1. Si rahisi kwa mindsets kama hizi za waisrael na aina ya kina
FaizaFoxy au
Malaria 2 na wenzao.
2. ZIngatia waisrael wanaamini wapalestina ni kama wanyama tu wasiostahili kuishi. Buza hapo
MK254,
Moisemusajiografii na wenzao wafia dini wa namna hIyo wanawakilisha. Wafia dini hawa wajulikani ni wa dini gani maana mwisrael Wala SI dini yao!
3. Hawa wengine nao wanaamini ni vita dhidi ya uislam japo wapalestina hawajasema hivyo. Hawa ni wafia uislam, piga ua hawa damu kutoka masikioni haibadilishi kitu!
4. Shughuli yake waiona hapo? Vita vya kidini si anashinda Mungu? Si balaa la kufaa mtu hilo? Hadi aje Mungu mwenyewe kuweka mambo yake sawa.
5. Suala la vita vya ardhi limevamiwa na la wenye agenda zao. Basi tena disco limevamiwa na wamorani. Kuna kupona mtu hapo?
Waiona shughuli ilivyo pevu ndugu?
a) Wafia Uislam: Hawa kwao dini ni uislam tu, tena ule wa kwao. Huwashangaa wengine wote na dini zao. Haiwaingii akilini iweje usiwe mwislam wa aina yao. Hawana uvumilivu na wengine. Mbingu na pepo wanayoijua ni ile yao tu, si ya wengine. Adui yao mkuu ni yeyote asiyekuwa mwislam na hasa mwisraeli.
b) Wafia Ukristo: Hawa wanaamini dini ni ukristo tu, tena ule wa kwao. Wanaamini Israeli ni taifa teule na kuwa tena si binadamu wa kawaida. Lolote afanyalo mwisraeli ni sawa tena dunia yote ilipaswa kuwasabiria. Hakuna ovu lolote dhidi ya Israel, na waarabu kwao, hawana haki yoyote.