Maskini Baba Diamond, azidiwa ghafla




Si alimkana Diamond kuwa sio mwanawe tangu akiwa mdogo? sitaelewa unataka kumaanisha nini kwa kweli. baba aliambiwa mtoto wake akasema sio wake akasepa. Mama amebaki na mtoto wake labda mtoto aliishia mikononi mwa baba mwingine. sioni sababu ya kumuhitaji Diamond kwa sasa au kulaumiwa Diamond au kutafutwa, huyu mzee ni mtu mstaharabu sana hataki shida.
 
Nimeipenda sana hii,ni ukweli usio pingika wanawake mara nyingi wana influence kubwa sana kwa watoto (power of a woman),kitu kinachowafanya hata kuwachukia baba zao bila ya kujua ukweli wa tatizo.Najua kuna watakao pingana na mimi kwa kuwa malezi yao sio ya kuunga unga kama ya kina sie ambao tume experience hivi vitu kakatika makuzi yetu.
 

Sijaelewa unachoeleza hapa. Baba alisema mtoto sio wake na akaondoka kabisa. Ina maana huyo diamond sio mtoto wa huyo baba. Diamond hatajutia nini wakati huyo sio baba yake na huyo mzee alisema sio mwanawe.
 
Kama unatambua kuwa ni mwanao na umekosana na mama weka utaratibu wa kulea mtoto. Mtoto unayetelekeza sijui anakuwa na kosa pia? Kama mama ni tatizo inakuwaje kuacha kulea mtoto au unakuwa ni mkwepa majukumu?.
 
Mzee arudi nyuma akumbuke alichokifanya kuwa haya ndiyo mavuno,picha zinaonyesha kuwa hazikupigwa kikachero bali ni dhamira kwakuwa waliopo kwenye picha wote wamejiandaa kuangalia camera.
Aendelee kula ujana wake mbovu,na iwe fundisho kwa VIJANA UCHWARA,mabingwa wa kukataa mimba huku wakiwa mafundi kwenye "KUSIMAMIA"
 
Kama unatambua kuwa ni mwanao na umekosana na mama weka utaratibu wa kulea mtoto. Mtoto unayetelekeza sijui anakuwa na kosa pia? Kama mama ni tatizo inakuwaje kuacha kulea mtoto au unakuwa ni mkwepa majukumu?.
Najua ni ngumu sana kuelewa hii kitu,kweli wapo wanaofanya makosa kwenye maamuzi ya jinsi ya kumlea mtoto,lakini ninachotaka pia ufahamu ni kuwa utamu au ladha ya kuwa na mtoto huwezi kuujua kama huna mtoto,na inapofikia mpaka baba anaamua kuacha kuhudumia mtoto kwa sababu nyingine tu ukiondoa kuwa labda kabanwa na nyumba ndogo and the like ujuwe kuna zaidi ya hayo yanayosemwa na watu ambao hawajui kiundani.
 
Sijaelewa unachoeleza hapa. Baba alisema mtoto sio wake na akaondoka kabisa. Ina maana huyo diamond sio mtoto wa huyo baba. Diamond hatajutia nini wakati huyo sio baba yake na huyo mzee alisema sio mwanawe.
Baba D nae aache kulia lia. Je D aisngekuwa nazo hataishi? Aishi kiume as if mwanae hana kitu. Akiamua kumsaidia ni kwa ridhaa yake na sio lazima. Tunawajibika kuwaendeleza watoto wajitegemee na siyo watutegemeze.
 
Diamond anakosea sana. Yaani anahangaika na Zari halafu anamuacha babake anateseka
sidhani kama unajua unachokiongea. Diamond alishawahi kueleza hadi kutoa machozi maisha yake ya mateso utotoni wakati baba yake akila bata na mke mwingine na hakuwahi kumsaidia, zaidi ya kumfukuza. mwache huyu mzee avune alichopanda. ndio dawa ya wazee wenye kukataa damu zao
 
Lazima tujifunze kuwa na roho ya kusamehe. Hayo mambo yalitokea kipindi cha nyuma na hatuwezi kujua ni nini chanzo chake. Diamond anapaswa kuelewa kuwa duniani kuna baba mmoja na mama mmoja tu.
 

Ameridhika na mama yake aliyepigana kufa na kupona kuona maisha ya mwanae yanafanikiwa wakati baba ambaye hakumtambua kipindi hicho akila bata na mke mwingine. acha aonje joto ya jiwe, ndio dawa ya mababa suruali.
 
Lazima tujifunze kuwa na roho ya kusamehe. Hayo mambo yalitokea kipindi cha nyuma na hatuwezi kujua ni nini chanzo chake. Diamond anapaswa kuelewa kuwa duniani kuna baba mmoja na mama mmoja tu.

mama yake ali play part zote mbili na maisha yalienda wakati huyo baba anaishi maisha mazuri. sidhani kama ulisikiliza kipindi cha Diamond maisha aliyoishi na alivyofukuzwa na huyu anayejiita baba wakati alienda kuomba pesa za kaptula ya shule ambayo ilikua imekwisha, ilhali uwezo alikua nao.
achene Diamond ale bata na mama yake ambae hakuwahi kumtupa hata siku moja katika shida zote walizopitia.
 
Dedication kwa wababa wote mnaokimbia wtt,wakifanikiwa mnakuja kifua mbele mkome mnatakiwa mtulie km kipindi kile cha kulea,my dady is one of them cmchukiii na nimemsahame,ila moyoni mwangu hayupo kama mm nicvyokua moyoni .wake
 
Baba ni baba
 
tumwache Diamond na maisha yake. ni mtu mzima. yaliyo nyuma ya pazia hatuyajui. wababa ndio mpate fundisho hapa, tabia za kukataa watoto wakiwa wadogo muache maana hujui baadae atakua nani na wewe utakua nani. sio muanze kulia lia na waandishi wa habari utadhani una act movie, kisa umetelekezwa, wakati mtoto alipokuhitaji hukuwepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…