Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Asakwe Hadi apatikane na akome kudili na wachaga the chosen oneMuhuni mwingine huyu hapa tutakusaka hadi mvunguni pumbavu mkubwa wewe.
Yaani nyie ndiyo mnamkwamisha Mama.
Tutadili na nyie perpendicular
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mmh; Kaya imeharibika. Ninachukua jembe nikalime. Safi sana, tena bambam.Naingia kwenye mada moja kwa moja nisiwachoshe. Baada ya mwendazake kufanikiwa kuiharibu hii nchi kwa kubaka Uchaguzi Mkuu wa 2020, sasa CCM inaongoza nchi nzima kuanzia Balozi hadi Rais. Mwendazake aliwahi kusema kwamba CHADEMA ndio wanamkwamisha kuwaletea wananchi maendeleo, hivyo akaamua hata mCHADEMA mmoja asirudi uongozini baada ya 2020. Na kweli mbinu yake ilifanikiwa kwa 101%. Sasa nchi nzima imefunikwa na kijani kibichi tu!
Nilitarajia wanaCCM wote sasa wangeridhika na kuunga mkono juhudi za Rais aliyepo madarakani. Lakini baada ya kifo cha mwendazake, limejitokeza kundi wa MATAGA (waliokuwa wakimuunga mkono mwendazake kindakiki) kumkwamisha Rais Samia kwenye harakati zake za kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli. Hiki kikundi cha MATAGA hakitofautiani na vikundi vingine vya kigaidi kama vile Mungiki, Janjaweed, Al-Qaeda, Boko Haram, Al-Shaabab au genge la kihalifu alilokuwa akilitumia Sabaya kupora mali za raia na kuhujumu uchumi wa taifa. Genge hili ni zaidi ya pimbi anayekurupuka kutoka kichaka A kwenda kichaka B lakini baada ya sekunde chache anakurupuka tena kurudi kichaka A. Kwa ujumla, MATAGA hawajui ni nini wanachokitaka!
MATAGA ni genge la hatari sana na endapo juhudi za makusudi hazitachukuliwa kuwadhibiti, watayumbisha mno maendeleo ya taifa hili. Na kibaya zaidi, baadhi ya wafuasi wa genge hili wameanza kujikomba kwa mama kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili wakae karibu naye wamharibie. Wanachama wa genge hilo wanajionyesha hadharani kwa vicheko vyao vya kinafiki huku mioyoni mwao wamejawa na husda na unafiki wa kupindukia.
MATAGA wapo kila kona ya nchi hii. Wengi wao wanatumia mitandao ya kijamii kuzusha mambo ya ajabuajabu kuhusu kifo cha mwendazake ili kumtoa mama kwenye reli. Nashukuru mama ameanza kuwashutukia baadhi yao na kuwachomoa mazima kutoka kwenye ulingo wa serikali yake. Kilichotokea majuzi ni ushahidi tosha kwamba janja yao ya nyani imeng’amuliwa mapema kupitia intelijensia ya uhakika.
Ingawa hivyo, namuomba mama Samia atumie mbinu kali kidogo kuwadhibiti CHAWA hawa kabla sumu yao haijasambaa sana kiasi cha kushindwa kudhibitika baadaye. Inasikitisha kuwa genge hili linatoka ndani ya CCM; badala ya kumsaidia mama kujenga nchi, wao wanasaidia kuibomoa. Hawa ni watu wabaya sana, sio wa kuwalazia damu hata kidogo. Hata ikibidi, basi wadhibitiwe kwa mbinu zozote mbaya na za hatari kabla mambo hayajaenda kombo.
Sikusikia sauti ya SSH hata kidogo zaidi ya kuguna. Hii ina ishara gani? Je, mlingoti umefika unapotakiwa.
Tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutuletea Rais huyu mpenda amani, mcha Mungu, mwanademokrasia na mpenda haki. Nchi hii itapata maendeleo kwa haraka sana.Sikusikia sauti ya SSH hata kidogo zaidi ya kuguna. Hii ina ishara gani? Je, mlingoti umefika unapotakiwa.