Kama Alihusika Moja Kwa Moja Mauaji Ya Hao Watu Na Yeye Atauwawa Ni Swala La Muda Tu.Hata wewe Jua Jambo Hilo Leo.Heri bongo miaka kumi halafu DPP anasusa unaanza moja.
Kenyatta alikuwa anamalizana na masheikh watuhumiwa wa ugaidi nje ya mfumo.eg Rogo, Makuburi.
Kuna sheria hiyo ?? SidhaniiiWalipwe fidia
Angusha nondo kidogoUlatule mitaa ya kivule ccm walitesa na kuua nikiwa kwenye 15yrs walikua wanaogopeka. Tuhuma si za uongo
Wakijifanya kukaza watarudi Tena na safar hii hawatatoka.Wamepewa second chance waache ugaidi
Ulikuwa na umri gani wakati wanakamatwa!!? Hao ni magaidi kweli kweli walikuwa tayari wamesajiriwa na Alshabab pia kwa muda walijaribu kufanya mipango ya kuwatoa gerezani kwa njia za kigadi lakini walishindwa wengi walifyekerewa mbali huko Rufiji acha kucheza na usalama wa TZ utakufa vibaya sana.Hao muamsho issue yao ilikuwa kisiasa zaidi na wala sio udini.
Kuna watu wale walisombwa tu hawajui a wala ba. Na wengi walikuwa wapemba na ni Wafuasi wa CUF kwa kipindi kile kabla CUF kusambaratika na wengi kujiunga na ACT
Walikuwa recruited hao na ni hatari sana hao wenye umri mdogo kwenye maswala ya kigaidi kwa kuwa ni rahisi sana kuwa brainwashed vijana wadogo.Kuna hao wawili
Mmoja miaka 34 na mwenzie miaka 29
Naona waliingia wakiwa bado vijana wadogo saaana,inasikitisha aisee
Huo uhalifu wao umeuthibitisha wapi?Wahalifu yamerudishwa mtaani, siku sio nyingi tutaanza kuona matukio ya uvunjifu wa amani, ukicheka na wahalifu utavuna mabua.
Yaani mtu akae miaka 10 mahabusu pasi na kuhukumiwa na amekamatwa kihalali,vipi asihukumiwe?Sidhan kwamba walikamatwa kimakosa mpaka kuwa mahabusu hapo wametolewa kwa huruma tuu
Hawana hatia? Unajuaje ! Kama wametubia huko! Mbona hukukamatwa wewe lakini wakafuatwa wale?Duh miaka 10 unasota gerezani tena bila hatia
Hii nchi inapitia kipindi kigumu Sana
Je ugaidi upo ama haupo?Pia kuna wajinga wenye dhamana, wakiona tu mtu anandevu wanajua ni gaidi, ujinga wa hali ya juu.
Kuna watuhumiwa wawili wamekufa wakiwa Gerezani na kesi iliyowahusu umefutwa, Je serikali inawajibika vipi kwa hili?Hizi power za DPP kuamua kumpeleka Mtu Mahakamani na Kisha kuamua tena kutoendelea na shitaka wakati Mtu Huyo kasota rumande miaka kibao, linapaswa kuangaliwa upya.
Hii mamlaka ya DPP Haina tofauti na kumpa Mtu mmoja madaraka ya kukamata, kuhukumu, na kuachia mtuhumiwa.
Or else watuhumiwa wanaotumia kama Hawa kwa kukaa rumande muda mrefu, ilihali wanaathirika kisaikolojia na kiuchumi, Walipwe fidia na dola.
Na mimi najiuliza na kiukweli natamani kujua ni watu wa wapi na pia kuna jambo gani walikutwa nalo mpaka wasombwe famiia nzima mpaka babu wa miaka 99 mwenye nondo zaidi tafadhali kwa maslahi ya jukwaa atumegee kidogo hawa ulatule ni kina nani?Hiyo familia ya Ulatule ilikuwaje wote wakajikuta 'mahabusu,' ?
Sio kidogo wamekoma haswaaa nna uhakika sio rahisi mtu tu aionee familia nzima lazima lipo jambo nyuma ya paziaNakupa siri usimwambie mtu, wale mabwana kweli kabisa bila wasi wasi walikua mafia na mipango yao ilikua mibaya sana sema si unajua tena mambo flani flani ila nna uhakika asilimia elfu nane WAMEKOMA.