Marufuku Mtanzania kujiunga Jeshi la nchi nyingine

Marufuku Mtanzania kujiunga Jeshi la nchi nyingine

Mbona sijawahi kuona wakikataza au kukemea yale matangazo ya barozi ya marekani wanatoaga kukaribisha vijana wanaotaka kujiunga na jeshi la Marekani kwa mkataba?
Kama utajari naomba link ya hayo matangazo mkuu
 
Wazalisje ajira za ndani, nipo kwenye mchakato wa kujiunga Wagner PMC
Bora wangekaa kimya tu yaani kwa press hii ni kama wamewatangaza hao wagner, jamaa wakija bongo kuchukua vijana watawapata wengi sana. Vijana tulivyopigika mtaani alafu tukatae fursa because of the so called kuvunja sheria.! as if hao wanaotupika mkwala mbuzi izo sheria wao wanazifata.
 
Kwa kujiunga kwao Hawakani Uraia wa Nchi yetu.

Kile kikundi ni kama vile mfano wa Knight supports tu ile Kampuni ya Ulinzi.

Hivyo Wanaojiunga hawalazimiki Kuwa Raia wa Nchi Ya Urusi.
Knight support na hao warusi ni vitu viwili tofauti.Knight support hawavuki mipaka kupigana vita kwa niaba ya Nchi yoyote.
 
Tax apiga marufuku kwa watazania kujiunga na la Jeshi la nchi nyengine. Alisema kwa mujibu wa sheria zao Mtanzania yoyote haruhusiwi kujiunga na Jeshi la nchi yoyote isipokuwa Jeshi la Tanzaia tu na kufanya hivyo kuvunja sheria za nchi.

---

SERIKALI: ‘Fuateni sheria na taratibu mkiwa nje ya nchi’

View attachment 2495178


Serikali imewataka Watanzania kuzingatia na kufuata sheria, kanuni na taratibu za nchi walizopo ili kulinda taswira nzuri ya nchi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Stergomena Tax kuhusu kifo cha Nemes Tarimo, Mtanzania aliyefariki dunia nchini Urusi, alisema:

“Nitoe rai kwa Watanzania kuhakikisha wanazingatia sheria kanuni na taratibu za nchi walizopo, na pia wawe mabalozi wazuri wa kulinda taswira ya Tanzania.

Ikumbukwe kwa mujibu wa sheria zetu, Mtanzania yeyote haruhusiwi kujiunga na jeshi la nchi yoyote isipokuwa Jeshi la Tanzania na kufanya hivyo ni kuvunja sheria,” amesema Waziri huyo.

Amesema Mtanzania huyo alikwenda nchini Urusi mwaka 2020 kwa lengo la kujiunga na Chuo Kikuu cha Moscow Technological University (MIREA) kwa masomo ya Shahada ya Uzamili katika fani ya Business Informatics.

Ameongeza kuwa Mwezi Machi 2022, Mtanzania huyo alitiwa hatiani kwa kuhusika na vitendo vya uhalifu na kwa mujibu wa sheria za Urusi alihukumiwa kifungo cha miaka saba jela.

Waziri Tax ameongeza kuwa Tarimo akiwa gerezani alijiunga na kikundi cha kijeshi cha Urusi cha Wagner kwa ahadi ya kulipwa fedha na kuachiwa huru, baada ya kumaliza muda wa kutumika vita na alifikwa na umauti akiwa nchini humo.

Waziri Tax amesema kuwa mwili wa marehemu umeondoka nchini Urusi leo Januari 24, 2023 na unatarajiwa kuwasili nchini muda wowote kuanzia sasa na kuongeza kuwa Serikali imekuwa ikiwasiliana na Serikali ya Urusi, ili kuhakikisha mwili wa marehemu Tarimo unarejeshwa nchini na kukabidhiwa kwa familia yake kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Waziri ametoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa na Watanzania kwa msiba huo.

Waziri Tax amewauhakikishia umma na Diaspora wa Kitanzania wakiwemo wanafunzi walioko masomoni duniani kote kuwa serikali itaendelea kuwapa ushirikiano wakati
Jeshi la Marekani lina Watanzania kibao ambao pia wamepigana vita nje ya Marekani.
 
Tax anasahau kwamba Tanzania imekuwa hadi na viongozi waandamizi ambao ni wanajeshi wa nchi nyingine, huku wengine wakiwa ni wanachama watiifu wa magenge ya umafia na uhalifu yanayoitesa dunia.

Afrika inatia sana huruma....
 
Si lazima kuikana uraia , Marekani mtu ukiwa permanent citizen Tu unaweza ingia jeshini na kufanya kazi na bila hata ya kubadilisha uraia ,raia wengi tu watz ni wanajeshi wa US army ,marine NK , huyo maza ni mpuuzi kama wapuuzi wengine .
Waropokaji wa ccm ni vichwa maji
Ya uhamiaji na makazi. Kama uko interested na majeshi ya nchi zingine, ukane uraia wa tz kisheria then chukua uraia wa nchi husika ambapo utataka kujiunga na jeshi hilo
 
Tax apiga marufuku kwa watazania kujiunga na la Jeshi la nchi nyengine. Alisema kwa mujibu wa sheria zao Mtanzania yoyote haruhusiwi kujiunga na Jeshi la nchi yoyote isipokuwa Jeshi la Tanzaia tu na kufanya hivyo kuvunja sheria za nchi...
Hivi kiukweli kijana anawekwa jela huku na kuambiwa tunakuachia lakini ukapigane kwenye vita atachagua lipi? Na inawezekana kalazimishwa. Badala ya kufanya kazi viongozi wetu wanaweka lawama kwa vijana ambao hata hatujui wameingiaje jela huko Russia
 
Mi namjua mmoja yupo France legion
Huyu Mama nadhani kakurupuka
Yeah ! hata France pia Wana kikosi cha kijeshi cha wapiganaji kinachojumuisha wapiganaji raia toka nchi nyingine ,na masharti ni rahisi ni wewe kuingia tu pale France na kuingia headquarters kuenlist then unaingia kufanya test , au mtihani wa kupima utimamu wa mwili then mnaingia bootcamp ,Ila bootcamp lake si la kitoto ,kama wewe ni mlenda mlenda au urojo lazima uikimbie au wakuteme ,so hiyo kuingia jeshini na uraia wa nchi nyingine kwa wenzetu ni kawaida kabisa
 
Knight support na hao warusi ni vitu viwili tofauti.Knight support hawavuki mipaka kupigana vita kwa niaba ya Nchi yoyote.
Ni vitu viwili tofauti lakini ni Muktadha Sawa kwamba yote ni kama makampuni ya Ulinzi ila Moja inashiriki Vita Kwa ajili ya Nchi yake.
 
HAYA KUMEKUCHA SASA, VITUKO VIMEINGIA KIMATAIFA. NIKAJUA HIVI VIJAMAA VITAIKEMEA URUSI. Naona hata haya kulijadili hili taifa huku International Forums!...!
-----------------------------
Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema kwa mujibu wa sheria za nchi, Mtanzania yeyote haruhusiwi kujiunga na jeshi lolote la nchi nyingine kwani ni kosa kisheria.

Ameyasema hayo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax wakati akitoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari kuhusu kifo cha Mtanzania Nemes Tarimo aliyeuawa wakati akishiriki vita nchini Ukraine.

“Nikumbushe kuwa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, Mtanzania yeyote haruhusiwi kujiunga na jeshi lolote la nchi nyingine, ukifanya hivyo ni kuvunja sheria na taratibu za nchi yako. Unaruhusiwa tu kuandikishwa na jeshi la nchi yetu kwa taratibu zilizowekwa, katiba ziko wazi kwamba Mtanzania hawezi kutumikia jeshi la nchi nyingine,

Aidha, amesema Wizara imeendelea kuwasiliana na Serikali ya Urusi kuhakikisha mwili wa Mtanzania Nemes unafikishwa nchini na kukabidhiwa kwa familia yake, na kwamba mwili huo umeondoka nchini Urusi asubuhi Januari 24, 2023 hivyo unategemewa kuwasili nchini wakati wowote.

Hata hivyo, Dkt. Stergomena ametoa rai kwa Watanzania wote walioko nje ya nchi na ndani kuwa wana wajibu wa kutimiza matakwa ya kisheria ya nchi bila kujali mahali walipo.
 
Back
Top Bottom