Mashindano ya kumtafuta bingwa wa draft Tanzania 2022

Mashindano ya kumtafuta bingwa wa draft Tanzania 2022

Cisco namksia ila personally simjui, ronaldo ana title kubwa huyu namjua

Aisee noel alipotea goli 5 kwa Cisco?
Cisco huyu hapa

Yupo tayari muda wowote kukichafua ,
 

Attachments

  • IMG-20220703-WA0008.jpg
    IMG-20220703-WA0008.jpg
    51.7 KB · Views: 57
EXCLUSIVE



Timu: Omary Kiwembe Vs Dogo Shukuru ( Confirmed )




Mdhamini : Mzee Java ( Raisi wa wakongwe wa madanali )




Zawadi: 70,000/= ( Winner 60k na looser 10k )




Lini: Alhamisi, tarehe 7 July 2022 Saa Tisa Kamili




Uwanja: kitunda stadium




Michezo: 24-Omary John + Tege 10 za mzee Ngapu



Mratibu: Masta Mtemi ( 5000)




Photograper:Masta mtemi( 5000 )




Kamisaa: Dogo Hansi (5000)




Note: Hakutakuwa na mshindi wa pili ila tutakuwa na nauli ya Shilingi elf 10 kwa atakaefungwa



Boss Java amefungua turbo vijana washindwe wao na Sasa Fundi Kiwembe anatembe kifua mbele,, Ikumbukwe tu Fundi Kiwembe alilala karibia miezi Sita bila ya kupata mechi njoo kitunda stadium
 
EXCLUSIVE



Timu: Omary Kiwembe Vs Generali Mboma ( Confirmed )




Mdhamini : Mzee Java ( Raisi wa wakongwe wa madanali )




Zawadi: 80,000/= ( Winner 70k na looser 10k )




Lini: Ijumaa, tarehe 8 July 2022 Saa Tisa Kamili




Uwanja: Mbagala Kizuiani




Michezo: 24-Omary John + Tege 10 za mzee Ngapu



Mratibu: Masta Mtemi ( 5000)




Photograper: Fidelisi( 5000 )




Kamisaa: Haji Nguya (5000)




Note: Hakutakuwa na mshindi wa pili ila tutakuwa na nauli ya Shilingi elf 10 kwa atakaefungwa



Boss Java amefungua turbo vijana washindwe wao na Sasa Fundi Kiwembe anatembe kifua mbele,, Ikumbukwe tu Fundi Kiwembe alilala karibia miezi Sita bila ya kupata mechi njoo Mbagala Kizuiani
 
EXCLUSIVE



Timu: Saiya Vs Mtanga ( Confirmed )




Mdhamini : Mzee Java ( Raisi wa wakongwe wa madanali )




Zawadi: 80,000/= ( Winner 70k na looser 10k )




Lini: Jumapili, tarehe 10 July 2022 Saa Nane kamili Mchana




Uwanja:Kitunda Stadium




Michezo: 24-Omary John + Tege 10 za mzee Ngapu



Mratibu: Masta Mtemi ( 5000)




Photograper: Masta Mtemi( 5000 )




Kamisaa: Riro (5000)




Note: Hakutakuwa na mshindi wa pili ila tutakuwa na nauli ya Shilingi elf 10 kwa atakaefungwa



Hii inaitwa mama Mkanye Mwanao Fundi Saiya anakwenda kukutana na Mtanga Uso kwa uso kama Semi trailer na kichwa cha treni Njoo mjini kitunda Stadium
 
EXCLUSIVE



Timu: Noeli Namaloe Vs Kiwembe




Mdhamini : Kamanda Issa ( Raisi wa watu huru )




Zawadi: 120,000/= ( Winner 100k na looser 20k )




Lini: Jumamosi tarehe 9 July 2022 Saa saba kamili mchana




Uwanja: Kinondoni Manyanya




Michezo: 24-Omary John + Tege kumi za Mzee Ngapu



Mratibu: Masta Mtemi




Photograper: Mkorea(5000)




Kamisaa: Beka ( 5000 )




Note: Hakutakuwa na mshindi wa pili ila tutakuwa na nauli ya Shilingi elf 20 kwa atakaefungwa na kama ngoma 24 zitaisha sare basi hawa jamaa watapewa elf 30 kila mmoja kama kifuta jasho
 
naomba nikusaidie hapa , wanaposema washiriki watapitishwa na mikoa yao wana maana hii, mfano Iringa wachezaji wazuri wa draft tunawajua , sasa ni sisi wanairinga kuamua kupendekeza ni nani akatuwakilisha baada ya kujadiliana kwenye club zetu au kuamua kuandaa mashindano ambayo yatawakilisha wachezaji wotee wa mkoa afu mshindi atashinda ticket ya kwenda kutuwakilsha Dar es salaam katika mashindano ya kitaifa.

Baadhi ya mikoa kutokuwepo kabisaa , hii inatokana na mikoa hiyo kutokuwa na clubs za mchezo wa draft na kupelekea ugumu fulani katika kuwasiliana na wahusika wa mkoa usika lkn pia baadhi ya mikoa kutokuwa na upenzi na huu mchezo au kutokucheza huu mchezo katika sheria pendekezwa hapo juu. Mwisho ni baadhi ya mikoa (katika historia ) kutoa wachezaji wenye uwezo mdogo mnoo .

Unajua huu mchezo haupo kama wengi wajuavyo . Hawa wenzetu wa dar wametuzidi pakubwa mno ktk huu mchezo, kuna kigezo hapo cha omary john 14 hivi hapo umekielewa hicho kigezo ?
- ngoja nikufahamishe ni hivi, wachezaji wengi wanajiona au wanaitwa mabingwa kwasababu ana namna fulani ya kucheza huu mchezo , lkn katika omary john kila mcheza anatakiwa aanze kete zote 7 za vyumba vya mwanzo yaani anatakiwa aanze

Pasati , nugza , meja , kavimba, taa ya treni , mabano na tege . sasa wachezaji wengi wa mikoani utakuta anajua meja lakini mabano hajua au tege hajui , sasa mikoa iliyotajwa kidogo wanaufahamu juu ya hiyo sheria ya omary- john
Kwanin wanaiita omary- john ni kama njia ya kuwaanzi wachezaji wa wili omary na john ambao walipenda kucheza katika utaratibu huo wa kuanza kete zote za mwanzo na kuzipa majina niliyotaja hapo juu.

- Katika mchezo unaoitwa tege . Kuna sheria imesema watacheza tege 4. kwanini wamesema tege na siyo meja , nugza au pasati ?
ni hivi tege ni mchezo unaotaka mchezaji aanze kete ambayo wachezaji wengi wanaamini ni kete dhaifu kama utaanza na kupelekea ufungwe kirahisi na mpinzani wako. Sasa kwasababu wengi wanajua hii itapelekea sare ziwe nyingi na kupelekea mashindano yawe marefu , hivyo kwa kupendekeza wacheze tege basi tunaweza kuokoa muda kwa kuepusha sare zisiwe nyingi.
umedadavua vizur omary john hahah
 
Sasa hilo ndio tunacheza sana Kanda ya ziwa .... Hayo madraft yenu mtu anapita nyuma yako kizembe SI tunakula kichwa ....inabidi uzame sana laboratory kupata majibu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] eti mtu anakatuza nyuma yako na huwezi mfanya kitu daah....
Daah..ilinipa muda sana kuja kulizoea hili draft la kwenda mbele tu.

Eti kete inapita nyuma yako unaiacha tu daah..

#MaendeleoHayanaChama
 
Wapo sahihi , tanzania tuna aina yetu ya mchezo ambayo inaitwa Tanzania draughts (sijui kama nimeandika vizuri ) .
-Hapa tunasheria zetu za namna ya kucheza ambazo kimsingi kwa namna fulani zinafanana na draughts za nchi nyingine kama vile American draughts /british draughts. Ila sasa sifa pekee ya Tanzania draughts ni kuwa king can make very long jumps, and can move back and forth . Wakatika american draughts /british draughts yenyewe inafanana kila kitu katika uanzaji wake na Tanzanian draughts lakini yenyewe king haiwezi kumake long jumps . Na kupelekea vitu kama force king kutokuwepo kirahisi ( wacheza wa draft wananielewa hapa nini nasema kama utacheza draft afu force king ziwe hazipo )

- sasa kwa upande wangu mimi nawapongeza sana waliondaa haya mashindano maana siyo tu wanaupromote huu mchezo wa draft Tanzania bali wanapromote kitu cha nyumbani ambacho dunia inatambua kuwa kwa sheria hizi na hizi zinachezwa Tanzania tu . Tofauti na french style of playing , ambayo kama tungeanzisha mashindano yake tunge promote kitu cha kigeni na siyo cha nyumbani.
Drafti ambalo king haimuvu kufuata kete iliyoko mbali haina tofauti na kibogoyo a aepambana kutafuna muhogo mbichi. Kunakuwa hakuna maana ya king sasa
 
Sasa hilo ndio tunacheza sana Kanda ya ziwa .... Hayo madraft yenu mtu anapita nyuma yako kizembe SI tunakula kichwa ....inabidi uzame sana laboratory kupata majibu 🤣🤣🤣🤣 eti mtu anakatuza nyuma yako na huwezi mfanya kitu daah....
Wacheze French Ili washiriki tuwe wengi ?
 
Aisee kuna mapambano makali sana naona round hii watu wameamua kuyaheshimisha hays mashindano kwa kuweka ligi nyingi zenye unafuu wa pesa tofauti na miaka ya nyuma ambapo ilizoeleka kuwa mchezo wa draft ni mchezo wa watu waliokosa kazi au wahuni tu.

Bigi up kwa huyo java nimemuona akiwa mstari wa mbele sana kujiyolea kudhamini mapambano mengi.

Ipo siku hii michezo itakuwa na mashabiki wengi na itakuwa chanzo tegemezi cha uingizaji kipato kwa watu wengi japo saizi inachukuliwa kama passion tu.
 
Tusaidie na picha za mabingwa tuwajue hata kwa sura tu

Kuna umuhimu wa kuwajua maana wana kawaida ya kutembelea kwenye vijiwe tofauti tofauti na kujifanya matula wanaomba wazuilishwe sare

Wakicheza friend mechi wanacheza kipimbi ili wakuvute, ukiingia kingi kuwapa sare umeumia. Sio kama atakufunga ila atakuwa anakupelekea sare hizo hizo kwa mfumo wa kipimbi ili baadaye ubadirishe mkataba useme mfungane.

Ukisema mfungane hapo ndio umepotea mwisho wa siku ataondoka na jackpot halafu dakika ya mwisho ukajikuta wewe ndio unazulishwa sare moja na hiyo sare moja nayo huipati.
 
Mngeongea na azam wangefanya jambo...kama waliweza kuchezesha PlayStation wasingeshindwa kufanya jambo kwenye draft
 
Kwenye hayo mashindano makubwa naona hapo bingwa wa kijiwe chetu ni dogo hamis anatuwakilisha
 
Ungeandika bingwa wa mashindano ya draft ( british). Hata mwanza kuna wachezaji husafiri hadi Nairobi kucheza draft, sema vimwanaume vya dar kazi kujisifia tu eti vinajua draft wakati binti anakupita nyuma hata humtazami makalio 😁😁
 
Back
Top Bottom