Masheik mahubiri ya maadili yasiishie kwenye ushoga, jumuisha HAKI, WIZI WA MALI ZAUMMA- REPORT ZA CAG, siasa safi, uongozi bora na mambo kama hayo

Masheik mahubiri ya maadili yasiishie kwenye ushoga, jumuisha HAKI, WIZI WA MALI ZAUMMA- REPORT ZA CAG, siasa safi, uongozi bora na mambo kama hayo

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
44,629
Reaction score
83,056
Mahubiri yenu yanaikumbatia serikali. Hubirini HAKI, wizi wa mali za Umma , uuzwaji wa rasilimali za nchi, MaDc, RC, kuwaonea watu , report za CAG na vitu kama hivyo. Maadili si ushoga/ubakaji tu.
Hubiri na kusema uongo si maadili ( Magufuli yuko ofisini anachapa kazi, kumbe yuko mortuary).

Hubirini kuhusu kupotea ka watu na kufa mikononi mwa polisi na mambo kma hayo!
 
Viongozi wa dini walikua zamani

Sasa hivi wengi wao wanaangalia pesa tu
Viongozi wa dini wanawathamini waumini wenye pesa kuliko wanyonge sembuse kuwathamini viongozi mafisadi kuliko wananchi!!

Dunia ya sasa hivi wanaojitoa akili, wanafki ndio wenye furaha na wanafanikiwa zaidi ya wenye utimamu wa akili na wasema kweli..!
 
Ney wamitego anawazidi viongozi wa dini kwa kukemea maovu
 
Unapoteza muda na bando. Wahubiri iliyo kweli wanyimwe ziara za ikulu weeeeeh. 😂️😂️😂️😂️😂️😂️
 
BAKWATA, UWT, UVCCM, WAZAZI,KKKT NI KITU KIMOJA.
Maneno yako ungeyaelekeza kwa SHURA YA MAIMAM. Huko ndio kwenye watu wanaoweza kuchambua Mambo.
 
Mahubiri yenu yanaikumbatia serikali. Hubirini HAKI, wizi wa mali za Umma , uuzwaji wa rasilimali za nchi, MaDc, RC, kuwaonea watu , report za CAG na vitu kama hivyo. Maadili si ushoga/ubakaji tu.
Hubiri na kusema uongo si maadili ( Magufuli yuko ofisini anachapa kazi, kumbe yuko mortuary).

Hubirini kuhusu kupotea ka watu na kufa mikononi mwa polisi na mambo kma hayo!
Hakika
 
Viongozi wa dini walikua zamani

Sasa hivi wengi wao wanaangalia pesa tu
Viongozi wa dini wanawathamini waumini wenye pesa kuliko wanyonge sembuse kuwathamini viongozi mafisadi kuliko wananchi!!

Dunia ya sasa hivi wanaojitoa akili, wanafki ndio wenye furaha na wanafanikiwa zaidi ya wenye utimamu wa akili na wasema kweli..!
Mtoto punguza uropokaji mitandaoni una uhakika na unachokisema kwa uthibitisho upi?
 
Nilisema makala humu inasema Mtume Mohammed alipewa Mafunzo pangoni kwa udhamini wa Bibi Hadija ndio Quran ikazaliwa

Ndio maana kwenye mafundisho anasema kwa msisitizo kiumbe ambae hajaguswa na Shetani ni Yesu pekee yaan Nabii Issa Bin Maryam Ila wengine wote na yeye akiwemo Pindi anazaliwa Shetani alimgusa

Ni masuala ya intelligence ya Dini zaidi
 
Tatizo ni wachumia tumbo, kumhofu allah hakumo ndani mwao, na sasa wanataman wawe kama mapadre na maparoko ili nao wasipande bodaboda.

Hakika pepo ni ngumu. Mola pekee atunusuru na kundi hili la wanafiq
 
Tatizo ni wachumia tumbo, kumhofu allah hakumo ndani mwao, na sasa wanataman wawe kama mapadre na maparoko ili nao wasipande bodaboda.

Hakika pepo ni ngumu. Mola pekee atunusuru na kundi hili la wanafiq
Wewe hupendi kupanda Gari unapenda uzulule na Bajaj huna hata Baiskeli unasemaje?
 
Wewe hupendi kupanda Gari unapenda uzulule na Bajaj huna hata Baiskeli unasemaje?
Kumtangaza allah na rehma zake yapaswa kuwa kipaumbele cha kila mja mwema. Mengine ni sunna na mswalie mtume.
 
Ni vigumu kuwaona wakiongelea baadhi ya mambo kwa sababu wengi wao walijikita zaidi kwenye elimu ya madrasa wakasahau Elimu ya darasani na kuna mambo kuyajadili lazima shule iwe ya uhakika sio ya kutoa ujinga tuu
 
Back
Top Bottom