzako wanapiga danadana.

Naomba kuuliza: what became of your formal education?

Ulisoma shule wapi na kama ulienda chuo chuo gani, shahada ya kwanza na ya pili kama zipo zilikuwa za nini na wapi.

Siko sana interested na shule ama vyuo na shahada za kujiendeleza ukubwani, nataka zile ulizosoma moja kwa moja toka utotoni bila kusimama na kuunga unga tafadhali. Ahsante.
 
Umesema ulikuwa unaenda mazoezini na vitabu vya kusoma wakati wenzako wanapiga danadana.

Naomba kuuliza: what became of your formal education?

Ulisoma shule wapi na kama ulienda chuo chuo gani, shahada ya kwanza na ya pili kama zipo zilikuwa za nini na wapi.

Siko sana interested na shule ama vyuo na shahada za kujiendeleza ukubwani, nataka zile ulizosoma moja kwa moja toka utotoni bila kusimama na kuunga unga tafadhali. Ahsante.
Buyaka,
Ndugu yangu sina elimu yoyote usitabike.

Elimu yangu inayonisaidia ni hii nilosoma kwa Maalim Haruna
yeye alinifunza mlango wa mnakasha, yaani mijadala na adabu
zake na vitu vingine vidogo vidogo.

Ilm hii ndiyo inayoniwezesha kuwa hapa JF.
 
Nikisoma khabari hizi za wakongwe kwanza majina yao ya asili na ya utani napata burdan hassan gobos omar Chogo mohamed chuma huku mkweche kule katolila Ibrahim kiswabi thuweni ally alloo mwitu Shaaban baraza. Basi hupata hamasa ya kujua wasifu wao.
 
Abunwasi,
Siku zimekwenda.

Kwenye maziko ya Abdulrahman Lukongo nilikutana na Hamisi
Kibunzi
nikamweleza mazungumzo niliyokuwanayo na marehemu
Athmani Kilambo kuhusu yeye na Arthur Mambeta, Yusuf Salum
na wengineo.

Nikamwambia kuwa Yanga wakiwahusudu sana baadhi ya wachezaji
wa Sunderland na akinitajia majina.

Kilambo anasema, ''Unajua kulikuwa na watoto kule Sunderland wana
mpira mzuri sana kama Kibunzi na Arthur Mambeta na Mzee Mangara
akiwataka awalete Yanga kuongeza nguvu ulinzi na ushambuliaji...''

Kilambo anasema kuwa Mzee Mangara anatuuliza, ''Mimi nikamwambia
kuwa hawa watoto akina Kibunzi na Arthur hata tukiwaleta Yanga
hawataweza kucheza mpira huku wana mapenzi makubwa sana na
Abidjan.''

Siku zile jina lingine la Sunderland ilikuwa ''Abidjan,'' na sijui lilitokana
na nini.

Kibunzi alikuwa hana habari hizi hata chembe.

Akacheka akanambia, ''Kilambo kasema kweli sisi tusingeweza kucheza
Yanga tukipenda sana Sunderland.''

Kilambo alikuwa mzungumzaji wangu mkubwa na akijua mie siipendi
Yanga sasa yeye ikawa kila siku kuniweka roho juu.

Mechi ya Yanga na Simba Zanzibar mwanzoni 1970s, Yanga walitokea
Nigeria, basi kanifata ofisini kunitisha ananiambia, ''Tumekufanyieni
fitna kubwa Zanzibar mnachukiwa kama Hizbu.''

Kweli Zanzibar tukafungwa Yanga wakachukua kikombe.

Kilambo alikuwa muungwana akiingiliana na wachezaji wa Simba vizuri
sana na akipenda sana kumtania Emmanuel Mbele ambae akipenda
kumwita, ''Fullup.''

m0AkTF7F_x7v3uUz2l23EpBUg-NuCixyFrth0Tb9uYA0crQq3KNKaXelEjFoRNlxHFUONs3932iil-jrro7ThdOFtCK4OJbIxeXITF01HigMjTKPcqpoNxAKuN0l192NamsWUTlv296Ip3oMJIexF0KtwXqD13xbZJPRayjMmnY4taN7X1TJ1DlLZiA5mzLXazFBLJAFseuk1P146pLPgvutcKSIT52ouzgr1BRO8FoAiEXBvuMUsSsojbL1zUNC0CZ7EtVwopylKgWKd3uPNGlk_zmL7Kt7N-2ZfZ37ltzp3OkmehLJGSUUBDC9bMcUVXAzaEf_Rkw-y_8lvWuaCeiQ7O8Igu9JksHFZ2RI6dHYce9X4yWhVwsdODcaOZTwo4wiSeCS5jgdbtppZtWMXn7TOyTQQ1VhZcRFkoPrFHXPFsuEGpBYONvF5kk4WVJsi3wYgcb8sTsv2608j8TLTonSeZSfD32Fehp36W0amrSqgS80S2BUncyiMsC379ii_fNZVYGfswq0h8bG5P1CV-62yKv9xQGueOrOuwR4Ezl_dhY-KLBKMNPSxeFR5B2XzcieroR0MEAm5G4eV-_4eT_iKhj-aXF6=w876-h657-no

Waliosimama wa tatu kulia ni Athmani Kilambo, wa tano Abdulrahman Lukongo
timu ya East African Cargo Handling Services



Akijua mapenzi yangu ya mpira na alikuwa akinipa habari nyingi sana za
Yanga hadi uchawi wa kuloga mechi.

Siku za mwisho za maisha yake tukiswali pamoja msikiti wa Manyema na
akija akiniona hataingia ndani msikitini sharti kwanza aje anisalimie.

XGLv9aiIr6aRQxikp3KyYIemtMOzk4wiDYGsKgXZBPoBx4Lvnzjjj_6InCUxJztppvycitZbf2umdl3cwi2otJcRzl1hJLtu2xQ35G7TMOJFipVN3pKHhDroX68OGm3xwzGTyzR48CCGtpXeLcHyfZupQA59VUMTLmMaLGN_WbQboAzLy5hnvKjcxJgV6VL2gjat8eMsUBQy4aWaQcr_TaIhlumWzuirk9mnF5is52gCmRQ9zTHG8wjGPtBh98lVmZZf5iENiVLXjZztr5jBpEZp4Kwyr4XQU0hbb5B7C82D0nC99pQ_NpTtkbA-4qDlRw4uqBc9gnWofHNj3G8zq0XE4D29dOi9NimCBpBKelwss7pmrnLQsIoRyV04AI6E-oFCUf8ccuinwK38CKaLdNYZh8Mwx0WGGpbyl2jPyud94FeGevOVNw9MU_dPPvz6L93r1--UQJ9Gph7MGwMzre6RCDSVtZgZeWZ0S3pBw5xUILlU--LPdlxkCRii1dPHd0lr2eqFspgNUmM3cEGqSPzuPlUlmbJkW5j6bBrUHBA_NXeCJnkk1GBgZPreFpevwVR-iuE1Mt9EOFMMUSxO7duU-LsuljQ=w330-h220-no

Athmani Kilambo (Yanga) kushoto na Abuu (Cosmo)
kulia kwenye khitma Saigon.

cVvBeW3-lqa-Sd7MqUlDplfoUmWunLyb39y1HpawtAKj8pHw3WNTEvxKiA7ZuHrnEkYeEVbWdPmM7h8Rw-gNsWNRmTRpYU6speUv4RGaooeiDXtbuOocZ1LWjosiMRYnLYZn62Eh4pJLSJdr3B-xiMLsnnAhuVOAjrd7BgX6SseyklnKhX3y-VDeD0bTO4oM195dRkI1PIYApi75HUH9ngf-TaMlPe6CTf5NgWy3ESnwxwdaOJQFLhwLbSUph0eYR8UF1p4RuUjCzvy263-LMhD5ZyM850psRTbRLcEK_Qd4JFf0XTuF2ltLiUh3ROOadG7SBQNaXkaGEE_QtEnYx60z1GmE8kgaYqUHd8-teqAL4ck2RYet6xe-JM-72LAQzKWdJdOmIiVZdLUx4TNID7BtQaBN1umspcDn31bgc5eithBOHlhhDB6HdfYPEqK302gmwfDeq97AzPSuUDF4OwAdTGBLK-LvH-ZGkwTCNrmu1klTT_PPyFsnR8F_PF7ox0SEsPIAlXli5sMmBurAIgCYX5iAJTbzEiDvvXBu1njpIhTcUvrMcgJYYwT_BJ8Ypp0zmI7fg1U9BwmAnUiTedwbQw9XMog=w986-h657-no

Kushoto wa kwanza mbele ni Hamisi Kibunzi, nyuma kulia wa kwanza Arthur Mambeta
anaemfuatia ni Emmanuel Mbele na wa sita ni Yusuf Salum.
Ahsante sana mwana kariakoo mwenzangu
 
Umesema ulikuwa unaenda mazoezini na vitabu vya kusoma wakati wenzako wanapiga danadana.

Naomba kuuliza: what became of your formal education?

Ulisoma shule wapi na kama ulienda chuo chuo gani, shahada ya kwanza na ya pili kama zipo zilikuwa za nini na wapi.

Siko sana interested na shule ama vyuo na shahada za kujiendeleza ukubwani, nataka zile ulizosoma moja kwa moja toka utotoni bila kusimama na kuunga unga tafadhali. Ahsante.
Ukisha jua zitakusaidia nini? Bw. Mohd Said ameandika kuhusu mambo ya michezo na wale aliyocheza nao pamoja na wanamichezo/mashabiki wa kweli wa enzi hizo sasa huko unakokwenda ni wapi???????
 
Umesema ulikuwa unaenda mazoezini na vitabu vya kusoma wakati wenzako wanapiga danadana.

Naomba kuuliza: what became of your formal education?

Ulisoma shule wapi na kama ulienda chuo chuo gani, shahada ya kwanza na ya pili kama zipo zilikuwa za nini na wapi.

Siko sana interested na shule ama vyuo na shahada za kujiendeleza ukubwani, nataka zile ulizosoma moja kwa moja toka utotoni bila kusimama na kuunga unga tafadhali. Ahsante.
Duuuuh!!!!!!!!!!!!!! wewe utakuwa mgeni JF
 
Nikisoma khabari hizi za wakongwe kwanza majina yao ya asili na ya utani napata burdan hassan gobos omar Chogo mohamed chuma huku mkweche kule katolila Ibrahim kiswabi thuweni ally alloo mwitu Shaaban baraza. Basi hupata hamasa ya kujua wasifu wao.
Guasa,
Hassan Gobbos
Yanga wakimwita King Hassan wa Morocco.
Alloo Mwitu na Hamisi Askari waliletwa kutoka Kigoma na
Hamisi Kilomoni waje wacheze Simba.

Wote wawili walikuwa wanacheza nyuma.
Chogo jina lake ni Juma alianza mpira Young Kenya.

Hii ''Chogo,'' ni sababu ya kichwa chake.
Kulikuwa na Said Ndomo.

Hii ''Ndomo,'' ni kwa ajili ya mdomo wake.

Said alianza mpira katika club ya mtaani New Port kisha akenda
Cosmopolitan.

Kwenye maziko ya Kilambo nilikutana na Said baada ua kupoteana
kwa muda mrefu sana.

Nadhani yeye kanishangaa mimi kwa kuona nimezeeka kama mimi
nilivyomshagaa yeye.

Kulikuwa na Mustafa Mabuge kwa kuwa miguu yake ilikwenda upande
kwa ajili ya funza.

Ndiyo hiyo ''Mabuge.''
Yeye alikuwa beki na mbili wa Cosmo ya 1960s mwanzoni.

Huyu alikuwa mwana Gerezani mwenzangu.
 
Ukisha jua zitakusaidia nini? Bw. Mohd Said ameandika kuhusu mambo ya michezo na wale aliyocheza nao pamoja na wanamichezo/mashabiki wa kweli wa enzi hizo sasa huko unakokwenda ni wapi???????
Abunuwasi,
Iko siku niko Marekani nafanyiwa utambulisho kabla sijapanda jukwaani
kuzungumza.

Mzungumzaji kanipamba mwisho wa kunipamba.

Ghafla inanijia picha ya marehemu mama yangu nina miaka mitano tuko
sokoni kwa muuza vitabu ananinunulia kitabu cha ''Jifunze Kusoma.''

Anamlipa muuzaji ananikabidhi kitabu na tulipofika nyumbani yeye ndiye
mwalimu ananianzisha alif kwa kijiti.

Kuna kitu kilipanda hadi kooni kikanikwama machozi yanataka kunitoka.

Najiambia, ''Ingekuwaje mama yangu, mwalimu wangu Bi. Mwanaidi biti
Sheikh
leo ungelikuwa hapa ukaniona mie mwanao nahadhiri chuo kikuu
Marekani na hawa Wazungu wameitana kuja kunisikiliza...''

Laiti mzungumzaji angeliendelea zaidi ningelihadhirika.
Ningeliwamwagia chozi...

Abunwasi,
Hayo mimi ninakutananayo kila siku wala yasikupe tabu.

Huyo anaugua maradhi ya nafsi na ni mabaya sana kwani tiba yake ni ghali
mno.

Ngoja nihitimishe.

Alikuja Mhariri wa Oxford Univeristy Press kutoka Nairobi kuja turekebishe vitu
fulani katika kitabu nilichoandika ili wakichape.

Tumeifanya kazi tushamaliza.
Kumbe huyu bwana ana kitu kinamchonyota.

Muda wote tukisema Kiswahili.

Sasa anafunga lap top yake ananiuliza, ''Mr. Said hiki kitabu uliandika kwa Kiswahili
halafu ukampa mtu akuwekee kwa Kiingereza?''

Jibu langu lilikuwa hapana.
Nikataka tufahamiane ili siku nyingine anipe kazi.

Nikamwambia nina First Class Merit Pass English Oral Cambridge Examination 1970.

Mimi nilimwia radhi kwa kuwa alikuwa akisikia Kiswahili changu kina ''heavy accent,''
ya usemaji wa Kidaresalama ikamjia fikra nyingine.
 
Iko siku niko Marekani nafanyiwa utambulisho kabla sijapanda jukwaani
kuzungumza.
hahahahahahaaaaaaaaaaa.....

Naona umerudi kivingine, nilidhani ulisema hujasoma vya ajabu!

JF hapa tupo waponda zege na wauza ulanzi na wahandisi na mawakili na madaktari na wauza simu na kila aina ya watu na tunajadili masuala ya kijamii kwa pamoja.

Sasa wewe uliyejinasibu kwamba uko hapa unatoa somo kwa sababu tangia utotoni ulikuwa unaenda mpirani na vitabu wakati wenzio wanacheza dana dana, basi hebu niambie synopsis ya elimu yako ni nini. Ulisoma msingi wapi, sekondari wapi, chuo kama ulienda ulienda lini, ulienda wapi na ulisomea nini Mohammed Said.

Utaonaje aibu kusema elimu yako wakati umejinadi kwamba ulikuwa unaenda uwanjani na vitabu wenzako wanacheza mpira? hahahahahaaaaaaaa...... !
 
Guasa,
Hassan Gobbos
Yanga wakimwita King Hassan wa Morocco.
Alloo Mwitu na Hamisi Askari waliletwa kutoka Kigoma na
Hamisi Kilomoni waje wacheze Simba.

Wote wawili walikuwa wanacheza nyuma.
Chogo jina lake ni Juma alianza mpira Young Kenya.

Hii ''Chogo,'' ni sababu ya kichwa chake.
Kulikuwa na Said Ndomo.

Hii ''Ndomo,'' ni kwa ajili ya mdomo wake.

Said alianza mpira katika club ya mtaani New Port kisha akenda
Cosmopolitan.

Kwenye maziko ya Kilambo nilikutana na Said baada ua kupoteana
kwa muda mrefu sana.

Nadhani yeye kanishangaa mimi kwa kuona nimezeeka kama mimi
nilivyomshagaa yeye.

Kulikuwa na Mustafa Mabuge kwa kuwa miguu yake ilikwenda upande
kwa ajili ya funza.

Ndiyo hiyo ''Mabuge.''
Yeye alikuwa beki na mbili wa Cosmo ya 1960s mwanzoni.

Huyu alikuwa mwana Gerezani mwenzangu.
Nimepata kujua namna gobbos alivyopata kuitwa pia nini kilitokea mpaka kukawa na yanga raizoni (rise on )na wengine kujiita kandambili au gongo wazi?
 
hahahahahahaaaaaaaaaaa.....

Naona umerudi kivingine, nilidhani ulisema hujasoma vya ajabu!

JF hapa tupo waponda zege na waunza ulanzi na wahandisi na mawakili na madaktari na wauza simu na kila aina ya watu na tunajadili masuala ya kijamii kwa pamoja.

Sasa wewe uliyejinasibu kwamba uko hapa unatoa somo kwa sababu tangia utotoni ulikuwa unaenda mpirani na vitabu wakati wenzio wanacheza dana dana, basi hebu niambie synopsis ya elimu yako ni nini. Ulisoma msingi wapi, sekondari wapi, chuo kama ulienda ulienda lini, ulienda wapi na ulisomea nini Mohammed Said.

Utaonaje aibu kusema elimu yako wakati umejinadi kwamba ulikuwa unaenda uwanjani na vitabu wenzako wanacheza mpira? hahahahahaaaaaaaa...... !
Bu'yaka,
Kweli sijasoma na sioni aibu kukwambia kuwa sijasoma.

Wewe kwa kuwa mgeni hapa majlis ndiyo hili jibu langu
linakustaajabisha.

Kuna mtu kakuuliza we mgeni?
Sababu mie nafahamika kuwa hamna shule hapa.

Ila toka utoto nikipenda kusoma.

Huyo George Orwell mie nimemsoma nikiwa na umri wa
miaka 15.

Unataka nijipe sifa nisokuwanayo?
Hii ndiyo itakuwa aibu.

Aibu siyo kusema kweli.

Kuwa natoa darsa hili mbona liko wazi?
Huku si kujinasibu.

Niko hapa majlis miaka mingi sasa nikitoa darsa.

Unataka nikueleze kuwa nilisoma mashule makubwa makubwa
ya Dar es Salaam wakati si kweli?

Au nimesoma chuo kadha wa kadha hapa nyumbani kisha Uingereza,
Marekani na kwengineko wakati si kweli si nitakuwa najifedhehesha?

Na ikiwa kweli nimesoma huko hii itakuwa si uungwana kwani itakuwa
najinasibu.

Waswahili sisi tumefunzwa na wazee wetu kutojinasibu kwani hiyo si
katika mafunzo ya adabu njema.

Kwani kwenu umefunzwaje?
Nipe ruhusa nikuelekeze jambo.

Unapoweka nukta zinatakiwa ziwe tatu...
Hizi ndizo kanuni za uandishi...

Huweki msururu......
Watu watakucheka watajua lipo tatizo la skuli...

Lakini mimi sitocheka kama ulivyocheka wewe.
Hapa ni mahali pa kufunzana mengi pamoja na adabu.
 
Back
Top Bottom