Mkuu
BANDOKITITA , mtu ukiwa hujui na unajua kuwa hujui, wewe ni mjinga, ukielimishwa, unaelimishika, unajua ujinga unakutoka unakuwa mwerevu.
Mtu ukiwa hujui na hujui kuwa hujui, bali unajidhania unajua, wewe ni mpumba.., hata ukifundishwa hufundishiki!.
Mimi ni mwalimu humu kazi yangu kufundisha. Kabla ya kuungana tulikuwa na nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.
Baada ya kuungana tumekuwa na nchi moja ya Tanzania, yenye sehemu mbili, Tanzania Bara, iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Ni Tanganyika ndio ililifuta jina lake na kutumia Tanzania Bara, lakini Zanzibar iliendelea kutumia jina lake la Zanzibar.
P