Maridhiano ya CCM na CHADEMA Ndiyo Kawaida ya Vyama vya Siasa Duniani Ilivyo?

Maridhiano ya CCM na CHADEMA Ndiyo Kawaida ya Vyama vya Siasa Duniani Ilivyo?

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
12,096
Reaction score
15,393
Mara nyingi sisi hupenda kuiga au kujilinganisha na hawa wenye demokrasia yao waliyoitengeneza kwa muda mrefu.

Sasa nauliza, hizi mbinu za CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe inakidhi kweli mlinganisho wowote na wayafanyayo Democratic Party na Republican wa Marekani au Chama cha Labour na Conservative vya Uingereza; au hata vile vilivyoko Ujeruman kwa namna yoyte ilei?

Nionavyo mimi, haya majadiliano na maridhiano ni njia tu za kutafuta ulaji kwa raha toka kila upande, bila kujali maslahi ya nchi na wananchi wake.

Ninaelewa, kuna mambo ambayo huwaleta pamoja hao wakubwa wa dunia, na yote ni yale yanayohusu siasa za nje, hasa wanapopambania maslahi ya nchi zao dhidi ya mataifa wanayoyaona kuwa hatarishi kwa maslahi yao.

Haiwezi hata siku moja ikatokea watu wa Democratic Party wakawaalika wenzao wa Republican kusherehekea shughuli zao za kichama. Hali ni hiyo hiyo na Labor party na Conservatives; na hata kule Canada, Australia, hata Japan, Korea Kusini na kwingineko.
Hii haina maana kwamba hawapendani kama ndugu, au kwamba kuna uhasama kati ya vyama vyao, lakini ndivyo ilivyo ni kama utamaduni kwao.

Sasa sisi tunaiga kitu gani, kama siyo njia tu za kuhalalisha kugawiana mafao ya jasho la wananchi.

Soma: Ujio wa Rais Samia Suluhu Hassan: Hadi sasa sijaona dalili yoyote ya utashi wa kuwepo kwa maridhiano ya kisiasa nchini
 
Maridhiano haya ni ubunifu wa CHADEMA na CCM ndio mtekelezaji.. Wengi wana wasiwasi kama huu wako, lakini CHADEMA ni chama chenye think tank kubwa sana na wasomi wenye weledi na maono ya kutosha sana

Kwa hatua hii ya kwanza tayari CHADEMA imeshatia mguu mmoja ndani ama kimjinimjini imeshaingiza kichwa ni hatua moja kubwa sana kwakuwa sasa CHADEMA itafanya siasa zake kwa uhuru bila woga wa kukamatwa. Kutekwa, kubambikiwa kesi. Kujeruhiwa na kudhulumiwa haki zake nyingi za msingi

Hatua ya pili na ya tatu zinakuja na mpaka 2025 CHADEMA itakuwa imeshamaliza kazi
Kuna vimatukio vidogo vidogo vinajengewa hoja nyepesi lakini CHADEMA haishughuliki navyo kwakuwa ilaeweza vipo kwa ajili ya kuwatoa kwenye reli na pia vinaletwa na wale wote waliochukizwa na haya maridhiano
 
Mara nyingi sisi hupenda kuiga au kujilinganisha na hawa wenye demokrasia yao waliyoitengeneza kwa muda mrefu.

Sasa nauliza, hizi mbinu za CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe inakidhi kweli mlinganisho wowote na wayafanyayo Democratic Party na Republican wa Marekani au Chama cha Labour na Conservative vya Uingereza; au hata vile vilivyoko Ujeruman kwa namna yoyte ilei?

Nionavyo mimi, haya majadiliano na maridhiano ni njia tu za kutafuta ulaji kwa raha toka kila upande, bila kujali maslahi ya nchi na wananchi wake.

Ninaelewa, kuna mambo ambayo huwaleta pamoja hao wakubwa wa dunia, na yote ni yale yanayohusu siasa za nje, hasa wanapopambania maslahi ya nchi zao dhidi ya mataifa wanayoyaona kuwa hatarishi kwa maslahi yao.

Haiwezi hata siku moja ikatokea watu wa Democratic Party wakawaalika wenzao wa Republican kusherehekea shughuli zao za kichama. Hali ni hiyo hiyo na Labor party na Conservatives; na hata kule Canada, Australia, hata Japan, Korea Kusini na kwingineko.
Hii haina maana kwamba hawapendani kama ndugu, au kwamba kuna uhasama kati ya vyama vyao, lakini ndivyo ilivyo ni kama utamaduni kwao.

Sasa sisi tunaiga kitu gani, kama siyo njia tu za kuhalalisha kugawiana mafao ya jasho la wananchi.
Ukijua maana ya conspiracy utaelewa mengi sana
 
Siasa zetu hazina budi kuzingatia mazingira yetu, desturi zetu, mila zetu, miiko na utamaduni wetu wa kitanzania na wa kiafrika na siyo lazima kufuata ya kimagharibi na vivyo hivyo kwa misingi ya maridhiano ya sasa uichukulie katika sura hiyo. Achana na Democrats na Labour
 
Marekani hakuna mfumo wa chama tawala, Ni nadra sana kukuta chama kimoja kimeshikilia Urais, House of Representative na Senate kwa wakati mmoja. Halafu pia bado kuna serikali za majimbo zinazokuwa za vyama tofauti. Katika hali hiyo huwezi kukuta chama kimoja kinakionea au kukikandamiza chama kingine na hivyo hakujawahi kuwa na haja ya maridhiano.
 
Uingereza na Ulaya kwa ujumla huwezi kusikia upinzani ukinyanyaswa, viongozi wake wakikimbia nchi, kupigwa risasi au, wakifilisiwa, kuhojiwa uraia au kufunguliwa kesi za kisiasa. Kuwepo kwa utawala imara wa sheria ,uhuru mkubwa wa kisiasa na kutodhulimiana kisiasa kati yao kunaondoa haja ya maridhiano kama yanayofanyika katika nchi nyingi za Africa.
 
Kinachoendelea ni wanasiasa kuungana kuwakandamiza wananchi.

Tukatae huu usanii unaoendelea maana sisi ndio tunaopoteza zaidi.

Kwani hakuna wa kuzungumzia hali ngumu za wananchi katika mazingira haya ambayo wote ni kitu kimoja.
 
Anzisha chama chaka au nenda barabarani na bango uwatetee wananchi na uzungumzie hali yao ngumu ya maisha, usikalishe tu makalio chini kusubiria wengine kama hii nchi ni yao peke yao.
Kinachoendelea ni wanasiasa kuungana kuwakandamiza wananchi.

Tukatae huu usanii unaoendelea maana sisi ndio tunaopoteza zaidi.

Kwani hakuna wa kuzungumzia hali ngumu za wananchi katika mazingira haya ambayo wote ni kitu kimoja.
 
Kinachoendelea ni wanasiasa kuungana kuwakandamiza wananchi.

Tukatae huu usanii unaoendelea maana sisi ndio tunaopoteza zaidi.

Kwani hakuna wa kuzungumzia hali ngumu za wananchi katika mazingira haya ambayo wote ni kitu kimoja.
Mbona unalalama humu? Kama umeona haki yako inaminywa push back, usitegemee upiganiwe wakati wewe umejificha na I'd fake hizi na elewa wewe sio msemaji wa Watanzania! Usinisemee mimi because mimi ninajipigania haki yangu bila kutegemea watu wengine wanipiganie.
 
Sijui kwanini unataka tuige wazungu wanachofanya kwenye kila jambo, hebu tuambie, umewahi kuona wapi kule uzunguni Democrats wakiongoza nchi wawanyime Republican haki yao ya kufanya mikutano ya siasa?

Mazingira yetu na wazungu hayafanani kabisa, hasa kisheria, hivyo hukutakiwa hata kidogo mambo yetu ya ndani kujaribu kuyalinganisha na wale walioendelea kidemokrasia, sisi hatuna demokrasia kama yao.

Pia bado nashangaa, kwanini Chadema kuanza kupokea ruzuku kumegeuzwa kuwa "kujitengenezea" ulaji, naona wengi wenu mlitaka maridhiano yaguse mengine yote kama kuruhusu mikutano ya siasa lakini sio Chadema kupokea ruzuku.

Hebu jiulizeni; kwani hiyo ruzuku ni haki ya Chadema kisheria, au wamepewa kama zawadi kutokana na maridhiano?

Kama jibu lenu likiwa ni haki yao kisheria, basi sioni sababu ya kuwepo haya malalamiko yenu, lakini kama mnaona wamepewa kama zawadi, basi ni haki yenu kuendelea kulalamikia asali.

Walichokifanya Chadema, walikuwa na msimamo tu wakupinga matokeo ya uchaguzi, lakini msimamo huo haukuwepo kisheria, sheria inawataka Chadema wachukue ruzuku wanayostahili, sasa kama mazungumzo yamewafanya kubadili msimamo wao wa mwanzo sioni kosa lao, kwasababu hawajavunja sheria yoyote.
 
kuitwa pumbavu sio kosa, ndivyo ulivyo maisha yako kulalama humu JF ili Zitto, Lema, Mbowe, etc etc wakupiganie wewe wakati unaogopa kivuli chako ni upumbavu wa hali ya juu. Binafsi always nina push back, na push back ya 1995 wakati nina elimu yangu na nguvu ya ujana ilimfanya Nyerere arudi kwenye siasa baada ya kung'atuka siasa
 
kuitwa pumbavu sio kosa ,ndivyo ulivyo maisha yako kulalama humu JF ili zitto, lema,mbowe, etc etc wakupiganie wewe wakati unaogopa kivuli chako, upumbavu wa hali ya juu, binafsi always Nina push back ,na push back ya 1995 wakati Nina elimu yangu na nguvu ya ujana ilimfanya nyerere arudi kwenye siasa baada ya kung'atuka siasa
Aliyemrudisha Nyerere kwenye siasa ni Mrema na ameshaondoka.
 
Kinachoendelea ni wanasiasa kuungana kuwakandamiza wananchi.

Tukatae huu usanii unaoendelea maana sisi ndio tunaopoteza zaidi.

Kwani hakuna wa kuzungumzia hali ngumu za wananchi katika mazingira haya ambayo wote ni kitu kimoja.
Wewe umezuiwa na nani kuzungumzia hali ngumu za maisha ya watu? Wakati chadema wanafanyiwa Kila aina ya uhuni na ukatili ulikuwa wapi hadi ukashindwa kukemea? Tatizo lenu nyie chipukizi wa ccm hamjui hata mnachohitaji zaidi ya kuwaza matumbo yenu tu.
 
Maridhiano haya ni ubunifu wa CHADEMA na CCM ndio mtekelezaji.. Wengi wana wasiwasi kama huu wako, lakini CHADEMA ni chama chenye think tank kubwa sana na wasomi wenye weledi na maono ya kutosha sana

Kwa hatua hii ya kwanza tayari CHADEMA imeshatia mguu mmoja ndani ama kimjinimjini imeshaingiza kichwa ni hatua moja kubwa sana kwakuwa sasa CHADEMA itafanya siasa zake kwa uhuru bila woga wa kukamatwa. Kutekwa, kubambikiwa kesi. Kujeruhiwa na kudhulumiwa haki zake nyingi za msingi

Hatua ya pili na ya tatu zinakuja na mpaka 2025 CHADEMA itakuwa imeshamaliza kazi
Kuna vimatukio vidogo vidogo vinajengewa hoja nyepesi lakini CHADEMA haishughuliki navyo kwakuwa ilaeweza vipo kwa ajili ya kuwatoa kwenye reli na pia vinaletwa na wale wote waliovhukizwa na haya maridhiano
Ingekua rahisi hivyo, CUF na NCCR wangeshafanikiwa
 
Sijui kwanini unataka tuige wazungu wanachofanya kwenye kila jambo, hebu tuambie, umewahi kuona wapi kule uzunguni Democrats wakiongoza nchi wawanyime Republican haki yao ya kufanya mikutano ya siasa?

Mazingira yetu na wazungu hayafanani kabisa, hasa kisheria, hivyo hukutakiwa hata kidogo mambo yetu ya ndani kujaribu kuyalinganisha na wale walioendelea kidemokrasia, sisi hatuna demokrasia kama yao.

Pia bado nashangaa, kwanini Chadema kuanza kupokea ruzuku kumegeuzwa kuwa "kujitengenezea" ulaji, naona wengi wenu mlitaka maridhiano yaguse mengine yote kama kuruhusu mikutano ya siasa lakini sio Chadema kupokea ruzuku.

Hebu jiulizeni; kwani hiyo ruzuku ni haki ya Chadema kisheria, au wamepewa kama zawadi kutokana na maridhiano?

Kama jibu lenu likiwa ni haki yao kisheria, basi sioni sababu ya kuwepo haya malalamiko yenu, lakini kama mnaona wamepewa kama zawadi, basi ni haki yenu kuendelea kulalamika.

Walichokifanya Chadema, walikuwa na msimamo tu wakupinga matokeo ya uchaguzi, lakini msimamo huo haukuwepo kisheria, sheria inawataka Chadema wachukue ruzuku wanayostahili, sasa kama mazungumzo yamewafanya kubadili msimamo wao wa mwanzo sioni kosa lao, kwasababu hawajavunja sheria yoyote.
Unajichanganya sana mkuu, katika andiko lako hili, ambalo umetumia "kisheria", sijui mara ngapi katika andiko fupi kama hili.

Ni "sheria" ipi iliyohalalisha uchaguzi na matokeo ya uchaguzi uliofanyika?

Lakini ngoja nirudi mwanzo wa andiko lako.
Unaniuliza "kwa nini ninataka tuige wazungu...", kwani ni mambo mangapi tunawaiga hao wazungu, hili kweli linaweza kuwa swali la kumuuliza mtu ajibu?
Kwa kuwa unaonekana kupenda sana mambo ya "sheria", nikuulize wewe, kwa nini CCM isifuate sheria, kama hao Democrats wanavyofuata sheria kwa kutowanyima haki zao wapinzani?

Kwa hiyo, unaposema "...mazingira yetu hayafanani...", maana yake sisi hatupashwi kufuata sheria tunazoiga kutoka kwa hao wazungu? Tumetunga sheria zetu wenyewe hapa, lakini hatuzifuati hizo sheria, sasa unadai ni mazingira yetu ndiyo yanayotufanya tukaidi kuzifuata?

Hata upende ku'spin' vipi kuhusu maamuzi ya CHADEMA wakati huu, haiwezekani kamwe kuondoa msukumo wa manufaa kwao katika kuingizwa kwao kwenye chaka nene hili waliloingizwa na Samia, kwa ufundi mkubwa sana wa Kinana, na pengine Kikwete.
 
Back
Top Bottom