hamis77
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 13,628
- 20,992
Unajua waliyoyafanya Hadi kuwepo hapoKuna hao wawili
Mmoja miaka 34 na mwenzie miaka 29
Naona waliingia wakiwa bado vijana wadogo saaana,inasikitisha aisee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unajua waliyoyafanya Hadi kuwepo hapoKuna hao wawili
Mmoja miaka 34 na mwenzie miaka 29
Naona waliingia wakiwa bado vijana wadogo saaana,inasikitisha aisee
acha upuuziTakbir, hakuna la kumshinda ALLAH S.W.
Watu wanashindwa kufatilia nini kilitokea Hadi wamefika hapo, Tena walikamatwa na Serikali ,Rais akiwa muislamuWatu wanawatetea tu ila hao jamaa walistahiki kupotelea hukohuko na ole wao wajifanye kama wanajikuna
ishu sio CCM, ishu ni ugaidi..kauli sahihi ni wameonewa na serikali ya Ccm.
..kuna Mashekhe walikamatwa wakati Raisi, na Igp, wakiwa Waislamu.
..wakati wa kampeni, mwanasiasa pekee aliyepanda jukwaani na kuwatetea Mashekhe wa Ansar Sunna alikuwa Tundu Lissu.
..pia Mheshimiwa Bwege alipokuwa mbunge aliwahi kuwasemea Waislamu waliopotezwa mikoa ya kusini.
..Tuiondoe CCM ili haki itawale ktk nchi yetu.
je kama walishiriki kwa namna moja au nyingine ku facilitate hayo magaidi wataachwaje kukamatwa?..hivi ugaidi unaweza kupangwa na familia nzima, mpaka wanawake?
Yaani hakuna nchi inayo endeshwa kihuni kama Tanzania chini ya ccm. Mtu unapotezea miaka 12 ya maisha yake halafu baada ya miaka 12 ya mateso unamwambia nenda nyumbani? Bila hata mjadala ! Hii sio sawa siku watanzania watakapo choke huu uhuni Tanzania itakuwa kama Samalia.Shura ya Maimamu Tanzania
KUTOKA MAHAKAMA KUU LEO TAREHE 4/3/2025
MASHEIKH 12, WATOKA GEREZANI. WATANO NI FAMILIA MOJA YA ULATULE.
MASHEIKH 12, walio kaa gerezani miaka 10, (2015-2025), kwa tuhuma za Ugaidi wameachiwa huru leo. Uamuzi huo umetolewa na Jaji wa Mahakama Kuu Mheshimiwa Kirekiano.
Kabla ya hukumu hiyo Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP, aliambia Mahakama upande wa Jamhuri hauna haja ya kuendelea tena na shauri hilo.
Akitoa uamuzi huo mheshimiwa jaji amesema amekubali ombi hilo la Mwendesha Mashtaka wa serikali.
Kwa muda mrefu Shura ya Maimamu Tanzania imekua ikimuomba Mkurugenzi wa Mashtaka DPP kulifuta shauri hilo kwa sababu za upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha tuhuma dhidi ya Masheikh hao.
Walioachiwa huru ni:
1. Ali Mohammed Ulatule (70).
2. Khamisi Mohammed Ulatule (61).
3. Nassoro Suleiman Ulatule (41),
4. Rajab Ali Mohammed Ulatule (34).
5. Na Ramadhani Khamisi Mohammed Ulatule (29).
Wengine ni:
6. Saidi Abdallah Chambeta.
7. Fadhili Shaabani Lukwembe.
8. Mnemo Qassim Mwatumbo.
9. Abdallah Bushiri kalukula.
10. Khamisi Ally Masamba.
11. Omari Abdallah Makota.
12. Na Mohammed Hassan Ungando.
Katika kundi la Masheikh walioachiwa leo, 5, ni wa familia moja ya Ulatule. Wao walikamatwa familia moja watu 16, na baada ya masiku kadhaa (ya kutofahamika walipo), hatimaye 7, walikutwa katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam baada ya kufikishwa Mahakamani na kusomewa shtaka la ugaidi.
Aidha wenzao 9, hawajulikani walipo mpaka leo. Kati ya 7, waliokua gerezani 2, Sheikh Suleima Mohammed Ulatule (99), na Sheikh Saidi Mohammed Ulatule (79), wamefariki dunia wakiwa gerezani.
Kufuatia kuachiwa kwa masheikh hao 12, idadi ya mahabusu wenzao waliobaki katika gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam ni 39.
Shura ya Maimamu Tanzania inawashukuru wale wote wanaoshiriki ipasavyo harakati za kutetea haki za binadamu.
=======================
JamiiForums imewasiliana na Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda kuhusu maamuzi hayo ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar, amesema
“Tunaendelea kuwasiliana na DPP kuhusu wale 39 waliosalia ndani, tumefanya hivyo kwa njia ya maandishi na hata Watuhumiwa wamekuwa wakiwasilisha maombi yao ya kutaka kesi ifutwe pia,
Ni mashauri ya muda mrefu n ahata hoja zinazotolewa hazina mashiko, zinakuwa nyepesi sana, mfano unakuta inaweza kupangwa mashahidi 70 watoe Ushahidi ndani ya wiki mbili lakini wanaotoa ushahidi unakuta ni wawili tu, hivyo inafanya kesi kwenda mwaka mzima bila kuwa na mwendelezo unaoeleweka.”
akili za kigaidi hiziYaani hakuna nchi inayo endeshwa kihuni kama Tanzania chini ya ccm. Mtu unapotezea miaka 12 ya maisha yake halafu baada ya miaka 12 ya mateso unamwambia nenda nyumbani? Bila hata mjadala ! Hii sio sawa siku watanzania watakapo choke huu uhuni Tanzania itakuwa kama Samalia.
Halafu wakishakamatwa kinachofuata nini, kufungwa bila mashtaka na kuuliwa?je kama walishiriki kwa namna moja au nyingine ku facilitate hayo magaidi wataachwaje kukamatwa?
je kama walishiriki kwa namna moja au nyingine ku facilitate hayo magaidi wataachwaje kukamatwa?
kuwekwa ndani mpaka akili zao zikae sawa ndio waachiweHalafu wakishakamatwa kibachofuata nini, kuuliwa na kufungwa bila mashtaka ?
Hapo kuna chuki binafsiHiyo familia ya Ulatule ilikuwaje wote wakajikuta 'mahabusu,' ?
Wapinzani.Hiyo familia ya Ulatule ilikuwaje wote wakajikuta 'mahabusu,' ?
Sema Nini Kuna mstari mwembamba sana unao tofautisha mwisilamu safi na gaidi ndo maana unakuta wakiona tu jamaa anandevu nyingi wanajua gaidiPia kuna wajinga wenye dhamana, wakiona tu mtu anandevu wanajua ni gaidi, ujinga wa hali ya juu.
adhabu ya kukaa ndani waliyoipata imetosha, wameachiwa waachane na harakati za kidini kuteteresha amani na usalama wa raia..kama walishiriki ktk jinai yoyote ile basi walipaswa kushitakiwa na kuhukumiwa.
.
sababu ya kukamatwa kwao ni ugaidi. Swali hili jibu lake ni mukhtadha wa kukamatwa kwaoHalafu wakishakamatwa kinachofuata nini, kufungwa bila mashtaka na kuuliwa?
16 walikatwa kwenye famulia moja, 7 wakaletwa mahakamani, 9 hawakuletwa.
Unadhani hawa 9 walifanywaje ?
Kwa hiyo Kikwete ali sign death warrant tisa. On paper wanasema wa mwisho kunyonga ni Mwinyi. Na hawa 9 je, walisamehewa na Kikwete wakapaa mbinguni ?
Hawa ni wanaofuata sera za al-qaida, al-shabab, boko haram n.k. kiufupi ni watu hatari kwa amani ya nchi.Hiyo familia ya Ulatule ilikuwaje wote wakajikuta 'mahabusu,' ?
Ukigombana na DPP tu anakutia ndani wewe gaidi unapigwa mvua baada ya miaka 10 anakuja mwingine anakuachiaOr else watuhumiwa wanaotumia kama Hawa kwa kukaa rumande muda mrefu, ilihali wanaathirika kisaikolojia na kiuchumi, Walipwe fidia na dola.
hapa umepiga kwenye mshono,...Nakupa siri usimwambie mtu, wale mabwana kweli kabisa bila wasi wasi walikua mafia na mipango yao ilikua mibaya sana sema si unajua tena mambo flani flani ila nna uhakika asilimia elfu nane WAMEKOMA.