Mimi ni Muslim.. Kuna siku Yule sheikh sharifu majini. Alikuwa na mkutano pale diamond Jubilee. Nikaenda.
Mambo yakaanza. Akaanza kuita majiniiiii majiniiiii. Mara wamama wakaanza kuanguka ovyo ovyo. Hakuna mwanaume hata mmoja aliyeanguka. Akajipaka mafuta mkononi akawa anawasukumiza kwa kiganja cha mkono usoni.
Mimi nikashtuka.
Wale wanaoanguka hawaanguki kwa nguvu ya mafuta. Kuna mawili. Moja wameandaliwa au wanasukumizwa.
Sasa wengine wanakuwa wagonjwa kweli. Ukimsukumiza tu chali.
Wengine sio wagonjwa. Unamsukumiza MTU kasimama tu.
Kwa nini usipigwe mtama?
Hawana lolote ni usanii tu, waangukaji wengi ni Wanawake, ikitokea dume basi ujue limejiendekeza tu.
Wanawake wana matatizo sana, wewe leo kusanya Wanawake pale Diamond jubelee, mtafute Manifongo, mpe "mboga" za kutosha (zikitokea Arusha itapendeza zaidi), avurumishe singeli la nguvu hapo, utashuhudia nusu kama sio wote ya Wanawake hapo watavua nguo wakisingizia kupandwa na mzuka.
Ni hisia zao tu wanaziendekeza na kuambukizana, hata wale Watoto wa kike wa shule wanaoangukaga hovyo na kusingizia mapepo sijui, hamna lolote...huenda mwenye tatizo ni mmoja hao wengine wanajipagawisha tu.
Mtoto ukishampa mastori ya mapepo utegemee tu hayo matatizo, na ukimlea bila asijue hayo mambo wala hatosikia hizo ishu.
Hakuna cha Mchungaji, sijui nabii wala hao wanaojiita mashehe majini, ni watumia fursa tu ya ujinga wa wenzao na wao kujineemesha.