Mashindano ya kumtafuta bingwa wa draft Tanzania 2022

Mashindano ya kumtafuta bingwa wa draft Tanzania 2022

Anaitwa nan maana Arusha wataleta bingwa wao, na huwa wanaleta bingwa wao anakufa vzr TU,

Unapozungumzia draft TZ unazungumzia Kinondon Manyanya ,hivi hamuelewagi

Mafund wote unaowajua ,lazima afike manyanya akaguliwe kwanza
Sure hapo ni draft college..ndio maana huko mikoa mingine isiyotajwa wachezaji wapo ila wanajijua hawana uwezo wa kutia miguu mashindano ya kitaifa
 
Hata
Tusaidie na picha za mabingwa tuwajue hata kwa sura tu

Kuna umuhimu wa kuwajua maana wana kawaida ya kutembelea kwenye vijiwe tofauti tofauti na kujifanya matula wanaomba wazuilishwe sare

Wakicheza friend mechi wanacheza kipimbi ili wakuvute, ukiingia kingi kuwapa sare umeumia. Sio kama atakufunga ila atakuwa anakupelekea sare hizo hizo kwa mfumo wa kipimbi ili baadaye ubadirishe mkataba useme mfungane.

Ukisema mfungane hapo ndio umepotea mwisho wa siku ataondoka na jackpot halafu dakika ya mwisho ukajikuta wewe ndio unazulishwa sare moja na hiyo sare moja nayo huipati.
haya mambo aliyafanya dogo ally ifakara alijiangushaa wee akafika adi mangula uko akaishia kurudisha pesa zake na faida..na kubwa zaidi kuna wasukuma waliliwa adi makreti ya soda na bia...

Nyingine personally nshawahi kumvamia kilaba nilipigwa hatari..ikabidi nimsemee kwa mkulima wa online draught tz acheze nae kwa dau la 5000 kila mchezo..ila kilaba alikimbia kucheza na mkulima...yani niliingia mkenge kiboya sana
 
hakuna mnyama hata mmoja hapo mi napiga wote nakata nafunua! wao wana madrafti yao ya kukariri ukianza tu kucheza wanakwambia jina la huo mchezo sasa huko mbele mi sichezi wanavyotarajia wao!
We tula tu.panda kitandani online nikuue
 
Wapo sahihi , tanzania tuna aina yetu ya mchezo ambayo inaitwa Tanzania draughts (sijui kama nimeandika vizuri ) .
-Hapa tunasheria zetu za namna ya kucheza ambazo kimsingi kwa namna fulani zinafanana na draughts za nchi nyingine kama vile American draughts /british draughts. Ila sasa sifa pekee ya Tanzania draughts ni kuwa king can make very long jumps, and can move back and forth . Wakatika american draughts /british draughts yenyewe inafanana kila kitu katika uanzaji wake na Tanzanian draughts lakini yenyewe king haiwezi kumake long jumps . Na kupelekea vitu kama force king kutokuwepo kirahisi ( wacheza wa draft wananielewa hapa nini nasema kama utacheza draft afu force king ziwe hazipo )

- sasa kwa upande wangu mimi nawapongeza sana waliondaa haya mashindano maana siyo tu wanaupromote huu mchezo wa draft Tanzania bali wanapromote kitu cha nyumbani ambacho dunia inatambua kuwa kwa sheria hizi na hizi zinachezwa Tanzania tu . Tofauti na french style of playing , ambayo kama tungeanzisha mashindano yake tunge promote kitu cha kigeni na siyo cha nyumbani.
Ajabu hiyo wanaita French huku Tz. Ndiyo wanayocheza waingereza(British). Sisi aina yetu ni ya kipekee sana.
 
naomba nikusaidie hapa , wanaposema washiriki watapitishwa na mikoa yao wana maana hii, mfano Iringa wachezaji wazuri wa draft tunawajua , sasa ni sisi wanairinga kuamua kupendekeza ni nani akatuwakilisha baada ya kujadiliana kwenye club zetu au kuamua kuandaa mashindano ambayo yatawakilisha wachezaji wotee wa mkoa afu mshindi atashinda ticket ya kwenda kutuwakilsha Dar es salaam katika mashindano ya kitaifa.

Baadhi ya mikoa kutokuwepo kabisaa , hii inatokana na mikoa hiyo kutokuwa na clubs za mchezo wa draft na kupelekea ugumu fulani katika kuwasiliana na wahusika wa mkoa usika lkn pia baadhi ya mikoa kutokuwa na upenzi na huu mchezo au kutokucheza huu mchezo katika sheria pendekezwa hapo juu. Mwisho ni baadhi ya mikoa (katika historia ) kutoa wachezaji wenye uwezo mdogo mnoo .

Unajua huu mchezo haupo kama wengi wajuavyo . Hawa wenzetu wa dar wametuzidi pakubwa mno ktk huu mchezo, kuna kigezo hapo cha omary john 14 hivi hapo umekielewa hicho kigezo ?
- ngoja nikufahamishe ni hivi, wachezaji wengi wanajiona au wanaitwa mabingwa kwasababu ana namna fulani ya kucheza huu mchezo , lkn katika omary john kila mcheza anatakiwa aanze kete zote 7 za vyumba vya mwanzo yaani anatakiwa aanze

Pasati , nugza , meja , kavimba, taa ya treni , mabano na tege . sasa wachezaji wengi wa mikoani utakuta anajua meja lakini mabano hajua au tege hajui , sasa mikoa iliyotajwa kidogo wanaufahamu juu ya hiyo sheria ya omary- john
Kwanin wanaiita omary- john ni kama njia ya kuwaanzi wachezaji wa wili omary na john ambao walipenda kucheza katika utaratibu huo wa kuanza kete zote za mwanzo na kuzipa majina niliyotaja hapo juu.

- Katika mchezo unaoitwa tege . Kuna sheria imesema watacheza tege 4. kwanini wamesema tege na siyo meja , nugza au pasati ?
ni hivi tege ni mchezo unaotaka mchezaji aanze kete ambayo wachezaji wengi wanaamini ni kete dhaifu kama utaanza na kupelekea ufungwe kirahisi na mpinzani wako. Sasa kwasababu wengi wanajua hii itapelekea sare ziwe nyingi na kupelekea mashindano yawe marefu , hivyo kwa kupendekeza wacheze tege basi tunaweza kuokoa muda kwa kuepusha sare zisiwe nyingi.
Unaijua kazi yako. Big up
 
Hata
haya mambo aliyafanya dogo ally ifakara alijiangushaa wee akafika adi mangula uko akaishia kurudisha pesa zake na faida..na kubwa zaidi kuna wasukuma waliliwa adi makreti ya soda na bia...

Nyingine personally nshawahi kumvamia kilaba nilipigwa hatari..ikabidi nimsemee kwa mkulima wa online draught tz acheze nae kwa day la 5000 kila mchezo..ila kilaba alikimbia kucheza na mkulima...yani niliingia mkenge kiboya sana
Hivi mkulima anajulikana ni nani? Jamaa anahesabu sana. Watu wanasema anagoogle, anacheza na simu mbili.
 
Draft ni miongoni mwa michezo inayosisimua sana na unayo wapenzi wengi ikisimamiwa vizuri kwa mpangilio maalumu ikanyanyuliwa hadhi yake itastajabisha sana kwa ushabiki wake na wapenzi wengi, HONGERENI.
 
Hao mabingwa wakubwa akina nani ambao kasikio hajawapasua,kifupi tu hao wambingwa wenu wote hakuna anayetia mguu kwa kasikio,muulize sukka ronaldo na mangwerere wanajua moto wake vizuri.
Mangwerere ni mstaafu siku hizi hachezi ila huyo kasikio anaweza akawa anatamba kwenu ila ukimuonesha hiyo list hapo juu lazima awe mnyonge

Au kama vipi mwambie aje ashiriki, sitaki kuamini kama yeye anajua draft kuliko hao halafu aiche milion 2 impite hivi hivi

Mwambie aje, afu baada ya game watu ndo tutajua ni kaskio au kajicho
 
Hao mabingwa wakubwa akina nani ambao kasikio hajawapasua,kifupi tu hao wambingwa wenu wote hakuna anayetia mguu kwa kasikio,muulize sukka ronaldo na mangwerere wanajua moto wake vizuri.
Mkuu kumekucha acha kuota..huyo kasikio mbona hata ubingwa wa taifa singida 2017 hakushiriki (kama yuko mwanza na kigezo ni umbali)..?? Au huwaga anachezea geto na wanawe. ?? Ivi mtu atoke kazuramimba aje amfunge ronaldo...!??
 
Mkuu kumekucha acha kuota..huyo kasikio mbona hata ubingwa wa taifa singida 2017 hakushiriki (kama yuko mwanza na kigezo ni umbali)..?? Au huwaga anachezea geto na wanawe. ?? Ivi mtu atoke kazuramimba aje amfunge ronaldo...!??
Cr7 yeye alijifunzia wapi
 
Hahaaha nao wadau wa british nao wanapiga vijembe draft la french wanakuambia kucheza french ni kuzidi kupigia kampani ushoga

Kwanini ule mbele na nyuma?
Hahaaa! Kwa hiyo british mnampigia chapuo king ndo ale mbele na nyuma tu?
 
Back
Top Bottom