Pre GE2025 Mashekhe wafanya ibada na kuomba majini yasaidie Rais Samia kushinda kwenye uchaguzi ujao

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hawa ni ndugu zake mswaki mbuyu
Mtag tuu mgalatia mwenzio na ameusoma vzr tuu waraka wa Papa Francis humu..eti mwnyw kaweka video mbili moja ya shekhe mkuu na nyngn ya shekhe mganga wapo wengi sanaa na hawa mashekhe wangekua wagalatia wasingetofautiana na mwamposa uzushi kauleta mwnyw na akajijibu mwnyw..
 
Nikupe mfano wa Dream incubation, ambapo ni njia ya kuweza kupata muongozo au suluhisho la jambo kupitia ndoto. Kwenye uislamu hutambulika kama Istikhara ambapo utaratibu wake ni sala na dua.


Sasa dream incubation wengine utaratibu wao hutumia njia ndefu tena za shirki kama kuomba kupitia miungu ili kupata muongozo wa mambo yao kupitia ndoto, lakini zipo taratibu nyepesi tu za kupata muongozo wa jambo kupitia ndoto kwa njia tu ya kuuliza swali unalota kupata muongozo kabla ya kulala na ukapata ndoto yenye huo muongozo.


Ndio maana nasema tatizo lipo kwenye njia tu zinazotumika, mambo mengine ni shetani tu kutaka kuwapoteza watu ndio huwapitisha kwenye njia za ushirikina.
 
Kwa taarifa yako kwa maneno uliyoandika hapa Dua na muongozo wa istikhara aliyofundisha mtume huijui ila umechanganya hadithi za pauka pakawa na Dua ya istikhara.
Ile Dua ukijua maana yake tu utajua kuwa swala la kuoteshwa halipo.
Kanunue kitabu cha Dua maarufu
حصن المسلم ( Hisnul Muslim/ Kinga ya muislamu ) kipo ambacho kimetafsiriwa kiswahili .
Umishakipata tafuta Dua ya istikhaarah soma ile tafsiri ya kiswahili halafu tuone hayo mambo ya kuoteshwa nani kayafundisha.
 
We Bin Mwamedi namtagije Mgalatia mwenzangu wakati hayo mambo ya majini yanawahusu ninyi?
 

Abou Shaymaa
Njoo huku uone majini yanavyowasaidia waislam kufanikisha mambo.
Pia fafanua, maana ninyi katika imani yenu kuna majini mazuri. Wakati sisi wengine ukisema jini maana yake pepo mchafu. Malaika muovu, aliyemfuata shetani kumuasi Mungu
 
Kwenye uislamu hakuna mahala tulipofundishwa kutegemea ndoto katika kupata miongozo ya mambo tunayotaka kuyafanya.
Waweza kuwa na nia ya kufanya jambo jema shetani akakuletea ndoto inayoonyesha kuwa ni jambo baya au unataka kufanya jambo baya shetani akakuonyesha ni jambo jema! Alaa kulli Haal ! Hakuna mafundisho katika uislamu ya kutaka mtu ndoto zimuelekeze mambo ya kufanya Wala Dua na swala ya istikhaarah haisemi hivyo!
 
Point ni kupata muongozo hivyo kuoteshwa ni moja ya njia ya kupata huo muongozo na si kwamba ni lazima upate huo muongozo kwenye ndoto.
 
Hakuna niliposema waislamu kutegemea ndoto kupata miongozo.
 
Point ni kupata muongozo hivyo kuoteshwa ni moja ya njia ya kupata huo muongozo na si kwamba ni lazima upate huo muongozo kwenye ndoto.
Hiyo njia ya kuoteshwa ili kupata muongozo nani kaifundisha ?! Je wewe dua ya istikhaarah umeihifadhi kweli au umeshawahi kuitumia kulingana na maelekezo ya mtume صلى الله عليه وآله وسلم ؟
 
mashetnai yapigweeeeeeeeeeeeeee! majini yapigweeeeeeeeeee kwa Jina la Yesu. dini gani hiyo wanaomba pamoja na majini, ati wanataka majini yakamuombee samia.
 
Hii nchi sasa imefika kilele chake cha vituko. Muda utazungumza hakika bila shaka.
 
We Bin Mwamedi namtagije Mgalatia mwenzangu wakati hayo mambo ya majini yanawahusu ninyi?
Sisi majini tuyatambua ni viumbe kama viumbe wengine...weeh picha ya Brian Deacon si unaitambua kama ya Yesu au sivyo?
 
Hiyo njia ya kuoteshwa ili kupata muongozo nani kaifundisha ?! Je wewe dua ya istikhaarah umeihifadhi kweli au umeshawahi kuitumia kulingana na maelekezo ya mtume صلى الله عليه وآله وسلم ؟
Waja wema walikuwa wakifanya istikhara kabla ya kulala.
 
mashetnai yapigweeeeeeeeeeeeeee! majini yapigweeeeeeeeeee kwa Jina la Yesu. dini gani hiyo wanaomba pamoja na majini, ati wanataka majini yakamuombee samia.
Aliyekuaminisha majini ndio malaika waliyoasi ndio kakosea, sidhani kama kuna maandiko yenye kueleza kuwa majini ni malaika waliyoasi.
 
Kwa aina ya siasa na watu wa nchi hii, tusingeweza kumtoa mkoloni hata kama mda wake ungekuwa umefika. Chawacratic society.
 
Haya MAJINI huwa yanakimbia vita, Kule HAMA na HezBullah wanapigwa hata hayazuii mabomu, binafsi naamini MAJINI hayapo ni story za kutishana tu.

Majini hayaleti pesa BAKWATA mpaka tunawachangia kujenga misikiti?
 
Jambo zuri kumuombea kiongozi.
 
Waja wema walikuwa wakifanya istikhara kabla ya kulala.
Hao ni watu waliofahamu vibaya maana ya istikhara!
Istikhara aliyofundisha mtume صلى الله عليه وآله وسلم Haina muda maalumu.
Unaweza kuifanya asubuhi , mchana, jioni au usiku .!
Muda wowote, huyo anayesema wakati wa kulala saa nyingine ni katika hao wanaotegemea kuoteshwa! Hadithi ya istikhara nitaileta hapa muda si mrefu na kutoa maelezo yake inshaa Allaah.
 
Aliyekuaminisha majini ndio malaika waliyoasi ndio kakosea, sidhani kama kuna maandiko yenye kueleza kuwa majini ni malaika waliyoasi.
kwa hiyo majini kwako wewe ni masafi, matakatifu, ndio maana mnaswali nayo. ajabu sana. sasa mbona tukitamka JIna la Yesu yanakimbia hadi yanajisaidia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…