Maswali kuhusu matumizi ya stendi mpya ya mabasi Mbezi (so-called Magufuli)

Maswali kuhusu matumizi ya stendi mpya ya mabasi Mbezi (so-called Magufuli)

inchi zilizoendelea
mfano wa nchi gani uliyotembelea ambayo kuna system uliyoi refer?. Mimi najua mfano, wanaokwenda Mtwara /Lindi watakuwa na stend yao huko, siyo lazima aje Mbezi, kunakuwa na shuttle buses kutoka Mbezi kuja Mbagala na kupanda mabasi ya Mtwara/Lindi.................. something of that nature
 
Zinahitajika stand kama hiyo Temeke/ Mbagal, Tegeta
Exactly, mabasi ya Mtwara/Lindi yabaki huko na stend yao Mbagala. Ukitoka Mbezi kunakuwa na shutle buses kutoka Mbezi kwenda Mbagala , then unapanda mabasi ya Mtwara!
 
kama zaman stand ilikuwa kisutu na watu walikuwa wanatoka mbagala hadi kisutu
Kulikuwa hakuna foleni kama sasa, it was easy to move from one point to another... sasa na hizi foleni mabasi yote yanayoingia Dar yaje Mbezi, foleni zitakuwa balaa! Nawza kitu kama hicho....
 
Mbagala hadi kisutu mbona sio mbali mkuu,

Imagine mbagala hadi mbezi Louis?! Wengine wanatokea mbande, chamazi mpaka mbezi mwisho?!

Wengine wanatokea kongowe, mwandege, kigamboni, kibada, kisemvule mpaka mbezi Luis ?!

Ukifahamu fika hakuna route ya basi la moja kwa moja kutoka mbagala, mbande, chamazi, kongowe, kigamboni au kisemvule mpaka mbezi ?! Si mateso hayo?!

Hii sio haki ni unyanyasaji mkubwa!

Mabasi yaruhusiwe kupakia abiria kutoka ofisi zao ndogo lakini lazima yapitie stend kuu ya mbezi, na sio kuyazuia kabisa kupakia kwenye stand zao ndogo!
Mbona stesheni ya reli ipo moja Dar na wote hupandia pale haijalishi unakaa mbezi, Bunju, kimara, mbagala au kigamboni
 
Hiyo ni kazi mojawapo, kwani ubungo kazi za ofisi za mabasi zinapakia abiria?

Mie sikuongelea hizo ofisi za kukatia tiketi na kutuma mizigo, nimelenga mabasi kama Dar Lux, Kilimanjaro, Dar Express na mengine ambayo licha ya kupita Kituo kikuu cha mabasi, walikya na vituo vyao binafsi vya kupakia na kushusha abiria, hivyo ndio nimehoji, vitaendelea kutoa hiyo huduma?
 
Tumeona na kusikia malalamiko ya uendeshaji mengi tu, tuliyategemea, hayako rafiki kwa wasafiri, itachukuwa muda wapatie, ila watu wanashauri hao waendeshaji, au waonyeshwe clip jinsi coach stations zinavyoendeshwa na wenzetu, kuanzia msafiri anapoingia mjengoni mpaka anasafiri, mbona kutanoga, ila hongera kwa maendeleo hayo...hivi vitu vigeni kwetu lazima tujifunze kwa wenzetu waliowahi..
 
Mbona stesheni ya reli ipo moja Dar na wote hupandia pale haijalishi unakaa mbezi, Bunju, kimara, mbagala au kigamboni
Mkuu Kim Jong Jr kikubwa ni geographical position.

Stendi ya Train ipo center, posta ni kati ya jiji na kiukweli sio mbali sana ukiliiinganisha na Mbezi Louis hasa kwa kwawakazi wa maeneo ya mbagala , kigamboni, kongowe nk

Stand ya train iwe ya TRC au TAZARA, iko pale kwa muda mrefu , na usafiri wakufika pale unapatikana kw a uhakika sio ubabaishaji kama kutoka maeneo ya pembezoni mwa jiji hadi mbezi Louis,

Stend ya mabasi imekuwa haitabiriki ina hamishwa hamishwa kwa muda mrefu kwakigezo cha kuleta msongamano,

Mkuu mimi sio mgeni hapa jijini, Niko hapa Dar kwa zaidi ya miaka 40 sasa, tulianza kupanda mabasi ya KAMATA, enzi hizo stend kuu ya mabasi ilikuwa pale kariakoo , gerezani, Kamata karibu na traffic lights.

Wakaja wakaihamisha ile stendi ikapelekwa pale Mnazi mmoja , kwakigezo cha msongamano katikati ya jiji,

Ikaja kuhamishwa tena na kupelekwa pale kisutu, kwakigezo kuwa pale mnazi mmoja ni padogo kulingana na wingi wa watu na mabasi,

Napo pia ikahamishwa tena na kupelekwa Ubungo, kipindi hicho ubungo ilikuwa pembezoni mwa jiji kama ilivyo mbezi Luis kwasasa.

Sijui na hapo Mbezi Luis stendi mpya itakaa kwa muda gani kabla ya kuhamishwa tena?! Tatizo ni watu wa mipango miji wanashindwa nini kubuni eneo permanent kama stend za railways, au basi wajenge stendi hata mbili au tatu mfano iwepo mbagala, bunju na mbezi.
 
Lengo la usafiri wa umma ni kuwasiaidia watu kurahisisha safari zao, lakini inapoweka mazingira kuwa magumu zaidi hapo hauwasaidii bali unawaumiza!

Unajua umbali uliopo kutoka mbagala mpaka mbezi Luis?! Hapo sijagusia ndani zaidi kama charambe, matitu, chamazi, mbande, kisewe, msongola, mvuti na chanika?!

Unajua umbali uliopo kutoka kongowe, kibada , mjimwema, kigamboni, mpaka mbezi Luis?!

Unajua umbali uliopo kutoka mwandege, kisemvule mpaka mbezi Luis?!

Kote huko hakuna basi la moja kwa moja mpaka mbezi stendi kuu, lazima upande madaladala mawili au matatu kufika mbezi bus terminal,

Hapo abiria anakwenda either moshi, arusha, tabora, singida, shinyanga, mwanza ,kigoma au kagera! Aamke saa tisa usiku kuwahi daladala kutoka kisemvule, asubiri ijae, bado hujagusia foleni, ashuke kariakoo au tandika, achukue daladala nyingine hadi mbezi , mtu huyu ana watoto na mizigo tele!

Hapo utakuwa umemsaidia urahisi wa safari yake au umemtwika mateso zaidi?! Serikali iliangalie hii upya kwa jicho la tatu. Wengi tulikuwa tunategemea urahisi wa kupandia stendi ndogo na ofisi ndogo za mabasi husika ya mikoani.
Naona watu wanachangamkia fursa kwa kujenga lodge pembeni mwa kituo, kuna mtu pale jirani amepiga kitu cha vyumba 16!kuwasaidia watu wanaotoka mbali akina Mbande ,Vikindu na wenzao, kwakweli kufa kufaana.
Anyway watu wa mbali itawa cost sana mfano Nauli ya kwenda Tanga ni 20,000/= itabidi utenge 20,000/= nyingine ya lodge na 10,000/= ya kula km una mpango wa kusafiri mapema unless umepanga kusafiri mchana.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Kim Jong Jr kikubwa ni geographical position.

Stendi ya Train ipo center, posta ni kati ya jiji na kiukweli sio mbali sana ukiliiinganisha na Mbezi Louis hasa kwa kwawakazi wa maeneo ya mbagala , kigamboni, kongowe nk

Stand ya train iwe ya TRC au TAZARA, iko pale kwa muda mrefu , na usafiri wakufika pale unapatikana kw a uhakika sio ubabaishaji kama kutoka maeneo ya pembezoni mwa jiji hadi mbezi Louis,

Stend ya mabasi imekuwa haitabiriki ina hamishwa hamishwa kwa muda mrefu kwakigezo cha kuleta msongano,

Mimi sio mgeni hapa jijini Niko hapa kwa zaidi ya miaka 40 sasa, tulianza kupanda mabasi ya KAMATA, enzi hizo stend mkuu ya mabasi ikiwa pale kariakoo , gerezani kamata , traffic lights,

Wakaja wakaihamisha ile stendi ikapelekwa pale Mnazi mmoja , kwakigezo cha msongamano katikati ya jiji,

Ikaja kuhamishwa tena na kupelekwa pale kisutu, kwakigezo kuwa pale mnazi mmoja ni padogo kulingana na wingi wa watu na mabasi,

Napo pia ikahamishwa tena na kupelekwa Ubungo, kipindi hicho nilikuwa pembezoni mwa mji kama ilivyo mbezi Luis kwasasa,

Sijui na hapo mbezi Luis itakaa kwa muda gani kabla ya kuhamishwa tena?! Tatizo watu wa mipango miji wanashindwa nini kubuni eneo permanent kama stend za railways, au basi wajenge stendi hata mbili au tatu mfano iwepo mbagala, bunju na mbezi.
Mkuu acheni kulialia watanzania sijui tukoje.

Hizo changamoto zigeuze fursa. Kama unaona watu watapata tabu kwenda Mbezi luisi kwa usafiri wa asubuhi anzisha usafiri wa kuwapeleka wateja stand hata na kigari kidogo kila asubuhi.


Mbona tunachezea fursa hivyo. Shida yako ni fursa kwa wengine. Kuna watu wanataka uumwe ili wapate hela. Ningetamani uombe stand ipelekwe nje ya mji kabisa ili uchangamkie fursa.

Jitahidi kila kitu uwe unakirafsiri kwa Jicho la kifursa utaona Kuna sehemu nyingi hela tunazipotezea.
 
Naona watu wanachangamkia fursa kwa kujenga lodge pembeni mwa kituo, kuna mtu pale jirani amepiga kitu cha vyumba 16!kuwasaidia watu wanaotoka mbali akina Mbande ,Vikindu na wenzao, kwakweli kufa kufaana.
Anyway watu wa mbali itawa cost sana mfano Nauli ya kwenda Tanga ni 20,000/= itabidi utenge 20,000/= nyingine ya lodge na 10,000/= ya kula km una mpango wa kusafiri mapema unless umepanga kusafiri mchana.

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
Tanga Kuna Gari muda wote kwanini ulale lodge.

Kwanini usitoke Nyumban asubuhi saa moja upande gari za saa 2 kwenda tanga.
 
Back
Top Bottom